Jumamosi, 5 Machi 2016

Kiwango cha chini cha maombi ni lisaa limoja?



Kiwango cha chini cha maombi ni lisaa limoja!.
“Kiwango cha chini cha maombi ni lisaa limoja!”ni moja ya mikazo ya wahubiri inayowatia watu katika kongwa kiasi ambacho wanashindwa au wanajikuta kuwa hawaombi kabisa hata dakika tano kwa nini kwa sbabu ya mkazo mkubwa kuhusu maombi baada ya kuokoka andiko linalotumika ambalo limetumika vibaya kuleta fundisho hili ni Mathayo 26;40-45. Tofauti na mikazo ya wahubiri Kristo hapa hakumaanisha kuwa kiwango cha chini cha kuomba ni saa moja Yesu alisema hivi “Hamkuweza kukesha name hata saa moja?” kwa tafasiri sahii za andiko hilo ni muhimu kufahamu kuwa wakati wa Yesu kihistoria saa zilikuwa bado hazijagunduliwa na kwa mujibu wa Waebrania waligawa muda kwa kutumia neno zamu hasa kwa wakati wa usiku zamu ya kwanza ilikuwa ikianzia saa moja mpaka saa tatu usiku zamu ya pili saa nne mpaka saa sita hivi kasha zamu ya tatu saa saba mpaka saa tisa hivi na zamu ya nne ni saa kumi mpaka saa kumi na mbili hivyo ndivyo wayahudi walivyogawa muda kihistoria lakini neno saa katika Biblia yetu ya Kiswahili liliingizwa na wazee wetu waliotafasiri Biblia mwaka 1952 wakati huu saa zilikuwa zimekwisha gunduliwa na katika kawaida ya Kiswahili saa moja pia humaanisha jambo dogo


 Biblia iliposema Ombeni Bila kukoma ilimaanisha Maombi hayana kiwango cha Muda

Kwa tafasiri ya Kiyunani neno hilo saa moja hutumika Neno “HORA” ambalo kwa kiingereza ni “a little while” ambalo kwa Kiswahili chepesi ilimaanisha hata kidogo au Mara kwa kiibrania neno linalotumika ni “SODI” ambalo maana yake ni ileile hata kidogo au hata mara moja kwa msingi huu tafasiri ya kweli ya kimaandiko ni kuwa wanafunzi wa Yesu siku ile hawakuomba hata kidogo yaani hawakuomba kabisa na matokeo ya kutokuomba kwao yanaonekana wazi baadaye kidogo kwa wao kushindwa kustahimili majaribu wakati wa kukamatwa kwa Yesu na ndio maana Yesu aliwaambia maneno haya “Ombeni ili msiinge majaribuni” Yesu mwenyewe aliomba hivo alitiwa nguvu kukabili majaribu ya kukamatwa na kusulubiwa aliweza kukabili mateso ya msalaba kwa ujasiri hiii maana yake ni kuwa kama mitume wangeomba japo kidogo tu wangetiwa nguvu kukabili majaribu aliyokuwa mbeleni lakini kwa kutokuomba kabisa walimkana Yesu, wakamwacha wakakimbia na kusambaratika Mkazo mkuu hapa ni kuwa wakristo hawapaswi kupuuzia maombi kabisa na kona kuwa dakika chache za kuomba si za muhimu ni za muhimu sana kwanini wakristo wengi leo waliookoka hawaombi kabisa je unafahamu hilo mimi najua nawafahamu wakristo weng ambao walipokuwa katika makanisa yao ya zamani kabla ya kuja katika makanisa ya kipentekoste walifundishwa maombi mafupi mafupi “Simple prayers” kulikuwa na sala ya Bwana, na sala nyinginezo zilikuwa nyepesi sana walipokuja katika jamii ya makanisa ya kipentekoste hawakufundishwa maombi mepesi badala yake walikutana na mkazo mkuu kiwango cha chini cha kuomba ni lisaa limoja! Kwa hiyo mwanzon walijitahidi lakini sasa wanapojaribu kuomba lisaa limoja wanajikuta kwa sababu ya shughuli nyingi hawawezi kufikisha lisaa limoja na kwa sababu hawakujifunza maombi mepesi sasa hata zile sala walizotoka nazo katika makanisa yao ya zamani hawazitumii tena na hivyo wengi hujikuta wamelala na kuamka bila kuomba kabisa sasa kwanini mkazo ulipuuzia maombi mafupi sasa matokeo ni nini? Kongwa limekuwa zito hawawezi lisaa sasa inakuwaje wanakuwa wapagani kuliko kabla hawajaokoka wana wa jehanamu mara mbili hawaombi kabisa!


Hili ndio tatizo la kongwa unapowabebesha watu kongwa kwa kutumia maandiko isivyo halali unawafanya wengi kuwa wana wa jehanam mara mbili  zaidi kabala ya kuamini kwao ni muhimun kufahamu uwa tunaweza kumuomba Mungu katika nyakati fulan maombi rahisi kwa ufupi na yakafanya kitu Kipofu Batholomeo alipiga tu kelele Yesu mwana wa Daudi unirehemu  na maombi yake yalisikilizwa, Mathayo 8;1-3 wakoma wale kumi waliomba maombi ukitaka waweza kunitakasa je walichukua masaa mangapi kujibiwa maombi yao je walifunga? Jibu ni la Mathayo 14;29-31 au je wanafunzi walpokuwa wanazama katika dhuruba walichkua msaa mangapi kumuamsha Bwana kuwa wanaangamia kumbuka kuwa maomi mafupi mafupi yakiombwa kwa kumaanisha yanafanya kitu kuliko kutokuomba kabisa Kristo alipokuwa msalabani pia alikuwa na muda wa kuomba maombi mafupi mafupi kama Mungu wangu Mungu wangu mbona umeniacha? Au Baba mikononi mwako naiweka roho yangu, kumbuka kuwa maombi hayana kiwango kila muhubiri anapenda wau wawe waombaji lakini ni muhimu kufahamu kuwa Munu anaheshimu kiwango chochote cha maombi chimi ya neema yake mtu atakachoomba kwa moyo wa kweli bila kujali anatumia masaa mangapi mbele za Mungu dakika ina faida na masaa pia yanafaida tukifahamu hili hakutakuwa na kiburi wala huwezi kujigamba kuwa wewe ni muombaji kumbuka kuwa ungu hafanyi kwa sababu unaomba saa anafanya kwa sababu ya neema yake na upendo wake na mkao wako wa moyo, wengi wa wale wanaotangaza kuwa wanaomba sana kimsingi hawatofautian na mafarisayo na wanataka kujilinganisha au kutuwekea kongwa kuwa ni kiwango fulani cha maombi ndicho Mungu hukisikia na kuwa kiwango kidogo Mungu hasikii ? hii sio dhana ya kweli kwa Mungu ambaye ni baba Yeye ni Mungu aliye Karibu. Maombi ni swala la siri kla mtu na aombe kwa kadiri ya neema aliyopewa kle kiwango chako utakachokuwa umefikia ni chako wewe sio cha mwengine usimpandikizie wala usidharau chakwake ninachokisema kuwa maombi yaliyo bora ni yale ambayo Mungu anayasikia na kuyajibu bila kujali kiwango ni vizuri kukaa sana miguni pa Mungu kama ukiweza lakini Mungu hajibu mtu kwa sababu anakaa sana anajibu kwa sababu yeye ni baba aliye mwema kuwapandikizia watu kubeba masaa na masiku kibao ya kufunga ni kuwabebesha kongwa hivyo pamoja na uzuri wa maombi ni muhimu kufahamu kuwa maombi hayana kiwango na ubora wa maombi ya mtu si wingi wake bali ni vile anavyojibiwa mwenye masikio ya kusikia na asikie. Asomaye na afahamu  

Maoni 2 :

Ode alisema ...

Imenisaidia

Ode alisema ...

Nimeisoma yote, na imenisaidia sana. Mungu akubariki sana mjenzi