Jumanne, 8 Machi 2016

Jinsi Quran Ilivyopatikana



      Kama woote tunavyofahamu kuwa Duniani ziko dini nyingi sana na zote zina vitabu vyake vitakatifu vinavyodaiwa kuwa ni neno la Mungu na kuwa ndio mamlaka ya mwisho ya dini hizo wahindu wana kitabu chao kiitwacho (Vedas),na sikhiism(Adigranth),Confusian(Analets),Shinto (Nihong),Na Budha (Dharma),Judaism(Torati),Islam(quran) na sisi wakristo Biblia agano jipya na Kale,na Kila mmoja anaamini kuwa ni neno la Mungu katika eneo hili tutakuwa tukijiuliza swali je Quran ni neno lu Mungu na tutafanya upembuzi yakinifu kwa kuzingatia vipengele vine vifuatavyo;-

·         Jinsi quran ilivyopatikana na muundo wake
·         Jinsi quran inavyopotosha kweli za kibiblia
·         Jinsi quran inavyomuelezea Yesu masihi
·         Jinsi quran inavyojikanganya yenyewe

Jinsi quran ilivyopatikana na muundo wake.
     Kabla ya kuchambua jinsi quran ilivyopatikana ni muhimu kujikumbusha kwamba quran ni nini? Quran ndio kitabu kitakatifu na mamlaka ya mwisho kwa waislamu,qurani ni neno la kiarabu cha kikuresh lanye maana ya “recitation” yaani yaliyo kaririwa,quran ilitokana na aya alizokuwa akizitoa Muhamad kwa madai kuwa zilitoka kwa Allah kupitia malaika Jibril,tangu alipomkaba na kumuamuru kuikariri kwa Kumwambia “Iqraa-bism-rabik” yaani soma na ukariri,Muhamad aliendelea aliendelea kutoa aya hizo kwa miaka 23, Waislamu huamini kuwa aya hizo zilitolewa kipandekipande toka katika kitabu halisi kilichoko mbinaguni,Muhamadi alitoa aya hizo kwa kuzisema kwa Maswahaba wake ambao walizikariri kichwani (Hawakuwa wanajua kusoma wala kuandika) baada ya kifo chake Muhamad aya hizo zilikusanywa toka kwa maswahaba mbalimbali na kuwa kitabu kimoja kiitwacho quran leo,Maswala mengine kuhusu Muhamad na maisha yake yamekusanywa katika vitabu vya hadithi ambavyo pia hutumika katika kutafasiri quran 

Muhamad alipokea aya hizo za Quran kwa namna zifuatazo (aya au wahyi)
      Kwa mujibu wa vyanzo vya kiislamu Muhamad alipokuwa anapokea aya hizo alikuwa anavamiwa na nguvu za kigeni zilizomuathiri sana na kumpa shida sana kama inavyokua kwa mgonjwa wa kifafa, aliunguruma kama mtoto wa ngamia huku akitoa povu mdomoni,Alitisha na kutia huruma hali hizi zilikuwa zikimpata kila alipokuwa anataka kutoa aya hizo,wanasema wakati mwingine alikuwa anaanza kusikia mlio kama kundikubwa la nyuki likimjia vinaeleza vyazo hivyo vya kiislamu! Jambo lililopelekea watu waliomuona kumpa majina yafuatayo

Ø  Walimuita aliyepagawa au mwendawazimu (Surat as-saafat 37:35-36,dukhan 44:13-14,at-tur 52:29,qalam 68:1-2,Takwyr 81:22).
Ø  Walimuita mchawi (Yunus 10;2,surat sad 38;4,az-Zumar 39:41)
Ø  Wengine walifikiri amerogwa (Ban Israel 17:47-48,fur-qan 25:4-5,8)
Ø  Aliitwa pia mpiga ramli au mtunga Mashairi (Tur 52;29, haqqah 39;41)

  Muhamad alidai pia kuletewa aya hizo na malaika Jibril ambae kwa mujibu wa quran ndie malaika mkuu, wakati mwingine alidai kusikia sauti ikimpa aya, na wakati mwingine alitoa aya hizo moyoni mwake au alioteshwa ndoto au kupewa ufunuo (Surat nasm 53:1-11)
  Muhamad alihubiri quran na mafundisho yake na kupata matokeo hafifu sana hali hii ilimkatisha tama hususani pale makka ambapo watu walimpinga sana akiwemo baba yake mdogo Abu Lahib na hivyo alimlaani na kumtaja kama mtu wa motoni kwa muongozo wa Allah soma kitabu maisha ya nabii Muhamad uk 19 kifungu cha mwisho n auk 20 kifungu cha kwanza na cha pili.Baada ya upinzani mkali Muhamad ili apatane na  watu wa makka alibadilisha aya  na kuleta aya inayoitambua miungu ya ndugu zake aya hiyo husomeka hivi “…….Je mumewaona lat.uzza na manta? Hawa watatu maombi yao (wanayo waombea) ni ya kutumainiwa (Surat sad 38;5-7).Miungu hiyo ni ile iliyoabudiwa na wapagani wa pale Makka na kufanyiwa hijja,alipoulizwa kuhusu kigeugeu chake cha kubadilisha  aya mara kwa mara alidai kuwa Zilitoka kwa shetani hivyo jibrili aliiondoa sehemu ya pili ya aya hiyo hivyo sasa inasomeka hivi(Surat nasm 53:19-20) Hivyo ndani ya quran ziko aya nyingi sana zinazopingana na nyingine zimebadilishwa na watu kama tutakavyoona mbeleni.
     Mungu wa Muhamad mwenyewe alikuwa na kigeugeu kwa kumletea aya na kuzibadili baadae mfano (al-baqara 2;106,an- nahil 16;101) hivyo Muhamad alibadili aya za quran katika maeneo mengi na kubadili nyingine,aya zilizoondolewa  ziliitwa “Mansukh” na zile zilizokuja kubadili nyingine ziliitwa “Nasikh” Hizi ni aya zilizo karabatiwa “the law of abrogation” bahati mbaya aya zoote hizi zimo katika quran na zilizobadilishwa zinakadiriwa kufikia kati ya “5-500” kwa mujibu wa mwanazuoni wa kiislamu Jalalud-din baadhi ya aya hizi ni pamoja na

Ø  ……Asilazimishwe mtu kuingia dini (Baqara 2;256)ilibatilishwa kwa (Surat as saf 61:10-12)
Ø  …....Muelekeo wa wakati wa kusali (Baqara 2:142) ilibatilishwa kwa(Baqara 2;147)
Ø  ……Amri ya kuomba usiku (al Muzzamil 73;2) ilibatilishwa kwa (al Muzzamil 73:20)
Ø  …..Adhabu ya wazinzi (an Nisaa 4;15-16) ilibatilishwa kwa (an-Nur 24:2)

Hizi ni baadhi tu ya aya zinazo jikanganya zenyewe Muda usingeweza kutosha kuandika na nyingine zinazopingana zenyewe kwa zenyewe.

  Muundo wa quran.
     Qurani imeundwa na baadhi ya mila na tamaduni mbalimbali za kiarabu na mchanganyiko wa dini mbalimbali,na mambo mengine yametoka katika vitabu vya tamaduni za kiyahudi za kiyahudi kama Talmud na Mishna,pia kuna tamaduni za kiajemi hii ni kwa sababu Muhamad alikuwa na rafiki wa kiajemi aliyeitwa Salman,pia kuna vihistoria toka kwenye Biblia ingawa vimepinda huenda ni kwa sababu ya Makosa ya kukariri au kwa sbabu ya kutokujua kusoma kwa Muhamad na maswahaba wake au kazi ya shetani kupotosha ukweli,aidha kuna tamaduni nyingi za kipagani hasa za pale arabuni makka na mawazo ya Muhamad mwenyewe.

Jinsi quran inavyopotosha kweli za kibiblia .
     Quran ni kitabu kilichojaa hadithi za kudandiadandia toka kwenye biblia  na ambazo nyingi haziko sahihi na zinapingana  na kupotosha kweli zilizomo katika biblia,Hadithi nyingi katika qurani ni tofauti na zile zilizomo katika biblia, Biblia ina masimulizi yanayojitosheleza yenye mwanzo mpaka mwisho,ni rahisi kujua kipi ni kipi na kipi utakipata wapi,lakini sivyo ilivyo katika quran hadithi zake ni za kudandiadandia hiki au kile wakati mwingine bila kujua mwanzo wala mwisho au kupata habari kamili labda ndio maana Muhamad alirejea mara kwa mara kuwataka waislamu kutuuliza sisi tuliopewa vitabu kabla yao hapa chini Tutachambua mambo ambayo qurani imepotosha au kudanganya tofauti na biblia;-
Ø  Q. Nuhu alikuwa na mtoto mmoja aliyekufa kwa gharika(hud 11;40-45).
Ø  B. Nuhu alipata neema machoni pa bwana yeye na uzao wake yaani watoto wake woote watatu (Mwanzo sura ya 6-7).
Ø  Q. Baba wa Ibrahimu ni azar (al anam 6:74)
Ø  B.  Baba wa Ibrahimu ni Tera (Mwanzo11;31)
Ø  Q. Musa aliokotwa na mke wa Farao (ak qasas 28;9).
Ø  B.  Musa aliokotwa na binti wa Farao (kutoka 2;5-10).
Ø  Q. Farao alimwambia Haman ajenge mnara wa Babel (al qasas28:38)
Ø  B. Mnara wa Babel ulijengwa na Nimrod (Mwanzo 10:32,11:4) pia habari hizi Quran imezungumza uongo kwani kuna tofauti Farao aliishi miaka 800 baada ya Mnara wa babel na Haman aliishi miaka 900 baada ya Farao hivyo kuna tofauti ya miaka 1700 tangu mnara wa babel na kuishi kwa Haman.
Ø  Q. Inafundisha kuwa mariam mamayake Yesu ni dada wa Haruni mtoto wa Imran (surat Maryam 19;17-28).
Ø  B. Huu ni uongo,Je hii ina maana Musa ni mjomba wa Yesu masihi kama Mariam ni dada wa Haruni kakaye na Musa? Naona hapa Muhamad na Allah wali Comfuse yaani walichanganya mada, Habari za Mariam mama wa Yesu na habari za Mariam (Miriam) dada wa Haruni na Musa zina tofauti ya miaka kama 1400 hivi k.k.
Ø  Q. Yesu alizaliwa chini ya mtende (Maryam 19:23)
Ø  B. Yesu alizaliwa katika hori ya Ngo’mbe (Luka 2;8-18)
Ø  Q. Zekaria alikuwa bubu siku tatu (Maryam 19:10-11).
Ø  B.  Zekaria alikuwa bubu mpaka alipozaliwa mtoto (Luka 1;8-22,57-64).
Ø  Q. Roho mtakatifu ni malaika Jibril (al baqara 2;87).
Ø  B.  Roho mtakatifu ni Mungu ni tofauti na malaika (Luka 1:26-35, Matendo 5:3-4).
Ø  Q.  Ishmael ndiye aliyetolewa sadaka na Ibrahimu ( as saafat 37:99-111)
Ø  B.   Isaka ndiye aliyetolewa sadaka na Ibrahimu (mwanzo 22:1-19).
Q……Inawakilisha Quran.
B……Inawakilisha Biblia.
     Yako mambo mengi sana ambayo quran inapingana na biblia ambalo ndio neno la Mungu,ndio maana tunaona kuna dosari nyingi katika quran zinazotuthibitishia kuwa si kitabu cha kuaminika sana kwani kilikuja baadae sana kuliko Biblia ambayo ni ya zamani zaidi lakini imetunza kweli kwa usahihi 

Jinsi quran inavyo Muelezea Yesu kristo.-
     Qurani na waislamu huwa wanapinga kuwa Yesu si Mungu huku quran yenyewe inamuelezea Kristo katika viwango vya juu na vya kipekee kuliko vya nabii yeyote na vya kipekee kuliko hata Muhamad, namna quran inavyomuelezea Kristo inamaanisha wazi kabisa kuwa Yesu ni Bwana.
  • Yesu alikuwa ni Muujiza kwa ulimwengu (al-Nabbiya 21;91)
  • Alizaliwa na Bikira (surat Maryam 19;20-21) kukubali hilo ni sawa na Kukubali kuwa biblia inasema kweli (luka 1;28-35,Isaya 7;14,9:6).
  • Alifanywa Ishara (muujiza waziwazi) surat az-zukhuf 43:63) hii ni sawa na kusema alifanywa ishara ili watu wamuamini yeye (Yohana 20;30-31,5;36)
  • Alikuwa mtakatifu hakuwa na dhambi (Maryam 19;21,21;19) sifa ya utakatifu ni ya Mungu peke yake.
  • Ni ishara kwa wanadamu woote(surat Maryam 19;21 al anbiyaa 21;19)Hivyo Yesu ni muujiza kwa watu woote ili wapate kumuamini   ( Yohana 6;25-35)
  • Qurani inamkiri Yesu kuwa ni Masihi (Surat an Nisaa 4;171-172),mtu yeyote anaekubali kuwa Yesu ni masihi maana yake amekubali kuwa Yesu ndie ufunuo wa mwisho kabisa wa mambo yote na kuwa ndie ambae watu walikuwa wakimgojea (Yohana 4;15-26).
  • Amejazwa roho mtakatifu (al Baqara 2;87) kwa kawaida waislamu hudai kuwa roho ni jibril (Luka 1;28-35)Roho ni tofauti na jibril lazima waislamu wajue kuwa Roho mtakatifu ni Mungu.(Mdo 5;3-7)
  • Alipaa Mbingini (surat an Nisaa 4;158)
  • Alilisha watu mikate (al Maida 5;112-115) kukubali Ishara hii ni kukubali kuwa Yesu ni nabii yule ajae ulimwenguni aliye tabiriwa na Musa (Yohana 6;1-14)
  • Ni alama ya kiama (Ishara) (al Zukhuf 43;61) maana yake mpaka yeye aje ndipo mwisho utakapokuja,yeye ndiye atakayehukumu na ndiye atakayefufua wafu soma ufafanuzi wa ayahii,atawafufua wafu akiwamo Muhamad( Yohana 5;22-23) soma pia injili ya barnaba uk 11.
Quran na aya za shetani.

Kama tulivyoona hapo juu kuhusu kuweko kwa kigeugeu kati ya mungu wa muhamad  ambaye alimletea aya  na kasha kuzibadili baadaye  Al-Baqara 2; 106 na an nahil 16;101 hivyo Muhamad  alibadili aya Mansukh na kuleta aya nyingine Nasikh ambazo nyingi zilikuwa zinagusa mahitaji yake kama kuoa wanawake aliojitakia hata wakiwamo wake za watu, kuna wakati ambapo Muhamad mwenyewe aliulizwa kuhusu kigeugeu alicho nacho na alidai kuwa shetani alikuwa amemdanganya  na kumletea aya zisizostahili Mwandishi maarufu wa Novel wa kiingerezamwenye asili ya kihindi bwana Salman Rushdie aliweza kukosoa  kiasi kikubwa cha aya hizo katika novel; yake iliyopewa jina la Aya za shetani (The Satanic Verses)


Pichani Bwana Salman Rushdie Mwandishi maarufu wa Novel nchini uingereza ambaye alilazimika kukaa mafichoni baada ya kuandika kitabu chake kiitwacho Aya za shetani mwaka 1988 Jambo lililopelekea Ayatollah Khomein Kiongozi wa kidini wa Iran kuagiza kuwa bwana huyu auwawe, wengi wa waislamu walifikiri kuwa kitabu chake kinaushambulia uislamu.

      Ukweli kuhusu kitabu hiki unaweza kubaki palepale nasema unaweza kubaki palepale hasa unapoangalia mfumo mzima wa Quran na uislamu na tamaduni zake na maisha ya nabii Muhamad kwa ujumla utaweza kuona zinaa ikihalalishwa kwa visingizio vya kuletewa aya, uchawi, uhusiano na majini, msisitizo wa ugaidi, mfumo wa kukubali kuua au kuuawa kwaajili ya mwenyezi Mungu hata ingawa anatajwa kuwa mwingi wa rehema lakini mfumo mzima wa kiislamu hauonyeshi kivitendo kama kweli Mungu ni wa Rehema  na badala yake sisi tunaona utendaji mkubwa wa shetani ukitenda kazi kwani Kristo alisema kazi ya ibilisi ni kuvunja, kuiba, kuchinja na kuua Yohana 10;10 “Mwivi haji ila aibena kuchinja na kuharibu mimi nalikuja ili wawe na uzima kisha wawe nao tele”Kazi ya Yesu Kristo na agizo lake katika injili ni kuleta uzima na sio kuua kama yalivyo maagizo katika Quran.
Kama wewe ni Muislama ukishaifahamu kweli hii Okoka haraka acha kupoteza Muda!

Hakuna maoni: