Ijumaa, 5 Februari 2016

Vijana na athari ya Utandawazi !



Somo la kumi na tatu

Vijana na athari za Utandawazi

Utandawazi Globolaization ni mwingiliano mkubwa wa maendeleo ya kisayansi, kiteknolojia, kiuchumi, kihabari na hata kitamaduni ni mkaribiano wa mataifa makubwa yaliyoendelea na mataifa ya dunia ya tatu yanayoendelea ambapo zamani ule upande wa pili tulikua tunausikia kama mbinguni lakini kwa sasa kwa sababu tumeungwa katika utandawazi dunia imekuwa kama kijiji yaani yanayotokea upande wa pili sasa kwa sekunde tu yanakuwa  yameenea dunia nzima na lolote utakalo kulijua unalijua bila kipingamizi kupitia teknolojia kutokana na mwingiliano huu kuna athari za kitabia kimaadili na kitamaduni zinazojitokeza kwa sababu ya utandawazi.
Tutaliangalia somo hili fupi kwa kuzingatia vipengele vitatu vifuatyavyo;-

  • Athari za utandawazi kitamaduni.
  • Tofauti ya tamaduni za mashariki ,Afrika na Tamaduni za kimagharibi.
  • Mambo ya kuyazingatia.
Athari za utandawazi kitamaduni.
 Kwa kawaida watu amabao hawajawafahamu sana wazungu hupenda kuwaiga tabia zao lakini kumbuka kuwa si mambo yoote ya wazungu ni mazuri au yanafaa na hasa mataifa na tamaduni za kimagharibi,kihistoria woote tunajua kuwa ustaarabu na uungwana uko mashariki zaidi kuliko magharibi,aidha ni muhimu kufahamu kuwa kama kuna watu ambao wangeeathiriwa sana kitamaduni ni watu wa Afrika ya kusini maana wamekaa na wazungu kwa muda wa karne nyingi sana lakini kwa sababu ya tabia mbaya ya kibaguzi na unyanyasaji waliyonayo wazungu kwa watu weusi jamii ya watu wa Afrika ya kusini walitunza tamaduni zao na hata leo tunaziona bila kuathiriwa na wazungu

Tofauti ya tamaduni za mashariki Afrika na Tamaduni za kimagharibi.
  Kuna tofauti kubwa kati ya utamaduni wa Afrika na tamaduni za kimagharibi,Sisi tunathamini jamii wao wanathamini uthamani wa mtu binafsi,utambuzi wa kijamii utambuzi wa mtu binafsi,kuishi kwa umoja kuishi kibinafsi,Muingiliano wa familia kubwa familia peke yao,umuhimu kwenye matukio,umuhimu kwenye Ratiba,Maisha halisi maisha ya kanuni,kiroho,kisayansi,mazungumzo maandishi,Heshima kwa wakubwa heshima kutokana na elimu,kurithishana madaraka,kupigiana kura,Hizi ni baadhi tu ya tofauti za kiafrika na kimagharibi yapi ni maisha bora nay a kuiga na ya kibiblia ni haya tunayoishi wa afrika kwa msingi huu basi hatupaswi kufikiri tu kuwa kila kilichochema ni cha wazungu tu.

Mambo ya kuyazingatia.
  Tunaweza kuiga na kujifunza mambo ya msingi ya maendeleo kama ya kiteknolojia lakini tusiruhusu utandawazi kutuharibia tamaduni zetu wakati umefika wa sisi nasi kuwa na mambo ambayo wazungu watayaiga kutoka kwetu

Hakuna maoni: