Alhamisi, 28 Januari 2016

JINSI YA KUSTAWI KAMA MTENDE.(Flourishing like a palm tree)



Zaburi 92:12-15.

     Nyakati hizi tulizo nazo kumekuwepo na wimbi kubwa sana na shauku ya watu kutakakufanikiwa,   na watu wengi sana wanafanikiwa kwa vile wana nia ya kufanikiwa, hata hivyo, mafanikio ya watu wengi sana hustawi kwa muda mfupi na baada ya muda hufilisika na kuishiwa kabisa au kubakiwa na historia ya jinsi walivyofanikiwa!

     Mungu katika mapenzi yake anataka tufanikiwe sana, lakini zaidi anataka tufanikiwe na mafanikio yetu yaweze kudumu kizazi na kizazi, Biblia inapozungumzia ustawi wa kudumu inazungumzia miti miwili yaani mtende na Mwerezi wa Lebanon, hii ni miti inayotumiwa na biblia kutufundisha mafanikio ya kudumu, lakini katika somo hili leo tunauangalia zaidi MTENDE tutajifunza somo hili kwa kuzingatia vipengele vitatu vifuatavyo

                                                                          Mtende!


  • ·         Ufahamu kuhusu mti wa Mtende
  • ·         Mambo ya kujifunza kutokana na Mtende
  • ·         Jinsi ya kusitawi kama Mtende.


Ufahamu kuhusu mti wa Mtende.

Kwa kawaida miti jamii ya mitende iko Mingi sana, kuna jamii zaidi ya 2600 ya mitende, lakini iliyo maarufu ni miwili, acacias palm tree na coconut palm tree kwa msingi huo miti jamii ya minazi ni jamii ya mitende, Mawese ni jamii ya mitende. Kama utataka kujua kwa undani kuhusu miti hii unaweza kutafuta google Palm tree/Wikipedia. Kwa Kiaramu na Kiethiopia mtende unaitwa “TAMAR” Kiarabu “Date” na wengine huiita Phoenix.

Mti huu katika Biblia umetajwa kama moja ya miti Maarufu sana ambao hutumika kuelezea Ushindi, amani na Ustawi. Katika Israel mti huu huhesimika sana na unatumika kama moja ya nembo ya Taifa ukihusihwa na Taa ya vinara Saba. Biblia inautaja mti huu kwa sababu ya mafundisho kadhaa
1.       Ushindi na amani na Ustawi  Kutoka 15:27  watu wa Mungu waliburudika baada ya Ushindi
2.       Ni Malimbuko ya Canaan Mji wa kwanza kupewa na Mungu kwa Israel Yeriko ulikuwa na mitende mingi sana na uliitwa mji wa mitende Kumbukumbu 34:1-3, Waamuzi 1:16
3.       Mtende unazungumzia Faraja na furaha na kurejeshwa 2Nyakati 28:15
4.       Katika Biblia kama mtende umekauka ilihesabika kuwa Furaha imeondokwa kwa wanadamu Yoeli 1:10-14 na ilihitajika maombi na toba kurejesha furaha hiyo
5.       Mitende ilitumika kama mapambo na sifa ya uzuri 1Falme 6:28,32, wimbo bora 7:7
6.       Ni alma ya Ushindi wa sasa na ujao Yohana 12:12-12, Ufunuo 7:9-10

Mambo ya Kujifunza kutoka na Mtende.
1.       Jamii ya mitende ni miti inayostawi popote na hustahimili ukame Inazungumza kuhusu Uvumilivu.
2.       Miti jamii ya mitende haina muda wa kubughudhi miti mingine, inakua kuelekea juu
3.       Mitende Haiweki kinyongo inapukutisha Majani ya zamani na kuzalisha Mapya Inazungumzia kusonga mbele bila kujali ni magumu gani unayapitia
4.       Miti ya mitende inawafanya watu waangalie juu, inakumbusha kuabudu, inaelekeza kwa Mungu inakumbusha watu kumtegemea Mungu.
5.       Mitende inawapa watu Burudani, inawapa watu makazi, inafunika inazungumzia Amani
6.       Miti mingi ya mitende Imenyooka Straight,Upright Inazungumzia Unyofu wa Moyo,Ayubu 1:1 na Joshua 1:7-10

Jinsi ya Kustawi kama Mtende
1.       Ishi maisha ya Haki, unaweza kujiuliza mtu wa haki ni Mtu wa namna gani
a.       Hawana muda wa Kuaibisha wengine Mathayo 1:19
b.      Hukaa katika maagizo ya Bwana bila lawama Luka 1:5-6
c.       Anakuwa Mcha Mungu Luka 2:25
d.      Utamtegemea Mungu katika hali zote ziwe njema au mbaya na hatima yako ni suhindi
Warumi 8:33-39. (Yesu alipoingia Yerusalem alishangiliwa kwa matawi ya miti ya mitetende kumaanisha Ushindi, utawala na Amani ya Mungu wa Kweli)
Mwisho wa Yote, Utaishi Maisha Marefu, ukiwa na Matunda wakati wote, na hutayumbishwa na upepo wakati wote bila kujali ukame au mvua utazaa matunda na haya ndio mafanikio ya Mtende.

Hakuna maoni: