Jumapili, 31 Januari 2016

MZEE NIKAMWAGA SERA!



Ilikuwa ni mwaka 1998 nikiwa kidato cha pili jijini Dare es salaam, Nakumbuka nilikuwa napedna  sana kucheza soka na vijana wenzangu mtaani, katika mtaa tuliokuwa tukiishi kulikuwa na kiwanja  hakijajengwa nyumba bado, kiwanja hiki ndicho tuilichokuwa tunakitumia kwa michezo , kwemye timu niliyokuwa niiichezea nilikuwa na rafiki ambaye hatukuwa tunasoma shule moja  lakini wakati wa kujisomea nilikuwa nikienda kwao tukisoma pamoja  na kusaidiana  kimasomo,kwani yeye alinizidi kidato kwa kuwa mama yake alikuwa mwalimu alipenda kutusisitiza kimasomo.

                                                       Nkrumah Hall Chuo kikuu cha Dar es Salaam


Rafiki yangu alikuwa na wadogo watatu, wawili wakiwa ni wasichana na mmoja ni mvulana, lakini huyo msichana huyo msichana alikuwa kidato cha tatu kama kaka yake kwa kweli dada wa rafiki yangu aluikuwa ameumbika ajabu, Katika kipindi chote  nilipokuwa nikifika pale kwa rafiki yangu kujisomea  nilikuwa nimevutiwa sana na huyu dada yake,nilijikuta namtamani hali ambayo tumezoea kuiita kupenda, wakati wa kujisome ukifika tulikuwa tukisoma pamoja  sebuleni lakini ikifika saa mbili yuel rafiki yangu alikuwa akitumwa kwenda kununua mayai kwani ni biashara amboyo mama yake alikuwa akiifanya basi hapo ndipo ilikuwa nafasi  ya kupata muda wa kuongea na yule dada wa rafiki yangu.

Ilikuwa ni ngumu kunielewa awali kwani hakutegemea wala kuamini kuwa ningeweza kumtamkia maneno kama yale, lakini siku zilivyozidi kwenda niliendelea kumsumbua, ni afadhali angenipa jibu la ndiyo au hapana, badala yake aliamua kujifanya nataka – sitaki. Mimi matumaini yangu yakaongezeka siku zikapita kwa kasi huku nikizidi kumsomea mtoto sera zangu za upendo wa dhati.
Siku moja kama kawaida yangu nilipofika pale nyumbani kwaajili ya kujisomea nilimkuta dada Yule wa rafiki yangu akiwa peke yake mezani, kidume nikaanza kujitutumua mzee nikwamwaga sera ! huku Yule dada akiwa bize akipekua kurasa za daftari baada ya kumaliza kusema hovyo kwangu aliniuliza umemaliza? Mimi nikamjibu ndio, mara nikasikia akimuita kaka yake atoke chumbani kwake kwani chumba kilikuwa karibu na sebule, mara akatoka Yule rafiki yangu sura amaikunja na kuniuliza kama kile ndicho kilichonileta pale kwao. Nilikuwa kama nimeloweshwa maji,

Bila kuuliza huku nikiwa natetemeka nilichukua kila kitu kilicho changu na bila ya kuaga mtu hadi leo sijakanyaga nyumba ile nasikia Yule dada yuko chuo kikuu kwani walikuja kuhama mtaa ule nilioishi kwa kweli anastahili kwenda chuo kikuu. Unagoja nini sasa we huoni kuwa ni fedheha hii?.misikio mipana kama tembo

Hakuna maoni: