Jumapili, 31 Januari 2016

BIBI MWENYE KIDONDA NDUGU AKAJA KWANGU!



Nataka kusimulia haya yaliyonikuta kwani nimeona ni heri niyaseme ili nipate ahuheni kuliko kuendelea kuyaweka moyoni na kuendelea kunitesa, Ni baada ya kumaliza elimu yangu ya sdekondari nilijiuynga na chuo cha uhazili, Tabora kwa mafunzo ya ukatibu muhtasi, Nilipata ajira kwenye shirika Fulani hapa nchini, baada ya masomo yangu nilifanya kazi muda mfupi kabla yakupata mchumba na kuolewa, Mume huyu alikuwa ni bosi kwenye kampuni Fulani, nilikuwa siwapendi watu wenye fedha  au wenye uwezo mkubwa kwani wengi wao ni wanyanyasaji ama kwa wake zao au kwa walalahoi, lakini ilikuwa ni tofauti sana kwa bwana huyu hakuwa na tabia za dharau na manyanyaso kama walivyo wengi wenye kipato kikubwa.

 wakati wewe unacheka wako wengine wanalia, wakati wewe unalimbuka na Utajiri wako Masikini

Habari zilifika nyumbani kwetu kuwa nimeolewa na kizito mmoja na kuwa tayari nina mtoto ambaye nilimpata kwa njia ya upasuaji, mama yangu alishitushwa na habari hizo kiasi kwamba alikosa usingizi. Ukweli ni kwamba tuliishi maisha magumu sana na familia yangu kwani baba alifariki nikiwa darasa la kwanza, ilibidi marta nyingi nikatishwe masomo yangu na mama yangu ili kumsaidia kulea wadogo zangu, wakati mama alipokuwa akifanya vibarua mbalimbali, ila waalimu wangu walinipenda sana kwa sababu nmilikuwa najitahidi darasani hivyo walinitia moyo na hata nilipofaulu kwenda shule ya sekondari ya Songea gils kijiji kizima walinichangia,Mume niliye naye tulifgahamiana nikiwa Tabota chuoni, tulikuwa marafiki – wachumba  na hatimaye kuoana, alinisaidia sana kunipa mahitaji muhimu  ikiwa ni pamoja na pesa  wakati nikiwa chuoni. Kosa kubwa nililolifanya kwenye uhusiano wetu ambalo naomba wengine wasilifanye  kama mimi ni kuwa nilumueleza kuwa sikuwa na wazazi, ndugu waka jamaa, wote walikufa na mimi nililel;ewa na uongozi wa kanisa tu, kwa vile huyu bwana alinipenda  na alikuwa na nia ya kweli ya kunioa alinishauri twende kwa mkuuu wa wilaya tukafunge ndoa kisheria.

Kumbe duniani hakuna siri wadaku walipeleka taarifa kuhusu ndoa yangu na kujifungua kwangu mtoto ilibidi mama akope nauli na alisafiri kutoka nyumbani mpaka Dar tulikuwa tunaishi Masaki na mpambe alimleta mama mpaka getini.Nilisikia mbwa wanabweka walibweka sana na kutoa ishara kwamba kuna mtu getini au mgeni, Nilimtuma msichana wangu wa kazi aangalie kuna nani mlangoni  jibu ni kuwa kuna bibi mmoja mchafu,chafu aliyevaa nguo zilizoraruka raruka vipende vipande na aliukuwa amechukua mzigo uliokuwa umefungwa na kaniki na alikuwa na kidonda mguuni, nilishituka sana na kuhisi kuwa ni mama yangu kwani alikuwa na kidonda ndugu, Yule msichana akaniuliza nimfungulie mlango, nilimzuia nikimwambia asubiri kwanza . Wakati nikiwa najishauri kwenda kumuangalia huyo mgeni wa ajabu mara mume wangu alipigfa honi na haraka msichana wangu wa kazi akaenda kufungua geti, Tulishangaa baada ya kuingia na kusimamisha gari alimsalimia Yule mgeni na kumshika mkono na mkno mwingine akashika ule mzigo uliofungwa kwa kaniki akamleta hata sebuleni.

Kumbe bwana alikuwa ni mama yangu mzazi kweli, Mume wangu alifungua kabati langu la nguo na kutoa vitenge, khanga na gaunilangu akampa mama ingawa vilikuwa havimtoshi, alimuongoza mama bafuni, Yuel mgeni baada ya kuoga mume wangu alimsafisha kidonda na kumfunga kasha alikaa naye mezani na kula naye chakula. Wakati hayo yote yanafanyika mimi nilikuwa nimejiinamia kwa fedheha huku nikijilaumu kwa nini nilificha upande wangu wa pili na nilimlaumu mama kwa kuja kwake pale kwangu, Nilisubiri baada ya kumaliza kula ndipo nikapata nguvu ya kumsalimia, lakini aliniitikia bila ya uchangamfu.

Kesho yake mume wangu alimwambia msichana wangu wa kazi amwandaye mama ili ampeleke hospitali ya kazini kwake. Baada ya vipimo akamridisha nyumbani, kwa ujumla suala la mawasiliano lilkatika kwani sikuulizwa lolote na mume wangu na alionyesha uungwana na kumpenda sana mama yangu, Baada ya wiki moja mama alimshukuru mkwewe kwa yote mazuri aliyomfanyia na alimuombea kila la kheri awe na Baraka katika maisha yake na alimuomba amruhusu arudi nyumbani ingawa mume wangu alimuomba asubiri majibu ya hospitali,ili kujua kwamba kidonda chake kinaweza kikawa kansa , lakini mama alikataa na kung’ang’ania kurudi nyumbani. Baadaye aliruhusiwa na tulimkatia tiketi kurudi nyumbani.

Baada ya mama kuondoka looh! Mbona nilikoma, nilichambuliwa kama karanga, siku zote tulizokaa na Yule bwana sikujua kama alikuwa na maneno ya nyodo kiasi kile,kwa kweli niliyataka mwenyewe kwani sikuwa mkweli toka mwanzo na pia nilishindwa kukubali hali yangu ya umasikini iliyonikuza hadi kukutana naye na akanipenda  siwezi kumlaumu sana mumwe wangu ila najilaumu mwenyewe kwani nlijitakia unafikiri ataniamini tena? Kama unafikiri hivyo sizani kama akili zako ziko sawasawa lakini kuna kusameheana na kuchukuliana.

Hakuna maoni: