Jumanne, 8 Machi 2016

Mambo yaliyokuwako kabla ya Uislamu



     Ni muhimu kufahamu kuwa yako mambo yaliyokuwepo kabla ya uislamu na ambayo waislamu huyaamini na kuyaabudu hata sasa umuhimu wa kuyajua haya ni kupata uthibitisho ulio dhahiri kuwa uislamu ni upagani ulioboreshwa tu na kuwa Muhamad hakuleta jambo jipya

Mungu anayeabudiwa na waislamu aitwae allah.
   Mungu huyu anayeitwa allah kwa asili sio Mungu wa Ibrahimu na Isaka na Yakobo aliyewatoa Israel huko Misri kwa mkono wa nguvu na kujitambulisha  kwa Musa kwa jina la Yehova katika (Kutoka 6;2-3)Kinyume na huyu allah alikuwa ni mungu wa wapagani ambae awali alikuwa  na mabinti zake watatu au wakeze watatu ambao waliitwa al- lat (mungu jua),al-manat (mungu sayari venus au nyota) na al-uza (mwenye nguvu)Mkuu wao aliitwa Hubal ambae baadae alikuja kujulikana kama allah na ndiye aliyekuwa mungu wa mji wa makka (Surat an najim-nyota 53;19-20)Mungu huyu ndiye anayeabudiwa na waislamu leo na jitu lililomtokea Muhamad lilimuamuru kumuabudu mola huyu wa nji wa makka soma(surat Naml-sisimizi 27;91) miungu hii ilikuwa maarufu pale makka wakati Muhamad anazaliwa (Najm 53;21-23)na huyu allah alikuwa mungu mwezi,inaaminika na baadhi ya wasomi kuwa jina allah au al-llah linatokana na jina Ilah ambae alikuwa mungu mwezi wa Arabia ya kusini ambao waliamini mungu mmoja bila kudharau mingine hivyo kwa asili waislamu wanaabudu mwezi na nyota hata Muhamad mwenyewe alipotaka kuapa aliapa kwa Nyota soma (Najm 53;1)  miungu mingine iliyokuwepo ni pamoja na  wadd (pia mungu mwezi) suw’a,yaguth na nasr soma (surat Nuhu 71;23)

Jiwe jeusi katikati ya msikiti wa makka “Hajar al aswad”.
    Jiwe hili jeusi hajar al aswad ni nyota au kimondo kilichoanguka zamani sana,Jiwe hili ndilo lilikuwa al kaaba ya wapagani, Ambao waliliabudu na kulisujudia soma kitabu maisha ya nabii Muhamad  ukurasa wa 15-16 kifungu h. mahali hapa muhamad alipozaliwa tu alifanyiwa duwa na babu yake soma kitabu hicho uk wa 5 kifungu cha mwisho.Hapa ndipo wanapoabudu waislamu woote duniani huelekea hapo wakati wa sala na huenda hapo kufanya hija na hulisujudia jiwe hili na kuliabudu  kama unabisha soma kitabu vipi uhiji uk 29 cha shehk A.Suleman.Lazima ulisogelee jiwe hilo uweke mkono na kulibusu na kulisujudia mara tatu.Muhamad alipofikisha miaka 35 kabla hajapewa utume aliitwa kutatua ugomvi wa jamii ya makuresh kugombea kuliweka jiwe hili baada ya ukarabati wa al kaaba yeye akaliweka jiwe hili na ugomvi ukaisha soma kitabu maisha ya nabii muhamad cha sheikh abdulla Saleh Fars uk 15-16 kifungu h.


     Pichani juu mahali lilipohifadhiwa jiwe jeusi katikati ya msikiti wa makka kama linavyoonekana leo baada ya kuboreshwa mahali hapa inaaminika ni kamsikiti kadogo ka kwanza kalikojengwa na nabii Ibrahimu na mwanae Ishimail kwa ajili ya kumuabudu Mungu wakitumia jiwe lililotumiwa na nabii Adamu  Picha kwa hisani ya maktaba ya Mwalimu wa somo Mchungaji Innocent Kamote

Ibada ya Kutufu.
    Ibada hii pia kwa asili ilikuwa ya wapagani ambao walikuwa wakitufu uchi wa mnyama kabisa kutufu ni ibada ya kuzunguka al-kaaba hufanywa na waislamu wanapokwenda hija kwa sasa waislam wameiboresha ibada hii kwa kuwa huvaa migolole miwili bila kuvaa chupi ndani kwani nguo zilizoshonwa ni najisi soma kitabu hija na maamrisho yake cha sheikh awam shaaban kaifta uk wa 27 mambo yanayo harimishwa point namba mbili. Ili kuthibitisha kuwa ibada hii ilifanyika uchi soma Maisha ya nabii Muhamad
uk 4 kifungu a mwishoni. Unapokwenda kwenye jiwe hili jeusi hajar al aswad unaligusa na kuliabudu na kulisujudu mara tatu na kusema allh akbar (yaani mungu mkubwa) huku ukiliashiria lile jiwe kwa mikono yote kisha unasema maneno yafuatayo “Allah humma imana bika watasdika bikita bika biadhika watiiba lisunnat nabiyyika salla ilaahu wassalim” yaani “Ewe mola kwa imani yangu juu yako na kwa kuthibitisha kitabu chako na kwa kutekeleza ahadi yako na kuufuata mwenendo wa nabii wako natekeleza sala hii” kumbuka sala hii huelekezwa kwenye jiwe lile jeusi upo?

Ibada ya hijja ifanywayo na wislamu.
       Ibada hii pia ina asili ya Kipagani,wapagani walikuwa wakifanya hija pale al kaaba kwa kuzunguka wakiwa uchi wa mnyama wanaume kwa wanawake wakiamini kuwa nguo ni kitu kinachopata uchafu yaani najisi na hivyo haistahili kuvaliwa ibadani soma kitabu maisha ya nabii muhamad uk 3-4 kifungu a. pia inaeleza jinsi mahujaji wa kipagani (majahili) walivyofanya ibada hizo na jinsi Makureshi kabila ya muhamad walivyokuwa wakifanya huduma mbalimbali kwa mahujaji.makuresh walikuwa na jamii 12 tano kati yao walifanya huduma hizo jamii hizo ni 
Ø  Siqaya-Kutengeneza maji ya wanaokuja kuhiji
Ø  Rifad-Kutengeneza chakula kwa wale wasiojiweza
Ø  Hijaba-Kushika funguo za al-kaaba
Ø  Liwaa-Kupigana vita na kusaidia kuongoza misafara
Ø  Nad-wa- Kuongoza vikao vya makureshi
Hivi leo waislamu wanapokwenda kuhiji huelekea palepale na hufanya yaleyale ambayo wapagani walikuwa wakiyafanya na quran imewaamuru wakahiji hapa (surat Imran 3;96-97).Mwenye masikio ya kusikia na asikie!

Mwezi wa mfungo wa Ramadhani.
      Funga ya ramadhani pia ilikuwa funga ya wapagani,iliadhimishwa hata kabla ya Muhamad na uislamu soma kitabu maisha ya nabii muhamad uk 16 kifungu cha 3 sura ya 4 “….Hata siku moja mwezi wa ramadhani 17 jumatatu mwaka wa 40 unusu wa umri wa Muhamad alienda pangoni…..”Hii ina maana funga ya ramadhani  ni ya wapagani na muhamad aliifunga kama mpagani kabla ya utume na ndiyo funga hii ambayo waislamu wameamuriwa kuifunga katika quran soma (Surat al Baqara 2:183) al baqara-ng’ombe jike, soma pia ufafanuzi katika al-Bukhar vol 16 no;-28…. “walikuwa wakifunga majahili kabla ya Muhamad pale makka” majahili ni majinga inashangaza ibada hizi za majinga ndio alla anawaamuru waislamu kuzifuata.!

Msikiti wa Mecca.


Msikiti wa Mecaa kama unavyoonekana katika pichani leo msikiti huu ni maarufu kama al-Haram uko Saud Arabia ndio mahali panaposadikiwa kuwa patakatifu zaidi katika misikiti ya waislamu al –kaaba  iko katikati ya msikiti huu, mji wa mecca ndio mji aliozaliwa Muhamad mwanzilishi wa Uislam na ndio mji ambao waislamu wanapaswa kufika kwaajili ya kuhiji japo mara moja katika maisha kama wana uwezo na ndipo mahali ambapo wakisali wanatakiwa kuelekea Kibla .

Hakuna maoni: