Alhamisi, 4 Februari 2016

Wenyeji wetu uko Mbinguni!



Mstari wa msingi wafilipi 3;20 “Kwa maana sisi wenyeji weytu uko mbinguni kutoka huko tena tunamtazamia mwokozi Bwana Yesu Kristo”

 kwa maana sisi wenyeji wetu uko Mbinguni

Tumaini letu kuu watu tuliookoka ni kwamba Yesu Kristo Mwokozi wetu atakuja mara ya pili, safari hii hatakuja kwa ajili ya kutufia bali anakuja na utukufu mkuu kuja kuwachukua watu waliookoka kwa kuwanyakua ili tumlaki yeye mawinguni Waebrania 9;28  “ Kadhalika Kristo naye akiisha kutolewa sadaka mara moja azichukue dhambi za watu wengi  atatokea mara ya pili pasipo dhambi kwa hao wamtazamiao kwa wokovu”

 Kwa sasa Kristo amekwenda kutuandalia makao soma Yohana 14;3 ili pale alipo na sisi tuwepo
1Wathsalonike 4;17 Kisha atakuja tena na kutunyakua  ili tumlaki yeye mawinguni  ni siku gani au lini Yesu anakuja kutuchukua swala hili ni siri kwani Kristo atakuja kama mwivi 1Wathesalonike 5;1-4, ujio wa Kristo utakuwa wa ghafla sana  na hakuna mtu ajuaye siku wala saa Mathayo 24;36 Biblia inatuambia kuwa bado kitambo kidogo sana atakuja wala hatakawia Waebrania 10;37

 Ni mambo gani ya kufanya ili kujiandaa na ujio wa Kristo?
·         Dumu katika wokovu ili usiaibike 1Yohana 2;28, Yakobo 5;7-8
·         Kuhakikisha kuwa tunajiweka tayari kila iitwapo leo Luka 12;40

Jinsi ya kujiweka tayari
Mathayo 3;8 Inatupasa kuzaa matunda yapasayo toba  lolote ambalo ni dhambi ni muhimu kuliacha kabisa  ishi maisha yanayoendana na kutubu kwako pia chukua hatua zifuatazo ili kujihadhari na kurudi dhambini
i.                     Punguza urafiki na marafiki wa zamani ulioshirikiana nao katika dhambi Zaburi 119;63. Mithali 22;24-25
ii.                   Waeleze rafiki zako wa zamani kuwa wewe sasa umeokoka , kumbuka kuwa wokovu ni kitu cha thamani hivyo hatupaswi kuuonea aibu Marko 8;38, 1Petro 3;15
iii.                  Endelea kutamani mafundisho ya neno la Mungu ili uweze kuukulia wokovu 1Petro 2;2. “ Kama watoto wachanga waliozaliwa sasa yatamanini maziwa ya akili yasiyoghoshiwa ili kwa hayo mpate kuukulia wokovu”

Hakuna maoni: