Alhamisi, 28 Januari 2016

Mwanadamu ni nini hata Umkumbuke?



Ujumbe: Mwanadamu ni nini hata Umkumbuke?
(“What is Man that You Are Mindful of Him?”).
“Waebrania 2:5-8”Zaburi 8:3-4”

Ni muhimu kwetu kwa kila mmoja wetu kujiuliza, kuwa katika akili zetu ni nani tunampa kipaumbele kikuu kila siku? Tunaweza kuhisi kuwa wengi wa wale tunaowapa kipaumbele kwanza wanaweza kuwa ni wana familia zetu, wapenzi na marafiki na labda Mungu!
Au kama kuna mtu mwingine uneyeweza kumpa kipaumbele zaidi anaweza kuwa mtu unayemchukia, adui yako anayekusumbua na kukunyima raha, Kwa kawaida tunapenda kufikiri vile vyenye umuhimu katika maisha yetu na vile visivyona umuhimu au mguso tunaweza kuvipuuzia na kuvitupa kando.  Ni uwazi ulioje kuwa kuweko kwa Mungu kumekuwa ni kama dhana inayofikiriwa kuwa ni ya kusadikika tu, wengi wetu kwa ndani sana tunaweza kufikiri kuwa Mungu hayuko na hajishughulishi na chochote kuhusu wanadamu na hususani tunapopitia nyakati ngumu tunafikiri kama Mungu yupo kweli angelitazama hili bila kushughulika nalo?
Wagiriki wengi walikuwa hawaamini katika Mungu na hivyo walikuwa na miungu mingi dhana kuhusu Mungu haikuwa halisi katika maisha yao na hivyo waliabudu miungu mingi ili kutafuta msaada na kutafuta kuwezeshwa na miungu hiyo baadhi ya miungu yao ni kama hii

1.      Aphrodite alikuwa Mungu wa Mapenzi
2.      Apollo alikuwa Mungu wa Music na Uponyaji
3.      Ares alikuwa Mungu wa Vita
4.      Athena alikuwa Mungu mke bikira na mungu wa Hekima
5.      Hermes alikuwa Mungu wa Ujumbe
Pamoja na miungu kadhaa wa kadhaa

Biblia inatufundisha kwamba Mungu tunayemuabudu yeye ni wa tofauti kabisa ni Mungu anayemjali mwanadamu na kujishughulisha naye bila kujali hali yake, kwamba ni msomi au mjinga ni masikini aua tajiri, mweusi au mweupe ni wahali ya juu au ya chini, ni mwanamke au mwanamume, ni mtakatifu au ni mwenye dhambi, Mungu anapendezwa na Mwanadamu sana, Watakatifu waliotutangulia waliona upendo huu wa Mungu kwa ndani sana akijishughulisha na wanadamu kwa namna ya kupita kawaida Katika tafakari zake mfalme Daudi alifikiri hivi? Na kujiuliza maswala haya hasa baada ya kugundua namna Mungu anavyomjali Mwanadamu

Waebrania 2: 5-8 “Maana hakuuweka chini ya malaika ulimwengu ule ujao tunaounena, ila mtu mmoja ameshuhudia hivi mahali fulani, akisema, 6. Mwanadamu ni nini hata umkumbuke, Ama mwana wa binadamu, hata umwangalie? 7. Umemfanya mdogo punde kuliko malaika, Umemvika taji ya utukufu na heshima, Umemtawaza juu ya kazi za mikono yako;  8. Umeweka vitu vyote chini ya nyayo zake. Kwa maana katika kuweka vitu vyote chini yake hakusaza kitu kisichowekwa chini yake. Lakini sasa bado hatujaona vitu vyote kutiwa chini yake.”

Katika Mistari hiyo hapo juu kuna maswala Matatu Muhimu ambayo Mungu anamfanyia mwanadamu kuonyesha namna alivyomthamini “Hata umkumbuke” “Hata Umwangalie” “Umemtawaza juu ya kazi za mikono yako” haya yanadhihirisha uthamani na upendo mkuu wa Mungu wetu kwetu.
           
1.      Mungu humkumbuka Mwanadamu “Mindful of Him”.
Biblia inaushahidi mwingi unaodhihirisha kuwa sisi ni wa thamani machoni pa Mungu na kuwa Mungu anatuwazia sisi kama kipaumbele chake hata kama sisi hatumjali  na kumuheshimu yeye alituumba kwa  mfano wake alitupenda mno Zaburi 8:3 Isaya 43:4. Biblia inathibitisha kuwa Mungu hajatuacha wala hatatusahau, anatuhurumia na kuwa ametuchora katika vitanga vya mikono yake Isaya 49:15-16 Kama ilivyongumu kwa Mama kumsahau mtoto wake anyonyaye ndivyo ilivyo na kwa Mungu wetu.Ndugu yangu Mungu hajakusahau Mungu hajakutupa Umejaa katika wazo la Mungu.

2.      Mungu humwangalia Mwanadamu “Care of Him”
Licha ya Mungu kujawa na binadamu katika akili zake ni muhimu pia kufahamu kuwa Mungu anakuangalia!, anajali Mungu anapokuangalia anajisikia kukufanyia mambo makubwa sana anaguswa na maumivu yako na huzuni ulizonazo na anajali Luka 7:11-16 Hataweza kukuachia hata umezwe na huzuni na jaribu kuliko uwezo wako ataingilia kati na kuleta faraja Kama alivyo mfanyia mjane huyu katika Luka na watu wakakiri kuwa Mungu amewaangalia watu wake tunaye Mungu ambaye huangalia.

3.      Umemtawaza juu ya kazi zako “ You put everything under his feet”
Mungu ameweka kila kitu chini ya miguu yetu, ametupa kutawala, ametiisha hata malaika hutuhudumia mwanadamu ametukuzwa na Mungu kwa kiwango kikubwa cha kifalme Luke 10:18-19 Mungu ametiisha kila kitu chini yetu hatupaswi kuogopa, tunapaswa kuelewa jinsi Mungu anavyotujali, anavyotukumbuka na anavyotuangalia  na uwezo aliotupa, Mungu anapendezwa na wanadamu kuliko hata malaika, waoa wanatajwa kama roho wanaotumwa kuwahudumia wale watakaourithi wokovu Waebrania 1:13-14. Kama ikiwa Mungu anatujali kwa kiwango hiki………

Swali la Kumalizia ni kuwa wewe je unampa Mungu kipaumbele? Umamuheshimu, Unamuogopa au unamvunjia Heshima?
Mwandishi wa zaburi alikaa chini akatafakari na kugundua kuwa mwanadamu ni sehemu ndogo  sana ya uumbaji wa Mungu, ndogo mmno lakini akajiuliza swala kwa vipi Muumba anatoa nafasi kubwa kwa wanadamu? Daudi mwandishi wa zaburi hii alikuwa anaona kwa Mbali jinsi Kristo atakavyoacha enzi na utukufu na vyote na kuja kumkomboa mwanadamu kwa Damu yake ya Thamani jambo linalotudhihirishia Uthamani mkubwa sana alio nao mwanadamu, swali
Mwanadamu ni nani hata umkumbuke? Kamwe hatuwezi kutambua uthamani wetu kama Mungu sio Kipaumbele cha Maisha yetu Kadiri tunavyojifunza kuhusu Mungu ndivyo tunatambua uthamani wetu na kusudi la kuweko kwetu duniani.
Yeye aligharimika mno kwaajili yetu Yohana 3:16 Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda Ulimwengu” Biblia ya kiyunani ingesomeka hivi Katika namna isiyoweza kuelezeka Mungu aliipenda Dunia iliyojawa na uasi na udhalimu na desturi zenye kila aina ya machukizo “Cosmos” hata akamtoa mwanae wa Pekee, Maisha yetu yamegharimu Damu ya Yesu
“Wewe sio matokeo ya vile watu wanavyosema wewe ni matokeo ya vile Mungu anavyosema”
Mkuu wa wajenzi Mwenye Hekima
Rev. Innocent Kamote.

Hakuna maoni: