Jumanne, 26 Januari 2016

JAMAA AKAANZA KUPONDA HASA.

Imepita miaka mine sasa tangu nilipopatwa na mkasa huu , wakati huo nilikuwa mkoani ambako nilikwenda kusalimia ndugu na jamaa kufuatia kupata vijisenti kidogo kwani nilikuwa sijakwenda huko kwa mia karibu mitano, kwa sisi wengine ambao maisha yetu ni ya kubahatisha kwa kiasi Fulani  inabidi ujiwekee vijiakiba vya kubahatisha kwa muda mrefu  kabla hujapata kiasi ambacho kwa hicho unaweza kwenda kusalimia nacho kwenu bila kuadhirika, kuna wakati inaweza kukulazimu kukomba hata nauli ya kurudia  huko sasa ndo kuadhirika kwenyewe.

wasema kweli huitwa wapondaji/wanafiki

Ninaishi Dar es Salaam kwa muda wa miaka 16 hivi sasa na shughuli zangu ni kubangaiza. Lakini kijijini kwetu wote wanajua kuwa kwamba mimi ni mfanya biashara maarufu huku Dar.Kwa hiyo ninapoenda  najitahidi kuwaonyesha wana kijiji kuwa mambo yangu si haba , ingawa kwenye familia yetu wanajua kuwa mimi nimechoka vilivyo, siku hyo nikiwa hapo kijijini nimewanunulia jamaa bia  huku nikiwa natamba sana  mara akatokea jamaa mmoja ‘ Du umekuja lini mshikaji mimi niko hapa tangu wiki jana alisema’ jamaa huyu huwa tunabangaiza wote kule mjini lakini sikuwa na jua kuwa ni mwana kijiji wa pale ingawa najua kuwa ni mwenyeji wa wilaya yetu, siku hizi mimi ni mwana kijiji mama aliolewa hapa na mzee, alimtaja moja ya wazee hao, Sasa mzee lete stori maana ngalambe zetu mjini tunazijua wenyewe alianza kusema na taratibu nilihisi hatari ikija halafu aliendelea , Washikaji huyu jamaa yangu kabisa wiki iliyopita tu  tulikuwa tuna kabiliana na mwenye nyumba ,Jamaa akaanza kuponda hasa, kwani tumepewa notisi geto yetu si unajua maisha ya bongo yalivyo mtu sita chumba kimoja  mambo magumu washikaji msije mjini kabisa asiwadanganye mtu…’ Kila nikifanya bidii ya kumzuia asizungumzie naona mwenzangu anazidi kuchanja mbuga na kumwaga siri za maisha yetu kule Dar , mwsho wale wapambe wangu wakaanza kuhoji kuhusu anachosema Yule jamaa, jamaa aliendelea  kusema ukweli kuhusu maisha yetu kule mjini, nilipoona vile na kwa sababu namjua ni mgomvi niuliona bora niondoke badala ya kubishana naye kwa kweli kesho yake  nikakuta taarifa zimeenea kijiji kizima kwamba huko Dar niliko ninabangaiza tu ilibidi niondoke siku hiyohiyo na kwenda kulala kijiji kingine na kusafiri siku iliyofuata  kurudi Dar Lakini nashukuru jamaa alinisaidia kwani baada ya pale niliamua  kuwa mkweli, leo hii hata hivyo maisha yangu yamebadilika na yamekuwa mazuri kiasi cha kutosha lakini siku zote sasa nimejifunza kuwa mimi tu na sitaki kujipandisha zaidi ya nilivyo katika hali halisia 
Rev. Innocent Kamote
Mkuu wa wajenzi Mwenye Hekima

Hakuna maoni: