Jumapili, 31 Januari 2016

UJUMBE: KWAAJILI YA HAYA NALIZALIWA!


Mstari wa Msingi Yohana 18:37.

Biblia inasema hivi katika Mstari huo “37. Basi Pilato akamwambia, Wewe u mfalme basi? Yesu akajibu, Wewe wasema, kwa kuwa mimi ni mfalme. MIMI NIMEZALIWA KWA AJILI YA HAYA, na kwa ajili ya haya mimi nalikuja ulimwenguni, ili niishuhudie kweli. Kila aliye wa hiyo kweli hunisikia sauti yangu. 38. Pilato akamwambia, Kweli ni nini?”


Kila mtu duniani anapaswa kuwa na ufahamu wa kutosha kuwa ni kwanini yuko Ulimwenguni!, kutokujua ni kwa nini uko Duniani ni tukio baya sana, watu wengi sana wamepoteza muelekeo na kufupisha maisha yao au kufa kabla ya wakati kwa vile hawajui kwanini wanaishi!,Aidha wengine wamekosa kugundua umaana wa maisha  na kufikiri kuwa labda huenda heri wasingalizaliwa ama walizaliwa kwa bahati mbaya kwa vile tu hawakujua kwa nini wamezaliwa? “Mjenzi mmoja alisema kama mtu hajui kwa nini anaishi amekufa tayari ingawa anaishi”

Mungu anapenda tuwe na ufahamu na tutambue umuhimu wa kuwepo Kwetu, ndani ya kila aina binadamu Mungu alikwisha kuweka kusudi lake, ili tulitumikie na kuliishi tukiwa duniani, wengine walielezwa mapema na kwa uwazi makusudi ya kuwepo kwao Mfano 

Yeremia 1:4-8 4. Neno la Bwana lilinijia, kusema,  Kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua, na kabla hujatoka tumboni, nalikutakasa; nimekuweka kuwa nabii wa mataifa. Ndipo niliposema, Aa, Bwana MUNGU! Tazama, siwezi kusema; maana mimi ni mtoto. Lakini Bwana akaniambia, Usiseme, Mimi ni mtoto; maana utakwenda kwa kila mtu nitakayekutuma kwake, nawe utasema kila neno nitakalokuamuru. Usiogope kwa sababu ya hao maana mimi nipo pamoja nawe nikuokoe, asema Bwana”. 

Ni wazi kwamba Yeremia alifunuliwa Kusudi la Mungu katika maisha yake mapema sana akiwa kijana mdogo, wako wengine wazazi wao walifunuliwa kusudi la watoto wao hata kabla hawajazaliwa ili waweze kuwasaidia kulitimiza kusudi hilo Mfano Samsoni Waamuzi 13:2-5 Samsoni alizaliwa akiwa na kusudi la kuwaokoa Israel na mikono ya wafilisti, Yohana Mbatizaji Luka 1:5-17 Yohana Mbatizaji alizaliwa kukiwa na kusudi la kurejesha mioyo ya watu kwa Bwana, Muda usingaliweza kutosha kuona watu wengi waliozaliwa na waliopata neema ya kujua kusudi la kuwako kwao Mungu ana makusudi nawe pia!, hujazaliwa kwa bahati mbaya kuna kusudi la Mungu katika kuweko kwako!

Yesu alikuja Duniani kwa Makusudi makubwa na mengi na kwakuwa Yeye nikiongozi mkuu wa wokovu wetu tunapopitia kusudi la kuzaliwa kwake tunapata kugundua siri ya kwanini tuko ulimwenguni na hili litatusaidia sisi nasi kuishi kwa Makusudi KWA AJILI YA HAYA NALIZALIWA

1.       Kuwaokoa watu na dhambi zao Mathayo 1:21
Dhambi ni moja ya matatizo makubwa sana
2.       Kuwapatanisha watu na Mungu Yohana 1:35,29
3.       Kuharibu kazi za Ibilisi 1Yohana 3:7-8
4.       Kutafuta na kuokoa kilichopotea Luka 19:10
5.       Kufanya Mapenzi ya Baba yake Yohana 6:38
6.       Kuwa Nuru ya Ulimwengu Yohana 12:46
7.       Kutoa Uzima wa milele Yohana 10:10
8.       Kuhukumu Ulimwengu Yohana 9:39
9.       Kufunua kusudi la kweli la Maisha ambalo ni “ kutumika” Mathayo 20:28
10.   Kufa Msalabani ili awaokoe wanadamu Yohana 12:27

Kuifunua Hekima ya kweli na neno la Mungu, nah ii ndio kweli, ni muhimu kufahamu kuwa Israel walikaa na kuishika torati kwa maelfu ya miaka lakini hawakuielewa, ilikuwa kana kwamba imefichika machoni pao, katika neon la Mungu kuna siri ya ajabu ambayo mtu wa asili ya kawaida hawezi kuielewa siri hii ndio Kweli Mathayo 13:35, kweli hii ni siri inahitaji neema na ufunuo kutoka kwake kuielewa  Luka 24:27

Kazi na mkuu wa wajenzi mwenye Hekima

Hakuna maoni: