Alhamisi, 4 Februari 2016

Yeye Ashindaye !



Mstari wa msingi Ufunuo 21;7 “Yeye ashindaye atayarithi haya nami nitakuwa Mungu wake naye atakuwa mwanangu”
                                                                       Yeye ashindaye


Safari ya mbinguni ni safari ya mashindano;

Mara baada ya kuokoka unapaswa kuwa na Ufahamu kuwa umeingia katika mashindano  ni yeye atakayeshinda ndiye atatakayeipokea taji  ya milele na milele  kila siku katika wokovu itakuwa ni siku ya mashindano  na vita lakini ni lazima tushinde  na kuumaliza mwendo kwa kuilinda imani 2Timotheo 4;7-8

“Nimevipiga vita vilivyo vizuri mwendo nimeumaliza imani nimeilinda baada ya hayo nimewekewa taji ya haki ambayo Bwana muhukumu mwenye haki atanipa siku ile wala si mimi tu bali na watu wote waliopenda kufunuliwa kwake”

Kwa msingi huo ni lazima kuvipiga vita vya imani maana pasipo imani haiwezekani kumpendeza Mungu Waebrania 11; 6 maisha ya wokovu ni maisha ya imani na kumtegemea Mungu katika kila jambo katika maombi na neno la Mungu kinachotakiwa katika mashindano haya ni kujizuia katika kila jambo linalokuja kinyume na mapenzi ya Mungu 1Koritho 9;25 “Na kila ashindanaye katika michezo  hujizuia katika yote  basi hao hufanya hivyo kusudi wapokee taji iharibikayo bali sisi tupokee taji isiyoharibika”

Unaweza kushangaa kwamba wakati unajiandaa kwenda ibadani ndipo wageni wanakujia tena wa muhimu ili usihudhurie mafundisho kumbuka haya ni mashindano ni vita na inakupasa kupambana wageni waambie twendeni kanisani pamoja kwa nini waje wakati unakwenda kanisani? Wakati mwingine siku za ibada ndo kunatokea kila aina ya vikwazo na vizuizi jua hiyo ni vita na kuwa adui yetu shetani yuko kazini kutuzuia tusiende kubarikiwa kupitia maneno ya Mungu, uwe radhi kwenda ibadani hata kama ni mbali au kama hauna nauli na utashangaa Baraka za Mungu zinamiminika kwako.

Siku zote kuanzia sasa lenga kukua zaidi kiroho na katika wokovu usikose vipindi vya mafundisho kanisani  kila unapopata nafasi soma Biblia na kufanya maombi japo mafupi mafupi  kwamba bwana Yesu akusaidie kudumu katika wokovu na kushindana  1Timotheo 6;12 “Piga vita vile vizuri vya imani  shika uzima ule wa milele ulioitiwa ukaungama maungamo mazuri mbele ya mashahidi wengi” Tumia bidii uliyo nayo usiwe mlegevu katika kujifunza  uwe na bidii yote Nunua daftari la kuandikia mafundisho yote na kuyatendea kazi na uwe na tabia ya kuyapitia , uliza lolote kwa viongozi ambalo hujalielewa vema  Warumi 12;11 “ Kwa bidii si walegevu mkiwa na juhudi katika roho zenu mkimtumikia Bwana” lolote utakalojifunza lisiiishie katika dafatari bali ulifanyie kazi kwa vitendo , usiwe msikiaji wa neno tu bali mtendaji Yakobo 1;22-24  ni muhimu kustahimili siku hadi siku  kwani tukistahimili tutamiliki pamoja naye 2Timotheo 2;12 Kama tukimkana yeye naye atatukana sisi.

Hatimaye tusikubali kabisa kurudi nyuma katika wokovu tulioupokea usimkane Yesu halafu naye aje atukane sisi, shindana hadi mwisho, Yako mengi mmno ambayo utazidi kujifunza kila siku kanisani yashike na kuyatendea kazi , siku chache zijazo nawe utakuwa mwalimu ukiwafundisha watu wengine  waliookoka nyuma yako  ili nao wasimame katika wokovu, simama  kiume  ni lazima ushinde katika jina la Yesu, zidi kwenda kanisani kwa mafundisho mengine zaidi kumbuka Ufunuo 2;7 Yeye ashindaye  nitampa kula matunda ya mti wa uzima ulio katioka Bustani ya Mungu. Ubarikiwe sana Amen.

Hakuna maoni: