Jumanne, 8 Machi 2016

Kwanini Waislamu Humchukia Paulo Mtume?



     Paulo Mtume ni moja ya nguzo muhimu sana Katika Ukristo na ulimwengu kwa ujumla kuliko hata Muhamad,Waislam wanaamini kuwa kila jamii ina mtume wake na kuwa Muhamad ndilo jibu la Matumaini ya umma wa Kiarabu, na mataifa mengine, Lakini ilivyo ni kwamba Matumaini ya mtume anayefiti anayestahiki kwa ulimwengu Mzima yanajibika kibiblia kuwa Paulo mtume ndiye Jibu hilo na ndio maana waislamu wanamchukia, ni wazi kuwa kama jinsi ambavyo ni kufuru kumlinganisha Muhamad na Yesu kristo kwani Ni Mungu, lakini ni kumvunjia Kristo heshima kwa kumlinganisha Paulo na Muhamad.

 Paulo Mtume ni Mkuu Kuliko Muhamad mwanzilishi wa dini ya Kiisalamu

    Paulo ni Mtume wa Mataifa. Kama Waislam walikuwa wanaona kuna hitaji kwa kila taifa kuwa na Mtume wake ni Muhimu kwao kufahamu kuwa Mpango wa Mungu tangu mwanzo haukuwa kuwapendelea wayahudi tu, yeye tangu mwanzo alimkusudia Ibrahimu kuwa Baraka kwa jamaa zote za dunia (Mwanzo 12;1-3),Baraka hii ilitimizwa kupitia Yesu kristo ambaye alitolewa kwa kusudi lileliel la kiulimwengu (Yohana 3;16),Katika mpango huu mzima wa kuwafikia Mataifa yoote Masihi aliwaagiza wanafunzi wake kuihubiri injili kwa kila taifa (Mathayo 28;19) inashangaza sana kufikiri kuwa Manabii waliotumwa Pamoja na Ujio wa Kristo duniani uliihusu Israel tu au wayahudi tu na ndio maana hata ile siku ya Pentekoste Roho mtakatifu alipo washukia wanafunzi wa Yesu waliwezeshwa kuzungumza lugha mbalimbali ikiwemo kiarabu soma (Matendo 2;1-12).Hii maana yake ni kuwa Mungu alitaka kuufikia Ulimwengu mzima kupitia Taifa teule alilolitenga la Kiyahudi maana huko ndiko wokovu unakotokea(Yohana 4;22), na mwokozi wa ulimwengu ni mmoja tu (Yohana 4;39-42).

  Ni katika kusudi zima la kuufikia ulimwengu Mungu alimchagua Paulo mtume aifanye kazi hii (Matendo 9;1-15). Ni dhahiri kuwa hata Roho Mtakatifu alithibitisha kuwa amemuita Paulo kwa kazi hii maalum (Mdo 13;1-3).Jambo hili lilikuwa bayana hata kwa Paulo mwenyewe kuwa neema na utume alioitiwa ulikuwa maalum kwa mataifa (Warumi 1;5, Wagalatia 2;7-8,9-9).Mungu bado hata sasa aweza kutumia watu mbalimbali na wakawa ni viongozi Maarufu sana duniani toka jamii ya mataifa lakini woote watakuwa na kazi moja tu kumhubiri Yesu Kristo, Hivyo kama ilikuweko haja ya mtume kwa waarabu angeinuliwa na angemhubiri kristo na sivinginevyo,Kinyume chake basin a waafrika tutahitaji nabii wetu, Wahindi nao, wazungu, nao nk. Kilichokuwa kinahitajika ni mtume na sio injili Nyingnie  kwani yeye aliyeleta injili nyingine amelaaniwa!(Galatia 1;6-9).

Paulo alipewa mafunuo Makubwa sana kuliko Muhamad.
     Woote tunajua kuwa Paulo Mtume alipewa mafunuo makubwa sana kuliko aliyopewa muhamad,Injili aliyoihubiri si ya namna ya kibina damu kwani aliipokea na kufundishwa kwa ufunuo wa Kristo Yesu mwenyewe aliyemuita (Wagalatia 1;10-12),Paulo alinyakuliwa mpaka peponi na kufika mbingu ya tatu kwa ajili ya maono na mafunuo ya Bwana (yaani Yesu) soma (2Koritho12;1-7),Mungu alimtumia Paulo mtume kwa namna ya kupita kawaida Biblia inasema (Matendo 19;11) “Mungu akafanya kwa mikono ya Paulo miujiza ya kupita kawaida;” Neema ya Mungu iliyokuwa juu yake hailinganishwi kamwe na utume wa Muhammad kwanini waislamu wasione wivu zaidi ya yoote tunaweza kuseama mambo ya msingi yafuatayo kumhusu Paulo.
Paulo ni Mtetezi Mkuu wa Ukristo na Mafundisho yahusuyo kuhesabiwa haki kwa imani.Paulo alizungumza, kufundisha, Kufafanua na kutetea  mafundisho yahusuyo haki inayotokana na Imani mafundisho yanayooonekana kuwa Mwiba na tishio kwa waislamu ambao hufundisha kuwa haki inapatikana kwa matendo, Kwa waislamu matendo mema yanahesabiwa kuwa thawabu na yanampa mwislamu nafasi ya kuingia Paradiso, Hiki ambacho waislamu wanafundisha ni matendo ya sheria kuwa mtu anaokolewa kwa matendo, na bidii ya kibinadamu nakwa kufuata matendo ya sheria na Sikukuu zao,Paulo anafanyika mwiba wa mafundisho hayo na ndio maana wanamchukia.(Galatia 2;15-16,3;10 Kolosai 2;16-22).

Paulo alikuwa na bidii na kuusambaza Ukristo duniani.(Mdo 13;46-48).
     Paulo alifanikiwa kuipeleka injili nje ya mipaka ya Israel na mipaka ya iliyokuwa himaya ya Rumikutoka huko injili ilifika hata ulaya na hatimaye ulimwengu mzima wa wakati ule, Waislamu wanaona kuwa Paulo hakufanya sahihi alifanya makosa kwa kuipeleka injili nje ya mipaka ya Wayahudi, Ukristo kwa waislamu wanaamini kwamba uliwahusu wayahudi tu wanaamini ukristo ulikuja kwa ajili ya kuwakosoa wayahudi,kuwarekebisha na kuwaongoza wao, Kwa kuupeleka kwa Mataifa Paulo ameharibu ukristo halisi, na hivyo ameufanya Ukristo kuenea dunia nzima hili linawaudhi sana waislamu na ndio maana Humpinga.

    Wakolosai 1;3-6, Leo injili imezaa matunda na kusambaa ulimwengu mzima kutokana na kazi aliyoifanya Paulo Mtume Unadhani shetani atampenda? Sisi kama wasomi wa Biblia tunakubaliana kuwa Paulo anamchango mkubwa sana usiopingika katika kusambaza nuru ulimwenguni hivyo kumchikia yeye ni kuichukia nuru, aliisambaza injili kwa mafanikio kwa amani wala hakutumia upanga kama Muhamad.Paulo mtume alikuwa na neema kuu sana ambayo Muhamad hawezi kuifikia hata leo.

Hakuna maoni: