Alhamisi, 4 Februari 2016

Furaha katika Maisha ya Wokovu !



Mstari wa msingi Mithali 16;20 “ …….Na kila amuaminiye ana Heri”

Ni vigumu kujifunza katika somo moja kama hili furaha zinzoambatana na wokovu, hata hivyo tutaangalia kwa ufupi sana maeneo machache katika furaha hii maana furaha hii haina mwisho, inaanzia hapa duniani na itaendelea mbinguni milele na milele,siku ile ulipokata shauri ulifanyika kuwa mtoto wa Mungu  Yohana 1;12-13, “Bali wote waliompokea aliwapa uwezo kufanyika watoto wa Mungu ndio wale waliaminio jina lake waliozaliwa si kwa mapenzi ya mwili wala si kwa mapenzi ya mtu bali kwa Mungu” wewe sasa ni mtoto wa Mungu hapo mwanzo wewe ulikuwa mtoto wa Ibilisi kwa sababu kila atendaye dhambi ni wa Ibilisi na tamaa za ibilisi ndizo apendazo kuzitenda Yohana 8;44,1Yohana 3;7-8 sasa basi kwakuwa wewe ni mtoto wa Mungu Mungu anajishughulisha sana mambo yako yote na hivyo mkono wa Mungu uko juu yako katika maswala kadhaa wa kadhaa kama yafuatayo.

                                                             Nanyi mnalindwa na Nguvu za Mungu!

*      ULINZI
Wewe sasa unalindwa na nguvu za Mungu kwa sababu umekuwa mtoto wake na umtii kwake alipokuita ulikubali kutubu dhambi zako na kumfuata hivyo tangu sasa inakupasa kumtegemea yeye kwa ulinzi wa kila aina haupaswi kuogopa Uchawi wala wachawi, nguvu za giza hazina nguvu kwako tena unapoonewa sasa Mungu ndiye ngao yako yeye ndiye anayekutetea moja kwa moja huna haja ya kuogopa tena 

§  Zekaria 2;8 “…………..awagusaye ninyi aigusa mboni ya jicho langu”
§  Zaburi 34;7 “Malaika wa Bwana hufanya kituo akiwazunguka wamchao na kuwaokoa”
§  2Nyakati 16;9 “Kwa maana macho ya Bwana hukimbia kimbia duniani mwote ili ajionyeshe mwenye nguvu kwaajili ya hao, waliokamilika moyo kuelekea kwake”
§  Zaburi 91;4-7 “Kwa manyoya yake atakufunika , chini ya mbawa zake utapata kimbilio…”
§  Zaburi 125;2 “Kama milima inavyoizunguka Yeruselem Ndivyo Bwana anavyowazunguka watu wake tangu sasa na hata milele”

*      WATU WANAOKUPIGA VITA AU KUKUONEA MUNGU ATASHUGHULIKA NAO.
Kuanzia ulipokata shauri kuokoka wewe ni wa thamani mno machoni pa Mungu  hivyo vita si vyako tena bali ni vya Bwana  wako Yesu Kristo 2Nyakati 20;15 Yeye Bwana ni mtu wa Vita Kutoka 15;3 na anauwezo wa kukupigania wewe nawe utanyamaza kimya  Kutoka 14;14  yafuatayo ni maandiko kwaajili yako
§  Yeremia 15;20-21 “nami nitakufanya kuwa kama ukuta wa  boma la shaba juu ya watu hawa nao watapiganna nawe lakini hawatakushinda maana mimi nipo pamoja nawe  ili nikuokoe na kukuponya asema Bwana , nami nitakuokoa na mkono wa watu wabaya  nami nitakukomboa katika mkono wao wenye kutisha”
§  Isaya 54;17 “Kila silaha itakayofanyika juu yako haitafanikiwa, na kila ulimi utakaoinuka juu yako katika hukumu utauhukumu kuwa mkosa huu ndio urithi wa watumishi wa Bwana na haki yao inayotoka kwangu mimi asema Bwana”
§  Isaya 43;1-2 “Lakini sasa Bwana aliyekuhuluku Eee Yakobo yeye aliyekuumba Ee Israel asema hivi Usiogope maana nimekukomboa , nimekuita kwa jina lako,wewe u wangu, upitapo katika maji mengi nitakuwa pamoja nawe na katika mito haitakugharikisha, uendapo katika moto hutateketea wala mwali wa moto hautakuunguza”

*      KWA HABARI YA MAGONJWA AU MATESO
Mapenzi yake Bwana aliyetuokoa ni wewe uwe na uzima  tena uwe nao tele Yohana 10;10 kazi za magonjwa ni kazi za Ibilisi lakini Kristo alidhihirishwa ili azivunje kazi za Ibilisi 1Yohana 3;8 kwa msingi huo litumie jina la Yesu kukemea mateso ya aina yoyote na magonjwa yanayokutesa wakati wote amini maandiko yafuatayo kwa ajili ya uzima wako.
§  Zaburi 34;19 “Mateso ya mwenye haki ni mengi lakini Bwana humponya nayo yote”
§  Kutoka 15;26 “Akawaambia kwamba utaisikiza kwa bidii sauti ya Bwana Mungu wako na kuyafanya yaliyoelekea mbele zake na kutega masikio usikie maagizo yake na kuzishika amri zake, mimi sitatia juu yako maradhi yo yote niliyowatia wamisri Kwa kuwa mimi ni Bwana Mungu wako nikuponyaye”
§  Yeremia 30;17 “Maana nitakurudishia afya asema Bwana Kwa sababu wamekuita mwenye kutupwa wakisema Ni sayuni ambao hapana mtu autakaye”
§  Torati 7;15 “ Na Bwana atakuondolea ugonjwa wote wala hatatia juu yako maradhi yoyote mabaya uyajuayo ya Misri”

*      KWA HABARI YA MAOMBI.
Maombi yako kabla ya kuokoka Mbele za Mungu yalikuwa ni kama kelele tu Mungu alikuwa hakusikilizi dhambi zilikuwa zimekutenga mbali naye Isaya 59;2 “Lakini maovu yenu yamewafarikisha ninyi na Mungu wenu na dhambi zenu zimeuficha  uso wake msiuone hata hataki kusikia” sasa baada ya kuokolewa anashughulika na maombi yako hivyo lolote utakaloliomba atashughulika nalo zaburi 55;22, Umtwike Bwana mzigo wako naye atakutegemeza hatamwacha mwenye haki aondoshwe milele 1Petro 5;7 Yohana 16;24 tumuombe Mungu kwa jina lake Yesu naye atatusikia huu ndio ujasiri tulio nao kwake kuwa tukiomba kitu sawa na mapenzi yake anatusikia  1Yohana 5;14-15, Hatupaswi kumuomba Mungu kupitia majina ya watakatifu waliotutangulia na Badala yake tunamuomba Mungu kwa jina la Yesu tu si Petro, au Paulo au Mariam kuomba kupitia wao sio mpango wa Mungu Yohana 14;13-14 kumbuka mitume na hata Mariam naye alimuomba Yesu soma Matendo 1;14 Kumuomba Mungu kupitia mtu mwingine ni machukizo kwa Mungu  na ni kulitia unajisi  jina la Bwana Isaya 48;11 Jina la Yesu ni jina lililo juu ya majina Yote Wafilipi 2;9-10.
Wewe tangu sasa umekuwa kiumbe kipya  2Koritho 5;17  na kwamba unao ndugu wengi kwa kuwa sasa umaeingia katika familia ya Mungu kila aliye katika kristo Yesu yeye ni ndugu yako  undugu huo hauna mipaka ya nchi ,wala rangi wala kabila  sote ni mwili wa Kristo sisi tu wana wa Mungu na Mungu alituchagua tangu asili  soma Warumi 8;29 “Maana wale aliowajua tangu asili aliwachagua tangu asili wafananishwe na mfano wa Mwana wake ili yeye awe mzaliwa wa kwanza miongoni mwa ndugu wengi” Karibu sana katika familia ya Mungu.

Hakuna maoni: