Jumapili, 31 Januari 2016

MTU ANAYEUPENDEZA MOYO WA MUNGU:


1Samuel 13:13-14 Biblia inasema hivi “Naye Samweli akamwambia Sauli, Umefanya upumbavu; hukuishika amri ya Bwana, Mungu wako, aliyokuamuru; kwa maana Bwana angaliufanya ufalme wako kuwa imara juu ya Israeli milele.  Lakini sasa ufalme wako hautadumu; BWANA AMEJITAFUTIA MTU AUPENDEZAYE MOYO WAKE, naye Bwana amemwamuru yeye kuwa mkuu juu ya watu wake, kwa sababu wewe hukulishika  Neno lile Bwana alilokuamuru” 

Daudi alikuwa Mtu aliyeupendeaza Moyo wa Mungu



Paulo Mtume alipohubiri kule Antiokia katika mahubiri yake aligusia kwa ufupi Historia ya Isarael na kugusa kile ambacho Mungu alikisema kuhusu Daudi Matendo 13:22 “ ….ambaye alimshuhudia akisema, Nimemwona Daudi mwana wa Yese, MTU ANAYEUPENDEZA MOYO WANGU,”
Kila mmoja wetu anagefurahi kuitwa na Mungu “MTU ANAYEUPENDEZA MOYO WANGU”  kila mkristo anapaswa kuhakikisha kuwa anaupendeza moyo wa Mungu, Yesu aliishi maisha ya ya kumpendeza Mungu kiasi ambacho wakati akibatizwa Mungu alisema “HUYU NDIYE MWANANGU MPENDWA NINAYEPENDEZWA NAYE” hii ni sifa kubwa mbele za Mungu Hususani katika ulimwengu huu wa sasa.

Hata hivyo ili sisi nasi tuweze kumpendeza Mungu na Mungu kuvutiwa nasi kama ilivyokuwa kwa Daudi  ni muhimu kwetu kutafakari kwa vipi Daudi aliupendeza moyo wa Mungu au kujiuliza Daudi alikuwa mtu wa namna gani kiasi cha kufikia kuitwa mtu aliyeupendeza Moyo wa Mungu, ili sisi nasi tuweze kufuata nyayo zake:  Yako mambo kadhaa ya kujifunza kutoka kwa Daudi
1.       Alilipenda Neno la Mungu
a.       Aliipenda sheria ya Mungu Zaburi 119:97 (Sheria ya Mungu ni Neno lake)
b.      Aliliweka moyoni neno la Mungu ili asitende dhambi Zaburi 119:11(Alilifanya kuwa Muongozo wake)
c.       Neno la Mungu lilikuwa ndio faraja yake wakati wa Mateso Zaburi 119:50 (kila tatizo alilisuluhisha kwa kuutafuta Uso wa Mungu)
d.      Neno la Mungu lilikuwa ndio chimbuko la amani ndani yake  Zaburi 119:165
Je wewe unaliweka neno la Mungu moyoni, unalisoma, unalipenda unaliishi unalitafakari? Ni muhimu kulifanya Neno la Mungu kuwa kinga yetu na dawa yetu kwa kila tatizo hata ikiwemo dhambi.
2.       Alipenda kuomba (Maombi)
a.       Alisema nitaliitia jina la Bwana maadamu ninaishi Zaburi 116:1-2
b.      Alitambua kuwa Mungu amembariki na atambariki sana Zaburi 116:12-13
c.       Alitambua kuwa maombi yanamuweka Mungu karibu naye Zaburi 145:18
d.      Yesu pia alikuwa mwombaji Luka 5:16
Je ni kiasi gani tunapenda maombi, je tunaomba bila kukoma kama yanenavyo maandiko je tunajilinda katika maombi?
3.       Alipenda Kumsifu Mungu
a.       Alimsifu Mungu kwa sababu ya haki yake Zaburi 119:164
b.      Alimpenda Mungu kwa sababu ya ukuu wake na wema wake Zaburi 95:1-7
c.       Aliamua kuwa atamsifu Mungu maadamu anaishi Zaburi 104:33
d.      Yesu alipenda kuimba na kumsifu Mungu Mathayo 11:25-26 na 26:30
Je ni kiasi gani unapenda kusifu na kuabudu ni kiasi gani unajishughulisha na kuimba na kusifu na kuabudu?
4.       Daudi alipenda Umoja miongoni mwa watu wa Mungu
a.       Alipenda ndugu wakae kwa umoja aliona inapendeza Zaburi 133:1
b.      Alikuwa na ushirika wa karibu sana na Jonathan 1Samuel 18:1
c.       Alitambua pia uchungu wa migawanyiko katika familia 2Samuel 13
d.      Yesu pia alipenda umoja alituombea tuwe na umoja Yohana 17:20-23 Alikufa msalabani  ili tuwe wamoja Efeso 2:13-16
Je wewe unapenda umoja, unawafanya watu kuwa kitu kimoja au unapendelea watu na kuuvunjavunja mwili wa Kristo? Wako watu wengine leo wanafurahia wengine kupatwa na mabaya, kutengwa na kuwa mbali nao na kuuharibu mwili wa Kristo
5.       Daudi hakupendezwa na njia za uongo
a.       Alichukia uwongo akiwa na ujuzi wa kutosha kuhusu mtazamo wa Mungu Zaburi 119:104
b.      Chuki yake dhidi uongo iliathiri shughuli za uchaguzi wa Marafiki na shughuli zake Zaburi 101:3-4,6-7.
Yesu alichukizwa na uongo na njia zisizo sahii za mafarisayo
Je wewe unachukia njia za udhalimu? Upendo haufurahii udhalimu, ni muhimu kwako kuukemea udhalimu kwa Upendo, bila kumsahmbulia mtu, bali kuishambulia tabia isiyofaa
Biblia inaeleza kuwa Daudi ndiye awezaye kufanya mapenzi ya Mungu yote, Mtu atakayefanya mapenzi yangu yote, alikuwa tayari kufanya yote aliyomuamuru Mungu. Moyo wa Daudi ulikuwa tayari kutimiza kusudi lote la Mungu alilolikusudia. Ni muhimu kuishi Duniani kwa kulitimiza kusudi lote lile ambalo kwalo Mungu ametukusudia

Mkuu wa wajenzi mwenye Hikima
Rev. Innocent Kamote.

Hakuna maoni: