Jumanne, 8 Machi 2016

Huzuni ya kuuza Haki yako ya Uzaliwa wa Kwanza !



Msatari wa Msingi Genesis 25:29-34

Utangulizi:
1.      Esau ni moja ya watu muhimu katika Biblia lakini habari zake zinatupa masikitiko Makubwa
a.       Alikuwa Mzaliwa wa Kwanza wa Isaka na Rebeka na Pacha la Yakobo Mw 25:21-26
b.      Alipendwa na baba yake Isaka sana na alibarikiwa kuwa Mwindaji Hodari Mw 25:27-28
2.      Alikuwa ni Mtu mwema sana
a.       Alionyesha wema wake kwa ndugu yake aliyemdanganya Mw 33:1-16
b.      Alisaidia wakati wa Mazishi ya Baba yake Isaka Mw 35: 29
3.      Lakini Mara mbili bila Huruma alitendewa visivyo haki na Ndugu yake Yakobo
a.       Yakobo alimuuzia Esau ndugu yake haki ya uzaliwa wa kwanza alipokuwa na njaa kali Mw 25:29-34
b.      Mara ya pili wakati Isaka amekusudia kumbariki Esau Yakobo alijiingiza kwa hila Mw 27:1-41
Katika somo hili tutaangalia zaidi katika eneo la Kwanza ambalo kwalo linaweza kutufunza maswala kadhaa katika maisha.


I.                   Esau auza Haki ya mzaliwa wa kwanza.
Katika mila na desturi za Israel Uzaliwa wa kwanza kilikuwa ni cheo chenye faida kadhaa za kimwili na Kiroho, Neno la kiyunani kuhusu Mzaliwa wa kwanza ni Prototokos “Prototokos” Ambalo maana yake ni wa kwanza katika Cheo cheo hiki kilikuwa na maana pan asana! Na faida zifuatazo
a.      Faida za Kimwili
-          Kupata Urithi Maradufu kutoka katika urithi wa baba yako Mwanzo 36:6-7
-          Kuwa kiongozi wa Familia na mtunga sheria wa familia Mwa 27:29
b.      Faida za Kiroho
-          Kuwa mrithi wa ukuhani wa kifamilia baba yako anapofariki
-          Mrithi wa matamko yote ya Baraka juu ya ukoo wako
-          Kurithi Baraka zote ambazo Abraham alikuwa ametamkiwa Mw 28:4:12:1-3
-          Kupata haki ya kutamkiwa Neno la Baraka kubwa na mzazi wako anapokaribia kufa.
-          Hili ndilo Jambo kubwa ambalo kila mmoja katika Familia alikuwa analitamani. Kwa Esau na Yakobo.

II.                Mtazamo wa Esau na Yakobo:-
Mtazamo wa Esau
-          Esau alitazama haki ya uzaliwa wa kwanza kwa mtazamo wa mwilini kuliko wa Rohoni.
-          Alikuwa na mtazamo wa sasa kuliko wa baadaye, alizarau haki ya msingi kwaajili yam lo mmoja tu na kwa sababu hii aliitwa mtu asiyemcha Mungu Waebrania 12:16, haki ya Uzaliwa wa kwanza inakuunganisha na Mungu moja kwa moja.
-          Esau alipuuzia jambo hilo kwa kujumuisha kiapo wakati anakubali kumuuzia Yakobo.
-          Alipuuzia umuhimu wa Baraka za wakati ujao, aliweza kujali mlo mmoja tu ambao ungeondoa njaa ya siku moja na kusahau kuwa kesho angehitaji tena hivyo anafananishwa na Muasherati, waashetari hutamani kuitimiza shuku ya mwili kwa wakati huo tu bila kujua madhara na matokeo ya matendo yao na kusahau kuwa kesho watahitaji tena tendo la jinsi ileile.
-          Alifananishwa na mtu aliyetaka kupata raha ya muda na nafuu ya muda tu, akasahau kuwa anajitia katika tatizo kubwa litakalogharimu maisha yake, Viongozi wengi sana wa bara la Afrika wana mitazamo kama ya Esau wanaingia mikataba ya kushangaza wakifikiri watatatua matatizo ya wananchi wao, baadaye wanakuja kugundua kuwa wamejiingiza pabaya na kuwa mikataba hiyo itagharimu maisha ya waafrika wengi, si vema kuingia katika mikataba ya aina yoyote eti kwa sababu una njaa tu, wengi wameoa au kuolewa kwa mitazamo ya kuona karibu, anafikiri kuwa kwa maisha ya ndoa atafurahia ulimwengu, atakuwa ameuchinja lakini wengi sasa wanajuta kwa kufanya maamuzi yanayogharimu maisha yao na umilele wao, huolewi tu kwa sababu wengine wanaolewa wala huoi tu kwa sababu wengine wanaoa, ni lazima ufikiri kwa kina na kumuhusidha Mungu kwa vile maamuzi hayo yatagharimu maisha yako.
-          Wengi tunaingia katika chuki na wivu na kuwapiga vita wengine kwa sababu tunaangalia vichache walivyo navyo na tunasahau kuwa Mungu amekusudia kuimbariki kila mmoja wetu. Katika kristo sote ni wazaliwa wa kwanza, tunazo ahadi na Baraka za Mungu tusijaribiwe kwa kuanza kupiga vita wengine.
III.             Somo kuu la Kujifunza kwetu
-          Sisi nasi ni warithi wa ahadi zilezile pamoja na Ibrahimu kwa njia ya Imani Galatia 3:29
-          Tuwarithi pia pamoja na Kristo Warumi 8:16-17
-          Tu warithi wa tumaini lile la milele Tito 3:7
-          Tu warithi wa ufalme ule tulioahidiwa Yakobo 2:5 na 2Petro 1:11
-          Katika Kristo vitu vyote ni vyetu 1Koritho 3:21-23 na Ufunuo 21:7
-          Tuna urithi usioharibika mbinguni uliotunzwa kwaajili yetu 1Petro 1:4, Marko 10:28-30.
Tahadhari:-
-          Sisis nasi tunaweza kuuza Urithi wetu wa Mzaliwa wa Kwanza kwa kufuata anasa na raha ya dhambi za dunia hii Waebrania 11:24-26
-          Kwa tamaa ya maswala ya dunia hii bila kumtanguliza Mungu 1Yohana 2:14, Yakobo 4:4
-          Kwa kuufuata Mwili na kukataa kuongozwa na Roho wa Mungu Wagalatia 5:16-26
-          Ni lazima tuhakikishe tunashika nafasi yetu ya uzaliwa wa kwanza kwa gharama yoyote
Tunawezaje kupoteza haki zetu za Uzaliwa wa Kwanza?
1.      Imarisha uhusiano wako na Mungu na tafuta kuwa na amani na watu wote Waebrania 12:14
2.      Usikubali kuipungukia Neema ya Mungu Waebrania 12:15
3.      Ishi maisha ya utawa na kumtegemea Mungu wakati wote 1 Koritho  9:24-27; 1 Tito 4:7-8.
Kumbuka !
-          Esau hakuangalia mbali aluidharau Baraka za Mungu zilizokusudiwa kwake
-          Alisikiliza tamaa za mwili na kutekeleza maswala ya Muda mfupi
-          Sisi nasi tunaweza kumpuuzia Kristo, tunaweza kufanya makosa yaleyale
-          Mungu atusaidie tusije tukajisahau na ikawa ngumu kwetu kupata tena neema ile hata tujapolia kwa machozi Waebrania 12:17.


Tuitimishe ujumbe huu kwa kuimba Tenzi hii Mungu amenihurumia
Wimbo: Mungu amenihurumia
1. Mungu ametuhurumia, tendo hili kubwa sana,
sikustahili jambo hili, nimelipata bure tu!
sasa najua hayo yote, sasa najua hayo yote,
nasifu rehema zake, nasifu rehema zake
2. Nalistahili kupotea, lakini nahurumiwa,
Mungu amenipatanisha na yeye kwa Yesu Kristo,
sababu hii namtumikia, sababu hii namtumikia,
nasifu huruma yake.
3. Mungu mwenye huruma nyingi, usininyime huruma,
naitafuta siku zote nikiulizwa na watu,
hivi vyote vyatoka wapi? hivi vyote vyatoka wapi?
Nasema ni huruma tu!

Hakuna maoni: