Jumapili, 31 Januari 2016

DADA MREMBO AKAADHIRIWA NA TUMBO LA KUHARA!



Maswahibu haya niliyashuhudia kwa macho yangu mwenyewe ingawa hayakuwa yamenipata mimi lakini aliyekumbwa nayo basi niite alikumbwa na fedhea la mwaka  na nimeona nikusilimie ili uweze kujifunza na wengine wajue kwa faida yao.

Ilikuwa mwaka jana nasafairi kutoka Dar kwenda Arusha kwa ajili ya kwenda kula sikukuu ya Krismasi, wale wanaosafiri na  magari hayao  nafikiri wanafahamu kuwa wakifika katikati kwenye safari  wenye mabasi hayo huyaingiza hoteli  iliyoko karibu na njiani  ambayo sipendo kuitaja  jina  na kondakta  akaamuru  abiria washuke wakapate chochote lakini kwa dakika kumi , kama kawaida kwa sababu mimi nilikuwa karibu na mlango  nilikuwa wa kwanza kushuka  nikawahi hotelini  na kuangiza bisikuti pakiti mbili na soda  nikawa nimekaa kwenye kiti naendelea kula taratibu huku nikiangalia saa yangu  ya kwenye simu ya mkononi ili niende na muda wa kondakta wa basi.

 Tumbo la kuhara huwa halina Adabu!

Wakati naendelea ghafla  nikasikia sauti ya dada mmoja  akiita anko samahani naomba hiyo chumvi hapo mezani kwako, nilipogeuka nyuma ghafla  nikamwona aliyekuwa akinisemesha  ni dada mmoja aliyekuwa akila wali kwa mchguzi wa nyama pamoja na kachumbari, alikuwa ni msichana mrembo  kwa kweli jambo lililonifanya wakati nanyanyua ile chumvi kuimpa nikodoe macho kidogo kwa maana nyingine ni kama nilihamaki, muda wa kuondoka gari  ukawa umewadia  kwani gari lilishaanza kupiga  honi nami nikaelekea kwenye  basin a likaanza safari kuelekea Arusha  Baada ya safari kwa masafa ya kutosha nilimuona Yule dada akizungumza na kondakta wa basi jambo Fulani, Kondakta aliondoka na kumfuata dereva ambaye aliongea naye kwa sekunde kadhaa, basi lilisimama na ikatangazwa kwamba abiria wakajisaidie Nilijua Yule dada anataka kujisaidia, Abiria walirudi basini  na basi likataka kuondoka , lakini abiria mmoja alitahadharisha kuwa Yule dada aliyeomba basi lisimame alikuwa hajarudi na , ilibidi akina mama watumwe kwenda kuangalia kulikoni.

Baada ya muda tukaona wale akina mama waliokuwa wakienda kumfuatilia wakirudi na Yule dada aliyeniomba chumvi taratibu wanarudi kutoka nje  na kuingia kwenye basi, Na alipoingia alikwenda moja kwa moja kukaa kwenye siti yake huku abiria wengine wakimpa pole na wengine wakimwangalia tu bila kusema chochote na basi likaanza safari yake, lakini basi lilipotembea kama dakika hamsini hivi nikamwona Yule dada akinyanyuka tena kumwendea kondakta, na kwa sababu nilikuwa karibu na mlango  niliposikia maongezi ya safari hii kwani kondakata alikuwa akiongea na Yule dada kwa sauti kubwa baada ya kumuomba kuwa gari lisimame tena aende kujisaidia kondakta akaijbanza naye  kwa kumwambia haiwezekani  bwana tukimbize gari tukuwahishe hospitali, sisi tunakwenda kwa ratiba na kwa muda njiani trafiki watatukamata, Ghafla nikaona Yule dada akirukia mlango wa basi na kutaka kuufungua  huku basi linakwenda, ndipo abiria wengine wa basi wakataharuki  kulikoni huku wengine wakisimama kwenye viti vyao baada ya kuona tukio lile wakati Yule dada akiurukia mlango na kujaribu kuufungua  na kondakta kujaribu kumzuia,  nikamwona amechuhumaa chini  na huku amejiinamia na baada ya muda mfupi hariufu ya kinyesi ikatanda ndani ya basi zima na hususani  kwa siti za mbele , Na baadaye ikaonekana kuwa amejiharishia  tena vibaya mno, Ndipo tena wasamaria wema walipojitokeza na kwenda kumsaidia  na kubadilisha zile nguo kwa kumtaka atoke nje ya basi  lakini safari hii basi lilikuwa kwenye maeneo ya watu na sio zile sehemu maarufu za uchimbaji dawa, ndipo wakati huo ukazuka mjadala , wengine wakisema ashushwe akabadilishwe hivyohivyo mbele za watu nje ya basi, wengine wakisema asaidiwe ndani ya basi, wengine wakisema basi liwahishwe mpaka porini, wengine wakafungua mabegi yao kutoa mashati kumfunika wengine wakarudi viti vya nyuma kukimbia harufu ilimradi ilikuwa vurugu tupu tu.
Wakati hayo yakiendelea kukasikika kilio kingine cha sauti Para! t Para! Prataaaaapaa! Kumbe alikuwa amefanya tena vitu vingine palepale mlangoni, hayo yote yakiendelea akatokea mzee mmoja wa makamo  ndani ya basi akapaza sauti kwa nguvu nyie akina mama watu wa ajabu sana Yaani mwenzenu anaadhirika , badala ya kutoa khanga zenu mkaweka uzio wa dharula  hapo nje na kumsaidia mnaangalia tu,  Kweli wazo lile likafanya kazi kwa wengine hasa akina baba kufungua mabegi yao na kujitolea shuka na wengine waliotoa dawa ambazo walisafiri nazo wakati huo wakazi wa eneo lile walipoona uzio wa akina mama wamezunguka wakajazana kuona au kutaka kujua kulikoni, zoezi lile likakamilika  na safari ikaendelea  ambapo  dada Yule dada alishuka Moshi name nikaendelea  hadi Arusha huku nikijiuliza fedheha yote ile ya kujiharishia kwa Yule Dada huenda  shauri ya mikachumbari ile jamboa ambalo linanifanya hadi leo kuwa mwangalifu na kula hovyo hovyo njiani niwapo safarini.

Hakuna maoni: