Ijumaa, 5 Februari 2016

Vijana na Nguvu za Mungu !



Somo la kumi na nne

Vijana na Nguvu za Mungu

Hakuna jambo linalompendeza Mungu kama kijana kutembea na nguvu za Mungu,kila Upande ungependa kuwatumia vijana, Shetani hupenda sana vijana na Mungu hitaji sana vijana,n.k.Biblia inaonyesha jinsi ambavyo  wakati wa ujana  ndio wakati mzuri na unaofaa sana kwa kujitoa kumtumikia Mungu, Hii haimaanishi kuwa mungu hawapendi wazee au makundi mengine la hasha  ana wapenda lakini anataka uzee uwe matokeo ya kutembea na Mungu (Muhubiri 12;1-7) Kumkumbuka muumba wetu humaanisha kurudi katika kusudi la Mungu la kutuumba, shetani hakutuumba; Mungu ndiye aliyetuumba hivyo ni lazima tuishi kwa kutimiza kusudi lake,Tutajifunza somo hili kwa kuzingatia vipengele vitatu vifuatavyo;-

  • Kulitumikia shauri la Mungu.
  • Vijana na Nguvu za Mungu.
  • Vijana na kanisa la Mungu
Kulitumikia shauri la Mungu.
(Matendo 13; 36)Ni muhimu kwetu sisi vijana kuwa makini kuangalia Mungu anataka nini na kutimiza kile anachokitaka;Roho mtakatifu aliangalia kazi iliyofanywa na kizazi kilichofuata baada ya Adamu, lakini mambo waliyoyatimiza yalikuwa ni kuongeza idadi ya watu duniani tu kwa kuzaa, lakini wengi wao hawakufanya zaidi ya hayo wengi hawakutembea na Mungu (Mwanzo 5;6-21) ni Mtu mmoja tu Henoko yeye alifanya kitu cha ziada yeye alitembea na Mungu alienda na Mungu (Mwanzo 5;22-24)Mungu anataka watu ambao hawataishi duniani na kuzaa na kuongezeka tu, bali anataka  watu ambao  wanaliangalia shauri la Mungu na kulitumikia, Daudi siku zote alitaka kujua kua Mungu anataka nini na kufanya, Yeye aliitwa akiwa kijana lakini alitembea na Mungu kwa uhodari, ni lazima tumtumikie Mungu wetu tukiwa tungali vijana Yeremia,Yoshua,Yesu,nk. walitumika wakiwa vijana tu

Vijana na nguvu za Mungu
Ni muhimu kufahamu kuwa hatuwezi kulitumikia kusudi la Mungu Bila nguvu za Mungu, ili tuweze kufanikiwa kutembea katika utumishi kwa Mungu kila kijana ni lazima azingatie mambo muhimu yafuatayo ambayo yatachochea nguvu za Mungu maishani mwake kwa nini kwa sababu tunachangamoto nyingi zinazotuzunguka sisi vijana na Bila nguvu za Roho Mtakatifu ni vigumu kwetu kukabiliana nazo bila Roho. wake mambo ya muhimu ya kuyazingatia sisi vijana ni pamoja na;-
  1. Lazima tusome neno la Mungu.
Biblia inasema neno la Mungu na likae kwa wingi ndani yenu ni neno linaloweza kutusaidia katika wakati huu wa changamoto ngumu za kidunia (zaburi 119;9,Yoshua 1;7-8,!Falme 2;1-3).
  1. .Lazima Tupende kuomba kuabudu na kuishi maisha ya kumtumainia Mungu. Daniel, shedrak, Meshak na Abdnego waliweza kukabiliana na changamoto zilizowakabili kwa sababu walijaa Roho na walipenda kuomba Tumuombe Mungu atujaze kwa Roho wake kila siku.
  2. Lazima tujifunze kumfanya Mungu kuwa wa kwanza katika kila jambo (Mathayo6;33)
  3. Usijidharau wala kujiona kuwa u mtoto Mungu yu aweza kukutumia (Yeremia 1;4-7 1Timotheo 4;12-16)
  4. Jizoeze kufunga na kuomba na kufanya maombi ya alifajiri au meditations Mungu awe nawe.


Mkumbuke Muumba wako siku za Ujana wako Muhubiri 12:1-8 

Vijana na Kanisa la Mungu.
   Kanisani ndilo eneo lako la kujikuzia na kuchochea vipawa,Mtumikie Mungu kwa uaminifu kwenye kanisa lenu na chini ya Mchungaji wako waheshimu na kujionyesha kuwa wewe huna moyo wa kutaka kumuasi Mungu isibitishie jamii kuwa Mungu anaokoa vijana na anatembea nao na anawatumia hii itaondoa ile dhana ya watumishi wengi wa mungu kufikiri kuwa vijana wengi ni watenda dhambi huku wakisahau kuwa dhambi haina cha mzee wala cha kijana,kuwa karibu na watumishi wa Mungu jifinze kutoka kwao iige imani yao washirikishe mambo yako Heshimu wazazi wako, muheshimu kila mtu, simama barabara wakati wa majaribu. Mungu na akubariki sana nakutakia ujana mwema na ujazwe nguvu za mungu na uwe kiongozi bora katika taifa letu Niombee na mimi kwa kazi hii ngumu ya kutoa muelekeo kwa jamii ili niwe msaada kwa watu wengi Mungu atulinde hata tuonane,

Maoni 3 :

Unknown alisema ...

Ahsante sana mtumishi Mungu akubariki sana kwa mafundisho mazuri Na awe pamoja nawewe siku zote

Unknown alisema ...

Mungu akubariki

Unknown alisema ...

Mungu akubariki na azidi kukulinda milele,hata tuonane