Jumanne, 26 Januari 2016

MFULULIZO WA MASOMO YAHUSUYO UTETEZI WA IMANI (APOLOGETICS) 4



UKIRI WA IMANI YA MITUME.
a.       Maendeleo ya kuweko kwa Ukiri wa Imani
 Ukiri wa zamani zaidi wa imani katika kanisa la mapema uliitwa imani ya mitume kwa ujumla haukuandikwa na mitume  lakini ulikuwa ni mkusanyiko wa kiini cha mafundisho yao na ulikusanywa kwa mara ya kwanza kati ya mwaka 140 na ulikuwa ukitumika kama Katekisimo (Catechism) kwa kila mtu mara anapokuwa anakaribia kubatizwa kama ukiri wao wa imani
§  Kumuamini Mungu lilikuwa swala la asili kwa Wayahudi na Wakristo kwa msingi huo kumkiri Kristo katika ukiri wa imani  kulitofautisha kati ya Ukristo na Uyahudi na ubatizo ulikuwa ukifanyika kwa jina la Yesu kama ilivyokuwa katika kitabu cha Matendo ya Mitume
§  Hata kufikia mwaka 200 A.D. wale waliokuwa wanataka kubatizwa walikuwa wakiulizwa swali Unaamini? Baaday ilibadilishwa na hata ilipofikia Karne ya 12th C ilifikia hatua ya juu  na kukubalika  kwamba anayebatizwa ni muhimu kukiri ukiri wa imani uliosema hivi 

Namwamini Mungu Baba mwenyezi Muumba wa mbingu na Nchi na Yesu Kristo mwana wake wa pekee Bwana wetu aliyechukuliwa mimba kwa uweza wa Roho Mtakatifu akazaliwa na Bikira Mariam, aliyeteswa zamani za Pontious Pilato akasulibiwa, akafa akazikwa siku ya tatu akafufuka akapaa mbinguni ameketi mkiono wa kuume wa Mungu baba, toka huko atakuja tena kwa utukufu kuwahukumu watu walio hai na wafu na ufalme wake ahauna mwisho, Namwamini Roho MtakatifuKanisa takatifu la Kikristo,Ushirika wa watakatifu Msamaha wa dhambi,ufufuo wa mwili na uzima wa ulimwengu ujao Amen.”

HISTORIA YA BISHANO KUHUSU UTATU WA MUNGU.
Kuenea kwa injili ulimwenguni hususani kwa mataifa kunaifanya injili kuwafikia Wayunani nao wanakuwa sehemu ya kanisa wasomo, watu wenye uwezo wa kufikiri, wanasheria na kadhalika sasa wanaingia kanisani na kuchanganua mambo.
Justin Martyr 100-165.
-          Alikuwa mwanafalsafa kutoka Samaria ingawa wazazi wake waliishi Rumi Kama mwalimu aliuona Ukristo kama Una kitu cha ziada kuliko falsafa  na hivyo aliamini na kuokoka
-          Alifundisha kuwa Yesu ni mwana wa Mungu aliyeumbwa na Mungu kabla ya uumbaji, kwa msingi huo kabla ya hapo Mungu alikuwa peke yake ndani ya Mungu kulikuwa na Neno Logos, kwa hiyo Yesu ni mdogo kwa Mungu na anapaswa kumtegemea Mungu, kwa sababu ya msimamo huo Justin aliuawa mwaka 165 wakati wa utawala wa Marcus Aurelius huyu alikuwa mwana apolojetic wa kwanza.
Turtulian 160-220
-          Alikuwa mtetezi wa imani kutoka Misri.
-          Ibu la tatizo alilokuwa nalo Justin lilitatuliwa na mwanatheolojia huyu alikuwa mtu kutoka Carthage na alikuwa msomi alkuwa mwana Montanists alikazia utakatifu na kukemea udunia ndani ya Kanisa katiliki
-           
-          Alifundisha kuwa Baba na Mwana wanashiriki uungu mmoja na ni nafsi tofauti zikiwa na kazi maalumu hata hivyo alitoa nafasi ya Pili kwa mwana kuwa sio wa milele
-          Alisema Baba na Mwana na Roho Mtakatifu ni Mungu mmoja  na kila mmoja ni nafsi na huu ndio ukawa mwanzo wa msingi wa fundisho hili la utatu kuja kukubalika wakati wa mkutano wa Nicea.

MKUTANO MKUU WA NICEA NA TAMKO LA IMANI (IMANI YA NICEA).
-          Nicea ni moja ya miji katika inchi za asia ndogo
-          Mnamo mwanzoni mwa Karne ya Nne moja ya fundisho muhimu sana liliinuka na kuleta Utata miongoni mwa Kanisa, mijadala iliinuka kupitia wanatheolojia  wakubwa na wenye nguvu, pia kukiwa na utetezi wenye nguvu na mawazo mbalimbali  yaliyopelekea kuitishwa kwa mkutano wa Nicea
a.       Arius wa Alexandria  256-336
Alikuwa ni kiongozi mkubwa wa imani ya Kikristo na mwanzilishi wa imani ya Arianism moja ya imani potofi iliyokuwa inapinga uungu wa Yesu Kristo, Arius alikuwa mwana theolojia aliyesomea huko Antiokia (Antakya ya Leo huko Uturuki) alijifunza theolojia chini ya Msomi aliyejulikana sana aliyeitwa Lucian na huenda ndiko alikotoka na fundisho hilo alijulikana kwa kusisitiza maswala ya kihistoria na njia zanye kujenga na kuzalisha za kidini pamoja na maswala ya utafiti kuhusu umoja wa Mungu na Utatu mtakatifu shule yake ilijulikana pia kama shule iliyokuwa ikimuona Kristo kama  yuko chini ya Mungu Baba,.
Arius alizaliwa Afrika na alikuwa mwangalizi wa Kanisa la Alexandria nchini Misri, alikataa kuweko kwa ushirika wa milele kati ya Yesu na Mungu usemi wake maarufu unasema “kuna wakati ambapo Yesu Hakuweko”na kuwa Mungu alimpitisha Yesu kuwa mwana wake baada ya ufufuo wake na kumpa baadhi ya majukumu ya uungu alisema Yesu alikuwa na mwili wa kibinadamu lakini hakuwa na Nafsi ya Kibinadamu na hivyo hakuwa Mungu wala hakuwa mwanadamu wa kawaida Yuko mahali Fulani hapo katikati.
b.      Athanasius
Mtakatifu Athanasius aliishi kati ya mwaka wa 293-373 B.K. Ni mwanatheolojia mkubwa wa Kikristo na Doctor wa Kanisa Pia alikuwa Askofu ni miongoni mwa watu walioshindana na kusababisha kuundwa kwa Orthodox katika karne ya 4 akishindania imani dhidi ya Arianism alisimikwa kuwa shemasi akiwa kijana  akitumika kama Katibu wa askofu wa Alexandria na ndipo alipopata nafasi muhimu ya kitheolojia ya kuongoza mapambano dhidi ya fundisho la Arius ambalo lilijadiliwa katika mkutano wa Nicea mwaka wa 325 na kwa ujumla alikuwa na nguvu ya ziada ya kupambana na imani hiyo na aliweza kueleza sawia kuwa mwana wa Mungu Yesu Kristo ni sawa na Mungu Baba  ingawa Arius aliendelea kudai kuwa sio sawa kwani Yesu ni kiumbe tu aliye mkamilifu kuliko viumbe wengine na kuwa alitumiwa na Mungu katika uumbaji na kazi nyingine za uumbaji.
Mijadala hii ilipelekea kuzuka kwa mjadala mkubwa kuhusu Utatu wa Mungu mjadala huu ulikuwa umekita miguu yake katka kutaka kujua kuhusu Uungu wa Yesu kwamba je Yesu I Mungu? Na kuna uhusiano gani kati ya Roho na Mwili wa Yesu Je Mungu ni Watatu au mmoja? Na wana uhusiano wa aina gani?

KUITISHWA KWA MKUTANO MKUU WA KWANZA WA NICEA MWAKA 325
Mkutano huu uliitishwa wakati wa Utawala wa Constantine ambaye alifuatilia kwa ukaribu sana mjadala mzima wa maswala ya utatu na uungu wa Yesu ingawa Lengo lake la kuitisha mkutano huu lilikuwa la Kisiasa zaidi yaani katika kuhakikisha kuwa Himaya yake inakuwa na amani aliitisha mkutano huo 19th June 325 mpaka Augosti 25th ni mkutano wa siku kama 67 maaskofu wapatao 300 walihudhuria wengi wao wakiwa ni kutoka Msahariki.




Constantine the Great

Mfalme Constantine mkuu alikuwa Mtawala wa Kwanza wa Kirumi aliyeokoka wakati wa utawala wake, mwanzoni aliwatesa wakristo lakiini baadaye akawa mkristo, alipokuwa Mkristo aliruhusu uhuru wa kuabudu alitoa eneo kubwa sana Estate na zawadi nyinginezo kwa Kanisa alistawisha mji mkuu jimbo la Mashariki na kuliita kwa jina lake Constantinopple ambao kwa sasa unaitwa Instanbul huko Uturuki, aliitisha mkutano mkuu wa Nicea mwaka 325

Mjadala mkuu katika mkutano hu ulikuwa ni kuhusu Fundisho la Arius kuhusu Asili ya Kristo kwamba je ni mwana wa Mungu na kuwa si sawa na Mungu na kuwa aliumbwa na kuwa yuko chini ya Mungu Baba
Neno kuu lilkuwa ni neno la kilatini Homo-Ousios yaani wa wa aina moja Jambo ambalo Arius alikuwa akilipinga
Hitimisho la Mkutano huo lilikubaliana kuwa fundisho la Arius ni la Uzushi na wazo la kuwa kuna wakati mwana hakuwako lilikataliwa na pia swala la kuwa aliumbwa kwanza kabla ya viumbe vingine lilikataliwa na Tamko la Nikea lilikuwa hivi
  “Tunamwamini Mungu Baba Mwenyezi Muumba  wa kila kinachoonekana na kisichoonekana  na Bwana mmoja Yesu risto Mungu kweli kutoka katika Mungu kweli Mwana wa azali asiyeumbwa mwenye uungu mmoja na Baba  ambaye kwa Yeye vitu vyote viliumbwa vya mbinguni na vya Duniani”
Na hii ndio ikawa imani liyonyooka Orthodox, swala la Utatu lilikubalika kwa maneno kama hayo kuwa wote ni ungu katika umoja, Mkutano wa Nicea ulikubaliana kutoa tamko moja ambalo baadaye lilithibitisha katika mkutano wa Constantonople mwaka 381 na hivyo imani ya Arianism ikawa imefikia mwisho katika utawala wa kirumi kwa sababu ya imani iliyonyooka Orthodox.

MASWALA BAADA YA MKUTANO WA NICEA
-          Baada ya mkutano wa Nicea Ukristo ulifanywa kuwa dini ya kitaifa kwa utawala wa Rumi  wakati huu kuliinuka maswala kadhaa yaliyopelekea kanisa  kuwa dhaifu na kulikuweko na mafundisho kadhaa ambayo yaliingizwa na wanadamu zikiwemo baadhi ya Sacrament
Saint Augustine wa Hippo Afrika ya Kaskazini (354-430).
Mtakatifu Augustine, alizaliwa huko Souk-Ahras, Algeria, mwaka 354 A.D.  Ndiye aliyeleta mpangilio wa kifaklsafa wa theolojia ya Kikrisro (a systematic method of philosophy to Christian theology). AugustineAlikuwa mwalimu huko rhetoric mji wa zamani katika miji ya in Carthage, Rome, na Milan Kabla ya kubatizwa na kuwa Mkristo mwaka 387. Alijadili Maarifa kuhusu kweli na kuhusu kuweko kwa Mungu kulimvuta Karibu na Mungu na Biblia na kutoka kwenye Falsafa za kizamani za kiyunani alikuwa mwanasheria wa Roman Catholicism, Augustine aliendeleza mafundisho mengi alipokuwa akijaribu kutatua migogoro mingi ya kitheolojia. Ikiwemo imani za Donatism na Pelagianism, imani kubwa mbili za kizushi zilizokuwa zikiendelea wakati ule.




 Saint Augustine

-          Ni mmoja wa Mababa wakubwa wa kilatini na Daktari wa Kimagharibi wa Kanisa alikuwa Askofu wa Hippo
-          Alizaliwa November 13th mwaka 354 huko Tagaste, Numidia kwa sasa (Souk-Ahras Algeria) Baba yake Paticius alifariki mwaka 371 alikuwa mpagani lakini baadaye aliokoka lakini mama yake Monica alikuwa mkristo aliyejitoa sana  na aliyemsaidia mwanae na hatimaye kukubalika katika kanisa la Roman Catholic, alisoma kati ya umri wa miaka 15-30 huko Madura na Cathage, baadaye aliishi na mwanamke ambaye jina lake halikujulikana kati ya mwaka 372 na alimzalia mwana wa kiume aliyempa jina Adeodatus jina la kilatini lenye maana ya Zawadi ya Mungu
-          Aliishi maisha rahisi naya kimonaki maandishi yake yaliliathiri kanisa  hata katika nyakati za leo
-          Alifundisha kuwa dhambi inatokana na asili ya uovu uliorithiwa kutoka kwa Adamu kwa neema ya Mungu  asili ya dhambi inaweza kuondolewa kwa wale walioandikiwa kuurithi uzima wa milele lakini neema hiyo si kwa wale walioandikiwa kutokuurithi uzima wa milele
-          Fundisho hilo ndio uliokuja kuwa msingi wa mafundisho ya John Calvin, Presybyterian na Baptist katika miaka ya baadaye.
Pelagius aliishi kati ya Karne ya nne na Tano (360? - 420?)
-          Alikuwa mwanatheolojia wa Kiingereza (Romano-British) na mtawa aliyekuja Rumi kati ya mwaka 410, Yeye hakukubaliana na fundisho la Augustino kwa kudai kuwa kila mwanadamu ana utashi Free will na kwa utashi wake aweza kuamua kuokoka au kukataa alikataa juu ya dhambi ya asili kutoka kwa Adamu kuwa ndiyo inayotuamulia alisisitiza kuwa ni utashi ndio unaotuamulia kufanya mema au kufanya uovu
-          Alisisitiza kuwa Yesu alitusaidia kwa kuonyesha mfano namna ya kuupata wokovu lakini matendo ya mwanadamu  ni ya lazima
-          Fundisho la Pelegius lilihukumiwa katika mkutano wa Cathage mwaka 415 na kutangazwa kuwa ni Uzushi na Pope na Mtawala wa Rumi  na fundisho la Augustino lilikubalika kuwa Orthodox mpaka wakati wa Arminius wa Uholanza na John Wesley wa Uingereza.
MKUTANO WA EFESO AD – 431
-          Bishano lingine lilizuka kati ya watawa  wa ki Nestorian, Mababa wa mashariki Constantinople na ki cyxill Mababa wa Alexandria  kuhusu  asili mbili za Kristo Uungu wake na Ubinadamu wake
-          Nestorius alikazia kupita kawaida ubinadamu wa Yersu na kukataa mafundisho kuwa  Mariam ni “theotokos”neno la kiyunani ambalo maana yake ni Mama wa Mungu yeye aliweka wazi kuwa Mama wa Yesu maana yake ni Mama wa mwanadamu Kristo Yesu tu
-          Mkutano wa Efeso ulihukumu fundisho hilo la waanestirism na kumpeleka utumwani Misri jangwani mwaka wa 435.
MKUTANO WA CHALCDON – 451 A.D.
-          Bishano la wa Alexandria na wa Constantinople halikuishia pale kwani mababa wa ki konstantinople waliendelea kusisitiza kuwa Kristo ana asili moja tu baada ya kufufuka na asili hiyo ni ya kiungu tu
-          Huu ulikuwa ni moja ya mikutano ya kanisa ya kihistoria ambapo kanisa liliketi kushughulikia migogoro unaohusu kuilewa asili ya kweli ya Yesu, Mkutano huu ulifanyika kati ya October 08, 451 - November 01, 451 Fundisho lilianzishwa na Bynzantine mtawa wa ki Eutiko walioamini katika Monophysitism ambayo ilikuwa ikisisitiza kuwa asili ya Kristo ni Mungu na sio mwanadamu, fundisho hilo lilitangazwa kuwa ni Uzushi uamuzi ulipelekea kanisa la Kimisri kugawanyika miongoni mwa waliokuwa wakiamini hivyo.
Rev. Innocent Kamote
Mkuu wa wajenzi Mwenye Hekima

Hakuna maoni: