Jumatano, 2 Machi 2016

Jinsi ya Kuwa na Ushindi dhidi ya Uchawi !



Uchawi ni moja ya maeneo makubwa ya utendaji wa kazi wa ibilisi katika kuwaonea wanadamu na kushindana kinyume na Mungu, katika somo hili tutajifunza kwa undani asili ya uchawi na jinsi ya kuwa na ushindi dhidi ya uchawi makusudi makuu hasa ikiwa ni kukusaidia mtu aliyeokoka kutokuwa na hofu dhidi ya uchawi endapo utazingatia ufahamu utakaoupata katika somo hili tutazingatia vipengele vifuatavyo;-

·         Asili ya Uchawi
·         Jinsi ya kuwa na Ushindi dhidi ya uchawi.

Asili ya Uchawi.
Uchawi ni kazi ya Shetani na mtu yeyote anayejishughulisha na Uchawi ni mtumishi wa shetani anayekuwa amepewa kibali cha kuwatumia mapepo na majini kwa kusudi la kuwadhuru wanadamu na kuwafanya wanadamu wamuabudu shetani, kwa lugha nyepesi mtu awaye yote anayejishughulisha na uchawi anafanya ushirikiano na shetani kwa hiyo huitwa MSHIRIKINA, Biblia inakataza wakristo kushirikiana na shetani kwa gharama yoyote 1Wakoritho 10; 20-21 Matendo 13; 6-10. Ni muhimu kufahamu kuwa ili mtu awe na Ushindi dhidi ya uchawi anapaswa kwanza kuamini kwamba Uchawi uko ufahamu huu haukufanyi wewe kuwa na mawazo ya kizamani lakini ni ufahamu unaokubaliana na neno la Mungu ambalo lenyewe linatambua kuwa uchawi uko  Kutoka 7; 11 Nahumu 3;4 Matendo 8;9-10, Ezekile 47;8-15, Moja ya mbinu kubwa ya shetani anayoitumia ni kuwapandikizia watu wazo potofu kuwa kusema kuwa uchawu upo ni imani potofu zilizopitwa na wakati ni imani za kishirikina Huu ni uongo wa Ibilisi ili aendelee kutesa watu kupitia njia za kichawi huku wao wakidhani kila kitu ni cha kawaida tu!
Ni muhimu kufahamu kuwa Pepo wabaya wao walikuwa malaika ambao waliasi na wamekwisha kuhukumiwa na hatima yao ni katika ziwa la Moto waliowekewa tayari mileleWaefeso 6;12,Mathayo 25;41 Shetani na majeshi yake yote hayana uwezo wowote mbele za Yesu Kristo aliye Bwana na mwokozi wetu alipokuwa Duniani na hata akiwa huko mbinguni shetani na mapepo yanamuogpa sana Bwana Yesu kwani ana mamlaka ya kuwatesa Marko 5;1-13, tunapokuwa tumemuamini Yesu tunakuwa ndani yeke na kwa sababu yeye ndiye kongozi wetu Uchawi wa kila namna hauna nguvu tena ju yetu Ufunuo 3;20; Hesabu 23;23 Historia ya kibiblia inaonyesha kuwa wachawi wakati wote walipokumbana na nguvu za Mungu  walikiri kuwa Bwana ni mwenye uwezo na kuwa hawawezi kushindana naye Kutoka 7;10-13,8;16-19,9;9-11, Simeon aliyekuwa anaogopewa sana huko Samaria alipokutana na uweza wa Bwana alisalimu amri na kukiri kuwa Uweza wa Bwana ni mkuu Matendo 8;9-13, Elima Yule mchawi naye alisalimu amri wakati Paulo alipoliitia jina la Bwana kumshughulikia Matendo 13;6-12.
Ni muhimu kufahamu kuwa hata katika nyakati hizi tulizonazo watakuweko wachawi huko mitaani na vijijini na mijini na nyumba tunazoiishi watakuwa wakijaribu kupambana nasi ili kututia woga tutahisi miili ikisisimka, kutembelewa na viumbe vya ajabu dalini au usumbufu wa panya wasio wa kawaida n.k kila uonapo dalili hizo usiogope kwani tumepewa amri ya kukanyaga nyoka na nge na NGUVU ZOTE ZA YULE ADUI hakuna kitakachotudhuru! Luka 10; 19
Jinsi ya kuwa na Ushindi dhidi ya wachawi.
Tubu dhambi zako zote kwa kumaanisha kuziacha  ili muovu asiwe na nguvu juu yetu Mithali 28;13 1Yohana 5;18 1Yohana 2;1-3, Kataa kazi zote za kishetani na kuchoma moto aina zozote za maagano na hirizi Matendo ya Mitume 19;17-20, Kaa katika kweli ya Neno la Mungu Yohana 8;31-32, Hesabu 23;23.

Hakuna maoni: