Alhamisi, 4 Februari 2016

Furaha Baada ya Kuokolewa!

Mstari wa Msingi; (Luka 15;32); “Tena kufanya furaha na shangwe ilipasa kwa kuwa huyu ndugu yako alikuwa amekufa naye amefufuka,alikuwa amepotea naye ameonekana.”

        Utangulizi;

            Mara baada yakuwa Tumeokoka ni muhimu kufahamu kuwa kuna kitu cha ziada kimetokea katika ulimwengu wa roho, Kuokoka kwa mtu mmoja kuna thamani kubwa sana Machoni pa Mungu na malaika zake akionyesha umuhimu wa kile kinachotokea katika ulimwengu wa roho kwa mtu kuokoka Yesu anafundisha hivi soma (Luka 15;10 na Luka 15;7)Hiki ndicho kinachotokea mtu anapotubu dhambi zake kwa kumaanisha kuziacha kabisa.

Mwana mpotevu
    Hata hivyo ni Muhimu kufahamu kuwa katika Maamuzi yako haya upande wapili wa adui yaani kwa Shetani na malaika zake hakuwezi kuwa na Furaha badala yake kutakuwa na Huzuni kubwa na mipango madhubuti ya kuhakikisha anakurudisha nyuma ili uendelee kuwa wake na kumtumikia katika dhambi hapa atatumia kila njia iwezekanayo kukurudisha nyuma hivyo ni lazima uzingatie mambo ya msingi yafuatayo;-

1. Anza kufuata maagizo sahihi kutoka katika Neno la Mungu;
    Wanadamu wa kawaida hasa watu wasiookoka watatumiwa kukukatisha tamaa kuhusiana na uamuzi wako huu mpya watakuita umepotea jambo la kushangaza sana kwani ulipokuwa dhambini hakuna mtu aliyepiga kelele kukuonya uache lakini mara baada ya wokovu na toba na kuyaacha yote watatokea watu kukuambia kuwa umepotea! Lazima ukabiliane na changamoto hii ukijua  ni kazi ya shetani ndani yao na kuwahurumia kwani wao ndio wamepotea soma (2Wakoritho 4;3-4) ni lazima kwako kujifunza neno la Mungu na kujua kuwa Mungu ana mawazo gani kwako; akieleza mtazamo wa Mungu kwa mtu aliyetubu Yesu alifundisha yafuatayo;-

2. Wewe ulikuwa Umepotea sasa Umeonekana;
    Ilivyo ni kwamba kabla ya uamuzi wako wa toba wewe ndiye ambaye ulikuwa umepotea, ulikuwa ni mwanakondoo mpotevu katika kundi la Kristo Hivyo Muda wote tangu uzaliwe alikuwa akikufuatilia apate kukuokoa Wachungaji wako na viongozi wako wa dini hawakukuambia ukweli bali walizidi kukupoteza hata ukasahau kuwa pumziko lako ni Yesu Kristo, Yeye aliugua na kuhuzunika kwa upotevu ule  akiwalaumu viongozi wako kwa kusaidia kukupotezaa angalia (Yeremia 50;6)Yeye Yesu alikuja duniani kwa kusudi la kutafuta na kuokoa kile kilichopotea soma (Luka 19;10).

3. Wewe ulikuwa Umekufa sasa Umefufuka;
 Mtazamo wa kibiblia ni kwamba mtu awaye yote ambaye anaishi dhambini katika hali ya kuzaliwa  yaani kwa kurithi dhambi mtu huyu ni Mfu mbele za Mungu haijalishi mbele za wanadamu wenzake  anaonekana ni maarufu kiasi gani Mbele za Mungu hakuna cha Umaarufu kwani kama ni mtenda dhambi kwa Mungu anakuwa ni mfu tu, Mtu yeyote anayeishi katika dunia hii kwakufuata kawaida zake anamfuata mfalme wa uweza wa anga hili yaani shetani ambaye hutenda kazi ndani ya wote wanaoasi maagizo ya Mungu soma (Waefeso 2;1-3),hivyo mtu anapookoka sasa ndio anakuwa hai (Waefeso 2;4-5).

 Tangu sasa jina lako limeandikwa katika kitabu cha uzima.
   Siku ile uliyokata shauri na kuchukua uamuzi wa kutubu na kuacha dhambi ni siku ya wokovu wako ni siku ya kuikumbuka sana katika Maisha yako licha ya kuwa siku ile Mbingu zilishangilia pia jina lako limeandikwa tangu siku ile katika kitabu cha uzima Soma (Ufunuo 20; 15) Hivyo mpango wowote wa kuacha wokovu na kurudi dhambini ni kujifuta mwenyewe kenye kitabu kile cha uzima Hivyo basi si busara kusababisha huzuni mbinguni kwa kurudi nyuma, (Luka 15; 32). Mtu asikutaabishe kwani kila mtu atalichukua furushi lake mwenyewe (Galatia 6; 5);-



Hakuna maoni: