Jumapili, 7 Februari 2016

JE MUHAMAD AMETABIRIWA KATIKA BIBLIA?



 Waislamu wanaamini kuwa muhamad ndiye Nabii yule.
       Hoja hii hiliigusia katika kipengele muhimu cha umuhimu wa kukabiliana na changamoto za uislamu,Kwa mujibu wa waislamu nabii muhamad  alitabiriwa katika biblia kuwa yeye ndiye nabii yule hii inatokana na swali ambalo  Yohana aliulizwa na watu waliotumwa na mafarisayo,swali hili lina maeneo makuu matatu ambayo ndiyo yanayoundiwa hoja soma (Yohana 1;12-25).Maswali hayo yaliuliza habari za Kristo,Eliya,na Nabii yule,hoja huundwa katika eneo la Tatu la nabii yule ambapo hapo ndipo hudai kuwa nabii yule ni Muhamad ambaye Yesu mwenyewe alimtabiri katika (Yohana 14;26), kama “ paraklete” kwa kiyunani yaani aliyetukuzwa au Ahmad sawa na muhamad tutajadili hilo huko mbele,Nabii huyu hudaiwa ndiye aliyetabiriwa katika (kumbukumbu la torati 18;15,18),nabii huyu angetoka miongoni mwa ndugu za wayahudi ambao ni waarabu,Mwandishi wa kitabu  kiitwacho uislamu katika Biblia  Ngariba Musa Fundi na Kawemba Mohamed Ali waliamua kujichangamsha katika ukurasa wa 13 wa kitabu hicho wakitoa madai kama hayo kwa kuthibitisha kuwa nabii huyo atakuwa kama Musa hivyo walionyesha jinsi Musa anavyofanana na Muhamad kuliko Masihi



*     Musa alizaliwa akiwa na Baba na mama sawa na Muhamad sivyo ilivyo kwa Yesu.
*     Musa alioa na kuzaa watoto sawa na Muhamad Yesu hakuoa wala kuzaa.
*     Musa alikubalika kwa watu na Muhamad, Yesu alikataliwa.
*     Musa alikuwa nabii na kiongozi wa kisiasa kama Muhamad Yesu alikataa siasa (kufanywa mfalme).
*     Musa alitoa sheria na Muhamad pia Yesu alileta neema na kweli.
*     Warithi wao waliiteka kanaani,warithi wa Yesu walihubiri tu.
*     Musa alikufa na Muhamad na walizikwa,Yesu alipaa mbinguni.
Hivyo nabii kama Musa kwa vyovyote ni Muhamad na si Yesu na hivyo Biblia imemtabiri,Tunaweza kuuweka mpango huu katika jedwali kama ifuatavyo.

         Musa
      Muhamad
       Yesu masihi
Alikuwa na wazazi wote
Alikuwa na wazazi wote
Hakuwa na baba ila mama tu
Alioa na kuzaa watoto
Alioa na kuzaa watoto
Hakuoa wala kuzaa
Alikuwa nabii na kiongozi wa kisiasa
Alikuwa nabii na kiongozi wa kisiasa
Nabii lakini si kiongozi wa kisiasa
Alitoa sheria Torati
Alitoa sheria Quran
Alileta neema injili
Warithi waliiteka kanaani
Warithi waliiteka palestina
Warithi walihubiri tu
Alikufa na kuzikwa
Alikufa na kuzikwa
Alipaa kwenda Mbinguni

Namna ya kutatua Tatizo hili.
     Tukianzia na swala la Muhamad kuwa ndiye nabii Yule kama inavyodaiwa kusemwa na Yohana katika (Yohana 1;12-26).Ni kweli kuwa kuna maswali matatu yanaulizwa katika mazingira ya andiko hili,Nataka kuwakumbusha waislamu tena katika eneo hili kuwa Biblia haitafasiriwi kama quran ambayo hujitegemea kwa kila aya,Biblia ni kitabu cha wanazuoni ni kitabu cha wasomi huwezi kuchukua andiko na kulifasiri kama utakavyo tu , Katika moja ya kanuni za kutafasiri biblia ambazo kwa faida ya wengi nitaziweka kwa mukhtasari katika somo hili huko mwishoni,Kanuni inayopaswa kutumika hapa ni kanuni ya mazingira ya kihistoria na kanuni ya kufasiri unabii, kanuni ya mazingira ya kihistoria “Principle of historical context” inasema ili mtu afasiri Biblia kwa ufasaha anapaswa kujua historia ya andiko au maandiko ili kupata maana halisi ya kile kinachozungumzwa hivyo kihistoria tujiulize ni kwanini wayahudi waliuliza maswali yale matatu?

      Kihistoria Wayahudi walimtofautisha Nabii yule (anayetajwa katika Kumbukumbu 18;15-18) na Masihi ambaye ni mwana waDaudi(Mathayo 22;41-46), wao walifikiri nabii Yule na masihi ni watu wawili tofauti,wakati wa Musa nabii ndiye alikuwa kiongozi,walipoanza kuwa  na Mfalme Mungu alihaidi kupitia Daudi kuleta kiongozi wa kifalme hivyo kimsingi nabii zote hizi zilimhusu Yesu Kristo Yeye ndiye alikuwa nabii mkuu (Luka 7;16b)na Mfalme wa wafalme(Ufunuo 19;11-16).Waislamu hawajui historia hii na wanachanganywa zaidi kwa vile Muhamadi alivyojikinai akitaka kujithibitisha kuwa  ni nabii wa kweli na kuwa naye alitabiriwa alishusha ay  a hii(Al-A-raaf mwinuko 7;157). Ayah ii inadanganya waislamu na kuwafanya watafute katika kwa nguvu katika biblia (Torati)na injili  wakidhani wataona unabii unaomhusu Muhamad,ukweli ni kuwa Yesu ndiye mwisho wa unabii na si zaidi ya hapo kama Muhamad alitabiriwa katika biblia tungelimwamini lakini bahati mbaya hayumo kabisa (Ebrania1;1-4)
Nabii miongoni mwa ndugu zako kama Nilivyo mimi, Nabii mfano wako wewe. (kumbukumbu 18;15,18)
    Mistari hii hutumiwa na wanaharakati wa kiislamu  wakifikiri kuwa inamtabiri Muhamad nabii wa Waislamu,kwa bahati mbaya kama nilivyogusia hapo awali kua Biblia au unabii hautafasiriwi kama apendavyo mtu Fulani (2.Petro 2;20-21),Waislamu hapa hufasiri biblia kama wapendavyo wao wenyewe,Hapa kanuni iliyokiukwa ya kufasiri maandiko  ni sheria au kanuni ya kifungu kizima “The Principle of context” Unaposoma maandiko ya kibiblia  kanuni hii inataka usome kifungu kizima  juu na chini pia kabla ya kunyofoa  aya moja pekee,hivyo unaposoma aya hizi kwa mfano neno “miongoni mwa Ndugu zenu” hii haiwahusu waarabu,kifungu kinaonyesha kuwa Mungu alikuwa anazungumza na  na kabila ya walawi moja kati ya kabila kumi na mbili za Israel, hivyo maneno miongoni mwa ndugu zenu, ilihusu zile kabila kumi na moja nyingine  nje ya walawi soma (Kumbukumbu 18;1-2) mstari wa pili hapo utakutana na neno hili, Wala wasiwe na urithi kati ya Ndugu zao (miongoni mwa).Hapa Mungu anawatenga walawi na zile kabila nyingine zinaitwa ndugu zao lugha kama hii inatumika katika torati (Kumbukumbu 17;14-15) utakutana na Maneno kama haya “….Umweke mmoja katika ndugu zako awe mfalme juu yako

Kwa muundo wa lugha hapo juu je unafikiri Mungu aliwataka wayahudi wakitaka mfalme waweke mwarabu? Ambao ni ndugu wa wayahudi? Jibu ni hapana kwani Mungu hapa anazungumza na wayahudi jamii ya walawi.
     Jambo lingine ambalo wasomaji wa Biblia wanapaswa kulitilia maanani ni kuwa manabii walipozungumza,walizungumza katika namna kuu mbili moja na jamii ya wakati ule (Forthtell) na jamii ya wakati ujao (Foretell),Hivyo unabii huu katika hali ya kawaida ulimhusu nabii anayefuata baada Musa ambae alikuwa anakaribia kufa,nabii aliyemfuata Musa kwa kawaida(Literal) alikuwa ni Yoshua ambae kwa asili hakuwa mlawi alitokea kabila ya Yuda,hivyo Mungu alipozungumza na walawi na kusema atainuliwa nabii miongoni mwa ndugu zenu alimaanisha kiongozi nje ya kabila ya walawi.Hivyo nabii huyu alikuwa Yoshua na kinabii (Foretell)Alikuwa anatabiriwa Masihi ambaye angetokea kabila ya Yuda.

      Kimsingi nabii Musa anafanana na Yesu Kristo kwa mfano tu kwani Yesu halinganishwi na mtu,Yeye yuko juu na nibora zaidi ya Musa(Ebrania 3;1-5)
     1. Musa alikuwa Mpatanishi kati ya Mungu na wanadamu (Israel)kama walivyojiombea wenyewe (Kumbukumbu 18;16,Hesabu 14;11-19),aliombea wakosaji.SasaYesu kristo ndiye mpatanishi kati ya Myngu na wanadamu kwa ulimwengu mzima (1Timotheo 2;5).
2. Musa alimjua Mungu uso kwa uso;Musa alipataneema ya kuwa na uhusiano na Mungu wa moja kwa moja tofauti na manabii wengine wote (Kutoka 33;11)Jambo ambalo Quran imelikubali(An-Nisaa 4;164) na kuwa inathibitisha ya kuwa hakuna mwanadamu aliyestahili kuongea na Mungu moja kwa moja (Ash-shuura 42;51),Yesu alimjua Mungu uso kwa uso  na alitoka kwake (Yohana 7;29,6;46).Musa alipozungumza na Mungu uso wake uliangaza (kutoka 34;29-30).,Yesu alipozungumza na Mungu uso na mavazi yake yaliangaza kama jua (Mathayo17;2). Hatusomi popote ambapo nabii wa waislamu alipatwa na Hali kama hii.

3. Musa alifanya Ishara na miujiza Mikubwa.
    Musa alifanya miujiza mikubwa sana kwa jina la Mungu kule Misri kulikuwa na ishara kama kumi,jangwani watu walilishwa kwa mana,na miujiza mingine mingi sana,hakuna nabii yoyote atakaedai kuwa anafanana na Musa kama hana muujiza hata mmoja unaofanana na Musa,tunajua kua Muhamad hakuwa na muujiza hata mmoja na ndio maana wapagani wa kiarabu walimuuliza mbona huna muujiza wowote kama wa Musa ?(Al-qasas 28;48)kama Muhamad ndiye nabii aliyefananishwa na Musa mbona hakuna ishara hata moja ya kumlinganishia na Musa? (Kmbukumbu 34;10-11).mistari hii inakazia wazi nabii atakayekuja atakavyokua kama Musa.

4. Yesu pia alifanya miujiza mikubwa.
     Kuna habari za miujiza mingi sana aliyoifanya Yesu alipokuwa duniani ambayo pia inafanana na ile ya Musa wote walikuwa na nguvu dhidi ya Bahari (Kutoka 14;21,Marko 4;39) wako mana bii waliokuwa na nguvu dhidi ya maji ya mito kama Eliye na Elisha (Yoshua 3;13,2Falme 2;14),lakini hakuna hata mmoja aliyekuwa na nguvu dhidi ya bahari,Yesu alitembea juu ya bahari ya galilaya na zaidi ya yoote upepo na bahari vilimtii jambo lililopelekea watu kumuogopa sana (Mathayo 8;27).Musa alilisha watu kwa mikate maarufu kama mana iliyonyesha kila siku juu ya nchi,Yesu alipofanya muujiza wa kulisha watu mikate (wanaume zaidi ya 500) bila kuhesabu wanawake na watoto woote walihisi na kuelewa wazi kuwa huyu bila shaka ndiye nabii yule ajae ulimwenguni (Yohana 6;14) angalia mstari huu kwa makini “.. Hakika huyu ni nabii yule ajaye ulimwenguni.”muujiza huu alioufanya ulibainisha kuwa yeye ndiye yule aliyetabiriwa na Musa (Torati 18,15,18) kwa msingi huu Kristo anatimiza sifa zinazo tajwa katika (Torati 34;10-11)Mitume wa Kristo walielewa wazi kuwa  unabii huu ulimhusu masihi na katika mahubiri yao mara kwa mara walinukuu  mistari ile ona (Matendo 3;22) na Stefano pia alinukuu katika (Matendo 7;37),Pia ni muhimu kufahamu kama Yesu alikataliwa Musa pia alikataliwa (Matendo7;27).   
                                           
Jinsi maisha ya Musa yanavyofanana na maisha ya Kristo.
Musa
Yesu
Mtoto wa kifalme kwa farao
Mfalme wa wafalme mbinguni
Mrithi wa farao
Mrithi wa Mungu
Aliishi kama mtu maalumu ikulu
Alikuwa na enzi na utukufu mbinguni
Aliishi kama mtu dini jangwani
Aliishi kama mtu duni duniani
Mchungaji wa kondoo jangwani
Mchungaji mwema wa watu woote
Alijinyenyekeza na kuwa mpole
Mnyenyekevu na mpole
Alipata mateso na kuwa mbali na ndugu
Aliteseka Msalabani na akiwa peke yake
Ni mjumbe wa agano la kale
Ni mjumbe wa agano la kale
Mpatanishi wa Israel
Mpatanishi wa ulimwengu mzima
Aklitoa sheria
Alileta Neema na kweli na uzima
Alifanya miujiza mingi mikubwa
Alifanya miujiza mikubwa ya kushangaza
Alimjua Mungu uso kwa uso
Alikuwa Mungu na alitoka kwa Mungu
Kiongozi wa Israel
Ni kiongozi wa kanisa

     Ni muhimu kufahamu kuwa Muhamad hakutabiriwa kabisa katika torati na manabii na injili kwa kweli kama angetabiriwa tungemwamini,sisi tunaamini maandiko sana tusingeweza kukanusha kile ambacho tunakijua lakini hatuwezi kushuhudia uongo labda muhamad mwenyewe angelikuwepo angetusaidia kujua kuwa ametokea wapi bahati mbaya hayuko hai lakini Kristo yu hai leo kaburi lake liko wazi,yeye ni wa kutumainiwa na anastahili kuabudiwa ni vema kumtukuza yule ambaye Mungu amemtukuza,Yeye ni alfa na omega hatuoni mwingine zaidi yake.
    Niwaase tu wanaharakati wa kiislamu waachane na tabia ya kupenda kuyasingizia maandiko kwa kutafuta kama yana mtaja muhamad ukweli ni kuwa Muhamad hayumo katika maandiko yoyote yaani Torati,manabii na injili,yeye yumo katika Quran na khadithi tu hatujui atokako.

Je Muhamad ndiye Msaidizi mwingine? (Yohana 14;26).
     Katika swala zima la kutafuta visingizio kuwa Muhamad alitabiriwa katika Biblia waislam hudai kuwa Yesu alizungumza au kutabiri habari za kuwaletea msaidizi mwingine (Mfariji) mwingine ambaye wao hudai ni Muhamad na quran inathibitisha upotofu huo!
     Madai haya ya waislamu kuwa Muhamad ametabiriwa katika Biblia yanatokana na ahadi ya Yesu kwa wanafunzi wake ambayo ahadi ambayo imekaririwa mara nne katika injili ya Yohana,kuwa baada yake atakuja mwingine atakayetumwa  kutoka kwa Mungu,jina lake ni mfariji(mshauri
/msaidizi) na wanadai huyo ni Muhamad nabii wao jambo ambalo liko wazi hata kwa wakristo wa kawaida kuwa anayezungumzwa hapo ni roho mtakatifu! Hii inatokana na waislamu kudanganyika kupitia aya katika (An- nisaa 4;157)aya hii hudai kuwa nabii wao ametabiriwa ndani ya Torati na Injili,hebu tusome vizuri (Yohana 14;26) unasema hivi
  • “….Lakini atakapokuja huyo msaidizi,huyo Roho Mtakatifu ambaye Baba atampeleka kwa jina langu atawafundisha yote na kuwakumbusha yote niliyowaambia”
  • Soma pia Aya zifuatazo (Yohana 16;7,14;16,15;26).
   Waislamu hutumia aya hizo na kuzitumia kumthibitisha Muhamad kwa madai kuwa yeye ndiye aliuongoza ulimwengu katika kweli na kwa sababu ya matumizi ya maneno nafsi “Yeye huyo”nk.wanahoji kuwa semi hizi zinamhusu mtu na sio Mungu,pia haimuhusu Roho mtakatifu kwa sababu  kwa sababu yeye amekuwepo tu wakati woote na hata Daudi aliomba kuwa asiondolewe huyo (zaburi 51;11) na Yohana alijazwa tangu utoto akiwa tumboni,(luka 1;15).
     Jibu la maswala haya ni rahisi sana ningependa kuwarudisha tena wahubiri wa kiislam kuwa biblia haisomwi kama Quran au gazeti au kitabu kingine hii (biblia ina kanuni zake kwanza wasome kifungu kizima (Principle of context),Pia wazingatie kanuni ya kulinganisha (Principle of Hermonization),Hii ni kanuni ya ushahidi wa andiko zaidi ya mawili,maandiko yote yaonyesha wazi kuwa Yesu alikuwa ana mzungumzia Roho mtakatifu,yako mambo ambayo yanabainisha wazi kuwa maandiko hayo hayamhusu Muhamadi ambaye alikuja karne sita baada ya Kristo angalia vizuri habari za Roho matakatifu,Roho mtakatifu atakaa nasi hata milele(Yohana 14;16 ).Muhamad alikufa hayuko nasi milele,Roho mtakatifu hatatambuliwa na watu wa dunia hii,wala kupokelewa anakaa ndani yetu (Yohana 14;17)Atatumwa kwa jina la Yesu na kutukumbusha au kutufundisha mambo ya Kristo (Yohana 14;26).Roho mtakatifu atamtukuza Yesu,atanena atakayoyasikia kwa Yesu,(Yohana 16;13-15).Tunasikitika kuwa Muhamad alijitikuza mwenyewe wala hakunena yale aliyoyanena Yesu,Bali yakwake mwenyewe. Hivyo Muhamad sio Msaidizi mwingine,kwani hakai nasi milele na Yuko kaburini amekufa Roho yuko milele,Jana leo na milele.

 Aidha wana harakati wa Kiislamu Katika kutafuta kutetea hoja hii walikwenda kutafuta neno wanalofikiri kwa asili linamhusu Muhamad neno hili la asili la kiyunani ni neno “Paracklutos” ambalo maana yake ni “Praise one” ambalo kwa kiarabu ni Muhamad.Hata hivyo kwa asili neno hilo wamelikosea neno linalotumiwa katika Biblia ya kiyunani ni “Paracletos” ambalo maana yake ni Mfariji,Mshauri,au Msaidizi ambalo hutumika kwa Roho mtakatifu na si kwa Muhamad,hivyo mkristo uwe macho na maneno hayo yanapotumiwa na waislamu kwa lengo la upotoshaji Mungu atupe neeema ya kuugundua uongo wao na kudumu katika kweli katika jina la Yesu.

Maoni 2 :

Bila jina alisema ...

Hiyo comparison ya yesu na Musa hazifanani kabisa jaribu kusoma upya

Fredy Fabiano Ayoma alisema ...

AMINA AMINA AMINA