Jumatatu, 7 Machi 2016

Ufahamu kuhusu shule kuu sita za Kiislamu !



Waislamu duniani ni zaidi ya billioni moja na milioni mia nane ni dini inayokuwa kwa kasi sana na walio wengi zaidi ni kutoka dhehebu la suni wakifuatiwa na wengineo tutayachambua madhehebu hayo kama ifuatavyo;-

·   Suni “Sunnite”
Hii ndio shule au dhehebu lililo kubwa zaidi kuliko yote asilimia 90% ya waislamu wote duniani ni wasuni, wasuni wanaamini mafundisho kutoka kwa Makhalifa wakuu wanne ambao wanaamini kuwa ndio wakwanza waliomrithi Muhamad moja kwa moja baada ya kufa na si vinginevyo.Wasuni wako kwa wingi huko mashariki ya kati na na pwani ya Afrika mashriki nchi.


                                                Imamu mkuu wa Madhehebu ya Suni Nchini Irani Khamenei


·   Shiha “Shiites”
     Hii ndio shule au dhehebu la pili kwa ukubwa, jina shiha linawahusu waislamu wa mwanzo kabisa  wanaoamini mafundisho ya Imam Ali mwana wa kufikia wa nabii Muhamad ambaye wao huamini kuwa ndie kiongozi mrithi wa Waislamu aliyemrithi Muhamad ambae alifuatiwa na maimam kumi na mbili ambao nao walikuwa viongozi na wengi wao waliuawa, wao walidai kuwa Ali alikuwa mzee wao,na imam wa mwisho kabisa aliitwa Muhamad yeye alitoweka kama mtoto mwaka 878 bk. Inaaminika kuwa atakuja tena kwa watu wake kimuujiza (mahdi) na kwa njia ya mwili wa mtu mwingine na atafanya uislamu uchanue duniani kabla ya siku za mwisho(….will bring the golden age before the end of the world).(ndio maana rais wa sasa wa Iran hujifikiri ni yeye kwa kuwa anaitwa Mohamed Nejad na kiburi cha nyukilia) tofauti na wasuni washiha ingawa ni wachache kuliko suni washiha ni maarufu sana duniani hasa baada ya mapinduzi ya kiislamu yaliyofanywa na Ayatollah Khomein na kuchukua uongozi wa Iran mwaka 1979 na kuifanya Iran kuwa nchi ya kiislamu ya dhehebu hilo na hivyo wako kwa wingi katika nchi ya Azerbaijan, Bahrain, Iraq, Afaghanstan na Pakistan.Hawa ni maarufu kwa siasa kali.

·   Ismailia “Ishimailites”.
Hii ni shule au dhehebu la tatu la kiislamu ni jamii ya washiha ambao wanaamini mafundisho ya Imam aliyeitwa Ismail ambaye inaaminiwa kuwa ndie imam wa mwisho tofauti na shule nyingine wao wana kiongozi wa kidunia wa dhehebu lao ambaye ni billionaire bilionea  ambe huitwa Prince Agha Khan.
                              Prince Karim Agha Khan kiongozi wa madhehebu ya Ismailia Duniani


·   Ahamadia “ahamadiyan”.
Hii ni shule au dhehebu la nne la kiislamu ambalo limeanza hivi karibuni kwenye miaka ya 1800 hivi ilianzishwa na mtu aliyeitwa Mizra Ghulam ahmad aliyeishi kati ya (1839-1908) huko Punjab nchini India alidai kuwa yeye ndiye masihi na kuwa ndie mfano halisi kamili wa Muhamad alifundisha kuwa Yesu alizimia na kutibiwa kwa madawa na kupona na kwenda kuishi huko Kashimir nchini India alikofia, Ahamadia wana vikundi vikali sana vyenye kuushambulia ukristo na hukataliwa kuwa wao sio waislamu 

 Mizra Gulam Ahamad

·   Shafi “Sufi”.
     Hii ni shule ya tano ya kiislamu au dhehebu la tano hawa hupingwa sana na waislamu wenzao kama wasuni na washiha na wanaitwa kuwa ni imani potofu wazushi hasa kwa sababu ya mafundisho yao ambayo hukiri kuwa Mungu si mmoja na kuwa mwanzo wa uislamu ulikuwa miungu mingi na kuwa allah alikuwa mungu mwezi jambo linalopingwa na wislam ingawa ni la kweli kihistoria kama tutakavyoona.

·   Ansar “Ansar suni” .
     Ni jamii mpya ya shule au dhehebu la hivi karibuni inawezekana kuwa ni jamii ya wasuni hata hivyo neno ansar kwa kiarabu maana yake ni nzuri au safi au njema inawezekana kuna mambo hawakubaliani nayo katika Usuni kama Ibada za wafu,ushirikina, uchawi nk ni wenye siasa kali na msimamo mkali huwahi kufunga ramadhani siku moja kabla ya wenzao na husheherekea iddi siku moja kabla ya wenzao hivyo ni wasuni safi hata hivyo hadi tunakuja mitamboni utafiti zaidi kuhusu shule hii ulikuwa unaendelea kwani ni dhehebu jipya.

Hakuna maoni: