Jumanne, 26 Januari 2016

Mkristo na Uchumi


UTANGULIZI:

Umasikini ni moja ya matatizo makubwa sana duniani na hususani barani Afrika, katika inchi 52  zilizoko bara la afrika 40 ni masikini sana, miji yao imejawa na watu duni waliokosa mahitaji ya msingi ya maisha, kuna wimbi kubwa la watu wasio na makazi, wakimbizi, omba omba, watoto wa mitaani, watu wasiojua jioni watakula nini, wenye Afya zisizo ridhisha, siasa zisizoleta matumaini, na kila aina ya unyonge na ujinga  katika makundi ya watu hao walio masikini wengi wao ni wale waliookoka na kukimbilia makanisani ili kujiridhisha kwa Mungu, katika somo hili ni makusudi kabisa ya Mungu kujifunza somo hili Mkristo na Uchumi kwa kusudi la kutoa mafunzo kwa wakristo ili kupata majibu ya Kibiblia kuhusu Uchumi Mwanzo 9;1-3,2Falme 6;24-29. 

      Hali halisi ya umasikini ni mbaya kiasi cha kutisha barani Afrika  kwa mfano njaa peke yake  inaonekana kuwa tatizo kubwa kuna watu wengi ambao hawashibi chakula  utafiti uliofanyika kati ya mwaka 188-1990 unaonyesha kuwa  waafrika zaidi ya milioni 168 wameathiriwa na njaa kali  na inasemekana kuwa kuna ongezeko la watu milioni 40 kila baada ya miaka kumi  ambao nao watakuwa wenye njaa, mamilioni ya watoto wa kiafrika  wanaugua Kwashakoo hii maana yake ni kuwa wanadumaa kiakili kimwili na kimaendeleo na hata kufa 

Naandika kitabu hiki nikiwa na matumaini kwamba Kanisa lina uwezo wa kupambana na umasikini kivitendo hata ingawa Yesu alisema kuwa masikini mnao siku zote Mathayo 26;11 lakini Bado alitufundisha kuwa tunaweza kuwasaidia  na kufanya mambo ya kupita kawaida kwa ajili yao Hatutaki kutoa matumaini hewa kama zifanyavyo serikali nyingi Hapa Afrika kwani kanisa limeagizwa na kufundishwa kuwa moja ya njia ya kuwa wakamilifu ni pamoja na kuacha kabisa ubinafsi na kufanya kitu kwaajili ya masikini Mathayo 19;21

Ssi tunaweza kuonyesha upendo hata wakati ambapo hali inaonekana kuwa isiyoridhisha, tunaweza kutoa tumaini pasipo na tumaini  tunaweza kufundisha watu na kuondoa ujinga na kuwaonya kuwa waache uvivu na wafanya kazi kwa bidii yao tunaweza kuwakumbusha kuwa watumie karama ya akili walizopewa na Mungu kubuni na kujituma na kuzalisha mali hata kwa kuanzia na mitaji midogo sana na hatimaye kufikia miradi mikubwa hii inawezekana kwa waliosoma na hata wasio soma ni wajibu wetu ni wajibu wangu kuwajulisha watu na kanisa kuwa Mungu anahusika sana na maswala ya uhitaji wa watu wake  na hivyo kuna umuhimu mkubwa wa kanisa kuwa na mafundisho kama haya ili kuamsha hari ya waamini wetu kuwa tayari na maswala ya kukuza uchumi kwa kufanya kazi ka bidii kuwa wabiunifu huku tukimuomba Mungu, ni makosa kuwapa watu tumaini la muujiza pekee kwani inaweza kusababisha wau kuwa wavivu na kutokufanya kazi wakisubiria kulishwa na kunguru tu huo sio mpango wa Mungu wa kudumu Ingawa Mungu aweza kufanya kwa Muda, lakini asili ambayo pia ji matokeo ya uumbaji wa Mungu iliumbwa kwa ajili yetu na ni muhimu kitumia juhudi jumlisha na kumomba Mungu jibu ni kuwa tutakuwa na uchumi ulio imara Mungu akubariki sana unapopitia somo hili, ndimi mjoli mwenzenu katika shamba la Bwana Rev. Kamote.

Tutajifunza somo hili kwa kuzingatia vipengele nane vifuatavyo;-.
*      Maana ya Uchumi
*      Mwanzilishi wa Uchumi
*      Madhara ya dhambi katika Uchumi
*      Umuhimu wa kuwa na Miradi ya kiuchumi
*      Mambo ya muhimu ya kuzingatia katika kuendesha miradi
*      Mkono wa shetani dhidi ya Miradi ya watu wa Mungu
*      Namna ya kupata mtaji na elimu ya miradi
*      Faida za kuwa na Wakristo wenye uchumi mzuri
*      Funguo kumi na mbili za Mafanikio.

SOMO: MAANA YA UCHUMI

Muhubiri; Mchungaji Innocent Mkombozi Kamote

 A.  MAANA YA UCHUMI:
Uchumi ni sayansi ya Uzalishaji mali na matumizi ya Utajiri wa asili tuliopewa na Mungu Ni mfumo wa uzalishaji mali katika jamii kupitia mitaji ambayo tumepewa na Mungu. Ni sayansi ya uzalishaji wa mali katika jamii, namna ya kusambaza bidhaa na utafutaji wa masoko, Tangu zamani sana watu wenye akili waliweza kutumia akili na ujuzi waliopewa na Mungu ili kuboresha maisha yao inasemakana kuwa akili ndio karama kubwa na mtaji mkubwa wa kwanza ambao Mungu aliwapa wanadamu moja ya majibu makubwa ya maana kwanini nchi yetu inaendelea kuwa masikini jibu ni kwa sababu tumeshindwa kuitumia karama ya akili tuliyopewa na Mungu katika kuyaendeleza maisha yetu, inasemakana kuwa kisaikolojia mpaka wanadamu wanakwenda kaburini hata kama wameishi sana hutumia asilimia 30% ya akili walizopewa na Mungu na kuwa asilimia 70% huzikwa mchangani bilakutumika Katika biblia iko mifano ya watu wa kwanza kutumia akili ambao ni waanzilishji au mababa
§  Badala ya kuhangaika kwenda kuwinda wanyama waligundua na kuamua kufuga wanyama waliokuwa wamepewa na Mungu Mwanzo 4;20
§  Badala ya kukaa wakiwa wapweke baada ya shughuli za kutwa nzima za mahangaiko walitegeneza vinubi na filimbi Mwanzo 4;21
§  Na badala yakutumia zana duni za mawe walianza kutumia akili na kufua shaba na chuma Mwanzo 4;22
Mungu anataka kila mwanadamu mwenye viungo vilivyo kamili kuzalisha mali alipomuumba mwanadamu hakutaka akae vivihivi alitaka mwanadamu aitunze Bustani na kuilima Mwanzo 2;15 “akamweka katika Bustani ya Eden ailime na kuitunza” ni muhimu kufahamu kuwa sio mapenzi ya Mungu watu kukaa na kutokufanya kazi ili Mungu ampe mtu mali na uhitaji inahitajika kila mtu kujibidiiisha katika kila alifanyalo Mungu anachukizwa na uvivu Paulo mtume alisema yeye asiyefanya kazi Kula na asile 2Thesalonike 3;10-12. Inashangaza kuona kuwa watu wengi waliookoka ndio wanakuwa na uvivu wakiacha kujishughulisha Bwana ampe neema kila mmoja aweze kujishughulisha katika jina la Yesu.

B.     MWANZILISHI WA UCHUMI:
Mtu awaye yote ambaye atazungumzia maswala ya uchumi  au vyanzo vya uchumi au mwanzilishi wa uchumi bila kumtaja Mungu mtu huyo ni dhalimu kupita kawaida, Mungu Yehova ndiye mwanzilishi wa Uchumi swala zima la uchumi haliwezikuwa na kibali kama utamuweka Mungu pembeni Yeye ndiye aliyetoa mitaji yote ya Uchumi tuliyonayo wanadamu zaidi ya yote ndiye aliyetupa akili abao ni mtaji mkubwa na mkopo wa hali ya juu na ndio maana Mungu anapotudai zaka au sadaka na matoleo ni haki yake kabisa kwani vitu vyote vinatoka kwake wala sio kuwa Mungu anatudhulumu no Hapana kama mwanzilishi wa uchumi. Miradi na mitaji pamoja na mkopo si vibaya akipata kitu kutoka kwetu
-          Mungu  ndiye mwanzilishi  wa uchumi
-          Miradi, mitaji na mikopo
Mtu anaweza kuuliza swali ni kwa vipi na kwa namna gani Mungu ameanzisha maswala ya uchumi au kwa naman gani anatoa mikopo mitaji na miradi?
Katika ulimwengu huu wa kawaida Mwanzilishi wa Uchumi anajulikana kama Adam Smith lakini katika imani yetu  Mwanzilishi wa Uchumi Ni Mungu
 


Adam Smith
Adamu smith mwandishi maarufu wa maswala ya uchumi wa Mataifa anajulikana sana kama mwanzilishi wa aina ya uchumi ulioko sasa Duniani “Founder of Morden Economics” alishauri kuwa Mashindano Binafsi na huria au soko huria linamchango mkubwa sana wa kukua kwa uchumi kuliko masoko yanapoongozwa na serikali Tangu mwaka 1776 Wakati smith alipoweka wazi kazi zake mjadala wake unaoonekana kuhalalisha mfumo wa kibepari zaidi kuliko wa kijamaa na unakataza serikali kuingilia maswala ya kibiashara Smith aliamini kuwa Biashara huria hukuza uchumi kwa kasi sana na kwa matokeo mazuri kama kwa mkono usioonekana. 


 KWA VIPI MUNGU ALIANZISHA UCHUMI:
Aliumba Dunia na vitu vyote vilivyomo kabla ya kumuumba mwanadamu, na kumtengenezea mazingira yenye kuruhusu uzalishaji mali, mwanadamu aliumbwa siku ya mwisho ili kwama mali, mitaji na miradi iweze kumtangulia kwa hivyo mwanadamu alikuta kila kitu kutoka kwa Mungu na alipewa akili ili atawale kila kitu na kukitumia na kukitunza ( Mwa. 1: 1-31) Kila wakati Mungu alikumbusha kuwa amewapa wanadamu kila kitu Mwanzo 1;27-31, 9;1-3.
MAZINGIRA YENYEWE NI KAMA:
1.      MAJI ( Bahari,  Maziwa na  Mito na chemichemi) asilimia kribu 70 ya ulimwengu ni maji na katika maji kuna utajiri mkubwa sana kuna maswala ya
o   Uvuvi, kilimo, uzalishaji, umeme,umwagiliaji
o   Maji ya kunywa. kufulia nguo na kuoga na kustarehe kwa kuogelea
Kupitia uvuvi Mungu ameweka kila aina za samaki ni wajibu wa mwanadamu kutafuta namna atakavyowatoa na kuwauza samaki wengine ni wa thamani sana Mungu amewaumba wa kila aina kwa maji chumvi na maji baridi ni chakula kutokakatika maji kumbuka hakuana mvuvi amewaweka humo au anayeaga asubuhi kuwa anakwena kuvua mali yake angalia ni Mungu amewapa wanadamu wamo katika maji, tunaweza kuyatumia maji kwa kumwagilia mboga, kwa kunywa, kwa burudai na michezo kwa nguvu za umeme usafiri na kadhalika, maji ni asili mali kubwa sana sehemu nyingine  maji yasikopatokana huzwa kwa thamani na hata watu wanao yatengeneza kwa kuyasafisha na kuweka kwenye chupa na kuyapa majina ya aina mbalimbali kwa hakika hawatumii maji yao wanatumia maji ambayo Mungu ametupa unaona! Kumbe basi Mungu hapaswi kulamiwa kwa Umasikini wetu ametupa kila kitu

2.      ANGA.
o   Anga ni mtaji mwingine tuliopewa na Mungu angani leo kunatumika kwa mambo mengi Kwa safari za Ndege, kwa mawasiliano ya satellite na mawasiliano ya Redio Televisheni na simu za mkononi aidha anga linaweza kutumika kwa utafiti wa kisayansi kwaajili ya nyota na sayari,na hata kwa maswala ya ulinzi na vita anga linahusika na ukuaji wa mimea na uletaji wa hewa nzuri nguvu za upepo na mbingu ziletazo mvua kwaajili ya kilimo pamoja na  Burudani

3.      ARDHI, (NCHI)
o   Ardhi ni utajiri mkubwa sana inahusika katika kutuletea chakula kinachotokana na kilimo cha vitu vya aina mbalimbali, kuna kila aina za udongo kwaajili ya ujenzi, chokaa simenti, Mafuta, lami, gesi, ujenzi wa barabara majengo, Mazao nguo Madini ya kila aina hakuna aliyeviweka ni Mungu ameweka humo, kuna makaa ya mawe kwaajili ya nishati na matumizi ya nyumbani kuna miti ambayo ni dawa kuna miti ya mbao za kila fanicha na matumizi ya ujenzi kwa kweli Mungu ametupa kila kitu kushindwa kuvitumia ni kwaajili yetu wenyewe kushinda kutumia akili tuliyoipewa na Mungu

4.      WANYAMA:
o   Wanyama tuliopewa na Mungu  ni hazina wanatumika katika kila Nyanja kuna wanyama wa kutubebea mizigo kama Punda na ngamia, kuna wanayama wanaoweza kufanya kazi za kilimo kama punda na madume ya ng’ombe kuna wanayama wa ulinzi kama mbwa paka,kupitia wanyama tunapata maziwa, mayai,ngozi za viau, mikoba urembo,nyama mbolea  Mwanzo 9;1-3 wako ndege wa kupendeza nchi nyingine hutumika kwa utalii na mapambo kaa kasuku chiriku mbuni n.k.
5.      MIANGA JUA, NYOTA, MWEZI
o   Mianga ni ya muhimu sana mwanga wa jua una vitamin D, unasaidia katika ukuaji wa mimea Photosynesis, nguvu za umeme joto la mwili la kukaushia nguo kwa udobi kuanikia bidhaa nyota na mwezi pia hutumika kwa maswala ya kisayansi piam inasemekana kuna uhusiano wa ukuaji wa nywele za binadamu na mwezi, nyota hutumika kama alama au mifano mfano watu maarufu huitwa super stars, Abrahamu alionyeshwa uzao wake kuwa kama nyota za angani,Nyota hutumika pia kwa utukufu wa Mungu na kadhalika
6.      MBEGU.
o   Mungu ametupa mbegu Karibu kila mmea una mbegu duniani, mbegu ni mtaji tunazipanda na Mungu huziongeza Mwanzo 1;29, 26;12, hatupaswi kuziharibu mbegu kufanya bading ni kinyume cha maandiko Biblia imakataza kufanya buding ya mimea kwani kwa kufanya hivyo tutapoteza asili ya mbegu tulizopewa na Mungu Torati 22;9,Lawi 19;19.
o   Katika mazingira yote Mungu alivyomuumba mwanadamu. Utaona swala la uchumi  (uzalisha mali) likihusika Mungu alitaka wamadamu wawe na kila kitu na aliwapa kiloa kitu kwa msingi huo awaye yote anayezalisha mali ni lazima kwamba anatumia mazingira aliyayaoumba Mungu kunufaika kwa uzalishaji mali.
o   Mungu anataka wanadamu wazalishe mali hili lilikuwa ni mpango wake kabla ya anguko la mwanadamu kumbuka kuwa pia Mungu ndiye mwanzilishi wa miradi kama ilivyo kwa maswala ya uchumi.

MUNGU PIA NI MWANZILISHI WA MIRADI.
o   Mungu alimuanzilishia  Adamu  mradi wa  Bustani ( Mwanzo 2: 8: 15 - 16) Mungu alimwabia 
o   1.  Ailime 
o   2.  Aitunze na
o   3.  Ale matunda yake,
Mungu alitaka mwanadamu autunze mradi aliomuanzishia na kuuendeleza kabla ya anguko.
MPANGO WA MUNGU KUHUSU UCHUMI KABLA YA ANGUKO LA MWANADAMU.
o   Kufanya kazi ya uzalishaji mali pasipo jasho na uchungu kazi ilikuwa ikifanyika kwa  furaha maana alipewa kama zawadi.

MADHARA   YA DHAMBI KATIKA UCHUMI.
Mpango wa Mungu wa uchumi kwa mwanadamu kabla ya anguko ulikuwa sio wa majuto  wala kutoka jasho na uchungu kama ilivyo leo lakini baada ya anguko la aina binadamu shuhuli zote za uzalishaji mali zilibadilika na kuwa ngumu sana kama sehemu ya adhabu kwa sababu ya dhambi na kuiasi sauti ya Mungu Mwanzo 3;17-19
Kazi zote za uchumi/ uzalishaji mali zilibadilika zilikuwa ngumu sana kama  adhabu ya dhambi. (Mw. 3: 17- 19)
1.      Ardhi kulaaniwa.
2.      Mwanadamu alianza kula na kupata chakula kwa uchungu.
3.      Mwanadamu alianza kula kwa jasho.
4.      Mwanadamu alianza kuzalisha mali na chakula kwa uchungu huku Michongoma/ miiba imezaliwa katika ardhi ituchome.
5.      Kwa ujumla Upinzani  ni mkubwa katika mfumo  wote uchumi na upatikanaji wa mali hasa kwa njia za halali
UMUHIMU WA KUWA NA MIRADI YA UCHUMI
I.              
      KUWA NA MIRADI YA UCHUMI.
A:         MAANA YA MRADI.
Miradi ni shughuli yoyote ya halali inayoweza kusaidia mtu kuchuma mali na kumuingizia kipato, Mtume Paulo aliposema kila mtua ajishughulisha na kufanya kazi hakumaanisha  kuajiriwa tu  lakini kila mtu aliyeokoka anaweza kujiajiri 2Wathesalonike 3;11 ni dhambi na makosa kumsaidia mtu ambaye ana nguvu na akili kamili kwa kumpa chakula na mavazi ni kufuga ujinga lazima kila mtu ajishughulisha kufanya kazi
-          Ni  kazi yoyote ya  halali inayozungumzia mtu  upato.

B. AINA MBALIMBALI ZA MIRADI YA UCHUMI AMBAYO MWANADAMU ANAWEZA KUIFANYA

1.      MIRADI YA  MUDA MFUPI :
Miradi ya muda mfupi ni miradi ambayo inaweza kuanzia siku moja mpaka miezi sita  miradi hii ni kama kufanya vibaua, kubeba mizigo, kupiga kiwi na kufanya biashara za kimachinga, kupika chakula, kulima Bustani, kufuga kuku, nguruwe, kulima vibarua hii ni miradi ya muda mfupi kwaajili ya kutengeneza mtaji mkubwa zaidi kwa kawaida huanzia siku 1- miezi 6.

2.      MIRADI YA MUDA MREFU.
Miradi ya Muda mrefu ni shughuli za uzalishaji mali zinazoweza kufanyika kuanzia miezi 6 na kuendelea  miradi kama hiyo inaweza kujumuisha maswala ya kilimo kwa mfano Nuhu alianza kuwa mkulima wa zabibu Mwanzo 9;20, pia miradi ya muda mrefu inaweza kuhusisha swala la ufugaji wa wanyama kama ngo’mbe, mbuzi, kondoo na mfano ni Abrahamu yeye alitajirika sana kupitia mifugo Mwanzo 13;2, Isaka aliamua kuwa mkulima Mwanzo 26;12, Yako mazao mengine rahisi na yenye bei kubwa kama Pilipili, Soya,Mananasi, Michungwa, pia unaweza kuwa na miradi ya mashine za kusaga na kukoboa, uchimbaji wa madini, kilimo cha ndizi, ujezi wa shule, za chekechea, Msingi na sekondari, vyuo vya ualimu na vikuu, duka la dawa, na vifaa vya ujenzi, viwanda vidogo, ufyatuaji wa matofali kwa kawaida miradi hii kuanzia miezi 6 na kuendelea,  kilimo cha mahindi,  maharage, Mazao ya biashara. 

3.      KUELIMISHA WATU:
Kuelimisha watu pia ni mradi wa Muda mrefu sana  wachina wanausemi usemao “Usimpe mtu samaki bali mpe ndoana na kumuelekeza namna ya kuvua samaki” usemi huu una maana sana kuwa unapojaribu kumsaidia mtu katika mahitaji yake bila kumfundisha namna ya kuzalisha na kujitegemea nafanya kazi bure, mtu anayeomba samaki leo akapewa kesho atahitaji tena lakini aliyefundishwa namna ya kumtoa majini anajua mwenyewe namna ya kumpata anapoishiwa, Kuelimisha watu ni mradi wa muhimu sana hata ingawa ni wa muda mrefu watu wenye ujuzi wa kujenga, useremala, kupaua , ufundi umeme na kadhalika wana ujuzi ambao ni wa kudumu Mithali 9;9

II.                  MAMBO MUHIMU YA KUZINGATIA KATIKA  UENDESHAJI WA MIRADI:
A.     Maombi.
Tumejifunza kuwa Mungu ndiye mwanzilishi wa Mitaji na miradi na Uchumi kwa ujumla kwa mtu aliyeokoka ni muhimu sana kukumbuka kuomba kwa Mungu ili kwamba aweze kukupatia mtaji au mradi usizitegemee akili zako mwenyewe wala usimtagamee mwanaamu hata ingawa Mungu hutumia wanadamu Yeremia 17;5-11, Nehemia alikua na maonao a ujenzi wa ukuta wa Yerusalem hata ingawa hakuwa anajua namna atakavyouanza mradi huo wa ujenzi wa Yerusalem alimuomba Mungu na ndipo Mungu alipougusa moyo wa Mfalme na akasaidika kuppata vifaa kwa shugfhuli za ujenzi Nehemia 1;1-2;8.
B.      UTAFITI
Ni muhimu kufahamu kuwa ni lazima ufanye utafiti wa kutosha wa mazingira ya mradi . Mazingira ya eneo la mradi ni muhimu sana Musa na Yoshua Ingawa walikuwa wameahidiwa nchi ya kanaani na Mungu Bado walilazimika kutuma wapelelezi kuichunguza nchi Hesabu 13;1-3,16-20 hiyo ni ya namna gani watu wake ni wa namna ani na kuna mazao ya namna gani, kwa mfanya biashara ama mtu anayetaka kufanya mradi lazima awe makini kuchunguza vya kutosha kuwa watu hao wanataka nini na ni nini kifanyike kuwafikishia kile unachokitaka kukifanya, kama mahali hapana mashine ya Kusaga na watu wa mahali hapo wanahitaji weka mashine hiyo mahali hapo zingatia haya yafuatayo kwa ;-

1.       KILIMO:
Chunguza maswala ya muhimu yafuatayo;-
·         Hali ya udongo.
·         Majira yafaayo.
·         Hali ya Hewa.
·         Usafiri na wadudu waharibifu.
2.      BIASHARA:
Chunguza endapo kuna;-
·         Walaji/ wateja wingi/ Ushauri
·         Bidhaa inayopendwa na inayouzika
·         Ushindani ulioko (wingi wa wauzaji)
·         Usafiri (harama za usafirishaji)
C.      UPATIKANAJI WA MTAJI:
Moja ya maswali muhimu sana kwa mtu asiye na kitu ni kujiuliza kuwa atapata wapi mtaji? Ili aanze kufanya Biashara na kujikwamua kiuchumi hapa tunajadili namna mbalimbali za kupata mtaji wa kiuchumi

§     ZIPO NJIA SABA ZA  KUPATA MTAJI (MW. 41: 38- 40)
I.                    Akili
II.                  Akili ya kujifunza ( Elimu)
III.                Nguvu na Bidii ( Mith 31: 17)
IV.                Vifaa/ vitendea kazi mf. Toroli, Baiskeli, Mkokoteni.na n.k
V.                  Mikopo, Benki- au ndugu na rafiki.
VI.                Machinga; ( Mithali 12: 14)
VII.              Vyanzo visivyo Rasmi Zawadi – tuzo za uaminifu.
1.      House girly.
2.      Mtumwa
3.      Mtumishi  serikalini
4.      Mtumishi wa – Mungu
5.      Uwekaji wa akiba kidogokidogo
6.      Uchezaji wa bahati nasibu
7.      Urithi wa mali,Shamba, Baiskeli, Magari, nyumba,

1.      HEKIMA AU AKILI
Ni muhimu kufahamu kuwa kabla ya kuanza kufikiri kuhusu vyanzo vya kifedha na upatikanaji wa mitaji ya miradi  ni lazima ujihoji kuwa je una hekima  au akili? Kama utapewa dola milioni moja na hekima je utachagua nini? Wengi wanaweza kuchagua fedha  wakati fedha bila hekima  haina thamani  yoyote, ni muhimu kufahamu kuwa utajiri na mtaji mkbwa zaidi kuliko vyote ni hekima au akili  Mithali 3;13-16 wakati wote Mungu aliwaweka juu na kuwaimarisha wenye hekima na kuwaweka juu ya wapumbavu 2Nyakati 1;10 Yusufu aliwekwa juu kusimamia mradi mkubwa sana huko Misri kwa sababu Mungu alikuwa amempa hekima Mwanzo 41;38-40,1Wafalme 3;8-14, Hekima hii au akili hii nin ile inayomuweka Mungu mbele, mtu akiwa na uchumi mzuri kasha asimuweke Mungu mbele huweza kupokonywa mali na mtaji alionao kwa haraka sana Luka 12;16-21. Tunaweza kuwa na hekima kwa kuomba Yakobo 1;5, Mungu anafahamu kuwa kuwekeza mtaji mkubwa kwa mtu mbumbavu kuna uwezekano mkubwa wa kusambaratika na mtu huyo kuingia katika uharibifu mkubwa wako watu ambao Mungu akiwapa kamtaji Fulani na mambo yakaanza kuchanganya anaanza kunyanyasa watu Mithali 21;17, anaweza kufanya mambo ili watu wajue kuwa amebarikiwa au ataanza kunyanyasa watu 1Samuel 25;25;1-12 tu fedha kidogo tu tukiingia badala ya kuwaza namna anavyoweza kuzalisha tena  utaona anaanza kujipongeza  au kuanza kutesa Bila hekima ya Mungu Utajiri au fedha ni  msiba mtupu Mithali 10;22 watu wasiomcha Bwana  huishi maisha ya huzuni kama umeiba unakuwa na hofu ya kuibiwa Mungu hachanganyi Baraka zake na huzuni.

2.      AKILI YA KUJIFUNZA (Elimu) Mithali 12;1,4;13.
Njia nyingine ya kupata mtaji na mali ni kupitia akili ya kujifunza kupitia Elimu mbalimbali Kumbuka Bwana wetu Yesu alikuwa Fundi Kapenta kazi aliyojifunza kwa Baba yake, Tunaweza kujifunza maswala kadhaa kutoka kwa watru wengine kwa mfano wa
§  Ufumaji wa vitambaa, kofia za watoto, mikeka, vikapu n.k.
§  Utengenezaji wa mishumaa
§  Utengenezaji wa batiki
§  Kusomea elimu ya awali chekechea ufundishaji
§  Kujifunza upishi wa aina mbalimbali, ufundi, Baiskeli umeme magari ujenzi n.k
§  Wakristo wana nafasi ya kushikirishana vipawa Matendo 18;1-3
§  Ujuzi wa kufunga antenna na madishi ususi na ufumaji
Haya ni maswala ambayo tunaweza kujifunza kutoka kwa wenzetu kupitia elimu ya kujifunza

3.      NGUVU NA BIDII Mithali 13;4 6;6-11
Nguvu na bidii linaweza kuwa sababu ya kupata mtaji Mithali 31;10-25 Biblia inazungumzia kuhusu mke mwema kuwa ni mjasiriamali  17&25 mwanamke huyu ni mwenye bidii Biblia inapiga vita sana swala la uvivu uvivu ni ulegevu ni hali ya kutokuwa na bidii na uvivu unaleta umasikini Mithali 10;4 Mithali 20;13. Katika hali ya kawaida pia hata wale wanaofanya kazi wanatakiwa kuwa na bidii na juhudi katika kufanya kazi zao.

4.      VIFAA /VITENDEA KAZI (nyenzo).
Vifaa vya utendaji kazi wakati mwingine ni va muhimu kwani ni mtaji au ni nyenz ambayo inaweza kutupatia mtaji vifaa kama vifuatavyo vinaweza kabisa kutupa mtaji au kutupatia kazi ya kujipatia kipato
§  Mikasi ya kukatia michongoma
§  Baiskeli
§  Toroli
§  Fyekeo
§  Chepe/panga/mkokoteni.
§  Sindano na uzi wa kushonea viatu.
Ni muhimu kufahamu kuwa mkasi wa kukatia michongoma unaweza kukupatia fedha na wakati mwingine hata kisu na zana nyingine zilizotajwa hapo juu ni za muhimu sana katika kutupatia fedha kazi yetu kubwa itakuwa ni kunusa uhitaji uko wapi? Na kisha unajipatia ajira za muda mfupi na baadaye unaweza kufikiri juu ya kupanda kutoka hatua moja hadi hatua nyiongine.

5.      MIKOPO:
Moja ya njia ya kupata mtaji wa kiuchumi ni mikopo Mathayo 25;14-27 tunaweza kupata mikopo kutoka kwa watu binafsi, Benki, vyama vya kuweka na kukopa Saccos na kadhalika  jambo la msingi katika swala la mikopo ni kuzingatia masharti ya wenye kuutoa
Kumbuka wakat wote unapochukua mkopo hakikisha kuwa unakwenda kuzalisha mali  ambazo kwa ujumla utakuwa umezifanyia utafiti wa kutosha, andaa mbinu na mazingira ya uzalishaji mali, kumbuka kuwa usichukue mkopo kwa lengo la kununua vitu kama t.v, sofa n.k Hakikisha kuwa mkopo unazalisha vya kutosha unarudisha marejesho ya watu na faida  unaweza kuitumia katika kukuza mtaji na au kununua mahitaji yako
Jihadhari na kuweka Rehani mali zako kwaajili ya mkopo Miali 22;26-27 Wakati wote kumbuka usiwaze mambo makubwa sana unaweza kukopa lakini usikope fedha nyingi sana unaweza kukopa kwaajili ya biashaa ndogondogo na kisha ukaanza kuzitembeza machigays Machinga; ( Mithali 12:14) hata hivyo kukopa kwa mujibu wa Biblia kunakuafanya uwe mtumwa Mithali 22;7

6.      MACHINGA MITHALI 12;14.
Unaweza kufanya biashara ndogo ndogo kama za kimachinga kwa muda kasha mtaji wako unapokuwa unaweza kufanya kazi zingine

7.      VYANZO VISIVYO RASMI.
Vyanzo visivyo rasimi vinaweza kuwa sababu ya kupata mtaji lakini vinaitwa vyanzo visivyo rasimi kwa kuwa hutokea kwa nasibu tu jambo la msingi ni kuishi bila kuvitegemea lakini vinaweza kutokea hapa tunavizungumzia kuwa vinapotokea basi isiwe sababu ya kuvitumia vibaya badala yake iwe sababi ya kuzalisha mali zaidi ili kuweka uchumi wako kuwa mzuiri. Uwekaji akiba kidogokidogo nalo ni jambo la msingi inasemekana kuwa mtu anaweza kuweka akiba 20% ya kipao chake na kinapofikia hatua ya kuanzisha mtaji basi ni muhumu kuanzisha lakini baada ya utafiti wa kutosha kujua nini kitalipa
a.      Tuzo za uaminifu
b.      Zawadi za uchapa kazi bora/motisha n.k
c.       House girly. Mwanzo 30;25, Mwanzo 39;2 2wafalme 5;1
d.      Mtumwa
e.      Mtumishi  serikalini
f.        Mtumishi wa – Mungu
g.      Uwekaji wa akiba kidogokidogo
h.      Uchezaji wa bahati nasibu
i.        Urithi wa mali,Shamba, Baiskeli, Magari, nyumba,




MAMBO YA MUHIMU YA KUZINGATIA KATIKA KUENDESHA MIRADI
ELIMU YA MRADI:
§  Uwe na ufahamu  wa
1.       Soko la  bidhaa
2.      Faida na hasara
3.      Kutunza kumbukumbu.
4.      Kuwaheshimu wateja.
5.      Ushirikiano na wafanya biashara wengine.
BIDII / JUHUDI.
§  Wahi kazini  ( nidhamu)
§  Acha uzembe kazini. (muda ni mali)
UVUMILIVU;
§  Usikate tama.
§  Mvumilivu hula mbivu.

MAOMBI.
§  Ombea mradi
§  Usitegemee akili (                   4: 13- 17)
§  Nyenyekea ( I Petro 5: 6-9
KWA NINI.
    Kiburi huambatana na mafanikio
    Wengi wamemwacha Mungu.



MKONO WA SHETANI DHIDI YA MIRADI YA WATU WA MUNGU
Ni muhimu kufahamu kuwa Shetani kama alivyo Adui wa Mungu katika maeneo mengine pia ni adui mkubwa wa Miradi ya uchumu kwa watu wa  mungu kwa msingi huo ni muhimu kuwa na uelewa huo  ili shetani asipate kutushinda kwa kukosa kuzijua Fikra zake
-          Alishambulia  Miradi ya Uchumi Ya Ayubu ili kwamba aweze kumkufuru Mungu Ayubu 1;1-2; Ni muhimu kufahamu kuwa shetani atashambulia uchumi pamoja na Miradi ya auchumi ili kwamba mtu wa Mungu aghadfilike na kuchukizwa na njia za Mungu wengi wanapoharibikiwa na miradi yao ni rahisi pia kuuacha wopkovu na uadilifu kwa kuwa miradi yao ya Uchumi imeguswa.
-          Alimshambulia Yusufu ambaye kwa mikono yake Miradi ya Uchumi ya Potifa ilikuwa ikifanikiwa na akawekwa gerezani, Sheatani anweza kukushambulia kwa maneno ya uongo Kazini kwako kusudi upoteze kazi Mwanzo 39;1-21
-          Alishambulia Cheo cha Nabii Daniel Daniel 6;1-5, siku zote mipango na  mikakati ya shetani ni kutupeleka katika makanwa ya simba  ili tutafunwe na umasikini Shetani anaelewa wazi kuwa kufanikiwa kwa mtu wa Mungu ni kufanikiwa kwa kazi ya Mungu shetani ni mwivi na mwivi haji ila aibe kuchinja na kuua Mtu mmoja mwanafalsafa alisema hivi unapoanza mtradi wowote ule ongeza na kiwango cha maombi, hakikisha kuwa Unaombea mradi wako, na kukemea roho za upinzani, uwe na bidii na juhudi, uwe mvumilivu, na hakikisha kuwa unapofanikiwa unakuwa mbali na kiburi Yakobo 4;13-17.
-          Hakikisha kuwa unatmia hekima kwa kuwaheshimu wateja wako na kuzungumza nao kwa lugha nzuri uwe na uhusiano mzuri na wafanya biashara wengine.
ADUI MWINGINE WA UCHUMI.
Ukimuacha shetani adui mwingine wa Uchumi   na maendeleo ya Mkristo ni MADENI kwa kawaida mtu anapougua ugonjwa Fulani na akaenda Hospitalini kwa Daktari, kwa kawaida daktari hana haja ya kujua ugonjwa bali Sababu za ugonjwa kwani wanajua kuwa wanaweza kutibu ugonjwa lakini lakini ni lazima atafute chanzo cha ugonjwa Kama mtu ana madeni Dawa yake sio kupata fedha nyingi zaidi  bali ni kujua kwanini ana madeni na kuanza kushughulikia tatizo hilo kwanza.
Sababu za madeni
1.       Kumuibia Mungu na kutoa kipaumbele kwenye Mambo mengine yetu Malaki 3;7-11, Hagai 1;3-11 Ni muhimu kufahamu kuwa madeni yanayotokana na Mungu hayaponi mpaka utakapomrudishia zaka ni mali a Mungu ni 1/10 ya mapato yetu, kwa mujibu wa sheria ya zaka unaweza kuikopa lakini utarudisha riba ya zaka 1/5 mtu anayemuibia Mungu zaka anajiweka katika kuwa na hali mbaya ya Uchumi Mungu hata mkemea yeye alaye na mizabibu itapukutisha matunda kabla ya wakati wake, Mungu naweza kuruhusu panya kula nguo zako, watoto kuugua na fedha ukaipeleka Hospitalini na kadhalika kwa msingi huo ni muhimu kumtolea Mungu zaka.
2.       Kutumia fedha kabla Haijatufikia.
Hii ni hali ya kutumia fedha unayotegemea kuipata, nipatia hii kanga fedha zangu zikija tu nitalipa hii ni tabia inayokosesha amani wengi sio vema kutumia fedha kabala hujaipata Kumbuka kuwa Huna fedha Mpaka uepokea fedha Mithali 4;25-26 kwa maana nyingine ni kuwa unapoazima fedha ni kama unapoteza Muda yaani unaazima muda ja utakuwepo kesho kulipa? Warumi 13;8
3.       Kumuazima mtu kitu ambacho hawezi kukinunua
Mfano unamuazima mtu Baiskeli na unajua kuwa hana uwezo wa kuinunua kisha akaibiwa je hutaingia hasara Biblia inatufundisha kuhakikisha kuwa hatuwi mzigo kwa watu wengine 2Thesalonike 3;7-8 kama unaweza kukilipia au kukinunua tena azima, kwa msingi huo pia usipende kuazima kitu ambacho huna uwezo wa kukinunua au kukilipia gharama.
4.       Kutaka kuwa masihi wa kila mtu.
Kuna watu ambao wanataka kuwa wenye kumuhudumia kila mtu anayekuja na tatizo lake unapomuazima mtu fedha unamtia katika madeni Ni heri kutoa Luka 6;34-35 Ni afadhali kumpa mtu kitu au kiasi kidogo cha  kile ulichonacho kuliko kumkopesha  na kumtia katika madeni lakini wakati huo huo kumbuka kuwa huwezi kuwa Mkombozi wa kila mtu unaweza kumsaidia mtu kiasi kasha ukamuombea Mungu ampe kilichosalia  mfano amekuazima 2000 mpa 500 bila kumdai ni Heri kutoa kuliko kukopesha!  Yesu alifundisha hivi kwa sababu uhusiano wa mtu ni wa muhimu kuliko kile unachokiadai kwa nini uharibu uhusiano na nduguyo kwa kile kudaiana?
5.       Kumdamini mtu mwingine.
Halii hii ni ile hali ya mtu mwingine kukopa na kudaiwa Endapo hatalipa wewe uliye mdamini utalipa badala yake au kwa niaba yake Biblia inasema ujihadhari na hilo Mithali 6;1-5. Unaweza kujikuta unalipa madeni yasiyo kuhusu na kuruhusu mtikisiko wa uchumi kwenye familia yako au miradi yako.
6.       Ukopaji wa vitu dukani.
Katika mazingra Fulani hapa Tanzania tutajikuta tunakopa madukani au tunakuwa na vidaftari kasha tunalipa baadaye hili ni jambo zuri lakini inapotokea unachukua vitu kwa kukosa busara na ukajikuta una deni kubwa kuliko uwezo wako somola uchumi linakataza hali hiyo kwani haina tofauti na ukpaji wa fedha.
7.       Kutokubajeti /au kushindwa kusimamia mpango wako wa bajeti.
Moja ya namna nzuri ya kutatua migogoro ya kifedha nyumbani ni kuwa na bajeti au mipango ya pamoja  ya namna ya kutumia fedha,watu wengi hawapendi au hawana Tabia ya kukaa pamoja na kupanga  namna ya kutumia Fedha ,mara nyingi inaonekana kama jambo gumu au wengine wanafikiri si vizuri kufikiri kuhusu kesho kwa sababu ya andiko hili “Mathayo 6;34” Basi msisumbukie ya kesho kwakuwa kesho itajisumbukia, kumbuka kuwa wale wanawali watano waliitwa wapumbavu kwa sababu hawakujua bajeti hivyo walichukua mafuta ya taa yasiyotosheleza kumsubiri bwana harusi, Ni muhimu kupanga isipokuwa kama wakristo ni muhimu kupanga pamoja na Mungu (Yakobo 4;13-15).Katika kubajeti ni lazima bajeti izingatie maeneo makuu matatu Maisha yenu nyuma, mlipo na mnakokwenda, au kipato, matumizi na akiba
                                                                                                                                                             
                        Utokako                             Ulipo                                    Baadae            

Sifa kuu tatu za bajeti;-

1            Unabajeti kulingana na kiwango ulichopata au unachotarajia kukipata
2            Unabajeti kulingana na kiwango cha matumizi unayotaka kutumia
3            Unahifadhi akiba kulingana na Kiwango ulichokusudia kukiweka akiba
Bajeni ni muhimu ikazingatia maswala ya utoaji kwa ajili ya Mungu ushauri ufuatao unashauriwa kwa wanauchumi wa Kikristo kugawa mapato yao wakati wa kubajeti
Zaka 10%
Akiba 20%
Matumizi 70%
Kwa msingi huo endapo mtu anakipato cha laki moja 100,000 atatakiwa kuoa zaka 10,000=10%, Akiba 20,000=20% na 70,000=70% Matumizi.
8.       Kuishi zaidi ya uwezo au kipato.
Hii inaitwa hali ya kukosa kiasi ni hali ya kuishikwa ushindani .n.k. kila mtu ni lazima ajifunza kuishi kwa kadiri ya neema  aliyopewa na kuwa na  subira Mithali 25;8.
9.       Kiburi.
Kibiri ni adui mmoja mkubwa sana wa mafanikio na kuna uwezekano wa kufungua mlan wa madeni ni moja ya hatari inayoweza kumfana mtu akafilisika Mithali 16;5, 18-19,11;2 unapotaka kushindana na mtu mwenye kipato kikubwa zaidi yako unaweza kujikuta uko pabaya usiige kunya kwa tembo wala usishindane na mtu mwenye kipato kikubwa zaidi yako.
10.   Kumbuka kuondoa nadhiri Zaburi 66;13-16
Ukimuwekea Mungu nadhiri usikawie kuiondoa ndivyo Biblia inavyotufundisha hapa tunazungumzia ahadi za utoaji ambazo wau huziweka kisha wakasahau au kushindwa kuziondoa
NAMNA YA KUTOKA KATIKA MADENI.
1.       Maombi – Muombe Mungu akupa hekima  na namna na jinsi ya kuondoka katika madeni au kuepuka madeni
o   Kubaliana na hali halisi kuwa una madeni ukijua kuwa utajikwamua kumbuka kuwa hata serikali zinadaiwa kwa hiyo usikatishwe tama na kudaiwa
o   Mweleze Mungu kuwa unadaiwa na umekosea kuishi katika hali ya madeni
o   Mshukuru Mungu kwa kila jambo
2.       Orodhesha madeni yote uliyo nayo katia karatasi
o   Panga namna ya kushughulikia madeni yako
o   Tafuta namna ya kuongeza kipato
o   Anza kulipa madeni madogo madogo na yale yanayokuumiza au anza na makubwa malizia na madogo madogo
o   Panga kipindi maalumu cha kumaliza na kutokomeza madeni
o   Onea vizuri na  mdeni wako au anayekudai
o   Omba kusamehewa madenikama ikiwezekana Mathao 24;18-22,23-27
3.       Kuwa na tabia ya utoaji
o   Utoaji unatabia ya kutengeneza njia mbili utoaji na upokeaji hizi ni njia mbili zisizoachana Wafilipi 4;15 Yesu alisema wapeni watu vitu nanyi mtapewa kwa kipimo cha kushindiliwa na kusukwa sukwa ndivyo watu watakavyowatendea ninyi Biblia inasema
o   Kuna atawanyae  na huongezewa Mithali 11;24-25
o   Sadaka nzuri siku zote ni kile tunachokiona kuwa ni cha muhimu kwetu
o   Utoaji huleta Baraka kwetu ni heri kutoa kuliko kupokea
4.       Madeni na hasara zinapotokea jiulize kama ni uvamizi au upinzani wa adui
o   Endapo unaona vitu vina vinavunjika vunjika au ngo’mbe wako wanazaa dume tu au anazaa watoto wanakufa  unapoibiwa au kutapeliwa
o   Unapogunda kuwa ni upinzani kemea na usikubalikudhani kuwa kila kitu ni kawaida tu
o   Jiulize kama Mungu anakujaribu  ili kwamba usinung’unike Kumbu  8;26, Zaburi 66;10-11
5.       Jifunze kuridhika ni muhimU kujiuliza kuwa madeni yako yanatokana na nini je ni hali ya kutokuridhika kama ndivyo basi muombe Mungu akupe kuridhika

NAMNA YA KUPATA MTAJI NA ELIMU YA MIRADI
Ø  Tambua kitu au vitu gani vinaweza kuwa mtaji wa biashara zako au mahali pa kuanzia
Ø  Ishi maisha rahisi yakubali na kuyapenda ili kuzalisha zaidi
Ø  Jenga tamaduni ya kifamilia  usiwe na tabia ya kukusanya watu wengi tegemezi zaidi ya wale wa muhimu wa damu  isipokuwa inapokuweko sababu ya muhimu inayokuhitaji kufanya hivyo
Ø  Tafuta kazi ambayo ina kipato kikubwa zaidi
Ø  Tafuta uwezekano wa kupata fedha zaidi
Ø  Jiendeleze kielimu au endeleza mbinu za ujasiriamali
FAIDA ZA MTU MWENYE UCHUMI MZURI.

A:   HESHIMA.
1.      Maisha anayamudu.  Chakula, mavazi, nyumba.
2.      Akiba  ya watoto: (                       12: 14b,)
KIJANA – MAANDALIZI KABLA YA KUOA.
B.   KUONDOKANA NA UMASIKINI
         Baada ya kufikiri ule nini
         Unywe nini, uvae nini;
        Ukale wapi, usafiri, uhubirije n,k
          (2 Nyakati 9: 13- 28) 20:  22)   vip.
C.   KUMTUMIKIA MUNGU KWA UHURU,
Ø  ZAKA
Ø  SADAKA
Ø  MICHANGO
Ø  KUSAIDIA WENGINE
Ø  UJENZI , KUHUBIRI N.K
Ø  MF. DORKAS (MD0) KORNELIO.


FUNGUO KUMI NA MBILI ZA MAFANIKIO
Mungu alituumba kwa makusudi yake muhimu kabisa na kabala ya kutuumba aliweka mpango wa kusudi la kutuumba kwake, kwa kawaida fundi vyuma anapotaka kutengeneza geti la  hawezi tu kukata vyuma kabala hajabuni  ni geti la namna gani  anakusudia kulijenga , na kuwa litakuwa na sura gani ? Kadhalika Mungu naye alipotuumba alituuumba kwa kusudi hivyo ili tuweze kufanikiwani muhimu kwetu kurudi katika kusudi la Mungu la kutuumba na hiziz ndizo funguo za mafanikio kwetu.
1.       Tafuta kwanza ufalme wa Mungu.
Moja ya njia kubwa ya mafanikio au ufunguo wa mafanikio katika maswala ya uchumi ni kuhakikisha kuwa tunatafuta kwanza ufalme wa Mungu hapa tunazungumzia maswala yaimani Mathayo 6;33 wakristo wengi inapotokea maswala ya kiuchumi yana wachanganyia Mungu anakuwa hapewi kipaumbele
2.       Mtukuze Mungu katika kila ulifanyalo.
Wakati mwingine ili tufanikiwe ni muhimu kwetu kumtukuza Mungu katika kila tulifanyalo kuwa na mafanikio ya kifedha na mali bila kukumbuka kuwa tumeumbwa kwa utukufu wa Mungu kutapalekea mafanikio yetu kuishia pabaya  wengi wa watu waliofilisiwa na Mungu ni wale ambao hawakujua  au walikataa kwa kusudi kumpa Mungu utukufu na kumuheshimu kwa mali zao Efeso 2;10,1Koritho 10;31 Mali na fedha wakati mwingine  zinawaongoza watu katika kupingana na makusudi ya Mungu Yona kwa kuwa alikuwa na fedha alilipa nauli  ili kukimbbia makusudi ya Mungu Yona 1;1-3, 17,3;1-2 Laini Nehemia kwa kuwa alitaka kujenga ukuta kwaajili a utukufu wa Mung Mungu alimpatia kila kilichohitajika, watu wengine humtii Mungu baada ya kukongolewa kwa hali zao za uchumi mfano ni Yusufu upako wa kupelekwa juu au Musa upako wa kupelekwa chini.
3.       Ili tuweze kufanikiwa tunapaswa kuyatii mapenzi ya Mungu.
Adamu na Hawa walikuwa na uchumi mzuri walipokuwa katika Bustani ya aden wakiyatii mapenzi ya Mungu, kuyakataa mapenzi ya Mungu kuliharibu sio tu hali zao za kiroho bali pia halizao za uchumi, kuyatii mapenzi ya Mungu ni kuishi sawana kanni za Mungu na Neno lake Yoshua 1;5-8,1Falme 2;1-3 siku zote mtu asiposikiliza  sauti ya Mungu anaweza kujikuta anaingia katika halia ya kutokufanikiwa katika Torati mafaniko yalikuwa ni sambamba na ushikaji wa Toarati ya Musa mtumishi wa Mungu.
4.       Lazima tukubali kuwa Baraka kwa wengne.
Mungu alipombariki Ibatrahmu alimweleza wazi kuwa kusudi la kumbariki ni ili awe Baraka kwa wengine Mwanzo 12;2 Mungu anachukizwa na ubinafsi au choyo wastu weni wanapotoa hata kwa Mungu hawatoi kwa karimu wanatoa kwa moyo wa choyo au wanatoa ilikwamba Mungu awape  ukweli ni kuwa  tunampa Mungu kwa sababu vitu vyote ni mali yake na kila kitu kinatoka kwake 1Nyakati 29;14-15.
5.       Uwe na moyo wa mafanikio.
Moja ya vizuizi vikuu kwa mafanikio yetu a uchumi ni kuwa na Moyo wa kimasikini mtu mwenye mawazo ya kimasikini ndiye mtu mwenye moyo wa kimasikini Povert of Mind hiki ni kikwazo kikubwa, watu wa aina hii huwaza kuwa hawawezi,Haiwezekani, nitashindwa,ni lazima wakati wote tunapojaribu mambo tuwe na mawazo au mtazamo wa kufanikiwa A winngi attitude Yabesi ni moja ya mfano mzuri wa watu waliokuwa na mawazo ya kimafanikio hata pamoja na kuwa alikuwa duni hakukubali kuwa katika hali hiyo 1Nyakati 4;9-10.
6.       Tafuta Fedha za kuwekeza.
Ni muhimu kufahamu kuwa moja ya changamoto kubwa ya kufanikiwa kiuchumi ni pamoja na kutafuta fedha za kuwekeza, Hakuna ndoto yoyote ya mafanikio ya kiuchumi inayoweza kutimizwa na kuja kuwa kweli mpaka fedha za uwekezaji zimepatikana ni muhimu kufahamu kuwa ni gaharama sana kpata fedha kwaajili ya uwekezaji
§  Badili mtindo wa maisha - Wakati mwingine itakulazimu kutumia kitu Fulani kwa muda mrefu bila kukibadilisha Mfano usibadilishe simu yako ya mkononi kwa kukimbizana na fashion, au gari yako tumia kwa muda wa kutosha, peleka watoto wako shule za serikali zuilizo nzuri badala ya Private au inafsi, Nunua vitu kwa ujumla na tumia vizuri badala ya kununua reja reja, ukinunua kitu nunua kitu kizuri kinachodumu na sio kitakachoharibika haraka kwa sababu ya urahisi wa bei.
§  Endeleza Mbinu – Kama bado ni kijana jiendeleze kwa kusoma kuongeza Cheti kunaweza kukusaidia kuongeza kipato, jifunze mbinu mbalimbali za kibiashara na pia kujifunza kupika vitu kama keki na shughuli nyinginezo.
§  Badilisha kazi – Kubadilisha kazi hapa tunamaanisha kutoka katika kazi yenye kipato kidogo kwenda kwenye kipato kikubwa ikiwa ni pamoja na penisheni kwa maisha ya baadaye, wakati mwingine unaweza pia kuhama kutoka eneo moja kwenda eneo linguine kutoka kwenye mzunguko mdogo wa fedha kwenda kwenye mzunguko mkubwa wa fedha, au kutoka eneo ambalo mazao ulani hayasitawi au hakuna rutuba kuelekea kwenye eneo lenye rutuba, au kutoka katika aina ya biashara ndogo kuelekea kwenye biashara kubwa
§  Ishi maisha rahisi na ridhika nayo – Watu wengi wanaweza kuishi maisha rahisi na wakaridhika, hata kama una gari inayohitaji mafuta unaweza kuwwa na wakati unapanda daladala kama watu wengine wa kawaida
§  Punguza safari zisizo na msingi – moja ya sehemu inayotumia fedha sana ni maeneo ya usafiri badala ya kutumia mabasi ya kifahari luxury tumia ya kawaida kwani yote hufika au hutumia muda unaolingana
7.       Epuka utajiri wa haraka haraka – Paulo mtume alisema shina moja la mabaya ya kila namna ni kupenda fedha lugha hii ina maana ya kuweka mbele maswala ya utafutaji mali bila kujali sana maswala kuhusu Mungu, epuka njia zenye utata za kutafuta utajiri au fedha kwa njia za mkato mfano uuzaji wa madawa ya kulevya una fedha sana na utajiri wa haraka lakini ni kinyme na mapenzi ya Mungu na serikali njia yoyote ya kuktoa kwa harakaharaka sio njia nzuri
8.       Jifunze tabia ya kujiwekea akiba - uthamani wa mipango yote ya utafutaji wa mali unakamilisha sio kwa kile unachoingiza bali kwa kile uachoweka akiba unaweza kuweka asilimia kumi ya mapato yako kila mwaka na ukafanya hivyo hata kwa miaka 30 na kwa kufanya hivyo utajikuta unafikia wakati wa kujilipa mwenyewe wengi hufikia hatua ya kuwas wazee wakiwa masikini kwa sababu ya tabia ya kuto kujiwekea akiba na kujilipa mwenyewe.
9.       Beba jukumu la maswala ya uchumi wako wewe mwenyewe – moja ya njia inayoonyesha ukomavu ni uwezo wa kubeba majukumu yako wewe mwenyewe “Blame mania”Badala ya kulaumu wengine kwa sababu ya umasikini ulio naoni lazima ukubali kujilaumu mwenyewe, kama hujali swala la kujishughulisha na fedha wewe mwenyewe fedha zako zitawafanyia kazi wengine.
10.   Jifunze kukataa madeni – siku zote anayekopa ni mtumwa way eye akopeshaye alisema mfalme sulemani,Moja ya maadui wakubwa sana wa uchumi na maendeleo ya kifedha ni madeni, kuna falsafa  ambayo imeenea  duniani siku hizi  kwamba mtu atumie fedha za mtu mwingine “Other peoples money” OPM, kwa kweli hii ni hatari sana kwa maendeleo yako ya kiuchumi yaani kuwa na madeni, ziko sababu nzuri zinazoweza kukulazimu uwe katika Deni  lakini kwa ujumla sio vema sana kuwa na madeni madeni hupunguza kiwango chako cha maisha  yaani unafanyika masikini, endapo itakulazimu kufanya hivyo tafuta mikopo yenye masharti nafuu, Endapo unalazimika kukopa lazima ujiulize maswali ya msingi yafuatayo ;-
§  Je  ninaweza kulipa deni hilo keshi
§  Je ninaweza kulipunguza katika siku chache zijazo?
§   Je lina msaada wa kiuchumi na manufaa kwako?
11.   Wekeza kwa ajili yako -  Kanuni hii inataka uhakikishe kwamba fedha yako haifanyi kwaajili ya wengine bali kwaajili yako, sio tu ifanye kazi kwaajili yako lakini itumike kwa hekima kukunufaisha, endapo utatoa fedha zako zitumike na wengine itakupasa kuhakikisha kuwa wanapokurudishia unafaidika na faida sawa na wakati unapokwenda shule unatoa fedha unapata elimu ama unaweza kuwa na biashara yako mwenyewe ukaingia gharama kuifanya kisha  ukafaidika na faida zake zote wewe mwenyewe
12.   Usifungiwe nira pamoja na wasioamini – 2Koritho 6:14-18 Kwa wale wanaojishughulisha na maswala ya uchumi wanapaswa kufahamu kuwa hwapaswi kufungiwa nira na wasioamini, hii hujumuisha maswala ya uchumba, ndoa urafiki wa Karibu vyama vya siri na hatimaye Biashara uhusiano wetu na watu wasiookolewa unaweza kuwa katika maswala ya ujenzi wa jamii na uchumi na katika kuwaonyesha upendo wasioamini ili kwamba wapate kuokolewa, uhusiano wa Karibu na wasioamini unaweza kuathiri uhusiano tulionao na Kristo, mchangamano huo sio wa kukutenga kabisa ulimwenguni bali ni wa kujihadhari na  mfumo wa uovu wa ulimwengu na makubaliano na shetani kwa namna moja au nyingine tunapofanya biashara na watu wasiomcha Mungu ni rahisi kujikuta tukiingia katika matatizo yaliyo kinyume  na mpango wa Mungu.

Tunapohitimisha somo hili kumbuka Zaburi ya 23 1;-6
Bwana ndiye Mchungaji wangu
Sitapungukiwa na kitu,
Katika malisho ya majani mabichi hunilaza
Kando ya maji ya utulivu huniongoza,
Hunihuisha nafsi yangu na
Kuniongoza
Katika njia za haki Katika njia za haki kwaajili ya
Jina lake.
Naam nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti
Sitaogopa mabaya
Kwa maana wewe upo pamoja nami
Gongo lako na fimbo yako vyanifariji
Waandaa meza mbele yangu
Machoni pa watesi wangu
Umenipaka mafuta kichwani
Pangu,
Na kikombe change kinafurika
Hakika wema na fadhili zitanifuata
Siku zote za maisha yangu
Nami nitakaa nyumbani mwa
BWANA milele.
Ndimi Rev. Innocent Kamote 
Mkuu wa Wajenzi mwenye hekima
 

Maoni 27 :

merit hope alisema ...

(Merithope6@gmail.com)

Habari am Bibi, kiutamaduni na. Taasisi halali na kuaminika mkopo kwa Taasisi, er kutoa nyumbani mikopo, mikopo ya gari, hoteli mikopo, kutoa kibiashara, ambao lazima update wote wa hali ya kifedha duniani / kampuni ya kuwasaidia wale ambao kusajiliwa wakopeshaji fedha mikopo binafsi, rehani, mikopo ya ujenzi , kiwango cha riba ya 2% nk mji mkuu, mikopo ya biashara na mikopo mbaya mikopo kazi, kuanza up. Sisi kufadhili mradi katika mkono na kampuni yako / washirika na napenda kutoa mikopo binafsi kwa wateja wao kutoka USD $ 12,000 kwa $ 8,000,000, Euro na paundi tu. Mimi kutoa mikopo ya biashara,
mikopo binafsi, mikopo ya wanafunzi, gari mikopo na mikopo kwa kulipa bili. kama wewe
haja mkopo una kufanya ni kwa ajili yenu kuwasiliana nami moja kwa
Katika: (merithope6@gmail.com)
Mungu akubariki.
Kwa dhati,
Bibi: sifa Hope
Barua pepe: (merithope6@gmail.com)

Kumbuka: majibu yote upelekwe kwa: (merithope6@gmail.com). wasiliana nasi kupitia barua pepe kwa habari zaidi

Unknown alisema ...

Salamu Kila moja.

i am Mr Paul Williams binafsi mkopo Taasisi, sisi ni vyombo vya kibinafsi kutoa kila aina ya mikopo kwa watu ambao ni kifedha chini na katika mahitaji ya msaada wa kifedha, sisi kutoa mikopo kwa kiwango nafuu sana bila matatizo yoyote. kampuni yetu ni vizuri kusajiliwa na uwezo wa kutoa mikopo kwa watu binafsi na kushirikiana miili katika mazingira mazuri. huduma zetu ni haraka na rahisi. kama wewe ni nia ya kupata mkopo kutoka kwetu kindly wasiliana nasi juu ya kampuni yetu email: paulwilliamsfinance@gmail.com

kutembelea sisi leo kwa ajili ya huduma zetu za kuaminika
Regards
Mr Paul Williams.
Kampuni pepe: paulwilliamsfinance@gmail.com
Wasiliana nasi sasa.

Unknown alisema ...

Salamu Kila moja.

i am Mr Paul Williams binafsi mkopo Taasisi, sisi ni vyombo vya kibinafsi kutoa kila aina ya mikopo kwa watu ambao ni kifedha chini na katika mahitaji ya msaada wa kifedha, sisi kutoa mikopo kwa kiwango nafuu sana bila matatizo yoyote. kampuni yetu ni vizuri kusajiliwa na uwezo wa kutoa mikopo kwa watu binafsi na kushirikiana miili katika mazingira mazuri. huduma zetu ni haraka na rahisi. kama wewe ni nia ya kupata mkopo kutoka kwetu kindly wasiliana nasi juu ya kampuni yetu email: paulwilliamsfinance@gmail.com

kutembelea sisi leo kwa ajili ya huduma zetu za kuaminika
Regards
Mr Paul Williams.
Kampuni pepe: paulwilliamsfinance@gmail.com
Wasiliana nasi sasa.

Unknown alisema ...

ATTENTION ATTENTION ATTENTION

Mimi ni Mheshimiwa Smith Jones Alpha Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni binafsi mkopo, sisi kutoa mkopo kwa kiwango cha chini sana maslahi ya 1.5%. kama una kukataliwa na makampuni mengine mkopo, taasisi za fedha, Benki, kuangalia tena sisi ni hapa kukusaidia kutatua tatizo hilo yako haraka. sisi kutoa kila aina ya mikopo kama vile mikopo elimu, mikopo ya biashara, mkopo nyumbani, Kilimo mkopo, mkopo kibinafsi, Auto mikopo na sababu nyingine nzuri, kama vile ukitaka kuanzisha biashara, kampuni yetu inaweza kusaidia kwa mkopo. Sisi pia kutoa mikopo kutoka 5,000 - 2,000,000,000.Ruble, Dinar, Dola, Euro, na paundi, kwa kiwango cha 1.5%. Muda wa miaka 1- 50 kutegemea na kiasi unahitaji kama mkopo na wakati unahitaji kulipa nyuma. mkopo wetu imara ni kuwa nyuma na kuungwa mkono na Umoja wa Mataifa, kwamba ni kwa nini sisi tu kupata 1.5% kama kiwango cha maslahi yetu si kama taasisi nyingine za fedha kwamba anapata 2%, 3% au hata 5% kutoka clients.Get yao nyuma na sisi kwa habari zaidi kupitia barua pepe yetu: smithjonesloanfirm@gmail.com.

Regards, MR SMITH ALPHA JONES.

Bila jina alisema ...

Siku njema Mimi ni binafsi Taasisi mkopo, i unataka kuwajulisha wote kwamba sisi kutoa kila aina ya mkopo kama vile mkopo madeni ya kuimarishwa mkopo ofisi mkopo wa biashara binafsi mkopo
mkopo nyumba refinancing mkopo na hivyo zaidi katika chini
riba ya 3%. Kama nia ya kuwasiliana nasi kwa siku.
kupitia barua pepe: edmark.co.Ltd@gmail.com

Unknown alisema ...

Siku njema,

Sisi ni halali And Reputable fedha Wakopeshaji. Sisi mikopo fedha nje kwa watu binafsi katika haja ya msaada wa kifedha, sisi kutoa mkopo kwa watu kwamba wana mikopo mbaya au katika haja ya fedha za kulipia bili, kuwekeza katika business.Have Umekuwa kuangalia kwa mkopo? una wasiwe na wasiwasi, kwa sababu wewe ni katika mahali pa haki i kutoa mkopo kwa kiwango cha maslahi ya 2% hivyo kama wewe ni katika haja ya mkopo i nataka kuwasiliana tu na mimi kupitia hii ya mitaani email: mobilfunding1999@gmail.com

TAARIFA LOAN MAOMBI zinahitajika KUTOKA KWAKO.

1) Majina Kamili: ............
2) Jinsia: .................
3) Umri: ........................
4) Nchi: .................
5) Namba ya Simu: ........
6) Kazi: ..............
7) mapato ya kila mwezi: ......
8) Loan Kiasi Inahitajika: .....
9) Loan Duration: ...............
10) Madhumuni ya Mikopo: ...........

Shukrani kwa yako Ushirikiano

Kila la heri

Unknown alisema ...

Siku njema,

Sisi ni halali And Reputable fedha Wakopeshaji. Sisi mikopo fedha nje kwa watu binafsi katika haja ya msaada wa kifedha, sisi kutoa mkopo kwa watu kwamba wana mikopo mbaya au katika haja ya fedha za kulipia bili, kuwekeza katika business.Have Umekuwa kuangalia kwa mkopo? una wasiwe na wasiwasi, kwa sababu wewe ni katika mahali pa haki i kutoa mkopo kwa kiwango cha maslahi ya 2% hivyo kama wewe ni katika haja ya mkopo i nataka kuwasiliana tu na mimi kupitia hii ya mitaani email: mobilfunding1999@gmail.com

TAARIFA LOAN MAOMBI zinahitajika KUTOKA KWAKO.

1) Majina Kamili: ............
2) Jinsia: .................
3) Umri: ........................
4) Nchi: .................
5) Namba ya Simu: ........
6) Kazi: ..............
7) mapato ya kila mwezi: ......
8) Loan Kiasi Inahitajika: .....
9) Loan Duration: ...............
10) Madhumuni ya Mikopo: ...........

Shukrani kwa yako Ushirikiano

Kila la heri

Bila jina alisema ...

Habari Mpenzi wangu,
i am David Cruz ya Los Angeles katika Marekani kwa ajili ya kushuhudia kampuni hiyo ni hisia za binadamu na Mungu kuogopa watu, ambao nilikutana katika yahoo majibu katika si chini ya masaa 48, nilikuwa kutafuta kampuni zilizokopwa binafsi ambapo i wanaweza kupata usawa mkopo 590,000us inakadiriwa dola .so i aliona mtu kushuhudia kwa makampuni ambayo kutoa wake mkopo wa dola takriban 590,000us katika masaa 24 benki 'Kisha i kuwasiliana na kampuni kwa sababu i hawaamini ushahidi, hivyo i tu alisema basi mimi kujaribu kama kampuni inaweza kusaidia nje ya matatizo ya kifedha ni, Mheshimiwa Smith Alexanda mail yangu na yeye i na kujaza fomu ya kutuma mimi kwamba zitawawezesha kuendelea kwa mkopo mara moja na i hawana na i kufuata yote mchakato na wao alinipa, hivyo kushangazwa mkuu wa mkopo wangu alikuwa uhamisho wa akaunti ya benki si chini ya masaa 24. Sijui ni aina gani ya matatizo ya kifedha kwamba una au una ndoto ya kuwa na nyumbani yako mwenyewe. Makampuni haya ni uwezo wa kufanya ndoto yako ya kweli ya barua pepe ni sasa (smithloanfirm2016@gmail.com) na utakuwa na furaha kama sisi sasa i
Asante

Bila jina alisema ...

Siku njema,
Je, unahitaji haraka mkopo kuanza
up biashara, au unahitaji mkopo
kwa refinance, Je, unahitaji mkopo kwa
kulipa deni? Je, unahitaji mkopo
kununua gari au nyumba? Kama ndiyo wasiwasi
tena, Tunaweza kukusaidia !!! mawasiliano
nasi sasa kupitia E-mail kwa haraka yako
mkopo.
E-mail:
davidadelekeloancompany@yahoo.com
Asante.
Mr David Adeleke
-

Unknown alisema ...

Dear Valued Customer,

Do you need an urgent financial credit ***? * Very fast and direct transfer to your bank account * Repayment starts eight months after you get the money bank account * Low interest rate of 1% * Long-term repayment (1-30 years) Height * Flexible ***then monthly payment *. How long will it be financed? After submitting the application *** You can expect a preliminary answer less than 24 hours funding in 72-96 hours after receiving the information they need yours.

Contact this legitimate and licensed company authorized give financial assistance to anyone For more information and the application form ***

OUR COMPANY CONTACTS :
Company Email : (anatiliatextileltd@gmail.com)
Company Email : (Emaill: bdsfn.com@gmail.com)

I will relish the opportunity of doing business with you and also help to put your financial problems behind you by offering you a loan. You are in the right place. If serious and want to take a loan from our company, if you are interested fill the borrower"s information below so that we may commence the processing of your loan.

BORROWERS INFORMATION,if you are interested fill the borrower"s information below so that will can proceed.

LOAN INFORMATION NEEDED:

Name :
Country :
Phone number :
Amount Needed as Loan :
Purpose of Loan :
Loan Duration :
Monthly Income :
Have you applied for loan online before (yes or no)

OUR COMPANY CONTACTS :
Company Email : (anatiliatextileltd@gmail.com)
Company Email : (Emaill: bdsfn.com@gmail.com)
Company Motto : Your Happiness is our Award for Good Service (getting your financial stand is all we desire)

Thanks and do hope to hear from you soonest so that we may send you the loan Terms,Conditions and Repayment Schedule

Your swift response to this mail will be greatly appreciated.
All email must be sent to (Emaill: bdsfn.com@gmail.com)
Best Regards
Mrs. Magaret Becklas

Mendes alisema ...

Hii ni kampuni ya Canada na sisi kuwa na kusoma maelezo mafupi ya nchi yako, kuelewa sasa uchumi kuvunjika fedha. Tumeamua kusaidia kwa kutoa msaada wa kifedha, huduma ya mkopo, ruzuku na paket nyingine za kifedha. Tunatoa 2% kwa ajili ya mkopo mipango malipo ya kila mwezi. Kwa maelezo zaidi barua pepe:

Nilceia Teofilo
+1 (774-234-8947)
Barua pepe: nilceiateofiloinvestments@gmail.com

Elena Nino alisema ...

Ndugu Wanaotafuta Mkopo

Wewe katika matatizo yoyote ya fedha? Je, unataka kuanza biashara yako mwenyewe? Hii kampuni ya mkopo ilianzishwa Mashirika ya haki za binadamu duniani kote kwa madhumuni ya kusaidia maskini na watu wenye matatizo ya kifedha ya maisha. Kama unataka kuomba mkopo, kupata nyuma sisi na maelezo hapa chini ya barua pepe: elenanino0007@gmail.com

jina:
kiasi mkopo inahitajika:
Mkopo Muda:
Namba ya simu ya mkononi:

Asante na Mungu awabariki
kujiamini
Bi Elena

Bill alisema ...

Hello!

Unahitaji halali na ya haraka huduma ya mkopo?
Kwa sasa sadaka 3% Mikopo ya yote Aina mikopo ya biashara, Mikopo kibinafsi, Gari Mikopo, kilimo Mikopo, au fedha Project? Sisi kutoa mikopo kwa makampuni na watu binafsi duniani kote, konsolideringen madeni, hata kama una
alama ya chini ya mikopo na kutafuta ni vigumu kupata mikopo kutoka benki ya eneo lako au taasisi yoyote ya kifedha? , Na sasa kuwa na wakati mgumu kukabiliana na benki yako, au nyingine taasisi za fedha? Je, unahitaji haraka mkopo kama ndiyo Email yetu nyuma kupitia (ryanloaninvestment@outlook.com) sisi Kutoa kila aina ya Mikopo.

Omba Sasa na kupata fedha yako haraka!

* Kukopa kati 5000 na Euro 50,000,000
* Chagua kati ya miaka 1 hadi 30 kulipa.
* Flexible suala mkopo na masharti.

mipango hii yote na zaidi, wasiliana nasi sasa.

wasiliana nasi kupitia barua pepe: kwa ajili ya kampuni ya mkopo yeyote aliyenisaidia hapa ni maelezo yao mawasiliano (ryanloaninvestment@outlook.com)


kuhusu
Management.
Wito simu: +27 (0603170517)
Wasiliana Speedy yako Loan Sasa!

Unknown alisema ...

Loan Kutoa @ cha 2% !!!

kampuni yetu ni shirika ya kisheria ambayo iliundwa kusaidia watu ambao wanahitaji msaada, kama vile misaada ya kifedha. sisi ni USA msingi kampuni ya fedha.
Hivyo kama wewe ni katika matatizo ya kifedha katika fujo fedha, na unahitaji fedha ya kuanzisha biashara yako yenyewe, au unahitaji mkopo kulipa madeni au kulipa bili yako, kuanza biashara nzuri, au ana Matatizo zilizokopwa zaidi ya benki za mitaa, wasiliana nasi leo Barua pepe: ohioloans85@gmail.com


Mr Scotty

RAHEL COHRAN alisema ...

Hello.
Mimi ni Mr Rahel binafsi wakopeshaji mkopo ambao hutoa maisha wakati nafasi ya mkopo kwa watu binafsi, makampuni ya biashara, bima, nk Je, katika shida yoyote ya kifedha au katika haja ya mkopo wa kuwekeza au unahitaji mkopo kulipa bili yako kutafuta hakuna zaidi kama sisi ni hapa kufanya matatizo yako yote ya kifedha kitu cha zamani. Sisi kutoa kila aina ya mkopo katika dhehebu lolote fedha kwa kiwango cha 2% bila fee.I upfront wanataka kutumia kati hii kubwa ya kukufahamisha kwamba tuko tayari kukusaidia kwa aina yoyote ya mkopo kutatua kwamba tatizo.Kama yako ya kifedha ndiyo basi kupata nyuma sasa kupitia barua pepe (rahelcohranloan@gmail.com) kwa maelezo zaidi, wewe ni sana makala.

GREG OWEN alisema ...

Je! Unahitaji mkopo wa haraka, mrefu au mfupi kwa kiwango cha riba cha chini
chini ya 3%?

Gregowenloanfirm1@gmail.com

Tunatoa mkopo wa biashara:
Mkopo wa kibinafsi:
Mkopo wa nyumbani:
Mkopo wa Auto:
Mkopo wa mwanafunzi:
Mkopo wa kuimarisha madeni: e.t.c.

Haijalishi score.we yako ya mikopo ni uhakika katika kutoa nje
huduma za kifedha kwa wateja wetu wengi duniani kote.
Kwa vifurushi vyetu vya mikopo rahisi,
Mikopo inaweza kusindika na kuhamishiwa kwa mtu aliyepaa ndani
muda mfupi iwezekanavyo.
 
Ikiwa unahitaji kuwasiliana na mkopo haraka kupitia barua pepe:

gregowenloanfirm1@gmail.com

3% ya kuaminika mkopo kutoa uhakika.

GREG OWEN alisema ...

Je! Unahitaji mkopo wa haraka, mrefu au mrefu kwa kiwango cha riba cha chini
chini ya 3%?

Gregowenloanfirm1@gmail.com

Tunatoa mkopo wa biashara:
Mkopo wa kibinafsi:
Mkopo wa nyumbani:
Mkopo wa Auto:
Mkopo wa mwanafunzi:
Mkopo wa kuimarisha madeni: e.t.c.

Haijalishi score.we yako ya mikopo ni uhakika katika kutoa nje
huduma za kifedha kwa wateja wetu wengi duniani kote.
Kwa vifurushi vyenye mikopo rahisi,
Mikopo inaweza kusindika na kuhamishiwa kwa akopaye ndani
muda mfupi iwezekanavyo.
 
Ikiwa unahitaji kuwasiliana na mkopo haraka kupitia barua pepe:

gregowenloanfirm1@gmail.com

3% ya kuaminika mkopo kutoa uhakika.

Unknown alisema ...

Hi mimi ni WILLIAMS SARAH
Je! Ungetesha mkopaji / mkopo? Je! Unahitaji mkopo? Je! Unahitaji msaada wa kifedha wa haraka? Unahitaji mikopo ya papo hapo ili kulipa madeni yako, au unahitaji fedha ili kuboresha biashara yako? Tunatoa kila aina ya mikopo na viwango vya riba 2% kwa watu binafsi na kampuni yenye masharti na masharti ya wazi. Ikiwa unatoa mikopo yoyote kwa marudio yoyote, tafadhali wasiliana na sisi leo ili kupata mikopo yako leo. Tutumie barua pepe: (williamssarahloanfirm@gmail.com)

Vincent Shikhuyu alisema ...

How can I get a loan from your organization? I want to venture in transport business and afterwards hardwares.

Unknown alisema ...

Somohili ni mzurisana kiongozi wangu.nimelipendasana

WE OFFER ALL KIND OF LOANS - APPLY FOR AFFORDABLE LOANS alisema ...

Do you need a genuine Loan to settle your bills and startup

business? contact us now with your details to get a good

Loan at a low rate of 3% per Annual email us:

Do you need Personal Finance?

Business Cash Finance?

Unsecured Finance

Fast and Simple Finance?

Quick Application Process?

Finance. Services Rendered include,

*Debt Consolidation Finance

*Business Finance Services

*Personal Finance services Help

Please write back if interested with our interest rate EMAIL: muthooth.finance@gmail.com
Call or add us on what's App +91-7428831341

Bila jina alisema ...

Mimi mr samwel moroswa toka tanzania north mara naomba mkopo wa kilimo katika mifugo nahitaji kuwekeza kiwanda cha nyama.

Bila jina alisema ...

Nahitaji mkopo wa kuwekeza kiwanda cha nyama.

Bila jina alisema ...

Naomba mkopo wa kuwekeza kiwanda cha nyama

Bila jina alisema ...

Hallo nahitaji mkopo wa kuwekeza kiwanda cha nyama

Loan Offer. alisema ...

Je, unahitaji mkopo wa haraka? Tunatoa Mikopo ya Kibinafsi? Mikopo ya Biashara? Mikopo ya Nyumbani? Mikopo ya Kilimo? Mikopo ya Elimu? Mikopo ya Ujumuishaji wa Debit? Mikopo ya Lori? Mikopo ya Gari? Mikopo ya Hoteli? Mikopo ya Refinance? na Mikopo zaidi ya Shule? Mikopo ya Kuanzisha? .Tunatoa kwa riba ya 2%! Wasiliana nasi kupitia: richardcosmos5@gmail.com

Bila jina alisema ...

Habari Mtazamaji wangu mheshimiwa, naandika makala hii kuueleza ulimwengu jinsi Dr.diamond alivyomrudisha mpenzi wangu wa zamani kwangu, hii ndio sababu ya mimi kuchukua jukumu la kumshukuru mwigizaji huyu mkubwa anayeitwa Dr diamond kwa sababu kupitia wimbo wake. nisaidie maisha yangu yalizidi kujawa na mapenzi na nafurahi kusema kuwa Ex Boyfriend wangu ambaye tumeachana na mimi kwa kipindi cha miaka 3 alirudi kwangu akiniomba nikubaliwe, Hili lilikuwa tukio la kushtua kwani kabla sijawasiliana na Dr. diamonf ndiye niliyemsihi Ex Boyfriend wangu arudi kwangu lakini kwa msaada wa Dr.diamond sasa uhusiano wangu umerejeshwa. Unaweza pia kuwa na uhusiano bora ikiwa tu utamtumia barua pepe: ( drdiamondTemple@gmail.com ) WhatsApp +2349130958968