Jumamosi, 5 Machi 2016

Baraka za Kweli !



Jambo linguine ambalo linasababisha watu kuingia katika kongwa au nira katika mafundisho ya Ukristo ni mkazo wa Baraka za mwilini kuliko Baraka za kiroho, Mikazo mingi ya wahubiri wengi wa leo na wanaoshuhudia hukazia sana au kupita kiasi kuhusu baraka za kimwili kuliko za kiroho, hali  hii utaisikia katika maeneo mengi ikiwemo wanapofundisha maswala ya utoaji na pia wakati waksrito wengi wanaposimama kutoa ushuhuda wa mafanikio kadhaa  utaona mkazo mkubwa ni mafanikio ya kimwili zaidi na hayo ndio huitwa Baraka dhana hii huacha madhara kwani kwa upande wa pili wa mtu asiyekuwa na mafanikio anaweza kufkiri kuwa labda yeye Mungu hajambariki katika eneo hili nitafanya uchambuzi wa Neno Baraka kibiblia lina maana gani?


     Neno Baraka katika Biblia ya Kiebrania hutumika kama Neno “Barak” ambalo maana yake ni Neno la Kukufanikisha, au kunenwa vema au kusifiwa au kuitwa heri au kupongezwa au kupewa nguvu ya kubadilika kitabia na kimwenendo na kufanikiwa ni tofauti na neno la kiingereza “Blessing” ambalo maana yake ni msaada unaoaminika kutoka kwa Mungu au tendo la kidini la kumuweka mtu wakfu au maombi ya kushukuru wakati wa chakula pia ni tofauti na neno la kiingereza “Prosperity”ambalo maana yake ni mafanikio ya kifedha na uchumi, au kufurahia utajiri na mafanikio na hali nzuri, kimsingi maneno hayo yote ya kiingereza hayatoshi kuweza kuelezea neno “Barak” kwani msini wa msaada utokao kwa Mungu Blessing na mafanikio ya kifedha na uchumi haviwezi kulinganishwa na neno barak kwa Kiswahili Baraka kimsingi mafanikio ya kifedha na kiuchumi kila mtu aliyeko duniani anaweza kuyapata awe mkristo au mpagani mtu yeyote aweza kupata mafanikio lakini si kila mtu anaweza kupokea Baraka

     Kimsingi Biblia inapozungumzia kuhusu Baraka haizungumziii kabisa kuhusu wingi wa mali na vitu tulivyo navyo kama Baraka tafasiri yake si wingi wa vitu na mafanikio ya kiuchumi nchi nyingi za kiarabu zinautajiri mkubwa sana wa mafuta na maendeleo makubwa sana ya kiuchumi ziko nchi nyingi za ulaya zenye uchumi mkubwa sana, nchi kama Saud Arabia ni matajiri wakubwa sana lakini wengi hawamchi Mungu na wanaishi maisha ya anasa Haya ni mafanikio Prosperity lakini sio Barak sasa nije pale unapopasubiria bila shaka sasa unataka kujua Baraka hasa ni nini? Ndugu yangu kama nilivyokwisha kugusia “Baraka maana yake ni Neno la kukufanikisha” Baraka sio wingi wa vitu na mali wote tunafahamu kuwa Ibrahimu baba yetu wa imani alikuwa na mali nyingi sana  na alikuwa na fedha na mifugo na fedha na dhahabu Mwanzo 13;2 na wote tunafahamu kuwa alimwachia mwanae Isaka utajiri wote Mwanzo 25;5 kwa hiyo Esau na Yakobo walipozaliwa Baba yao alikuwa tajiri sana na kwa sababu hiyo nyumbani kwao kulikuwa na kila kitu hata ingawa Esau alipenda kuwinda wanyama wa mwituni na ilikuwa desturi kwa wazazi kuwaachia urithi watoto wao ni wazi kuwa Esau na Yakobo pia wangelikuwa matajiri waliofanikiwa sana lakini umewahi kujiuliza ni kwanini Esau na Yakobo walitaka sana kugombea mbaraka wa Isaka baba yao? Ugomvi wao haukuwa kuhusu mali bali walitaka mbaraka!,Mwanzo 27;18-38 Lugha ya kibiblia bado inaonyesha kuwa Baraka sio mafanikio kwani wote tunafahamu kuwa Yakobo alikimbia bila kitu chochote ili asiuawe na Esau alikwenda kuishi ujombani na kuoa huko kwa sababu alikuwa amebarikiwa huko pia alifanikiwa sana na kurudi akiwa na mali nyingi ya mifugo mingi Mwanzo 32;5 lakini alipokuja malaika usiku  ule akashindana naye mieleka malaika Yule alisema niache niende maana kunapambazuka yakobo alimng’ang’ania akisema sikuachi usiponibariki na hatimaye malaika wa Bwana akambariki huko Je umeshawahi kujiuliza Baraka ni nini? Yakobo hapa ana mali nyingi lakini anahitaji kubarikiwa kubarikiwa ni Nini? Kubarikiwa ni kupewa Neno la Kukufanikisha, au kunenwa vema au kusifiwa au kuitwa heri au kupongezwa au kupewa nguvu ya kubadilika kitabia na kimwenendo kwani baada ya Malaika kumbariki Yakobo pia alimbadili kitabia na Yakobo akawa mtu mnyenyekevu sana. Ni muhimu kufahamu kuwa mtu anapookolewa maana yake amebarikiwa kwa Baraka zote za rohoni Waefeso 1;3-7. Ndani ya Baraka ndiko kuna mafanikio ya kitabia, kiulinzi, Hata tunapohubiri kuhusu utoaji wa zaka na dhabihu kama inavyosema Biblia katika Malaki 3;7-12 utoaji huo huambatana na Baraka za kiroho ni wazi kabisa kuwa Ibrahimu alipotoa zaka kwa kuhani mkuu Melkizedeki alichokifanya kuhani huyu ni Kumbariki Mwanzo 14;18-20 na mara baada ya Ibrahimu kubarikiwa na Melkizedeki kilichotokea ni kuwa sura nzima ya 15 kitabu cha mwanzo Mungu alijifunua kwa Ibrahimu kupitia neno lake baada ya ukimya wa muda Mwanzo 15;1,4,13,18. Neno la Mungu ndio chakula kilichoahidiwa katika Malaki ndicho kinacholeta uponyaji na nguvu ya mafanikio na kazi ya huduma Yoshua 1;7-8,Waebrania 5;11-14 na Yohana 4;31-34 Mungu anamkemea yeye alaye ni wazi kuwa anazungumzia ulinzi Ayubu 1;7-10 kama alivyomwambia Ibrahimu kuwa anakuwa ngao kwake Mwanzo 15;1 Popote katika Biblia unaposoma kuwa mtu amebarikiwa utaanza kuona sifa za kiroho na ndipo wanapoonyesha mafanikio ya kimwili Ayubu 1;1-3, Kimsingi Yesu alipokuja katika mafundisho yake hakuwahi kumsifia mtu mwenye mali kama kipimo cha mtu aliyebarikiwa kimsingi wayahudi pia walipotea katika mtazamo ambao wakristo wengi wamepotelea wa kufikiri kuwa mafanikio ya kimwili kuwa ni Baraka za Mungu Yesu alionyesha kuwa mtu aliyebarikiwa ni mwenye sifa  zinazotajwa katika Mathayo 5;2-12 sawa na Malaki ambaye anasema Utaitwa heri na nchi ya kupendeza

Kongwa la Baraka za kimwili limewakumba watu wengi sana leo wachungaji na washirika wengi leo wanashindana katika ununuzi wa vitu kama magari na mafanikio ya kielimu, ujenzi wa nyumba na fanicha kisha wanasimama kushuhudia kuwa Mungu amewabariki ni jambo lisilo ingia akilini kwamba mtu ana kigari kimoja Mark II anasimama mimbarini kusema Mungu amembariki je anawezaje kusema mtu amabaye anamiliki mabasi, mashule, mashamba makubwa lakini hamjui Mungu Je yeye atasema amebarikiwa? Hapana hayo ni mafanikio na sio Baraka, kongwa la Baraka limewafanya wengi kuwa washamba wa mafanikio na kuwafanya wengine kuingia katika mitego ya ujanja ujanja ili wapate mali na kuja kushuhudia kuwa eti Mungu amewabariki Kristo alionyesha mfano wa Tajiri na Lazaro aliyekuwa masikini ambapo Tajiri alikwenda motoni na Lazaro aliyekuwa masikini alikwenda peponi ni wazi kuwa mafanikio ya kimwili so kipimo cha Baraka ninazozizungumza hapa nawafahamu watu ambao wamenunua magari kwa fedha za kanisa au kwa sadaka za watu masikini makanisani na wameyaandika majina yao na mitaani wanamsingizia Yesu kuwa amewabariki! Wakati huu ni binafsi na kujilimbikizia mali kwa sababu ya ubinafsi ni kweli wako waliopewa magari kwa sababu ya injili lakini wengi wamechomekea kuanzia mawazo ya kununuliwa magari na kujengewa majumba ili eti wadai kuwa Mungu amewabariki mtu aliyebarikiwa huanza kuwa na sifa za kiroho  wanajawa na rehema, wanasamehe, hawahukumu wengine, wanawajali wenye uhitaji, hawadhulumu mtu, ni wanyenyekevu, wanaheshimu watu, mafundisho yoyote ya injili inayosisitiza watu kuwa na mali lakini tabia zikawa haziendani sawa na injili hayo hayatokani na bwana wala sio mlango wa wokovu, leo hii wako watu ambao wamefikia hatua kuwa hawawezi kuombea watu mpaka wametoa fedha kwanza na zaidi sana Fedha hizo hazitokani na hiyari ya watu hao ila ni kwa sababu wana shida na uhitaji au kupitia njia za kijanja za wahubiri ambao wameanguka kupitia kupenda fedha na kudhulumu wau kupitia kuumia isivyo halali neno la Mungu, Msomaji wangu kama unafuatilia mahubiri mengi leo utaona kuwa mahubiri mengi leo yanalenga mafankio na utoaji huu ndo mkazo mkubwa sana wa wahubiri kuliko maswala ya Rehema na adili. Ni muimu kufahamu kuwa kuna ubadhirifu mkubwa sana wa sadaka leo makanisani na viwango vikubwa vya kujilimbikizia posho visivyo na uwiano kati ya kanisa na kanisa na hakuna mikakati mikubwa ya kiiinjili leo na kuwafikia wasiofikiwa au kuyatia moyo makanisa madogo na watumishi wasio na kipato aidha ukaguzi wa kimahesabu makanisani na udhibiti wa matumizi makubwa ya viongozi wa kikanisa umenyamaziwa huku tukifikiri kuwa watu hao wako sawa kimaadili kumbe wameharibika aidha nchi yetu inaharibika pia kutokana na kanisa kuwakumbatia mafisadi na kuwatakasa katika madhabahu zao hii ni kwa sababu Fisadi hawezi kumtoa fisadi ni lazima kanisa lijisafishe kwanza ndipo litakapokuwa na uwezo wa kuikemea serikali

Maoni 1 :

TRISHA NELSON alisema ...

HERPES/HIV is a serious and recurring disease which can't be cure through drugs or injections by an American doctors but the best way to deal with Herpes is by taking natural herbs medicine for it,  I have red about DR JAMES the great herbalist doctor who cured me from herpes  with his powerful herbal medicine.  I contacted him to know how he can help me and he told me never to worry that he will help me with the natural herbs!After 2 days of contacting him, he told me that the cure has been ready and he sent it to me via UPS SPEED POST and it got to me after 4 days i used the medicine as he instructed me (MORNING and EVENING) and i was cured!it's really like a dream but I am so happy!   for the people suffering from herpes and other diseases like  Rectum  effects, intestine damage, bowel obstruction, Ovarian disease,  Cancer, hypothyroidism, Herpes, COPD, HIV, Arthritis, Lyme disease,Hpv, Infections,Liver Disease, Autoimmune Diseases, Parkinson's disease,Lupus,Nephrology and Hypertension, Neurology, Obstetrics, Gynecology, and Women's Health, Oncology, Pediatrics, Pulmonary, ACUTE MYELOFIBROSIS, ALZHEIMER's symptoms, BREAST CANCER, DIABETES, HAIR LOSS AND HAIR TREATMENT, KIDNEY DISEASES, LEUKEMIA, MYELOID LEUKEMIA, STEM CELL TREATMENT 
 should contact him for his herbal medicine because i am a living testimony and i was cured of herpes and his medicine is legit.  I sent him what he requested and he sent me his medicine which  I took for 2 good weeks and today I am out here with a negative result. When I went for the test I was so happy after taking his herbal medication  I paid homage to his country to celebrate with him on his African festival which he told me it usually happens every year.  you can reach him through  VIA E-mail   drjamesherbalmix@gmail.com or whatsapp number:+2348152855846