Jumanne, 26 Januari 2016

SOMO: TUKARUDI MISRI!



Hesabu 14: 1- 4 “Mkutano wote wakapaza sauti zao wakalia; watu wakatoka machozi usiku ule. 2. Kisha wana wa Israeli wote wakamnung'unikia Musa na Haruni; mkutano wote wakawaambia, Ingekuwa heri kama tungalikufa katika nchi ya Misri, au, ingekuwa heri kama tungalikufa katika jangwa hili. 3. Mbona Bwana anatuleta mpaka nchi hii ili tuanguke kwa upanga? Wake zetu na watoto wetu watakuwa mateka; je! Si afadhali turudi Misri?  4. Wakaambiana, Na tumweke mtu mmoja awe akida, TUKARUDI MISRI.

Katika moja ya Matukio yasiyoweza kusahaulika Katika Historia ya Israel ni pamoja na tukio hili linalotajwa kutokea katika Mistari hii tuliyoisoma! Haya ni moja ya maneno yaliyotamkwa na watu waliokata tamaa, Hakuna jambo baya sana Duniani kama Kukata tama, watu wanapokata tamaa huweza kufanya lolote na kutamka lolote hiki ndicho kilichotokea hapa!

·        Misri lilikuwa ndio taifa la kwanza lenye jamii yenye maendeleo makubwa sana “Civilization”
·        Kihistoria jamii ya wamisri ilikusanyika kwa wingi kutokana na kukua kwa jangwa la sahara kati ya mwaka wa 7000 mpaka wa 5000 (K.K.)kabla ya Kristo
·        Jamii ya watu waliokusanyika waliweza kuwa na maendeleo makubwa sana kutokana na matumizi ya maji ya mto Nile kwa kilimo na umwagiliaji
·        Bonde la mto nile lilikuwa na rutuba ya kutosha kutokana na kutiririka kwa mbolea toka Ethiopia na maeneo mengine yenye asili ya mto nile

·        Kutoakana na kuwepo kwa rutuba hii kuliwafanya watu wengi kufanya makazi ya kudumu pale Misri na kukawa na maendeleo makubwa katika sekta ya kilimo
·        Misri ilianza kuwa taifa kamili kutokana na kuweko kwa jamii mbalimbali na falme ndogondogo zilizoungana na baadaye kuwa na mataifa makubwa mawili yaani Upper Egypt na Lower Egypt au Delta Nile maendeleo haya yalitokea karne nne kabla ya Kristo, mwaka wa 3200 baadaye falme hizi mbili ziliungana na kuwa ufalme mmoja chini ya watawala waliojulikana kama farao
·        Kutokana na ugunduzi wa chuma uliokuweko miaka mingi wamisri waliweza kuendeleza teknolojia ya vifaa mbalimbali kwa kilimo huku wakiwa na kiu ya ujuzi na maarifa na sanaa na taaluma mbalimbali, Misri ilipata neema ya kuwa na watu wengi, Uongozi imara na kukua kwa maarifa, wamisriwalikuwa na maarifa makubwa ambayo mengina yanatumika na ulimwengu huu wa leo tulio nao:-
*      Kulikuwa na ujuzi wa kuandika katika magombo ya karatasi ziitwazo “papyrus”
*      Walikuwa ndio watu wa kwanza kugundua na kutumia kalenda yenye siku 365
*      Walikuwa na ujuzi wa maswala ya nyota na unajimu
*      Uwezo mkubwa wa uhandisi na ujenzi kwa kutumia Mawe na ujuzi wa kutumia shaba na dhahabu, walikuwa na ujuzi wa Mathematics na Geometric
*      Wamisri walikuwa hodari katika maswala ya upasuaji na utabibu na hata kutunza maiti isiozekwa muda mrefu
*      Tawala za kisiasa zenye nguvu za kifarao ambazo zimedumu kwa zaidi ya miaka 3000 inasemakena ya kuwa Misri ndio taifa lililojiunda katika mfumo wa taifa na maendeleo kwa muda mrefu zaidi kuliko yote duniani
*      Kutokana na utaalamu huo waliweza kuwa na Jeshi kali lenye silaha na ujuzi wa kutumia farasi na wanyama wengineo
*      Utawala wa farao inaaminika kuwa ulidumu kwa miaka 3200 KK mpaka 352KK, kabla ya Kristo.
*      Hata hivyo kiroho Misri waliabudu miungu mingi sana miungu mikuu ilikuwa karibu kumi na Pharao mwenyewe na ukoo wake alihezabika kama uzao uliotoka kwa Mungu hivyo farao alikuwa Mungu
Pamoja na nguvu kubwa waliyokuwa nayo taifa Hili Mungu alilipigilia mbali na kuwaokoa watu wake, lakini katika namna ya kushangaza sana Israel wanagoma kuingia kanaani baada ya muda fupi tu kwa sababu ya habari za kukata tamaa walizozisikia toka kwa wapelelezi 12  Hesabu 12:26-31. Israel wanavunjika moyo na Mungu anakasirishwa sana na jambo hili na hivyo iliwachukua miaka 40 sasa kuimaliza safari kwa kuzungushwa Jangwani!
Kwa nini Mungu alikasirishwa sana
1.      Walimfanya Mungu aliyewaahidi kuwa atawapa inchi ile kuwa ni Muongo
2.      Walishindwa kukumbuka Fadhili na utendaji wa Mungu jinsi alivyowafanyia mambo makubwa sana
3.      Waliangalia taarifa ya wengi wakasahau taarifa ya wachache Mungu sio Mwanademokrasia utawala wake unaitwa “THEOCRASY”
4.      Waliona kuwa tatizo lililoko mbeleyao ni kubwa Kuliko Mungu
5.      Walisahau kuwa uko uwepo wa Mungu pamoja nao na kuwa Mungu hakuwaacha
6.      Walishindwa kumuamini Mungu na kuogopa kile kilichokuwa kinawaogopa
Yoshua 2:1-3, 8-11
Siku zote unapotaka kusonga Mbele kamwe usikae na watu waliakata tamaa, fanya lako ambalo unajua Mungu amekusudia ulifanye!
Mwamini Mungu!, angalia historia ya yale ambayo Mungu alikufanyia
Acha kuangalia mazingira Magumu au ukubwa wa changamoto zako bali angalia Ukubwa wa Mungu wako!

Hakuna maoni: