Alhamisi, 11 Februari 2016

Mfululizo wa Masomo yahusuyo Uongozi wa Kanisa 9



********************************************************************
                                                  Somo ;Wajibu wa msaidizi
Somo hili ni somo muhimu katika Mfululizo wa Masomo maalumu ya uongozi wa kanisa,kukosa Ufahamu katika somo hili kutalifanya kanisa kuwa bduni na dhaifu na kuwa katika nafasi ya kushambuliwa na iblilisi na kutekeleza mipango yake iliyo kinyume na mapenzi ya Mungu ufalme wa Mungu hauwezi kustawi kama ikiwa Viongozi wa kanisa watakosa maarifa yatokanayo na kujifunza somo hili kwa msingi huhuu itakuwa sio rahisi kwa kanisa kukua na kuongezeka na kuwa kanisa la maelfu ,malaki au  mamilioni ya watu,kuwa na mafanikio makubwa katika kanisa kutategemeana na jinsi gani Viongozi watalitendea kazi somo hili Bwana ampe neema kila mmoja wetu kuipokea maarifa yatokanayo na somo hili katika jina la Yesu Amen.Tutajifunza somo hili kwa kuligawa katika vingele sita vifuatavyo;-
*      Umuhimu wa kuwepo kwa wasaidizi wa kiongozi mkuu
*      Viongozi wa kanisa kama wasaidiszi wa kiongozi mkuu
*      Sifa za msaidizi
*      Wajibu wa msaidizi
*      Madhara ya msaidizi anayewasaidia waovu badala ya kumsaidia kiongozi mkuu
*      Mbinu kubwa anayoitumia shetani kuharibu huduma ya kiongozi mkuu na jinsi ya kuikabili.

Umuhimu wa kuwepo kwa wasaidizi wa kiongozi mkuu
     Hapo mwanzoni Mungu alimuumba Adamu Mwanamume wa kwanza kuishi duiniani na kumkusudia kutawala peke yake .Hata hivyo muda usio mrefu baada ya kuumbwa kwa Adamu Bwana Mungu alisema si vema huyo mtu awe peke yake nitamfanyia msaidizi Mwanzo 2;18. Kumbe mume anahitaji msaidizi Ni muhimu kufahamu kuwa katika mambo mengi ya kifamilia yana fanana sana na kanisa Waefeso 5;22-32 Kwa msingi huo si vema kiongozi mkuukatika kanisa kufanya kazi peke yake hivyo ni muhimu kuwa na msaidizi.

Viongozi wa kanisa kama wasaidizi wa kiongozi mkuu.
     Maelekezo ya Mungu kupitia kwa mkwewe Musa yalikuwa kama hayo Si vema  Musa kiongozi mkuu kuwa peke yake bila wasaidizi, kutokana na maelekezo hayo Musa alikuwa na wasaidizi waliokuwa Viongozi wa Maelfu na mamia na wa hamsini na wa makumi,hawa walimsaidia musa kuchukua mzigo wa kuwaongoza wana wa Israel au kanisa la jangwani kutoka 18;13-26,Matendo 7;37-38. Hivyo ni muhimukuwa na mgawanyo wa wasaidizi ili kuifanikisha kazi ya Mungu Mfumo huu umefanya kazi nzuri katika kanisa la Full Gospel of Yoido Seoul Korea kwa Dr David Yonng choi na Full gospel Bible Fellowship Tanzania kwa askofu Zachary Kakobe na Yaoundé Cameroun .

Sifa za Msaidizi
Kila kiongozi msaidizi wa kiongozi anapaswa kuwa na sifa zifuatazo na kupaswa kuhakikisha anakua nazo katika maisha yake ni sifa za muhimu na za kibiblia;-
  1. Kufanana na kiongozi wake mkuu.
Nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye (Mwanzo 2;18) Yeyote asiyefanana na kiongozi wake mkuu hawezi kuwa msaidizi anayefaa Mwanzo 2;19-20, Kufanana na kiongozi wako mkuu ni kuwa na nia moja naye kama ilivyokuwa kwa Timotheo kwa kiongozi wake Paulo Wafilipi 2l;19-20 kuwa na nia moja ni pamoja na kuwa na maono mamoja na kiongozi wako, yaani yale anayoyaona, anayoyataka yawe, yote hayana budi kuonekana vilevile kwa msaidizi mipango na maono ya kiongozi mkuu hayana budi kuwa ya msaidizi pia.
  1. Msaidizi ana paswa kuwa mwili mmoja na kiongozi wake  Mwanzo 2;18-24 lazima uhakikishe kuwa unakuwa upande wakiongozi wako mkuu kwa gharama yoyote ile 2samuel 5;1-4 Nyakati 12;1,17-18 hivi ndivyo masaidizi anavyopaswa kuwa tumika pamoja naye katika mswala ya injili katika utii kwake kama mwana na baba yake Wafilipi 2;19-22 Msaidizi anayefaa hatakuwa mfuasi wa Bwana Yesu tu bali na wa kiongozi wake 1Thesalonike 1;6 msaidizi anayefaa ni yule anayekuwa tayari kuwa mfuasi wa Kristo na wa kiongozi wake mkuu.
Wajibu wa msaidizi
      Jukumu kubwa la msaidizi kwa ujumla wake ni kusaidia na sio kuwa kinyume na kiongozi wake utamsaidia kiongozi wako mkuu kushinda maadui zake kutekeleza majukumu yote pamoja naye mipango na maazimio yakewasaidizi wanapojitoa hivi kuwasaidia Viongozi wao siku zote ndipo kanisa linapoweza kuwa Jeshi kubwa kama jeshi la Mungu, Kutoka 2;16-17, Yoshua 10;6, 2Nyakati 26;1, 15 2Samuel 21;15-17 1Nyakati 12;1, 14-18, 22.

Madhara ya msaidizi anayewasaidia waovu badala ya kumsaidia kiongozi mkuu
     Msaidizi anapoamua kuwa upande ulio kinyume na mipango ya kiongozi wake mkuu mtu huyo anakuwa anawasaidia waasi na waovu na kufanya hivi ni kutafuta adhabu ya Mungu 2Nyakati 19;2 Hatuna budi kuwa waangalifu tunapokuwa Viongozi Maneno ya washirika na hata wasio washirika yatatushawishi tusiwe upande wa kiongozi wetu mkuu na hivyio kuweko na usaliti na kumsaidia shetani kazi yake jambo hili linaharibu sana kazi ya Mungu ni vizuri kuwa upande wa Nabii na utapokea thawabu ya Nabii Mathayo 10;40-41.

Mbinu kubwa anayoitumia shetani kuharibu huduma ya kiongozi mkuu na jinsi ya kuikabili
 Tangu Mwanzo shetani amekuwa akiwatumia wasaidizi kuharibu huduma za Viongozi wao wakuu,alimtumia hawa kumsaidia shetani badala ya Adamu,pale alipompa tunda mumewe ale na hivyo kuharibu huduma ya adamu Mwanzo 3;4-6,Shetani alimtumia Sipora mkewe Musa msaidizi na hivyo ilibidi Musa aambatane na Haruni badala ya Sipora Kutoka 4;18-29 Shetani alimtumia mkewe Ayubu msaidizi kujaribu kuiua huduma na maisha ya Ayubu Ayubu 2;9 alimtumia Yuda mmoja wa Viongozi wasaidizi wa Yesu kumsaliti Yesu,na hii ndio maana Yesu alimuita Yuda Shetani Yohana 6;70 kwa sababu aliifanya kzi ya Shetani Hata leo shetani huwatumia  Viongozi wa kanisa katika kuharibu mipango ya mungu kwa kanisa Ni muhimu kuwa waangalifu kuhakikisha wakati woote tunakuwa upande wa Viongozi wetu na kuwalinda na kuwatia moyo na kufanya kazi pamoja nao Sehemu nyingi duniani ziko shuhuda za kutosha zinazoonyesha jinsi Viongozi wasaidizi walivyotumika kuharibu kanisa la mungu tuwe makini kwani Viongozi katika kanisa ni Nguzo Tunapo tetereka jingo yaani kanisa linakuwa katika wakati mgumu sana Wagalatia 2;9 Bwana atupe neema Tunapochaguliwa kuwa wasaidizi kutokukubali kutumiwa na Shetani katika Jina la Yesu amen.

Hakuna maoni: