Jumapili, 31 Januari 2016

Mashaka ya Nabii Musa!

Kutoka 3:1-4:17
1. Mungu alipomtokea Musa katika kijiti kilichokuwa na utukufu
a. Alimuita Musa ili kuwaongoza Israel kutoka katika Inchi ya Utumwa Misri
b. Musa alionyesha Mashaka Yake wazi na kutoa sababu zinazodhihirisha kwa nini hafai kwa Kazi hiyo
2. Musa alionyesha Mashaka yake wazi na Bwana Mungu alikuwa akimjibu Musa, Msahaka ya Musa ndio somo kubwa sana kwetu
a. Kwa sababu ni katika nia inayofanana watu wengi sana leo hupewa na Mungu wajibu Fulani na hata wito wa kumtumikia Mungu
b. Si kwaajili ya kuwatoa watu katika utumwa kama ilivyo kwa Musa kule Misri, lakini kwa Ulimwengu kwaajili ya kuwahubiri habari njema Marko 16:15 1Petro 2:9 ili waokolewe
c. Kama ilivyokuwa kwa Musa wengi wetu tunatoa Udhuru na kuonyesha Mashaka, Mashaka ya Musa yanaweza kugawanywa katika maeneo Matano yafuatayo

A. Mimi ni nani? Kutoka 3:11 Musa akamwambia Mungu, Mimi ni nani……
1. Ingawa Musa aliwahi kuishi katika Ikulu ya Farao mtawala wa Misri
a. Sasa alikuwa mchungaji wa mifugo ya mkwewe akiwa mtu duni
b. Miaka 40 ilikuwa imepita tangu alipoondoka kwa Farao
c. Sasa alikuwa mtu mzima mzee wa miaka 80, nguvu za ujana zimekwisha na yuiko na fimbo tu Musa aliweza kuwa na sababu za haki za kufikiri kuwa huenda yyeye si mtu sahii
2. Mungu alimjibu Musa Kutoka 3:12 asiwe na Mashaka kwani yeye atakuwa Pamoja naye
a. Bila shaka mimi nitakuwa Pamoja nawe
b. Mungu anapomuahidi mtu atakuwa Pamoja naye maana yake Yeye mwenyewe Mungu ni Utoshelevu wetu
c. Paulo mtume alisema kama Mungu akiwa Upande wetu yaani pamoja nasi ni nani atakayeweza kusimama kinyumenasi Warumi 8:31
B. Baadhi yetu leo tunatoa Udhuru au kuonyesha Mashaka kama Musa
1. Tunajiangalia wenyewe na kujipima na kuona kwamba hatutoshelezi/hatustahili kwa vigezo vya kuwa watumishi wa Mungu
a. Ni kweli kabisa hakuna mwanadamu anayetosheleza katika utumishi na huduma hii kimsingi hata mimi pamoja na kujiita Mkuu wa wajenzi katika Huduma hii kila siku najigundua kuwa sistahili kabisa kumtumikia Mungu, sio hivyo tu huwa namshangaa Mungu kwa nini anitumia mtu kama mie
b. Lakini Mungu ni Utoshelevu wetu 2Wakoritho 3:5-6 “ Si kwamba twatosha sisi wenyewe kufikiri neno lolote kwamba ni letu wenyewe, bali utoshelevu wetu watoka kwa Mungu, Naye ndiye aliyetutosheleza kuwa wahudumu wa agano jipya”
c. Unaudhuru gani Elimu? Angalia kuwa Mungu aliwatumia mitume ambao wengi wao walikuwa wasio na Elimu Matendo 4:13
d. Kama ilivyokuwa Mungu kwa Musa, Yesu Kristo anakutia moyo leo usiogope atakuwa pamoja nasi hata ukamilifu wa Dahari Mathayo 28:20
e. Kwa msaada wake tutayaweza yote Wafilipi 4:13.
C. Niwaambie Nini? Imekaa vema kwa kimombo what shall I say? Kutoka 3:13
1. Musa alijua kwamba anapaswa kuwaendea Israel, na wako kifungoni wakiwa na maswali lukuki
a. Wangemuuliza Mungu yupi aliye kutuma?
b. Kwa nini tuondoke hapa tumekuweko kwa miaka 400, tumezaliwa hapa haya ndio maisha yetu na tamaduni zetu
c. Ni kama Musa alukuwa akijiuliza ninaanzia wapi?
2. Mungu alilazimika tena kumjibu Musa, mwenye mashaka
a. Mimi niko ambaye niko, Utawaambia Kutoka 3:14-15
b. Mungu alikuwa na majibu kwa Musa kuhusu nini cha kusema
D. Baadhi yetu tunaweza kuwa na mashaka kuhusu nini cha kusema
1. Tuna mashaka kwa sababu wakati mwingine tunafikiri kuhusu maarifa yetu yasotosheleza
2. Lakini Mungu ataweka maarifa na nini cha kusema
a. Atakupa neno rahisi Marko 16:15-16
b. Na ni jinsi gani itakuwa Rahisi 1Koritho 15:1-4,2:2
c. Hata Musa alipokuwa ameelekezwa nini cha kusema akaibuka na sababu nyingine
E. Je wasiponiamini wala kunisikiliza?
1. Musa sasa amepewa Maarifa na anajua nini cha Kusema lakini anawasiwasi hawatamuamini walakumsikiliza?
a. Ni dhahiri kuwa Musa alikuwa anaogopa kukosea
b. Anaogopa matokeo magumu na amesahau kuwa Mungu alisema atakuwa Pamoja naye
2. Mungu alimsaidia Musa kuondoa mashaka na kumuaminisha kuwa yuko naye
a. Fimbo ya Musa iligeuka kuwa nyoka Kutoka 4:2-5
b. Mkono wake ulipatwa na ukoma
c. Maji yaliyogeuka Damu Kutoka 4:9.
F. Wengi wetu tunamashaka na majukumu na wajibu tuliopewa kuutumikia na kwa watu wa Mungu wana mashaka kama wanafaa kuwa chombo cha kuhubiri injili
1. kumbuka woga ni adui anayekuzuia katika kujaribu
2. Kama Mungu alivyomjibu Musa na kuondoa mashaka aliyokuwa nayo tunao ushahidi unaoweza kututhibitishia na kutuondolea mashaka juu ya kile Mungu anataka tukitimize
a. Neno la Mungu liko kwaajili yetu Warumi 10:17, Yohana 20:30-31
b. Yesu alikufa na maefufuka Yuko hai ni yeye anayetenda kazi ndani yetu
c. Migandamizo na kelele kutoka nje isikutie mashaka ukaacha kumuamini Mungu kuwa yu aweza kukusaidia na kuwa yuko pamoja nawe na kuwa vita si yako ni yake yeye na kuwa hata wajibu na kazi tuliyopewa ni kwa utukufu wake.
G. Mimi sio Msemaji, Mimi sio mwepesi wa Kusema!
1. Tunaona mashaka haya katika Kutoka 4:10
1. Musa alisema mimi sio mnenaji Mzuri? Je umeshawahi kuwasikia baadhi ya viongozi wakisema neno mimi sio Mwanasiasa? Unajua wanamaanisha nini? Wao sio wasemaji, sio wazungumzaji wazuri
2. Mungu hasukumwi na Udhaifu wa Mwanadamu anatujua tulivyo hata kabla hajakuita au kukupa wajibu
3. Anaujuzi wa kuwatumia hata waliodhaifu ndio si tuliumbwa kwa kusudi lake uwe na uwezo usiwe na uwezo yeye akiamua anakutumia
a. Mungu alimsaidia Musa kujua Yeye ndiye Muumba ndiye anayeruhusu mtu kuwa Bubu au kuwa msemaji, Mungu alikuwa anaelewa wazi udhaifu wake na kama udhaifu wake ungekuwa ni sababu ya yeye kushindwa kumtumia asingelimfuata
b. Mungu anauwezo wa kumsaidia kila mtu katika madhaifu yake
c. Mungu alimuahidi tena Musa kuwa atakuwa pamoja naye Kutoka 4:11
d. Mungu alimuandaa haruni kwaajili ya kumsaidia Musa Kutoka 4:14-16 Mungu wakati wote ataandaa watu wa kututia moyo na kufanya kazi pamoja nasi.
H. Sisi nasi tunaweza kuwa na mashaka na kutoa udhuru kama huu wa Musa,
1. Paulo mtume Hakuwa na ufasaha wa Maneno wala hekima kama zile za wagiriki, alikuwa dhaifu, mwenye hofu na mwenye kutetemeka sana 1Koritho 2:1-5, Lakini pamoja na hayo alimtegemea Mungu na sio hilo tu aliwatia moyo na wengine
“Imani yetu isiwe katika Hekima za wanadamu bali katika nguvu za Mungu”
Musa aliogopa kuwa mnenaji eti kwa vile alikuwa na Kigugumizi Kutoka 4:13 Mungu hakukiondoa kigugumizi kila japo angeweza kufanya hivyo Mungu alikusudia kumtumia pamoja na udhaifu wake
I. Tuma huyo utakayemtuma! Kutoka 4:13.
Mungu alikubaliana na Mashaka yote ya Musa na kila mashaka yake yalikuwa na Majibu lakini sasa Mungu anakasirishwa na tabia ya Musa wakati huu, Sasa Musa hataki kabisa kwenda!
1. Mungu ametuumba kwa kusudi lake ni lazima tutmika bila kujali udhaifu tulionao kwa vila kila aina ya udhaifu una majibu kwa Mungu
2. Ukikataa kumtumikia Mungu au kulitumikia kusudi la Mungu unajiweka katika wajibu wa kumtumikia shetani
3. Hasira za Mungu kwa Musa zilikuwa za upendo, Mungu alikuwa anataka kumtumia Musa ndiye aliyekuwa amamemuandaa kwa Muda mrefu kwa kusudi hilo
Ndugu zangu
a. Kila udhuru na kila sababu utakayoitoa kukwepa kutokumtumikia Mungu ni Upotoshaji wa haki ya Mungu
b. Ni kweli tungetamani kama Mungu angelimtumia mtu mwingine mbadala
c. Ni kweli hatupendi kutenda kila Mungu anachokitaka
d. Lakini ndugu hapo ndipo hasira za Bwana zinapowaka na kuwa kinyume nasi, hatuwezi kuacha kulitumikia kusudila Mungu wetu hata kama kuna hali zinazokataa endapo hali hizi zimetokea kwetu kutoa udhuru tunahitaji kutubu
Hatimaye!
Wote tunajua kuwa Musa alikubali, wito wa kwenda Misri
Wote tunajua kuwa Mungu alikuwa pamoja naye na kumsaidia
Wote tunajua dhahiri kuwa Musa sasa anaheshimika na kukubalika na watu wote kama kiongozi mkubwa sana wa manabii na baba wa taifa la Israel, Ukiondoa shaka na kumuamini Mungu atakutumia kwa viwango vya juu kwa utukufu wake.
Mungu hatuimii watu maalumu sana, Tunakuwamaalumu Mungu anapokuwa Pamoja nasi
God never use the superman, we became the superman when God is with us
Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima
Rev. Innocent Kamote.

Hakuna maoni: