Alhamisi, 11 Februari 2016

Mfululizo wa Masomo yahusuyo Uongozi wa Kanisa 8



*****************************************************************
                                Somo ; Umuhimu wa kuwa na maono

Tunaingia katika somo muhimu sana katika Mfululizo wa Masomo haya ya shule maalumu ya uongozi na kama livyo kwa Masomo mengine somo hili umuhimu wa kuwa na maono kwa Viongozi ni somo la muhimu na tutajifunza somo hli kwa kuzingatia vipengele  vitano vifuatavyo.
*      Umuhimu wa kuwa na maono
*      Maana ya maono.
*      Makusudi ya Kuchaguliwa kuwa kiongozi katika kanisa
*      Faida za kuwa wengi katika kanisa
*      Umuhimu wa kuwa na maono kivitendo.

Umuhimu wa kuwa na maono.
    Katika Mithali 29;18 maneno pasipo maono watu huacha kujizuia  katika Biblia ya kiingereza ya KJV (King James Version) yanasomeka “Where there is no vision ,the people Perish” tungesema kwa usahii kwamba pasipo maono watu  huangamia au huacha kujizuia kuangamia.Watu wanapokosa la kufanya kuhusiana na mapenzi ya Mungu  hawana budi kuangamia kutokana na kutokuyafanya mapenzi ya Mungu. Kiongozi wa kanisa akiwa ni mtu asiye na maono yoyote  watu anaowaongoza hawataacha kujizuia kufanya yasiyo mpendeza mungu na wanaweza tu kuyafanya yanayo mpendeza mungu  kwa kufanya mapenzi yake ikiwa kiongozi ana maono.

Maana ya maono
Neno maono linalozungumzwa katika Mithali 29;18 maana yake ni “mawazo ya jinsi ya kutekeleza mipango na makusudi ya Mungu “kiongozi mwenye maono maana yake nui mtu aliyejaa mawazo ya mipango mbalimbali inayoweza kufanya makusudi ya Mungu yakatimilika ni muhuimu kwa kila kiongozi kuwa na maono hayo.

Makusuidi ya Kuchaguliwa kuwa Kiongozi katika kanisa
Mungu anamchagua kiongozi katika kanisa kwa makusudi ya kulifanya kanisa liweze kukua kuzaa matunda na kuongezeka Yohana 15;16 mungu anapendezwa na tawi linalozaa matunda hivyo ni wajibu wa kiongozi katika idara au kanisa la nyumbani au eneo lolote la maongozi ya kikanisa kuhakikisha kuwa anayafanya hayo mapenzi ya Mungu na kuufanya ufalme mzima wa mungu kukua na kuongezeka endapo tunashindwa kufanya hivyo tawi hilo litakatwa Yohana 15;2  mungu anafurahi wakati woote anapoona kuwa kiongozi katika kanisa anasababisha kanisa kukua kiroho na kiidadi na kanisa kuwa kubwa hata kufikia kiasi cha kugawanywa ikiwezekana Viongozi wa jinsi hii  ndio wanao mtukuza mungu Yohana 15;8 ni muhimu kwa kiongozi kuhakikisha kuwa nafanya jitihada mbadala ili mti huo aliokabidhiwa uzae matunda Luka 13; 6-9 mungu huonyesha furaha kuu kwa mtunzaji wa shamba la mzabibu ambaye shamba lake linazaa na kuongezeka Yohana 15;16 kiongozi wa jinsi hiii  maombi yake huwa na matokeo makubwa sana na mungu hujibu hujibu maobi ya kiongozi hyo kwa ufanisi Yohana 15;16 Hivi ndivyo ilivyo ulimwenguni kote leo Viongozi ambao makanisa yao yanaongezeka na kukua kwa kasi kubwa maombi yao huwa na nguvu kubwa ya kuleta majibu kutoka kwa Mungu Viongozi Nyakatiza kanisa la kwanza maombi yao yalikuwa na matokeo makubwa sana kwa sababu tu makanisa yao yalikuwa kwa kasi sana  bwana atupe neema ya kuwa na maono na mipango ya kanisa kubwa katika Kristo.

Faida za kuwa wengi katika kanisa
     Kiongozi yeyote wa kanisa nanpaswa kuwa na mawazo ya kukua na kuongezeka kwa kanisa lake usiku na mchana Ndiyo maana utaweza kuona kuwa Nyakati za kanisa la kwanza  walizingatia wakati woote kuhesabu idadi ya watu katika kanisa ili waone kama wanaongezeka ? Matendo 2;41,4;4,5;14,6;1,7, 9;31,11; 24,16;5. Kwa ujumla hesabu yao iliongezeka kila siku  huu ndio mukhtasari wa Nyakati za kanisa la kwanza walivyokuwa wakitenda kila siku kila kiongozi wa kanisa anao wajibu wa kuhakikisha kuwa anawapandikizia moyo washirika woote kuwa na mzigo wa kuliona kanisa linaongezeka  bila kufikia kiwango cha kuridhika na idai yeyote ni lazima tulisisitize hili tena na tena  hata lizame katika mioyo yao  pia ni muhimu kuwaelezea watu umuhimu wa kuwa wengi kwamba sio tu kunamfurahisha Mungu na kumtukuza  na kutekeleza agizo la mungu 1koritho 10;31,Lakini kukua kwa kanisa pia ni kwa faida yetu, Kanisa linapokuwa kubwa tunaweza kushirikiana na watu wengi katika matukio kama Misiba,harusi,furaha za kujifungua mtoto  n.k kunakuwa na watu wengi sana na wa namna mbalimbali wa kushirikiana nasi  na kutupa msaada sio hilo tu tuankuwa na watu wengi wa kutuombea kwani kanisa ni lazima watu wawe wanaombeana wao kwa wao
Umuhimu wa kuwa na maono kivitendo.
     Ni muhimu kwa kila kiongozi wa kanisa kujua kuwa ni mapenzi ya Mungu na ni ahadi ya Mungu kutuongeza kiroho na kiidadi katika makanisa Yetu Mwanzo 28; 3, 35; 11, Kutoka 1;7, Kumbukumbu 12;20, Zaburi115;14, Zekaria 10;7-8 ni muhimu kufahamu kuwa kiongozi wa kanisa ana nafasi kubwa ya kufanya kanisa lake likuwe na kuongezeka lakini ili kanisa likue na kuongezeka kiongozi katika ikanisa hana budi kufanya mbao ya msingi yafuatayo

  1. Kuhamasisha anao waongoza
Kwa kawaida watu tunaowaongoza huwa wanangoja tuwambie nini cha kufanya kwa kuwahamasisha ndipo wapambe moto,kwani tukikaa kimya nao hufanya hivyo ni wajibu wetu kufungua zizi la kondoo na kuwaacha watoke nje  tukilifunga tu nao wataendelea kukaa humo Yohana 10;4 Mungu hutupa kondoo ili tuwatumie na sio kuwafurahia kuona wanakaa humo ni muhimu kuwatumia kondoo kuongoza idadi ya kanisa  hivyo kukua na kuongezeka kwa kanisa ni muhimu kuwa wimbo wa kanisa letu mpaka kieleweke

  1. Kuhakikisha watu wanawaalika wageni.Zekaria 3;10.
   Ni muhimu kuhakikisha kuwa watu au wageni wanaalikwa kwa wingi katika kuhudhuria ibada zetu, watu wenye uwezo mkubwa wa kuwaalika wageni sio wale walio na muda mrefu katika wokovu hii hufanya kazi kwa kiwango kizuri kwa wale waliookoka hivi karibuni yaani wachanga wao ni rahisi kuwaalika marafiki zake, wa zamani kabla hawajamkimbia kwa sababu ya wokovu mtu aliyeokoka karibuni maisha yake hayatofautiani sana na wasiookoka  na hivyo ni rahisi kwao kuwa wenye kupatana kwa urahisi  hivyo ni muhmu kuwahamasisha wale wachanga kufanya kazi ya kuwaalika wengine  na kuacha kupiga kelele hizi kwa wale wa zamani tuwafahamishe kuwa wanapowaleta wageni watatoa taarifa kwa Viongozi ili wapenyeze ujumbe wa wokovu kwa wageni hao na kuwaleta kwa Yesu

  1. Kushuhudia. Yohana 4;28-30,39;Marko 16;15. Wale waliookoka zamani tuwahamasishe zaidi katika maswala ya kushuhudia hata kama hawajapitia katika shule maalumu ya uinjilisti tuwafundishe namna wanavyoweza kushuhudia au kuambatana nao katika shughuli ya ushuhudiaji.
  2. Kuwafuatilia watoto wachanga Waebrania 5;13,1Petro 2;2. Tusi wangojee watu kufikia hatua ya kupitia shukle ya uinjilisti ili wajifunze ufuatiliaji ni lazima tuwafundishe sisi wenyewe na kuwakomaza katika kuifanya kazi nzima ya ufuatiliaji tukafanya hivi kwa upendo tutaweza kuona matokeo mazuri bila haja ya kukemea na kukaripia hasa kama ni watoto wachanga
  3. Kuhakikisha kuwa wanapata neno la Mungu Mathayo 4;4 Neno la Mungu ni muhimu  na lina uzito mkubwa hasa katika ibada za kanisa kuu hivyo tuwasisistize watu kuja ibadani na kulisikiliza neno la mungu wakati mwingine ghata kama ni kwa njia ya kaseti.
  4. Kufanya maombi kwa ajili ya kukua kwa eneo lako au kanisa lako. Kukua kwa kanisa hakuwezi kutokea bila kuwako kwa maombi ni muhimu kuwa na maombi ya aina mbalimbali kama ya kufunga au kufanya maombi ya mapatano  na kuwa na maombi maalumu pia kwa ajili ya ukuaji wa kanisa Zaburi 2;8.
  5.  Hakikisha ya kuwa unawajali kondoo.
Imani hutenda kazi kwa upendo Wagalatia 5;6  Ni muhimu kutilia mkazo kwa uzito mno kuhusika na wagonjwa na wenye shida ,misiba wasio na nauli za kuja ibadani wanaojifungua n.k ng’ombe anayetunzwa vizuri mara nyingi hutoqa maziwa mengi na mbwa mkali ni tule anayejaliwa na kutunzwa tukipunguza matedno ya ukarimu na upendo tunashusha chini kiwango cha ukuaji wa kanisa letu na kutoa mwanya wa kwenda mahali wanakoona kuwa wanajaliwa zaidi tukipungua katika eneo hili nqa kuwataka watu watende kazi tu tutaona upungufu mkubwa upendo ndio ufunguo mkubwa wa kukua kwa kanisa

  1. Washrikishe watu malengo
Eleza juu ya mahudhurio toa ripoti za aina mbalimbali ikiwemo maswala ya fedha na matumizi waeleze juu ya ongezeko la kanisa waeleze furaha ya Mungu ya kuona wakiongezeka  kama ni kanisa la nyumbani likifika idadi ya watu 250 ni muhimu luikigawanywa na kuendelea kuwa na matawi mengi zaidi ya nmakanisa ya nyumbani au cells  hii itakuwa nifuraha kubwa kwa Mungu Ezekiel 19;10;Marko 4;30-32,.

  1. Panga mipango mwingine ya kuongezeka kwa kanisa lako.
Kiongozi mzuri ni yule mwenye ubunifu mkubwa hata zaidi ya ule tulio jifunza katika mbinu za kijeshi kiongozi wa kijeshi anatakiwa kuwa Hodari yaani Mashal huyu ni mtu mwenye uwezo wa kuwa na mbinu ambazo ni zaidi ya zile alizijifunza  hizi unakutana nazo huku huko jkatikqa uwanja wa vita  jaribu na usiogope kukosea mtu anayeogopa kukosea hawezi kuwa kiongozi mzuri Petro alikuwa mwenye kujkosea sana na Yesu alimfanya kuwa kiongozi wa kanisa ukikosea utarekebishwa na utaendelea Mbele, Mungu akubariki sana

Hakuna maoni: