Alhamisi, 4 Februari 2016

Uwezekano wa kukataliwa na Mungu !



Mstariwa Msingi 1wakoritho 9;27 “Bali nautesa mwili wangu na kuutumikisha isiwe nikiisha kuwahubiri wengine mwenyewe niwe mtu wa kukataliwa”

           Adam na Eva wakifukuzwa katika Bustani ya Eden (Neno Eden maana yake Uwepo wa Mungu)

Tunapokuwa tumeokolewa kwa kutubu dhambi zetu kwa kumaanisha kuziacha  na kuliitia jina la bwana  na damu yake ili itutakase  dhambi zetu tunakuwa tumealikwa katika harusi ya mwana kondoo Yesu Kristo na furaha ya baba yetu aliye mbinguni, hata hivyo ni makosa kufikiri kuwa kila mtu aliyeitwa na kuokolewa kuwa atakwenda mbinguni bila kujali kuwa anafanya nini . Yako mafundisho potofu yaitwayo “Eternal Security” yanayoeleza kwamba mtu akiisha kuokolewa ameokolewa (once saved forever saved ) basi hata afanye nini  yeye ni mtoto wa Mungu na ataingia mbinguni na hutumia maandiko yafuatayo  kufundisha uzushi huo Warumi 8;33, Ni nani atakayewashitaki wateule wa Mungu?, Mungu ndiye mwenye kuwahesabia haki”Warumi 8;1”…..Hakuna hukumu ya adhabu juu ya hao walio katika Kristo Yesu” Yohana 10; 27-29 “….Nami nawapa uzima wa milele wala hawatapotea kamwe, wala hakuna mtu atakayewapokonya  katika mkono wangu” ni makusudi  ya somo hili basi kujifunza ili kuifahamu kweli juu ya jambo kama hilo ili tuwekwe huru mbali na mafundisho yaliyo potofu

Mfano wa safari ya wana wa Israel.
Safari hii ni kama mfano au kielelezo cha safari ya watu waliookolewa kuelekea mbinguni, kama vile wana wa Israel walivyookolewa kutoka Misri kuelekea kanaani, jambo la kushangaza ni kuwa  sio wana wa Israel wote waliotoka Misri kuelekea kanaani walifika. Neno la Mungu linatuonyesha kuwa wengi waliangamizwa Jangwani ili kuwa mfano kwetu 1Wakoritho 10;1-6.

Mfano wa Paulo Mtume .
Mtume Paulo ingawa alikuwa Muhubiri mkubwa wa injili na mwalimu wa Neno la Mungu mwenye wingi wa mafunuo na miujiza ya kupita kawaida iliyoambatana na huduma yake bado alikuwa anajua kuwa hajafika bado alijua kuwa anaweza kukataliwa ikiwa hata kishika kile alicho nacho mpaka mwisho 1Wakoritho 9;26-27 mtume Paulo hapa anasema hata mimi Mstari wa 26 ikiwa  Paulo angeweza kukataliwa baada ya kuitwa ni zaidi sana wewe na mimi.

Ulinganifu wa maandiko unaofundisha uwezekano wa kukataliwa baada ya kuitwa
Biblia imejaa maandiko mengi yanayotuthibitishia kuwa kuna uwezekano wa kukataliwa baada ya kuitwa, tunaona pia kumbe kuna uwezekano wa Mtu kufutwa katika kitabu cha uzima  maandiko haya ni pamoja  na
Kutoka 32;32-33, Yoshua 24;20, 1Nyakati 28;9,2Nyakati 15;2,Yeremia 18;10,Ezekiel 18;24 Ezekiel 33;12-13,Mathayo 5;13 ,10;22, Yohana 15;6,Warumi 11;22, 1Timotheo 1;19, Waebrania 3;12-14, 8;9 2Yohana 1;8, Ufunuo 22;18-19

Waitwao ni wengi bali wateule ni wachache Mathayo 22;14
Wateule ni wale ambao hata baada ya wokovu wanaendelea kumtii Mungu katika kila eneo la Neno lake, malaika walioendelea kumtii Mungu baada ya malaika mkuu Lucifer kuasi na ambaye sasa ni shetani  wanaitwa malaika wateule  soma 1Timotheo 5;21 Warumi 8;33 Biblia inaposema ni nani atakayewashitaki wateule inamaanisha wale ambao baada ya kuitwa wanaendelea  kuongozwa na kulitii Neno la Mungu hao hakuna atakayewashitaki  mtu anayempendezaa Mungu siku zote ni ngumu kupata jambo la kumshitaki kama ilivyokuwa kwa Bwana Yesu Yohana 8;29, kila mtu ambaye maisha yake yanaongozwa na neno la Mungu hawezi kuadhibiwa Warumi 8;1, Kristo Yesu ndiye neno la Mungu lenyewe Ufunuo 19;13 kila anayemfuata Yesu na kushika kielelezo chake  hataweza kuadhibiwa.

aidha ni muhimu kufahamu kuwa Biblia inaposema  kuwa wala hawatapotea kamwe wala hakuna mtu atakayewapokonya katika mkono wangu Yohana 10;28 ina maanisha nini kumbuka kuwa hakuna mtu aliyekuwa katika mikono ya Yesu kama Yuda Iskariote aliyekuwa mweka hazina  wake lakini amepotea yuko motoni  milele, pamoja na kutumiwa katika kuhubiri na kutoa pepo Yuda alipotea  ili mtu asipotee ni lazima aisikie sauti ya Yesu na pia kumfuata  maana yake ni kuwa lazima tuishi sawa na neno la Mungu  ili tusipotee Zabiri 119;9

Mambo sita ya msingi ya kuyaangalia ili tusiwe watu wa kukataliwa baada ya kuitwa
·         Maisha Yetu katika wokovu ni lazima yawe sawa na injili yuote na sio sawa na dhehebu fulani Warumi 2;16
·         Tusikubali kufarijiwa na kukataa kuonywa , kukaripiwa  na kukemewa kwa neno la Mungu  Ayubu 16;2, Isaya 30;20-21, Wafilipi 3;12-14
·         Penda mafundisho zaidi baada ya kuokoka kuliko mahubiri, mahubiri lengo lake ni kutuleta kwa Yesu na mafundisho ni kutupa maarifa ili kujua yatupasayo kujua kwani kuna aina mbili za dhambi (a). Kutenda yasiyotupasa 1Yohana 3;10 na (b). kutokutenda yanayotupasa kutenda Yakobo 4;17  bila mafundisho hatuwezi kufahamu yanayotupasa kutenda  mpaka tumedumu katika mafundisho Mambo ya Walawi 5;17
·         Tusikubali kuandamana na mkutano katika kutenda uovu,  neno mkutano maana yake ni watu wengi  hatupaswi kuridhika kufanya jambo eti kwa sababu watu fulani wengi wanafanya, wakati wa Nuhu watu wote ulimwengu mzima waliangamizwa na ni watu nane tu walioachwa hai  Luka 13; 22-23, Kutoka 23;2 tumwangalie Yesu tu na sio wanadamu Zaburi 37;37
·         Inatupasa kulifuata neno la Mungu bila kuchagua la kufuata Kumbukumbu 1; 35-36.
·         Kila unapogundua kuwa umamfanya Bwana dhambi inakupasa kutubu 1Yohana 2;1-2, kumbuka kumkana Bwana ni kujitafutia mauti Hesabu 15;30-31 tunahitaji kuvumilia hata mwisho ili kukamilisha wokovu wetu Mathayo 24;12-13. 

Hakuna maoni: