Jumanne, 26 Januari 2016

MFULULIZO WA MASOMO YAHUSUYO UTETEZI WA IMANI (APOLOGETICS) 3



MISINGI YA KIBIBLIA YA ELIMU YA UTETEZI WA IMANI.

Unaweza kujiuliza swali hili je watu wa nyakati za Biblia walijiingiza katika maswala ya utetezi wa imani? Manabii na mitume je walikutana na changamoto kama hizi tunazokutana nazo leo je waliitetea imani au kwa maana nyingine uko ushahidi wa kimaandiko unaoonyesha swala zima la kuitetea imani? Ni muhimu kwetu kuchukua safari fupi ndani ya maandiko ili kuthibitisha ukweli na maswali yaliyoko juu yetu

1.       Mfano wa Kitabu kizima cha Ayubu, ni wazi kabisa kuwa bi kitabu kinacho halalisha Matendo ya haki ya Mungu kwa wanadamu ni utetezi wa kazi sahii ya Mungu dhidi ya Rafiki ndugu na jamaa waliokuwa wakijaribu kumshawishi Ayubu kuachana na Mungu ni wazai kuwa mwandishi alikuwa akionyesha kuwa Mungu wa Israel ni tofauti na Miungu ya kipagani yeye ni mwaminifu
2.       Mfano katika kitabu cha Zaburi, ni wazi kuwa kwa mifano zaburi ya 19 & 119 zinathibitisha wazi kuwa Mungu yupo  na kuwa amejifunua wazi kupitia Neno lake na kazi zake ni wazi kwa mafano katika Zaburi 19 inaposema Mbingu zatangaza ni wazi kuwa nyota na mbingu ni kazi ya uumbaji wa Mungu uumbaji unatetea kuwekokwa Mungu.

3.       Mfano katika kitabu cha Warumi, sura ya kwanza na ya Pili kuwa kupitia uumbaji na dhamiri mwanadamu anao ushahidi unaomuonyesha kuwa anawajibika kwa Mungu bila kuwa na udhuru
4.       Mfano katika kitabu cha Matendo ya Mitume ni wazi kuwa tunamuona Paulo mtume akiitetea injili chini ya viongozi kama Felix, Festo na agripa, Kwa ujumla kitabu cha Matendo kinazungumza kwa upana namna injili ilivyoweza kutetewa. Kinatetea Ufufuo wa Yesu na uuungu wa Yesu, injili ya neema bila sheria ya tohara ya Musa na Hotuba ya Paulo mbele ya wanafalsafa wa kiyunani Matendo 17 hali yote hiyo ni Apologetics ni utetezi wa Imani
5.       Kwa ujumla hata nyaraka nyingi ziliandikwa kwa kusudi la kuitetea imani na kurekebisha mafundisho potofu na kuonyesha njia kupitia mafundisho halali ya kweli ya injili Wafilipi 1;7 ni wazi kuwa Paulo mtume alifanya kazi ya kuitetea injili, 1Petro 3;15 “Muwe tayari sikuzote kumjibu (Kujitetea) kila mtu awaulizaye habari za tumaini lililo ndani yenu lakini kwa upole na kwa hofu”  Be ready always to make Defense (Apologia) ni wazi kabisa kuwa Mitume waliifanya kazi hii ya kuitetea imani 

Utetezi wa Imani nyakati za Mapema baada ya Mitume.
Tangu nyakati za kanisa la kwanza Mateso yalikuwa yametapakaa na kupamba moto dhidi ya Kanisa  mapaka mnamo mwaka wa 250 hata hivyo watetezi wa imani wengi waliinuka na kuitetea imani, wengi wao walitumia mfumo wa mafundisho katika uandihi na baadhi ya watetezi maarufu wa mapema kabisa ni kama Aristide, Justine Matyr, Tatian, Tertullian, Origen Na Syprian walitoa hoja zao kwa watatwala wa kirumi, katika bunge la senet na kwa watu raia wa Rumi

Wao walitoa miito kadhaa kama miito ya haki.
Mfano Justin Martyr aliyeishi kati ya 100-165 alikuwa ni Mwanafalsafa, Mwanatheolojia na moja ya watetezi wa imani wa mapema sana katika kanisa alikata shauri kuikabili mamlaka kuacha kuwatesa wakristo kwa sababu walikuwa wakristo. Justin alizaliwa huko Flavia Neapolis ambako leo ni Nabulus ukanda wa mashariki wa miji ya kale ya Rumi huko shechem Samaria au Israel wazazi wake walikuwa wapagani, alipokuwa kijana alijitolea kusoma Falsafa kupitia maandiko ya Mwanafalsafa maarufu wa Kiyunani Plato na falsafa za wastoiki alikutana na Ukristo huko Efeso na baada ya kuokoka alikwenda Rumi na kustawisha Shule. Aliuawa huko Rome kama shahidi wakati wa Utawala wa Marcus Aurelius


Marcus Aurelius

Mtawala Marcus Aurelius aliitawala Rumi kati ya 161 na 180 utawala wake ulitawaliwa na maswala ya vita za marakwa mara  ni katika wakati wake ndipo Justin Martyr aliweza kuitetea imani.

Mfano wa mtetezi mwingine ni Tertulian ambaye aliandika miaka 50 baadaye baada ya Justin alukuwa ni moja ya watu muhimu sana katika ukristo na mwandishi wa vitini vingi vya kitheolojia katika lugha ya kilatini ambavyo kati ya hizo 30 zimesalia hata leo aliishi kati ya 190-220 ni mwana wa akida wa kikosi cha jeshi cha kirumi alikuwa amesomea sheria,aliokoka kati ya mwaka 190-95 alirudi kwao Cathage ambaye alioa na baadaye kuwa mwangalizi wa kanisa alikazia maadili na  nidhamu katika kanisa na alikuwa mtetezi wa imani mwenye kupinga uzushi alijaribu kukebehi miungu ya kipagani pamoja na sadaka zao za kuteteketeza zilizotolewa kwa miungu hiyo, aliitetea imani kwa nguvu akithibitisha kuwa Mungu anayetumikiwa na wakristo ndiye Mungu na kuwa tunamuabudu Mungu mmoja ambaye macho ya kawaida hayawezi kumuona ingawa Yupo.
Utetezi wa imani nyakati za karne ya Pili.
Wanatheolojia wa Kanisa la kiorthodox  (Imani ye kweli ya Kikristo) waliitwa watetezi wa karne ya Pili njia yao kubwa ya kiutetezi imekuwa njia kubwa ya muhimu ya kufuatawa na wanatheolojia na watetezi wengi wa kizazi hiki njia yao ilikuwa ni Kutoa Tamko, kutafasiri na kukanusha.

a.       Kutoa Tamko.
Utoaji tamko wakati wa utetezi unajumuisha Imani na kujiuliza mswali  kwamba imani Fulani je inahusiano na kile tunachokifikiri kuwa kweli kwa wakati huo kujiuliza maswali sio swala zima linalohusiana na imani na Imani haimaanishi wakati wote ni kujiuliza maswali Imani ni uhusiano wa mwanadamu na Mungu inampa mtu ujasiri kwa Mungu anayemtegemea hii ni imani endelevu kwa Mungu na ni Binafsi na inapimika kwani unaweza kuwa nayo nyingi au chache lakini imani inayozungumzwa katika Yuda ni imani  ambayo inaonekana ni mjumuisho wa kweli kamili iliyofunuliwa na Mungu katika neno lake yaani Biblia  na inaaaminiwa na wakristo hii ndio imani ambayo watetezi huikusanya pamoja kama misingi ya imani ya kweli ya Kikristo.
Kumbuka kuwa “Haitoshi kujua kile unachoamini, lakini ni muhimu kujua kwa nini unaamini unachokiamini”

b.      Kutafasiri.
Moja ya kazi nyingine ya Muhimu ya elimu ya Utetezi apologetics ni kutafasiri kweli ya Ukristo katika kipimo sahii cha elimu ya kanuni za kutafasiri maandiko.

c.       Kukanusha.
Ni kazi ya tatu ya elimu ya utetezi wakati wote katika historia kumekuweko na madai yaliyo kinyume dhjidi ya kanisa kwa kiwango fulani kwa mfano wayahudi waliifikiri imani ya Kikristo kuwa ni imani iliyokengeuka na kuiasi sheria ya Musa kwa warumi ilikuwa ni kikwazo, kwa wayunani ulikuwa ni ujinga 1Koritho 1; 21-24 kwa waislamu wanakataa kabisa swala la Yesu kuwa mwana wa Mungu na kuwa utatu ni uzushi. Kwa msingi huo uthamani wa Imani ya Kikristo ni Uhakika wa kweli na ulinzi dhidi ya maadui wa imani au mashambulizi ya kiimani.

MABARAZA NA MATAMKO YA IMANI.   (Councils & Creeds)
Matamko ya imani Creeds ni Neno la Kiingereza litokanalo na neno Credo la kilatini ambalo maana yake ni Ninaamini “Ibelieve” Matamko haya ya imani yalitokana na Mikutano au mabaraza ya kikanisa yaliyofanyika kwa nayakati tofauti kushughulikia maswala kadhaa ya kiimani.
1.       Mkutano wa kwanza wa kanisa.
a.       Mkutano mkuu wa kwanza wa kanisa ulifanyika Yerusalem kati ya mwaka wa 49 na 50 ukishughulikia swala la Wokovu kwamba je ni lazima mataifa waliookolewa kuishika sheria ya Musa na kupitia tohara ndipo wahesabike wameokolewa? Paulo na Barnaba walisimama kama watetezi wa imani na walishinda na kwa sababu hiyo kufungua mlango injili kwa ulimwengu kama matokeo ya ushindi huo.
b.      Mfumo wa kuweko kwa mamlaka.
Baada ya kufa kwa mitume Mateso pamoja na mafundisho mengi ya uongo yalijitokeza, Mitume walikuwa wametegemewa sana kama mamlaka ya mwisho kila kulipotokea tatizo na kanisa liliweza kustahimili mafundisho potofu na changamoto nyinginezo. Kwa kuwa mitume walikuwa wamekwisha kufa wote kanisa liliunda mfumo wa mamlaka
1.       Mfumo wa kuwepo kwa Maaskofu
2.       Kupitishwa kwa kanuni ya kupima maandiko
3.       Kustawishwa kwa kiriwa imani na matamko ya kiimani.
Hata kufikia mnamo mwaka 250 Kanisa lilikuwa tayari ni Taasisi yenye viongozi wake yaani Maaskofukatika miji mikuu na majimbo na kutokana na kuweko kwa mafundisho potofu kanisa lililazimika kuwa na Ukiri wa imani kwani kuweko kwa maaskofu na kanuni ya kupimia maandiko hakukusaidia kupambana na imani potofu kama imani ya Gnostics na nyinginezo.
Rev. Innocent Kamote
Mkuu wa Wajenzi mwenye Hekima

Hakuna maoni: