Jumamosi, 5 Machi 2016

Huitaji kutubu kupitia kwa Wanadamu !



Hatuhitaji kutubu kwa wanadamu.
Baada ya wokovu ni muhimu kufahamu kila mtu aliyeokoka anakuwa ameungwa kwenye uhusiano wa moja kwa moja na Mungu kupitia kazi aliyoifanya Yesu wewe sasa umekuwa mwana wa Mungu, Mungu amekuwa baba kwako huu ndio uhusiano tulio nao na Baba yetu, wote tunajua uhusiano wa kawaida tulio nao na wazazi wetu katika hali ya kawaida huwa unafanya nini uhusiano na baba yako au mama yako unapokuwa umeharibika? Kristo anatufundisha wazi jinsi ya kurejesha uhusiano na baba yetu wa mbinguni pale kunapokuwa na tatizo katika mfano ule wa mwana mpotevu Yesu alionyesha wazi jinsi toba ya kweli kwa mwana huyo aliyetumia vibaya urithi na mal alizopewa na baba yake kwa kutaka kujitawala ni wazi kuwa alipozingatia moyoni mwaka kurudi kwa baba yake kamwe hakuwaza kutafuta mpatanishi kati yake na baba aliamu kurudi moja kwa moja kwa baba Luka 15; 17-18 “alipozingatia moyoni mwake alisema Ni watumishi wangapi wa baba yangu wanakula na kusaza na mimi hapa ninakufa kwa njaa Nitaondoka nitakwenda kwa baba yangu na  Kumwambia baba nimekosa juu ya mbingu na mbele yako” ni wazi kabisa fundisho kuhusu toba ndani ya Agano jipya kwa mtu ambaye Mungu ni baba yake halihitaji kupitia kwa mwanadamu hata kidogo, tunaweza kuwaomba radhi au msamaha wanadamu wenzetu tunapokuwa tumewakosea lakini linapokuja swala la kumosea Mungu dawa sio mtu dawa ni kumuedea Mungu mwenyewe hakuna mwanadamu mwenye haki ya kutupatanisha na Mungu nje ya Mungu mwenyewe na sisi tuliomkosea Biblia inatuonyesha wazi kuwa Kristo ndiye kuhani wetu mkuu huyu ni Mungu na tunapomuendea Yeye hutupatanisha na Mungu Waebrania 4;14-16  “……Basi na tukikaribie kiti cha neema kwa ujasiri ili tupewe Rehema na kupata neema ya kutusaidia wakati wa mahitaji yetu” Kwa nini mitume wa bwana hawakuchukua nafasi ya makuhani badala yake walielekeza watu kuwa mpatanishi kati ya Mungu na wanadamu ni mmoja tu Kristo Yesu 1Timotheo 2;5 Biblia inasema hivi  Kwa sababu Mungu ni mmoja na mapatanishi kati ya Mungu na wanadamu ni mmoja , Mwanadamu Kristo Yesu” wahubiri wengi sana wamejitukuza aidha kwa kujua au kwa kutokujua na wamechukua nafasi ya Kristo msomaji wangu hata na mimi nilikuwa hivyo nilifikiri kuwa toba ya kweli lazima ipitie kwa mtumishi wa Mungu ili akuombee neema pia kuna wakati nilifikiri unapotubu dhambi zako na kuzikiri wazi kwa wanadamu unapokea msaaada kama ule anaoutoa Yesu yaani msamaha  lakini badala yake nilihukumiwa vibaya, wokovu umeingiliwa leo kuna watu ambao wanataka ukiri makosa yako kwao wao wamekuwa kama ndio Kristo wanahubiri hukumu na kuwafunga washirika  na watumishi katika vifungo vya hukumu wakichukua nafasi ya Mungu watu hawapaswi kuungama kwa mchungaji au kuhani mwanadamu au padre, hatuja wakosea wao tumemkosea Mungu peke yake Mtumishi wa Mungu Daudi ingawa alikuwa amefanya dhambi mbaya zenye kuumiza watu wengine hatuoni kamwe akielekeza toba yake kwa wanadamu Badala yake alimuelekea Yule mwenye haki  na mwenye rehema  angalia yu asema hivi katika Zaburi 51;1-4 “Ee Mungu unirehemu sawasawa na na fadhili zako kiasi cha wingi wa rehema zako uyafute makosa yangu unioshe kabisa na uovu wangu unitakase dhambi zangu maana nimejua mimi makosa yangu na dhambi yangu mbele yangu daima Nimekutenda dhambi, Wewe peke yako na kufanya maovu mbele za macho yako wewe ujulikane kuwa na haki unenapo na kuwa safi  utoapo hukumu” unaona Ni Mungu pekee anayehitaji kupelekewa toba zetu,yeye peke yake ndiye mwenye haki hatupaswi kufungwa na viongozi wa dini ambao ni vigumu kuwafikia kwa sababu a ukubwa walio nao leo hii Yesu ni rahisi kufikiwa na kuombwa radhi na kupokea msamaha tele kuliko kwa viongozi Fulani wa kidini ambao wanajifikiri kuwa ni miungu watu msomaji wangu mwendee Yesu kwa imani kwa kuvunjika sirini tubu uovu wako na dhambi zako atakusamehe kabisa huhitaji kumwambia Yeyote wao dhambi zao wanazitubia wapi? Ni lazima ujiulize na kujua kuwa wao pia ni watu na sio wakamilifu wengine wanaiba sadaka za kanisa wamenunua gari na majumba kwa sadaka za watu masikini kwa manufaa yao na kwa majina yao na wakisimama katika madhabahu utafikiri kuwa wao ndio miungu unapaswa sasa kuimama na neno la Mungu na kuliamini acha kwenda kujianika kwa wanadamu, Mungu angekuonyesha maovu yao wanayoyafanya sirini je ungewapelekea dhambi zako? Wao pia ni watu Makuhan wakati wa agano la kale walitakiwa pia kutoa dhabihu kwaajili yao binafsi na kwaajili ya watu wengine pia maana nao walikuwa wenye dhambi.


Toba ya kweli kamwe haipaswi kupitia kwa wanadamu wenye damu na nyama kama wewe atoba ya kweli huelekea kwa Mungu aliye hai peke yake

Watu wa Mungu wameteseka kwa Muda mrefu na kuishi chini ya hofu kwa kugopa kuhumiwa na wachungaji mapolisi na wakati mwingne wamekaa na dhambi kwa muda mrefu bila kuzitbia wakifikiri kuwa hawawezi kusamehewa mpaka kwa neno la Mchungaji au maombi yake Hapana ! hilo ni kongwa wamekufungia unaweza ukakosa ufalme wa Mungu Yesu u Karibu na wewe kuliko mchungaji wako na kwa kweli yeye ni mwaminifu ukiziungama dhambi zako atakusamee na kuondoa udhalimu wote changamka acha kujikunyata kwa mafundisho yasiyokupa furaha Dhambi ikitendwa kwa Mungu dawa yake ni Mungu na sio Binadamu swali la Eli Yule kuhani linajibika kirahisi leo kuliko wakati wao kabla Kristo hajaja Eli aliuliza hivi 1Samuel 2;25”Mtu mmoja akimkosa mwenzake Mungu atamuhukumu lakini mtu aklimkosa Bwana ni nani atakayemtetea?Ngoja nimjibu Eli jibu ni rahisi sana Yesu atamtetea mtu huyo kwa nini yeye ndiye kipatanisho kwa dhambi zetu,Mungu hawaweka Mitume,Manabii, wainjilisti, wachungaji na waalimu kwa kusudi la kusamehe dhambi au kusikiliza dhambi za watu na kutoa hukumu hiyo sio kazi yao wala sio kazi ya malaika Kazi ya watumishi hao ni kuujenga mwili wa Kristo yaani kanisa katika kuujenga wanaweza kuombea washirika kukua kiroho n.k lakini kamwe hawawezi kufanya kazi ya kutupatanisa na Mungu ndugu kinachohitajika ni ujasiri na kujisamehe ujasiri huu utokane na kulijua neno la Mungu na kufahamu kle unachopaswa kukifanya Waebrania 10;19-22 “Basi ndugu kwa kuwa tuna ujasiri wa kupaingia patakatifu kwa damu ya Yesu njia ile aliyotuanzia iliyo mpya iliyo hai ipitayo katika pazia yaani mwili wake  na kuwa na kuhani mku juu ya nyumba ya Mung na tukaribie wenye moyo wa kweli kwa utimilifu wa imani hali tumenyunyiziwa mioyo  tuache dhamiri mbaya tumeoshwa miili kwa maji safi” Msaada wa Mungu unapatikana kwa imani isiyo na shaka  ni imani ndiyo inayotuwezesha kumpendeza Mungu ndugu yangu amini katika wema wa Mungu , mjie kpitia Kristo kwa mo wa kweli  hu ndio unyoofu utapata rehema na neema msaada wako utatoka wapi utatoka katika Bwana wa majeshi huko utasamehewa ndugu yangu toba ni Ibada na hakuna ibada inayopelekwa kwa mwanadamu ikiwa haifai kuomba Mariam aliyemzaa Yesu kutuombea sisi wakosefu ni wazi kuwa haifai kupeleka dhambi zako kwa mwadamu awaye yote eti ili akuombee toba kwa Mungu, kuna faida gani kupeleka toba kwa Mungu kwake yeye anatujua umbo letu na kukumbuka ya kuwa sisi tu mavumbi Yeye ndiye aliyetuumba na anaoufahamu kamili kutuhusu anasoma mawazo yetu kabla hatujawaza Zaburi 139 1-12 na kuendelea inaonyesha jinsi Mungu anavotufahamu wachungaji wetu hawatufahamu na hakuna nguvu ya kuwaeleza kwa ukamilifu dhambi tuzifanyazo kwani wao nao hawatuambii zao basi tumwambie Mungu kwake Mungu tunaweza kumueleza kwa uwazi na upana na uhuru na kumuomba atusaidie na baada ya hapo atatusamehe wala hatutasikia mitaani dhambi zetu zikianikwa hata baada ya kuwa tumemueleza Mungu uovu wetu wote, lakini kama unataka kuaibika na kufedheheka duniani wapelekee wanadamu maovu yako utakoma! mimi sijajua mpaka sasa ni andiko gani wanalisimamia kutaka kusikia dhambi za watu au toba zipitie kwao hili ni kongwa Bwana akupe neema na kukuponya katika maumivu yaliyokupata kwa sababu Yoyote ile inayotokana na mafundisho yasiyo ya kibiblia na ambayo ni mapokeo ndio maana nilikuambia mapema kitabu hiki hakiko mkononi mwako kwa bahati tu kwani zawadi kutoka kwa Mungu kwa ajili yako Nanyi mtaifahamu kweli na hiyo kweli itawaweka Huru!

Hakuna maoni: