Jumanne, 26 Januari 2016

Umuhimu wa tiba ya Kukanda mwili ( Massage)




Ni muhimu kuwa na ufahamu kuhusu tiba maalumu ya kuukanda mwili ambayo kwa lugha ya kitaalamu hujulikana kama Massage au Massaging therapy, Jambo hili sio starehe kama wengi wanavyofahamu na wala sio anasa au dhambi, ni kwa sababu watu wengi hawana ufahamu wa kutosha kuhusu swala hili, ama kwa sababu linafanyika katika vilabu, baadhi ya viwanja vya ndege kwenye saloon na kadhalika tena kwa malipo, wengi wamefikiri kuwa hii ni Biashara ya anasa na huenda inafanyiwa watu wenye kupenda raha au starehe na wakati mwingine imedhaniwa kuwa ni dhambi kutokana na mazingira ya wanaotibu na pale watu wanapotibiwa na wale wanaozifanya wakiunganisha na tabia za kishetani za ufuska na sitaki kuunga mkono wafanyao hayo na huko lakini nataka kuweka siri hii wazi ili kuisaidia jamii kama Mkuu wa  wajenzi mwenye hekima


Tiba ya kukanda mwili (Massage) ni nini?
Kwa ujumla kuukanda mwili ni tiba inayohusu, kusugua kubonyeza ngozi pamoja na misuli na viungo kadhaa vya mwili, hii ni tiba yenye faida kubwa sana katika mwili na maisha ya Mwanadamu, shetani ameifanya yak wake ili apate nafasi ya kuiba na kupokonya siri zinazoweza kuwasaidia watu wa Mungu Massage licha ya kuzuia uwezekana wa kupata kansa pia inazuia uwezekano mkubwa wa kupooza au ugonjwa wa kiharusi stroke
Aina za ukandaji (Massage)
1.       Kukanda kwa kiswideen (Swedish Massage) hii ni aina ya kuukanda mwili kwa kuupigapiga kwa nguvu au kutetemesha mfano wa wachezaji wa mpira wanapokuwa wamekamatwa na misuli mtu mwenye ujuzi wa hili anaweza kkupigapiga na kwa kutetema na kuuzunguka mwili mzima na hivyo kuupa nguvu mwili na kuufanya usiwe na maumivu na huondoa uchovu
2.       Ukandaji wa ndani zaidi
Ukandaji huu hufanyika polepole na kwa kundamiza zaidi sehemu zenye misuli na viungo ili kwa kawaida kusaidia misuli isiweze kupata uharibifu
3.       Ukandaji wa kimazoezi (Sports Massage) huu ni ukandaji sawa na ule wa Kisweeden ambao hufanyiwa watu wanaoshiriki michezo kama bondia, Mpira kukimbia nk, kwa kusudi la kuleta utulivu wa misuli na kuipoza kutokana na majeraha ya kimichezo au mazoezi magumu
4.       Trigger point Massage ukandaji maalimu katika eneo maalumu lililojeruhiwa hii hufanyika kama sehemu ya kutibu eneo hilo
Faida za Ukandaji.
Ukandaji ni moja ya tiba muhimu baridi na tiba mbadala na njia ya kuepuka kemikali mwilini pia imekuwa ikitolewa kama tiba kamili pamoja na madawa, imebainika kuwa ni tiba kamili na yenye uwezo mkubwa wa kuondoa Uchovu na migandamizo stress na kuondoa maumivu ya misuli katika mwili na misuli iliyoumizwa wakati utafiti zaidi ukiwa unaendelea kuhusu tiba hii tayari maswala kadhaa ymabainika kutibiwa na tiba hii mbadala
1.       Kuondoa maumivu ya kichwa
2.       Mashaka na hofu au wasiwasi
3.       Kuondoa stress au migandamizo na athari zake
4.       Kuondoa maumivu ya misuli
5.       Kulainisha ngozi na kuzipa mazoezi cell za mwili
6.       Kuondoa uchovu na maumivu kwa mishipa ya fahamu
7.       Kuondoa maumivu yatokanayo na michezo na majerhaha au maumivu ya muda
Huko china tiba hii hufanywa na zaidi kwa wazee kwaajili ya kuwakinga na Kansa na stress lakini pia humpa muda mgonjwa wa kansa na kuongeza muda wa uhai, wajukuu wengi huwakandakanda wazee wao kila wanapokutana nao au nwanapoketi au wakiwa wamerudi kutoka matembezi ili kuondoa stress na kuwafanya wajisikie huru
Tahadhari kuhusu tiba ya kukanda
Pamoja na tiba hii kuwa ni yenye uwezo wa kuwafaa watu wengi sana ni muhimu kufahamu kuwa watu wafuatao haitawafaa
1.       Wenye kutoka damu au wenye kuchuruzikwa na damu bila mpangilio
2.       Wenye vidonda vibichi na vilivyo wazi au majeraha yaliyo wazi
3.       Wenye shida ya mishipa ya vein
4.       Waliotenguka au kupata nyufa katika mifupa
5.       Ukandaji pia haupaswi kuwa wenye kusababisha maumivu au usioleta faraja sema mara moja ikiwa ukandaji huounakusababishia maumivu na haupati kile unachokitarajia ni katika hatua chache wakati mwingine tiba hii huweza kusababisha  umwagikaji damu kwa ndani au kuharibu fahamu kama haitafanyika vema na au allege Nzio kama utatumia mafuta ya kulainisha ambayo hayapatani na anayetibiwa
Onyo:
Massage inaweza kufanyika Nyumbani kwako kama utawaelekeza vizuri wale wanaokuzunguka na wakupendao na kukutakia mema, wale ambao huenda saloon na vilabuni wana matatizo ya kisaikolojia na wanahitaji wokovu! Mada na Mkuu wa Wajenzi mwenye hekima. Rev Innocent Kamote.

Hakuna maoni: