Jumapili, 31 Januari 2016

Nitaweka mkono wangu Juu ya Misri



Mstari wa Msingi Kutoka 7:4-5 “Lakini Farao hatawasikiza ninyi, nami nitaweka mkono wangu juu ya Misri, na kuyatoa majeshi yangu, watu wangu, hao wana wa Israeli, watoke nchi ya Misri kwa hukumu zilizo kuu. 5. Na Wamisri watajua ya kuwa mimi ndimi BWANA, hapo nitakapounyosha mkono wangu juu ya Misri na kuwatoa wana wa Israeli watoke kati yao”.

Hii ni lugha nyingine ya Kibiblia “NITAWEKA MKONO WANGU JUU YA MISRI” Maana yake ni nini ? Mungu ataihukumu Misri kwa sababu ya kiburi cha maendeleo yao ataleta anguko kubwa kwa vile Pharao amekuwa jeuri ana moyo mgumu hataki kuwaachia Israel Mungu napoihukumu Misri ana hukumu nini ni muhimu kulichambua hili!

Hali ya kiroho ya Taifa la Misri ilikuwa mbaya sana ingawa walikuwa na maendeleo makubwa sana, Mungu atalihukumu taifa lolote na kusababisha anguko kwa Dola hata kama ina nguvu kiasi gani endapo tu itamuacha Mungu, Historia inaonyesha sababu nyingine za kuanguka kwa dola la Misri


·     Mpaka miaka ya 1550 – 1200 hivi Utawala wa Misri ulikuwa umeenea mashariki ya kati na mbali mpaka mto Frat
·         Hata hivyo kwa haraka sana utawala huu ulianza kuanguka na kupoteza uwezo baadaye ukifuatiwa na tawala nyingine kama Ashuru Syria mwaka 750 KK
·         Kisha Babeli 606 BC
·         Kisha Uamedi/uajemi au Iraq na Iran 530 BC
·         Kisha uyunani au Ugiriki 332 BC
·         Kisha Rumi mwaka wa 30 BC
Dola zote zilizofuata baada ya misri hazikudumu kwa miaka mingi kama Misri, kwa mujibu wa kihistoria kuibuka kwa Dola hizo nyingine ndio ulikuwa mchango mkubwa wa kuanguka kwa Misri, ushahidi wa kibiblia unaonyesha kuwa taifa linalomuacha Mungu Mungu huweka mkono wake juu ya taifa hilo kwa hukumu Mungu ndiye aliyeihukumu Misri na mataifa mengineyo!

Ni lazima kila taifa litambue kuwa Mungu ndiye anayetawala na kuwa ndiye anayeweka wafalme na kuondoa na tena ndiye anayeyainua mataifa kwa makusudi yake na kuyasimamisha kwa kusudi lake na kuyaangusha kwa kusudi lake na utukufu wake

Warumi 9:17. Biblia inasema hivi “Kwa maana maandiko yasema juu ya Farao ya kwamba nilikusimamisha kwa kusudi hili, ili nionyeshe nguvu zangu kwako jina langu likatangazwe katika inchi yote” unaona kumbe kusimama kwa Misri ilikuwa ni kusudi la Mungu ili Mungu atangaze  nJina lake Duniani

Ni vema neno la Mungu likawa wazi kwa kila kiongozi na kila taifa kuwa mtu akiwa na madaraka au akiinuliwa akubali na kutambua kuwa kuna kusudi la Mungu nyuma yake, hivyo kila Mtu na kila taifa linapaswa kumuheshimu Mungu na kumpa Mungu kipaumbele, na kuwa na utambuzi na kunyenyekea na kuacha majivuno Lazima kila mtawala ajue yuko kwa kusudi la Mungu, na kuwa kama hatalitimiza Mungu ataweka Mkono wake na kuhukumu!

Biblia inasema Hivi Daniel 4:17 “Hukumu hii imekuja kwa agizo la walinzi, na amri hii kwa neno la watakatifu; kusudi walio hai wapate kujua ya kuwa Aliye juu anatawala katika ufalme wa wanadamu, naye humpa amtakaye, tena humtawaza juu yake aliye mnyonge”. Unaweza kuona?
Mungu anatumia wanyonge na kuwainua Mungu hapendezwi na kiburi na majivuno alimshughulikia Mfalme Nebukadreza kwa kusudi la kumyemyekesha ili ajue kuwa aliye Juu yaaani Mungu ndiye anayetawala,  Mwisho mfalme wa Babeli alisema Hivi katika Daniel 4:37 “….Basi mimi Nebukadreza namhimidi mfalme wa Mbinguni namtukuza na kumuheshimu maana matendo yake yote ni kweli na njia zake ni za adili na wale waendao kwa kutakabari (kiburi) yeye aweza kuwadhili! Unaoana

Biblia inaonyesha kuwa kiongozi jeuri asiyemnyenyekea Mungu, Mungu anauwezo wa kumuadhibu ni kwa sababu hizi Mungu aliweka mkono wake wa Hukumu dhidi ya Misri kwa sababu ya viongozi wake ambao walijichukulia heshima ya Mungu na kusahau kuwa wao ni binadamu tu Farao na majeshi yake yalifutiliwa mbali na Misri ilianguka, Historia kamwe haiwezi kuonyesha sababu hizi za kiroho, Ushahidi uliowazo kuwa Farao alikuwa na kiburi ni jinsi mara nyingi alikaidi agizo la Mungu la kuwaachia Israel waende zao mfalme huyu aliwahi kumjibu Musa kuwa Huyo Bwana ni nani? Kutoka 5:1-2 Biblia inasema hivi …..Bwana ni nani hata niisikilize sauti yake na kuwapa Israel ruhusa waende zao? Mimi simjui Bwana wala sitawapa Israel Ruhusa waende zao! Ni maneno ya Kiburi dhidi ya Mungu aliye hai hii ni kwasababu wamisri walimtukuza sana Farao na kumuabudu wakiamini ni mwana wa Mungu jua aliyeitwa Re akiwa katika mwili wa kibinadamu, Hivyo, kuwatumikisha Israel ilikuwa ni kashfa kwa Mungu wa Israel kwa vile farao anajilindanisha naye huku akiwa hatambui uwepo wa Mungu aliye hai ni kwa sababu hii Mungu alisema Nitaweka Mkono wangu juu ya Misri yaani nitaihukumu Misri, Kitu chochote kile kinachomdhalilisha mtu wa Mungu na kumtesa ni wazi kuwa kimejitukuza dhidi ya Mungu aliye hai Bwana na aweke mkono wake juu ya kila kitu kinachokusumbua na kukutweza na kukuonea na kukutawala huku kikiwa hakitaki kukuachia natangaza kuwa wakati umefika lazima vilivyojiinua vishushwe Bwana anaweka mkono wake juu ya usumbufu wote na kuhukumu kwaajili ya utukufu wa Jina lake Kutoka 14:3,17-18
Ujumbe na Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima
Rev Innocent Kamote

Hakuna maoni: