Jumanne, 26 Januari 2016

Chapa za Yesu!



Ujumbe: Chapa za Yesu
Wagalatia 6:17 “ Tangu sasa mtu asinitaabishe; kwa maana ninachukua mwilini mwangu chapa zake Yesu”

Leo nataka tutafakari kwa pamoja mstari huu muhimu sana katika maisha yetu ya utumishi pamoja na kumfuata Yesu, yaani ukristo ni swala la kuchukua chapa za Yesu nini maana yake? Kuchukua chapa za Yesu?

Biblia ya kiingereza ya NIV inasomeka hivi “Finally, let no one cause me trouble, for I bear on my body the marks of Jesus”

Biblia ya kiingereza ya New Anerican Standard Bible inatafasiri msatri huo namna hii
we are arrested by the words “ I bear on my body the brand-marks of Jesus” neon hilo Brand ni kama “label” na Marks  ni “alama” au chapa maana yake hii ni alama ya kudumu katika mwili wa mnyama au mwanadamu aliye mtumwa

Nyakati za Biblia mtu alipokuwa na wanyama aliwaweka alama kwa kupasha chuma chenye moto na kumbadika mnyama huyo ili kuonyesha kuwa ni wake, swala hili pia lilifanywa kwa watumwa, mtu aliponunua watumwa na kuwamiliki watumwa pia waliwekwa alma kwa chuma cha moto katika mwili wao na kovu la kudumu lingebaki mwilini mwa mtumwa huyo kuonyesha uhalali wa kumilikiwa watumwa hao waliitwa Doulos kwa lugha ya kiyunani, hakuwa na uwezo wa kutoroka na anemtumikia bwana wake milele hata kufa

Paulo anazungumzia maisha ya kujitoa kwa Yesu moja kwa moja ya kuwa kila anayeamua kuwa mkristo hapaswa kuingiza mguu nusunusu kila mtu anayemtumikia Yesu anapaswa kutambua kuwa
1.       Yeye ni mtumwa ni lazima akubali kuwekwa alama na Yesu ya kuwa yeye ni bwana na kuwa ni lazima kumtumikia hata kufa 1Wakoritho 6:19-20 na Warumi 1:1
2.       Kila anayeamua kumfuata Kristo ni lazima akubali kuwa amekubali kujiandikisha jeshi yeye ni askari na yuko tayari kutumika akikabiliana na mazingira magumu 2Timotheo 2:3, 2Wakoritho 5:15
3.       Kila anayeamua kufuata Yesu ni lazima ajitoe kumuabudu Wafilipi 1:20, 2Wakoritho 4:5

Maoni 1 :

Bila jina alisema ...

Hakika tumepigwa chapa zake Yesu Kristo