Jumanne, 26 Januari 2016

MFULULIZO WA MASOMO YAHUSUYO UTETEZI WA IMANI (APOLOGETICS) 2



MAFUNDISHO POTOFU WAKATI WA KARNE YA PILI.
Marcionites.

Ni imani iliyoanzinswa na mtu aliyeitwa Marcion  aliyeishi kati ya Mwaka wa 100-160 alizaliwa huko Sinope-Pontus yaani Uturuki ya Leo inaaminika kuwa huenda alikuwa mtoto wa askofu wa mji huo Imani yake ya uzushi ilianzia huko Rome kati ya mwaka 140 hivi  Yeye alisisitiza zaidi sana kuhusu Upendo wa Mungu  kuliko haki yake  na alilipinga vikali agano la kale
Alikuwa mpinzani mkubwa wa wayahudi na pia alikataa sehemu kubwa ya agano jipya ambayo alifikiri kuwa inawapaka mafuta wayahudi au ina uhusiano na imani ya kiyahudi aliamua kuandika Injili yake ambayo ilikuwa ikifanana sana na ile injili ya Luka ingawaje alikuwa ameruka Karibu 1/3 ya injili hiyo.
 Alitengwa na kanisa kama mzushi na alianzisha imani yake hiyo watu wake walijikana na waliacha kuoa ,  imani ilikuwa ana kupata nguvu ikiwa na askofu wake  pamoja na sacrament ya Ubattizo na meza ya Bwana lakini hawakutumia kabisa mvinyo wa divai. Walipinga swala la Incarnation na maswala ya Yesu kusulubiwa, aliamini katika umilele wa vitu vyote, waliendelea kuweko mpaka mnamo karne ya nne na imani hizi zilipingwa vikali na wakristo akiwemo Justin, Irenaeus, and Tertullian.

Montanists.

Ni mojawapo ya imani ya kizushi iliyoanzia wakati wa karne ya pili imnani hii ilianzshwa na Nabii Montanus aliyeishi huko Phyrigia ambayo sasa ni sehemu ya uturuki imani hii ilianza mnamo mwaka 156, Bwana Montanus alitokea katika kijiji kidogo na alianza kutoa unabii akidai kuwa amesikia sauti ya Roho Mtakatifu,Yeye na vijana wawili wa kike Prisca na Maximilla alizunguka akihubiri na kufundisha katika Asia ndogo, alifundisha kuwa mtu akianguka katika neema hawezi kukombolewa tena, waamini walitiwa moyo kuyatafuta mateso na sio kuyakimbia,
Imani hii iliweka mkazo na kukemea ubaridi katika kanisa kwani wakati huu kanisa lilianza kupoa na kuchukuliana na ulimwengu walikuwa wakijiandaa na ujio wa Kristo wa mara ya pili na hawakujali maswala ya kawaida zaidi ya kujiandaa na kuja kwa Bwana mnamo mwaka 177 kiongozi wa kanisa alihofia mgawanyiko wa kanisa na hivyo aliitenga imani ya Montaninism imani hii ilipata nguvu kwa sababu iliungwa mkono na mwanatheolojia wa kipoman Tertulian mpaka karne ya 6 imani hii ilikuwa imetoweka.

Gnosticism.
Ni moja ya imani potofu ya kale na ya zamani zaidi au ya muda mrefu zaidi, Neno Gnosticism lina tokana na neno la kiyunani Gnosis ambalo maana yake ni Maarifa au ujuzi, imani hii ilichanganya maswala ya kipagani na Ukristo.
Walifundisha kuwa baada ya Mungu mkuu kuna miungu mingine mingi midogomidogo ambayo baadhi yao ni mibaya na baadhi ni wema na kuwa kupitia wao ulimwengu uliumbwa ukiwa na Mchanganyiko wa mambo mema na mabaya
Wanafundisha kuwa Kristo ni miongoni mwa miungu hiyo na kuwa uweza wa uungu ulikuwa juu yake kwa muda, waliamini kuwa maandiko ni hadithi na kuwa unaweza kutafasiri maandiko haya kama kila msomaji apendavyo na aonavyo

KWA NINI IMANI POTOFU HUTOKEA?
Jibu moja jepesi kwa nini imani potofu hutokea ni kwa sababu kanuni za kutafasiri maandiko hazikuweko au haizizngatiwi, kwa msingi huo ni Ushauri wa somo hili kwamba kila mwanafunsi wa Biblia ni lazima ajifunze  kanuni za kutafasiri Biblia na kufahamu kuwa maandiko hayawezi kutafasiriwa kama kila mtu apendavyo Paulo alimwambia Timotheo katika 2Timotheo 2;15 kuwa ni muhimu kwake kulitumia neno la Mungu kwa halali kwa msingi huo hapa tunaelekeza maswala kadhaa ya kuzingatia wakati tunapotaka kulitafasiri neno la Mungu.
1.       Ni lazima uzingatie Mazingira.
Ni muhimu kufahamu kuwa Biblia kwa mfano Agano la kale liliandikwa zaidi ya Miaka 3500 hivi iliyopita na huku wakati Agano jipya liliandikwa zaidi ya miaka 2000 iliyopita  kwa msingi huo Mtafasiri wa maandiko anapaswa kuzingatia swala zima ka Historia, siasa, Falsafa na Tamaduni za wakati huo kuwa zinatofautiana na za sasa  kwa msingi huo ni lazima Mtafasiri afikiri kuwa kifungu Fulani cha maandiko kliwezaje kuwafaa watu wa nyakati zile na baadaye kuangalia kinawezaje kutumiwa katika wakati tulio nao.

2.       Ni lazima uzingatie Mabadiliko ya Lugha.
Ni muhimu kufahamu kuwa lugha za asili pia zilizotumiwa kuileta Biblia kwetu zilikuwa Kiibrania na kiyunani na sehemu chache kiaramu kwa msingi huo ni muhmu kufahamu lugha hizo zilimaanisha nini kwa wakati ule na ukumbke kuwa maana ya meneo hubadilika baada ya Karne kadhaa.

3.       Ni lazima Uzingatia sheria ya Muktadha Context.
Watu wanaweza kukengeusha maana halisi ya maandiko na kupata mafundisho ya uongo kama Muktadha yaani kifungu cha maandiko hakitazingatiwa unapotaka kuchanganua maana ya aya Fulani lazima uanze kujisomea kutoka juu ya aya hiyo na pia chini ya aya hiyo kwa mfano katika Zaburi ya 116; 11b “Biblia inasema Wanadamu wote ni waongo” lakini unaposoma andiko hilo vema kuanzia 11a utaweza kuona mwandishi akiweka wazi kuwa “Mimi nalisema kwa haraka yangu” unaona?

4.       Ni lazima maandiko unayotumia yawe yanaungwa mkono na maandiko mengine (Harmony).
Mara nyingi waalimu wa uongo hujitungia Mafundisho yao  kwa tafasiri zao kumbuka kuwa 1Petro 1;20-21 Biblia inasema unabii haukuletwa popote kwa mapenzi ya mwanadamu  kwa msingi huo ni lazima maana ya ujumla ya neno la Mung iweze kuzingatiwa na sio kamstari kamoja tu Zaburi 119;160 Unasema Jumla ya Neno lako ni kweli.

5.       Ni lazima ufanye kazi ya kutafuta maana iliyokusudiwa kisha uitumie. (Exegesis)
Neno la asili la kuelezea au kutafuta maana linatokana na asili ya kiyunani Exegeisthai ambalo maana yake ni kuelezea kwa hiyo mtafasiri ni muhimu kutafuata maana iliyokusudiwa na waandishi na andiko na kulinganisha ukweli na maandiko mengine na kasha kuelezea maana inayokusudiwa na Biblia au neno la Mungu na hapo ndipo mtu anakuwa amehubiri neno la Mungu na sio kulisingizia neno la Mungu Eisogesis. Kujitafutia maana yako mwenyewe na kuyasingizia maandiko.

6.       Ni lazima uzingatie swala la kujirudia kwa unabii (Multiple Fullfillment.)
Baadhi ya unabii una tabia ya kujirudia katika kutimizwa kwake kwa zaidi ya mara moja  kwa mfano swala la kurudi kwa Yesu Mara ya pili  liko katika mazingira makuu mawili Unyakuo na Ufunuo, au kunaweza kuwa na wapinga Kristo wengi katika historia lakini hatimaye kutakuwa na mpinga Kristo mmoja tu.

7.       Ni lazima wakati mwingine ukubaliane na maandiko kama yalivyo (Simplicity.)
Wakati wote ni muhimu kuzingatia kwanza Tafasiri iliyowazi katika maandiko kabla ya kuanza kufikiri kuwa ni mafumbo chagua maswala rahisi kuliko kujichagulia maswala magumu.
Na mkuu wa wajenzi mwenye Hekima 
Rev Innocent Kamote

Hakuna maoni: