Alhamisi, 11 Februari 2016

Mfululizo wa Masomo yahusuyo Uongozi wa Kanisa 4



********************************************************************
                                          Somo;     Sifa za kiongozi wa kanisa
Somo letu la nne katika Mfululizo wa Masomo ya shule hii maalumu ya Viongozi ni somo sifa za kiongozi wa kanisa tutajifunza somo hili kwa kuligawa katika vipengele vikuu viwili vifuatavyo;-

*      Sifa za kiongozi wa kanisa
*      Kiwango cha kuanzia tunapoitwa kuwa Viongozi wa kanisa.

Sifa za kiongozi wa kanisa
     Neno la Mungu linaeleza waziwazi sifa za kuwa kiongozi wa kanisa na tutakapokuwa tunaichambua sifa moja baada ya nyingine itakuwa ni rahisi kwa kila mmoja wetu kujipima na kuangalia pale palipopungua kisha kumuomba Mungu neema ya kuzifikia sifa hizi za maongozi katika kanisa kama apendavyo Mungu.
  1. Awe Mwanafunzi wa Yesu;-
Neno la Mungu linaelekeza kuwa Kiongozi wa kanisa hapaswi kuwa mtu ambaye ameokoka hivi karibuni 1Timotheo 3; 6 Baada ya mtu kuokolewa anapaswa Kwanza kujifunza Neno la Mungu na kulitendea kazi hata kufikia ngazi ya kuwa Mwanafunzi wa Yesu. Mwanafunzi wa Yesu ni mtu aliyeokoka ambaye analitendea kazi Neno la Mungu bila ubishi au kulijadili na kukaa katika neno Yohana 8;31 wao wanakuwa watii si kwa neno tu Lakini wanaelewa pia faida za utii kwa Viongozi wake utii uhuu unafananishwa na ule wa kijeshi Wafilipi 2;5-8 askari hujifunza kutii amri za Viongozi wao hata kama amri hiyo itamsababishia kifo Mwanafunzi wa Yesu hali kadhalika ni askari wa Yesu 2Timotheo 2;3,Filemoni 1;2 , hivyo Mwanafunzi wa Yesu ni mtu aliyeokoka ambaye analitii neno la Mungu na Viongozi wake wa kiroho kama askari kwani watumishi wa Mungu ni wajumbe wa Bwana wa majeshi Malaki 2;7,Filemoni1;21 Yesu Kristo aliwatuma wale thenashara kwenda kwa niaba yake  baada ya kufikia kiwango cha utii kama wa askari wa kijeshi Mathayo 11;1 Makanisa mengi hayafanikiwi kwa sababu watu hawajafunzwa kuwa kama askari hivyo kunakila aina za uasi na majadiliano kuhusu maagizo yanayotoka kwa Viongozi wao, Mtu aliyeokoka hivi karibuni ataona ni ngumu kuyatii maagizo ya kiongozi wake kama askari hivyo hafai kuwa kiongozi akiambiwakama Anania “Simama Enenda” atafanya hivyo mara moja Matendo 16;1-3.
  1. Awe mume wa mke mmoja au Mke wa mume mmoja;-
1Timotheo 3; 2, 12 Mwanamume yeyote ambaye ana mke zaidi ya mmoja au mwanamke aliyeolewa na mume mwingine wakati mumewa kwanza bado yuko hai watu wa jinsi hiyo huwa hawapewi uongozi kibiblia Kristo ni mmoja na ni kichwa cha kanisa mwili ni mmoja vivyo hivyo mume mmoja kichwa na mke mmoja mwili.
  1. Awe anayaamini mafundisho yote.
2Koritho 4;15 Kiongozi wa kanisa anapaswa kuwa ni mtu anayeshika na kuyaamini mafundisho ya imani yetu kama vilevile anavyofundishwa Tito 1;9, 2Wathesalonike 2;15 ni muhimu kwa kiongozi wa kanisa kuwa anayeamini mafundisho yoote ya kanisa lake na sio sehemu tu fulanifulani Mafundisho hayo ni pamoja na Wokovu, ujazo wa Roho Mtakatifu, Ubatizo wa maji mengi, mafundisho ya toba na Malipizi, unyenyekevu na utii, kujitenga na dunia, uponyaji na miujiza kiongozi anapokuwa anapinga baadhi ya mafundisho kama hayo ya muhimu basi huyu  ni kiongozi wa watu waliomkamata Yesu kama Yuda Matendo 1;15-17,.
  1. Awe anaisimamia Nyumba yake vema.
Kama kiongozi wa kanisa ni Mwanamume basi kama kichwa anapaswa kuwa na msimamo mkali na thabiti utakaomfanya mkewe na watoto kufuata maagizo yake kama mwili unavyotekeleza maagizo yote ya kichwa kutoka katika ubongo aidha lazima awatiishe watoto wake katika ustahivu woote yaani watoto wake wawe katika hali ya kumtii na kumuheshimu mtu asiyejua kuisimamia nyumba yake mwenyewe moja je atawezaje kulisimamia kanisa lenye nyumba nyingi? 1Timotheo 3;4-5,12.Kama watoto wa kiongozi ni wakaidi jeuri na wasiotaka kutii ni lazima ithibitike kuwa amechukua hatua kali na thabiti katika kuwazuia kufanya wanayoyafanya na sio kuzungumzia nao kwa kuwadekeza 1Samuel 2;12, 22-25, 3;12-14. Mtu ambaye atawaona watoto wake hawafuati njia za Bwana kisha akawachekea tu bila kuchukua hatua kadhaa huyo hafai kuwa kiongozi wa kanisa
  1. Awe analifahamu neno la Mungu na kujua kulifundisha kwa uhakika akionyesha tabia na Matendo yanayolingana na neno analolifuindisha.
Kiongozi wa kanisa hana budi kuwa na bidii katika kulisoma neno la Mungu kulisikia Kupitia ibada na njia za kaseti, tv, Vitabu n.k na kujifunza ili alifahamu kwa uthabiti na kumudu kulifundisha 1Timotheo 1;7;3, 2, 4;13 Tabia na Matendo yanayoendana na neno analolifuindisha hayana budi kuwa yenye kuonekana katika maisha yake Kutoka 18;21, 1Timotheo 3;1-12, Tito 1;5-8
  1. Awe na moyo wa msamaria.
Kiongozi wa kanisa anapaswa kuwa mtu aliye tayari kuchukua mizigo ya waaminio na awe tayari kufanya hivyo kwa wakati unao faa na usio faa Luka 10; 30-35, 2Timotheo 4;2.
  1. Awe Mtu asiye na upendeleo.
Mtu awaye yote anayekuwa kiongozi wa kanisa hapaswi kuwa mtu wa upendeleo kwa namna yoyote ile wako Viongozi ambao hufanya upendeleo kwa watu wa kabila lake tu au kwa wasomi na matajiri kwa ajili ya mafungu au kuipokea uso wa mwanadamu mtu wa namna hii hafai kuwa kiongozi wa kanisa Kumbukumbu 1;17, Yakobo 2;1-9.
  1. Awe mtu wa kweli na mwenye kuchukia mapato ya udhalimu
Shetani ni baba wa uongo, kiongozi wa kanisa anamwakilisha Yesu ambaye ni kweli hivyo anapaswa kuwa mkweli wakati woote Mtu mwongo hafai kuwa kiongozi wa kanisa, aidha kiongozi wa kanisa anapaswa kuwa mtu anayechukia mapato ya udhalimu Kutoka 18;21. Aidha anapaswa kuwa mbali na mizaha na tabia zozote za kuchukiza Mithali 26;18-19; 19;29.
  1. Awe mtu ambaye uasherati au uzinzi haitajwi kwake
Uasherati au zinaa ni mwiko kutajwa kwa mtu yeyote anayedai kuwa ameokoka na ni zaidi sana kwa kiongozi wa kanisa Waefeso 5;3 Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa Mithali 6;32 Kumbukumbu 1;13.
  1. Awe mtu aliyejaa imani, anayeishi maisha matakatifu na aliyejaa Roho Mtakatifu na Hekima Matendo 6;3-6
 Aidha kiongozi wa kanisa anapaswa kuwa mtu mwenye Hekima anayeishi maisha matakatifu na aliyevikwa uwezo utokao juu yaani Roho Mtakatifu Luka 24;49 Anapaswa kuwa mstari wa mbele katika imani akiamini kwamba kwa Mungu yote yawezekana.
Kiwango cha kuanzia tunapoitwa kuwa Viongozi wa kanisa.
     Baada ya kujifunza sifa hizi ni rahisi kwa kila mtu mmoja mmoja kujihisi kuwa huenda Hastahili na ana upungufu katika eneo Fulani. Ni muhimu kufahamu kuwa Mungu hatuiti katika uongozi tukiwa wakamilifu mia kwa mia Mungu hakuwaita kina Petro wakiwa kama watu maalumu wala Yakobo na Yohana hawakuwa wakamilifu kulikuwa na mapungufu kadhaa wa kadhaa katika maisha yao Hivyo si ajabu kwetu kujikuta tukiwa na mapungufu Fulani na ndio maana Mungu hutufundisha hatua kwa hatua hata kufikia kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo Waefeso 4;11-13 jambo la msingi kwetu ni kumuomba Mungu atujazilize katika kile ambacho kimepungua katika maisha yetu na kufanya sehemu yetu ya kuipokea kwa imani na kulifanyia kazi neno Yakobo 1;5-7.

Hakuna maoni: