Alhamisi, 4 Februari 2016

UFAHAMU KUHUSU OSAMA BIN LADEN NA MASWALA YA UGAIDI



Osama Bin Laden ni mmoja wa matajiri wakubwa sana aliyeishi uhamishoni baada ya kuikimbia nchi yake ya Saud Arabia. Ndiye anayeaminika kuwa anahusika  na mashambulizi ya kigaidi Ya September 11 huko Marekani Mwaka 2001 ambapo katika tukio hilo watu Elfu tatu waliuawa (3,000) Ni mtu aliyekuwa na chuki kubwa sana dhidi ya Marekani, akiwa na usahawishi mkubwa miongoni mwa ulimwengu wa kiislamu,Osama alihusikka na mashambulizi mengine madogomadogo kuihusu marekani akiwa nchi ya ukimbizini yaani Afghanstan

 Osama Bin Laden Moja ya watu wenye akili sana Duniani ambazo shetani alizitumia

Osama Bin Laden alizaliwa Mwaka 1957 Huko Saud Arabia Ni miliomnea mkubwa sana duniani ambaye pia ni mwanzilishi wa kundi la ugaidi liitwalo Al-Qaida ambao ni mtanadao mkubwa sana wa kigaidi unaohusika na shambulizi baya la kigaidi lillilo fanyika Saeptember 11 mwaka 2001 huko Marekani, ugaidi uliofanyika kwa kusudi la kuishambulia Marekani, Pia alihusika na mashambulizi mengine yenye uhusiano na kuiudhi marekani yaliyofanyika Mwaka wa 1999, kulingana na uchunguzi wa shirika la utafiti la kimarekani federal Bureau of Investigation (F.B.I.) unathibitisha kuwa Osama alihusika na mashambulizi ya kigaidi  ya kuzishambulia Balozi za Marekani nchini Tanzania na Kenya  mwaka 1998, Wengi hawagahamu mengi kuhusu maisha ya Osama Bin Laden hasa watu wa mataifa ya Magharibi, Ingawa alirithi utajiri mkubwa sana kutoka kwa baba yake ambaye alikuwa na kampuni ya ujenzi iliyofanikiwa sana kutoka na na ukaribu wake na familia ya kifalme ya Saudia.

    Bin Laden alianza kupata umaarufu kimataifa kuanzia miaka ya mapema ya 1980 nchini Afaghanstan kwaajili ya umahiri wake katika kupambana na Majeshi ya Kisoviet akiwa Afaghanstan, Jamuhuri ya Kisoviet ilikuwa imaivamia Afaghan mmnamo mwaka 1979. Akiwa kijana  mdogo alipataq mafundisho ya msingi ya Kiislamu na aliamini kuwa uvamizi wa kisoviet kuwa ni dhambi isiyosameheka kwa katika ardhi ya Kiislamu, Bin Laden alisaidia kifedha na kwa kutoa msaada wa aina mbalimbali, alijenga Kambi za mafunzo ya kijeshi na Barabara na vyombo vya habari, Pia alifadhili usafiri wa wanajeshi mbalimbali waliosafiri kuja kujitoa wakitokea mataifa mbalimbali ya kiarabu.Wakati huo Marekani pia iliwasaidia wale waliokija kuipiga Urusi Jamuhusi ya Kisoviet wakati huo kwa uvamizi wake dhidi ya Afaghan. Mwishoni mwa mwaka 1988 Baada ya vita kuisha, Bin Laden alianzisha kundi la kigaidi liitwalo Al-Qaida ambalo maana yake ni “Arabic for the Base” maana yake “Waarabu kwa Maswala uya Msingi” hili ni kundi ambalo kwa madai ya maafisa wa kimarekani kimsingi linadaiwa kuhusika na kupanga uanzishwaji na uendeshwaji wa makundi mengine ya kigaidi yenye msimamo wa imani kali za kiislamu duniani kote.

      Mwaka 1989 baada ya vita vya Afghan Bin laden alirudi Saud Arabia na mwaka uliofuata Kuwait Ilivamiwa na Iraq na Marekani ilionyesha mwitikio kwa kuunganisha majeshi ya washirika na kuivamia Iraq katika vita vya ghuba ya uajemi, na kuanzia wakati huu Ufalme wa Saud Uliruhusu majeshi haya ya wavamizi kuitumia Ardhi ya Saudia  na Bin Laden aliudhishwa sana na kitendo hicho kwani aliona kuwa maadui wa Kiislamu wanaikanyaga Ardhi Takatifu Karibu na Mecca na Madina na ndipo alipoanza kuwakosoa viongozi hao Jambo lililopelekea miaka miwili baadaye 1992 kufutiwa uraia wa Saudia aliondoka huko na Kuelekea Sudan ambako wakati huo Uislamu wenye misimamo mikali ulikuwa uimepata nguvu, miaka miwili baadaye Sudan ilimuondolea uraia wake  na kutaifisha mali zake huko Saudia.

Wengi wa wapiganaji wenye asili ya Kiarabu wa vita vya Afaghan walijiunga na Osama huko Sudani ambako alianzisha biashara za aina mbalimbali, huku akimiliki kampuni mbalimbali za ujenzi na kufadhili ujenzi wa barabara na huko alianzisha vituo vya mafunzo na kuwasaidia mtandao wake wa kigaidi wa Al-Qaeda akisaidiwa na waarabu wenye asili ya Kiafghan, Mwaka 1996 kwaajili ya msukumo wa Kimarekani na sertikali ya Saudia Sudan walimfukuza Bin Laden na akaenda kuishi mafichoni huko Afghanstan

     Mwaka 1996 alitoa wito wa kwanza kabisa wa kutangaza vita takatifu Jihad dhidi ya Marekani na uwepo wake katika inchi nyingine na kwa mujibvu wa maafisa wa kimarekani tangu wakati huo alianza kuchukizwa na uwepo wa Marekani katika nchui za Kiarabu, huku akichukizwa na jinsi wanavyoiunga mkono Israel na kuiona Marekani kama inaendeleza vita takatifu ya Kikristo Crusades na akiamni kuwa Wakristo wa Magharibi wana mpango wa kuivamia ardhi ya waislam. Inaaminika kuwa ni kundi hili la Al-Qaeda linalosaidia kiuchumi vikundi vingi vya kigaidi ulimwenguniEx






Bin  Laden anaamini kuwa shughuli za Wamarekani katika mashariki ya kati zina uhusiano na  vita takatifu ya kikristo kwa mfano uongozi vibaraka huko Kuwait, kuiunga mkono Israel Al-Qaeda walikiri mara ya kwanza kabisa kuhusika na shambulizi la Bomu mwaka 1995 wakati wa muungano wa Saudia na Amerika katika mafunzo ya kijeshi huko Riyadh mji mkuu wa Saudia, ambapo watu watano waliuawa
 
     Mwaka 1998 walishambulia ubalozi wa Marekani nchini Tanzania na Kenya na tukio la shambulizi dhidi ya Manoari ya Amerika mwaka 2000, na bin Laden alihusishwa na mashambulizi hayo, Mwaka 2001 Ndege ziliongozwa kushambulia jumba la kituo kikuu cha kijeshi nchini Marekani maarufu kama Pentagoni na baadaye ndege mbili kuiga na kushambulia  minara mikubwa miwili ya kituo kikuu cha kibiashara cha kimataifa na kwa kufuatia matukio hayao U.S.A iliivamia Afghan na  kuiondoa madarakani serikali ya Kitaliban ambayo ilikuwa ikimkumbatia na kumuunga mkono Bin Laden na kundi la Al-Qaeda, mwaka 2002 Bin Laden alitoa kanda inayothibitisha kuhusika na tukio la September 11
World trade center Mahali magaidi walishambulia na kusababisha vifo vya watu zaidi ya 3000

     Mwaka 2004 Kabla kidogo ya Uchaguzi wa rais nchini Marekani Bin Laden alitoa kanda tena kupitia kituo maarufu cha habar Al Jazeera ambapo ndani yake Bin Laden aliwaonya watu wa Marekani kuwa kama “mtachezea hali ya amani yetu tutachezea hali ya amani yenu” Bin Laden aliongeza kuwa kilichompelekea kuishambulia  Marekani  na kuishambulia kigaidi kitendo chao cha tukio la mwaka 1982 ambapo Israel iliivamia Lebanon na nilipoangalia minara na magorofa ya Lebanon ikiangushwa chini nilijisikia kuwa hawa wasio haki wanapaswa kuteseka kama ilivyokuwa Lebanon yaani minara au magorofa marefu huko Marekani ni laimz iangushwe ili nao waonje maumivu ya kuangusha ya wengine na kuacha kuwaua watoto wetu na wanawake wetu” 

     Marekani ilipeleka majeshi yake nchini  Afaghanstan na kuayashambulia majeshi na ngome kubwa ya ugaidi duniani kwa muda mrefu na wakati mwingine wakifanyiwa mashambulizi ya kushitukiza hata hivyo mnamo tarehe 2 Asubuhi vyombo vya habari vilitangaza kuwa Osama bin Laden ambaye kwa muda mrefu alikuwa mafichoni kuwa ameuawa Osama aliuawa na majeshi ya Marekani usiku wa kuamkia 2nd  May 2011 Huko Pakstan ambapo Raisi wa Marekani Barack Obama alitarajiwa kuutangazia ulimwengu kuwa kiongozi huyo mkubwa wa mtandao wa ugaidi duniani siku zake zimekoma za kuweko duniani Hakuna marefu yasiyo na mwisho.Hata hivyo utata ulijitokeza kati ya nchi ya pakstai na Marekani kuwa ilikuwaje Osama ajifiche nchini humo bila Pakstan kuwa na taarifa, Pakstan walikiri kuwa hawakuwa na taarifa ya kuwa gaidi Huyo aliishi nchini humo.


Rais Barack Obama

Barack Obama alikuwa Seneta wa jimbo la Illinois nchini Marekani mnamo mwaka 2004, Alichaguliwa kuwa Rais wa Marekani mwaka 2008 kwa tiketi ya chama cha Democratic Katika kipindi cha utawala wake alipunguza kwa kiwango kikubwa majeshi ya Marekani nchini Iraq lakini aliongeza nguvu nchini Afaghan kwa kuzingatia kuwa ndio kituo kikuu cha uzalishaji magaidi Duniani kuongezwa kwa wanajeshi nchini huko kumeleta matokeo Mazuri ya kusambaratika kwa ngome kubwa za kigaidi ikiwemo kuuawa kwa Osama wengi walipongeza kuuawa kwa mjahidina huyo aliyeua wengi duniani kweli aushikaye upanga ataangamia kwa upanga.wengi walifikiri kuwa atakuwa mwenye msimamo Baridi kuhusu maswala ya wenye siasa kali duniani lakini sasa watu wamekubali ule usemi kuwa Paka ni paka tu hata akiwa mweusi Raisi  Jakaya Kikwete wa  Tanzania alipongeza kuuawa kwa bin Laden na kusema ni ushindi mkubwa kwa vita dhidi ya ugaidi alisema kuwa ingawa si vema kushangilia kifo ca mwanadamu yeyote hata kama ni adui yako lakini kuuawa kwake ni nafuu kwa vita dhidi ya ugaidi alisema kikwete

                 
UFAHAMU KUHUSU AL-QAEDA
     Al-Qaeda ni moja ya mtandao mkubwa wa kimataifa wa kigaidi ulioanzishwa na Osama Bin Laden uitwao al-qaeda ambao una makusudi ya  kushambulia nchi za magharibi kama sehemu ya kulipiza kisasi kwa nchi hizo zinzofikiriwa kuwa kinyume na uislamu na hususani Marekani, Mtandao huu unashikilia misimamo mikali ya sharia za kiislamu. Jina Al- qaeda maana yake ni “Waarabu kwa maswala ya Msingi”wao ni wana mapinduzi wa kiislamu ambao wako tayari kupambana katika kuhakikisha kuwa wanatetea maslahi ya kiislamu ulimwenguni

     Al-qaeda pia wanahusika na tukio la September 11,2001 ambapo kituo kikuu cha kimataifa cha biashara kilichoko New York City na Kituo cha kijeshi Pentagon kilichoko Arlington,Virginia Karibu na mto Potomac Karibu na mji mkuu wa Marekani Washingtone katika siku hiyohiyo, Magaidi wapatao 19 waliongoza ndege iliyokuwa na abiria wengine wane mara baada ya kuruka toka uwanja wa Boston,Massachusetts,Newark,New Jersey na Washingtone, Ndege mbili pia ziliruka na kushambulia minara mikubwa miwili ya kituo kikuu cha biashara kama ilivyoonyeshwa katika picha hapo juu jumla uya watu waliouawa kutokana na mashambulizi hayo ni  30,000.
     Al-qaida walihusika na shambulizi za ubalozi wa Marekani nchini Kenya na Tanzania tukio ambalo  lilitokea 1998, matukio mengine ni pamoja na lile la Manoari ya Marekani huko Aden Yemen, Kulipuliwa kwa mabomu huko Madrid Hispania mwezi March 2004 na watu 190 waliuawa na 1400 kujeruhiwa, hotel ya Paradise mjini Mombasa ambapo wayahudi kadhaa waliuawa kwa bomu la kujitoa muhanga.

KAZI KUBWA YA AL-QAEDA
Al-Qaeda kwa ujumla wanapigana vita takatifu ulimwenguni iitwayo Jihad kama tulivyojifunza na wanafikiri kuwa wao ndio watetezi wa kubwa wa tamaduni mila na dini ya kiarabu na mpango wao mkubwa ni kutawala dunia na kuifanya dini ya kiislamu kuwa dini itakayotawala ulimwengu ili kwamba ulimwengu uweze kuongozwa kwa mujibu wa Shariya (Sheriaza kiislamu)

Al-qaeda wanaiona Marekani na nchi nyingine za magharibi kuwa ndio kizuizi kikubwa cha mpango wao kwa sababu wana uhusiano na nchi nyingi sana ambazo al-qaeda wanaziona kuwa ni za kikafiri
     Al-qaeda wanaamini kuwa kuweko kwa majeshi ya Marekani huko Saudia ni aibu kwa ulimwengu wa kiislamu kwa sababu nchi hiyo ina misikiti mikubwa miwili iliyo mitakatifu ukiwemo ule wa Mecca na Medina, Bin - Laden amekwisha toa wito mara mbili (Fatwa) wa kuwaondoa wamarekani katika ardhi hiyo takatifu, Fatwa ya kwanza ilitangazwa mwaka 1998 kupigana jihadi kwaajili ya Wayahudi na Crusaders na ikitangazwa pia kuhusika na kuwaua wamarekani na kuainishwa kuwa ni wajibu wa waislamu kuwashughulikia watu hao kokote waliko, aidha tukio la kigaidi linahusishwa na ulipaji kisasi kwa uvamizi wa maeneo mbalimbali ya kiislamu ikiwa ni pamoja na Bosnia, Chechnya, Timor ya Mashariki, Philippines, Sudan na Somalia.

      Baada ya tukio la September 11 Rais wa Marekani wakati huo George W. Bush aliamuru majeshi kuivamia Afaghan  na kufanikiwa kusambaratisha kambi ya mafunzo ya magaidi, na makao makuu ya kijeshi katika inchi hiyo, maelfu ya watu waliuawa pamoja na viongozi wakubwa wa ugaidi ingawaje al-Qaeda wameendelea kuonyesha uwezo wao wa kuendelea na mashambulizi ya kigaidi kupitia vikundi mbalimbali ulimwenguni
     Mwaka 2002 kwa mfano al-qaeda walihusika na matukio ya mauaji huko Tunisia, Pakstan, Jordan, Indonesia, Kuwait, Philippines, Yemen na Kenya katika mipango yao hujumuisha kuwashambulia Australia, Ujerumani, na Israel, wengine ni wahandisi wa kifaransa na wanaubalozi wa kimarekani wakati mwingine hujihusisha na utekaji nyara wa watu kama waandishi n.k.

MTANDAO WA AL-QAEDA DUNIANI
Kwa mujibu wa uchunguzi wa ndani sana kuhusu watu kadhaa waliokamatwa kwa kuhusika na ulipuaji wa balozi za Marekani nchini Kenya na Tanzania inaaminika kuwa al-qaeda wana mtandao mkubwa wenye mawasiliano kutoka ngazi ya juu hadi ya chini na kwa kina na marefu huku Osama Bin Laden akiaminika kuwa ndie Jemedari mkuu wa Mtandao huu yeye kama amiri jeshi wa mtandao kazi yake ni kushughulika Kiroho,kimipango na muongozo na mbinu za mikakati ya kutekeleza maswala ya kigaidi hivyo anaheshimika sana na ndio mwenye kutoa mipango na amri za utekelezaji wa kigaidi hata kwa makundi mengine ( Meillis al – shura) Mtoa ushauri wenye kujenga.Vikundi vingi sana vya kigaidi hata vinavyoitwa kwa majina mengine vinafanya kazi chini ya Mtandao huu wa Al-qaeda.

ASILI YA AL-QAEDA
Vita vya Afghan na soviet
Pichani chini Mujahideen (Wapiganaji wa kiislamu) wakiwa wamesimama juu ya Helcopter waliyoiangusha chini huko Afghan mwaka 1979 Mwana milionea wa Saud Bin Laden alisaidia kifedha kujengwa kwa makambi ya mafunzo ya Mujahedeen waliopigana kinyume na majeshi ya Kisoviet walipoivamia Afghan na walikuwa wakifunzwa kutoka majeshi ya Marekani kupitia shirika la kijasusi la kimarekani Central Inteligence Agence (C.I.A), Maelfu ya wapiganaji hawa walijiunga na Al-Qaeda baada ya  vita na Soviet na kuwa mtandao mkubwa wa kigaidi duniani,

Al-Qaeda kwa asili walianza mwaka 1979 mara baada ya uvamizi wa majeshi ya kisoviet Union of Soviet Socialist Republic (USSR) Bin Laden alikuwa miongoni mwa maelfu ya wanajeshi wa kiislamu waliojitoa  kuikomboa Afaghanstan ili kuwafukuza wavamizi wa kisovieti Bin ladeni mwana wa mwana milionea wa Saud Arabia  alikuwa miongoni mwa maelfu wa vijana wa kiislamu waliojitoa kwenda  kuikomboa Afghan alijistawisha kama  mlezi mkuu wa wana jihad wapiganaji wa vita takatifu wengine ni pamoja na shekh Abdullah Azzam mwanzilishi wa jumuiya ya Makhtab al-khidamat MAK (Yaani Ofisi ya huduma) ilikuwa mwaka 1984 ambayo ilihusika na uandaaji wa makamanda wa kijeshi wa kimataifa watakaoipigania Afghan inasemekana ofisi hii iliandaa na kufundisha na kuwalipa fedha  mujahedeen kati ya 10,000 na 50,000 ambao walitokea inchi mbalimbali zipatazo 50 karibu nusu ya wanachama wa MAK walitokea Saud na wengine walitokea Algeria,Misri, na katika inchi za kiislamu  kama Yemen, Pakistan, na Sudan  na kutokana na uwezo mkubwa wa Bin Laden na ushawishi wake na umaarufu na utajiri wengi walimsikiliza na kumtii kama kamanda mkuu. Mwishoni mwa vita vya Afghan Bin Laden na Azzam waligombana kama kundi lake liendelee kufanya kazi ya ukombozi kwaajili ya Afghan aui kwaajili ya ulimwengu mzima , Lakini Bin laden alipata nguvu kubwa kwa sababu ya kuwa na imani kali ya kiislamu na theolojia aliyokuwa nayo iliyochangiwa na ushawishi wa Sayyid Qutb, mwanzilishi wa  kundi la Muslim Brotherhood huko Misri na Maulana Sayed Abdul A’la Maudoodi mzaliwa wa India  na mwandishi wa habari mwenye akili sana aliyehamia toka Pakstani 1947 ambao mafundisho yao yalikazia kuhusu Jihad kama swala Binafsi linalo takiwa kutekelezwa na kila Muislamu wa kweli na kuwa kamwe Uislamu hauwezi kutenganishwa na utawala wa kiserikali na kuwa mataifa ya magharibi ni mataifa adui wakubwa wa Uislamu. Na ingawaje al-qaeda ilianza kupata sura kati ya mwaka 1987 na 1988 ni baada ya Azzan kuuawa mwaka 1989 ndipo al-qaeda walijitenga na MAK na kuwa Wana jihad mpaka sasa na mwaka huohuo majeshi ya soviet yalijitoa Afghan na ndipo al-qaeda walipata nguvu kubwa miongoni mwa inchi za kiislamu huku Bin laden akiwa na umuhimu mkubwa na matukio ya kusambaratika kwa USSR yalifuatia na Ndipo Bin Laden alisema kuwa sasa USA nayo ni lazima iondoke katika inchi za kiarabu na ulimwengu wa kiislamu na kuuondoa umagharibi katyika inchi zao.

KUKUA KWA AL-QAEDA.

Mwaka 1989 Bin Laden alirudi SaudArabia na kupinga vikali kuweko kwa majeshi ya Marekani nchini saud na 1991 wakati wa vita vya ghuba ya uajemi aliushutumu vikali hadharani utawala wa kifalme kwa kuwakaribisha makafiri kutumia ardhi yake na april 1991 Vita ilipomalizika Bin Laden alikwenda Paksatan, 1992 alikwenda Sudan ambapo alikaribishwa na utawala National Islamic Front na kiongozi wake Hassan al-turabi ambaye alistawisha uislamu wenye msimamo mkali dhidi ya shariya
     Mwaka 1991 mpaka 1996 Bin Laden alikuwa kimya akijishughulisha na kuimarisha mtanadao wa al-qaeda kimataifa na kufanikiwa kuwa na matawi katika inchi kama 45 huku wakifadhiliwa sio tu na Osama mwenyewe bali pia na vyanzo vingine vya kifedha vinavyojihusisha na uchangiaji wa jihadi

TUKIO LA SHAMBULIZI LA KIGAIDI LA SEPTEMBER 11.

         
Hili hapo juu ndilo tukio halisi la September 11 2001, timu ya magaidi wapatao 19 wakiwa na mpango wa kujitoa muhanga walifanya shambulizi la kihistoria na kuua watu 3000 pichani ndege zilivyoweza kushambulia majengo ya minara miwili ya kituo cha kibiashara cha kimataifa  katika picha ya pili na picha  kwanza ni majengi hayo yalivyokuwa yakionekana kabla ya shambulizi Picha kwa hisani ya maktaba ya mchungaji Innocent Kamote

Ingawa haijulikani ni wapi mpango wa shambulizi la September 11 lilipangwa lakini inavyoonekana mpango wa kuyashambulia kwa ndege majengo haya kule new York na Washington DC, ulipangwa mwishini mwa 1999 wakati wa Mohamed Atta kiongozi wa kigaidi ambaye pia alikuwa ni Pilot aliyechagua ndege mbili ambazo zingetumika kwa shambulizi hilo
    Kwa mujibu wa habari kutoka ndani ya shirika la kijasusi la Marekani CIA inasemekana kuwa Pilot aliyeongoza ndege hizo hakuwa  na sifa  ya kazi hiyo, wala wazo la kuwa angeuawa hii ni kwa mujibu wa mkurugezi wa shirika hilo George Tenet magaidi walihakikisha kuwa hakuna mtu anafahamu mpango huo na kuhakikisha kuwa habari za mpango huo wa mauaji haujulikani na mtu  Bin Laden aliamini kwa kufanikiwa kwa mpango huo kungepelekea Marekani kuporomoka kiuchumi na kuwatishia sana raia wa marekani na serikali yake, Bin Laden aliita Marekani kuwa ni chui wa makaratasi na kuwa pigo hilo lingebadilisha msimamo wa Marekani kuhusu mataifa ya kigeni katika wizara yake ya mambo ya nje  na kuwa lengo la al-qaeda lingefanikiwa ikiwa ni pamoja na majeshi ya Marekani kuondoka Saud na Israel na kuwa Marekani ingeacha shughuli zake za kibiashara katika ulimwengu wa Nchi za Kiarabu   
                                                                                               
MATOKEO YA SHAMBULIZI LA AL-QAEDA LA SEPTEMBER 11.
Kinyume na matarajio ya al- qaeda Marekani ilipokea kwa masikitiko makubwa tukio hilo la kigaidi na kutangaza vita vya kidunia dhidi ya matukio ya kigaidi na magaidi.Na kampeni kubwa za kijeshi za kushughulikia magaidi zilianza na October 7 Mwaka 2001 Mashambulizi makali yalianza dhidi ya kityuo kikuu cha kigaidi huko afghan na serikali ya Kitaliban kuondolewa madarakani na Novembr 2001 serikali ya kitaliban ilishindwa vibaya na kuondolewa madarakani, al-qaeda wote walisambaratishwa vibaya na kuondolewa kabisa katika ngome yao huko afghan ingawaje Bin laden na watu wake wa Karibu kama Ayman Muhamad Rabi al-Zawahin walikimbia kukamatwa
Marekani na washirika wake walifanikiwa kuzuia vyanzo vya kifedha vyote vyenye kusaidia makunfdi mbalimbali ya kigaidi , sheria na miswada mbalimbali ya kupambana na ugaidi zilipitishwa na kila taifa na kupelekea magaidi wengi kukamatwa zaidi ya Mgaidi 1000 waliokuwa na uhusiano na al-qaeda walikamatwa katika inchi mbalimbali na mpaka mwishoni mwa 2003 magaidi wapatao 3000 walikamatawa na huku viongozi wengi wa mitandao ya kigaidi wakiuawa au kukamatwa mmoja wa watu waliofanikiwa kukamatwa ni Khalid Shaikh Muhamad ambaye alikuwa ni moja ya viongozi wa ngazi ya juu sana wa mtandao wa al-qaeda ambaye alisaidia kuongoza tukio la September 11 huko Pakstan.

Ingawaje al-qaeda wamedhoofishwa kwa kiasi kikubwa bado waliendelea na matukio ya kigaidi ambapo mwaka 2002 walifanya shambulizi huko Tunisia, Kuwait na Kenya na 2004 walifanya shambulizi huko Spain wakijitutumua kuwa bado hawajasambaratika hata hivyo inaaminika kuwa mashambulizi mengi yalikuwa yamekwisha kukusudiwa zamani hata kabla ya tukio la September 11.
HALI YA BAADAYE YA AL-QAEDA.
Mkanda wa sauti inayosadikiwa kuwa ya Bin Laden uliorushwa katika vyombo vya habari November 2002 uliokuwa ukiwasifiwa wote wanaopingana na desturi za kimagharibi baada ya kushindwa 2002 ulionya kuongeza vitosho kwa mashambulizi zaidi ya kigaidi, wakati huu Bin Laden alionekana kuitishia Australia, Beligium,Uingereza ,Ufaransa, Ujerumani na Hispania nchi zote ambazo  zilijihusisha na muitikio wa kuishambulia al-qaeda na kuisaidia Marekani katika vita dhidi ya ugaidi
Mwezi April 2004 alitoa mkanda mwengine ukiwaelekeza al-qaeda kuhakikisha kuwa wanaichana Marekani vipande vipande na washirika wake ulaya na ilitoa onyo kwa watu wa ulaya kuacha kuushambulia Uislamu na nchi za kiislamu au kuingilia maswala yake na alisema ukweli utathibitika pale ambapo askari wa mwiosho ataondoka katika nchi hizo ikiwemo Afghan  na Iraq, kwani Marekani na washirika wake waliiondoa serikali ya kitaliban mnamo 2001 na Kumuondoa Madarakani Rais Saddam Hussein mwezi April 2003

Kuachiliwa kwa mkanda huo kulifuatia tukio la mashambulizi ya mji wa Madrid Huko Hispania mwezi March 11 2004 ambapo watu 190 waliuawa na 1400 kujeruhiwa, na serikali ya Spain iliwakamata baadhi ya washukiwa wanaohusiana na mtandao wa al-qaeda  Jaji wa kihispania alithibitisha mtandao huo kuhusika kufuatia Spain kujiunga na majeshi ya washirika  na Marekani  na kupeleka vikosi vyake huko Iraq na hivyo kuzilzzimisha inchi za ulaya kujiondoa katika mpango wake wa kuisaidia marekani, Spain baada ya kupeleka kikosi cha askari 1300 baadaye kulitokea shambulizi linguine jambo lilolopelekea serikali iliyofuata ya Spain kuondoa vikosi vyake toka Iraq Hata hivyo inchi nyingi za Ulaya zilikataa mpango huo na kusema kamwe hawawezi kukubaliana na Magaidi

Maswala mengi kuhusu tukio la September yalieleweka vema bada ya uvamizi wa Marekani kwa Iraq ambapo ilibainika wazi kuwa Iraq haikuwa na uhusiano na kundi hilo hususani baada ya kuondolewa madarakani kwa serikali ya Saddam Hussein, Baadaye al-qaeda walijaribu kujihusisha na matukio ya uchaguzi wa Rais wa Marekani mnamo 2004 Laden alitoa mkanda  akiwaonya waamerika kuwa usalama wao haumo mikononi mwa chama cha Democratic cha mgombea John Kerry, wala Bush  au al-qaeda usalama wao uko katika mikono yao ingawaje uchunguzi ulibaini kuwa mkanda huo unakosa sifa za Osama mwenyewe kwani nhakuwa anazungumza kama Osama mwenyewe mwenye jazaba na kejeli nyingi na kubainika kuwa ulitengenezwa tu na waarabu  wanaopinga sera za marekani kwa mashariki ya kati ,Baadaye mkanda mwingine wa video wa Osama ulifuatiwa na ule wa Zawahiri  na huende ulirekodiwa kabla ya uchaguzi  ambapo bwana al- Zawahiri alisema kuwa matokeo ya uchaguzi wa Marekani hauna tija kwetu mpigie kura yeyote unayetaka Bush, au Kerry au Shetani mwenyewe hili halituhusu linalotuhusu sisi ni kukaliwa kwa ardhi yetu na makafiri, mnamo 2004 CIA walihisi kuwa huenda al-qaeda wana lengo la kum iliki nyuklia kufuataia kuhisiwa kuwa engineer wa kipakistan mmoja kutoa taaluma kwao kuhusu silaha hizo.

Ndugu msomaji wangu vyovyote vile iwavyo huu ndio msimamo wa mafundisho ya Quran ulivyo na unaopelekea  kuweko kwa amakundi ya kigaidi duniani  hivyo pamoja na jitihada za kimarekani na washirika wake kupambana nao ni muhimu kufahamu kuwa fundisho la ugaidi liko kwenye Quran  na ugaidi unaweza kuendelea kuweko maadamu uislamu uko na Quran iko ndugu mpendwa hii ni changamoto kubwa ulimwenguni hata kwa waislamu wenyewe kuhakikisha kuwa wanakuwa na tafasiri sahii ya Quran hasa kwa kuisoma injili inayosisitiza upendo na kuachana na mitazamo ya kizamani inayopelekea kuuawa kwa watu wengi wasio na hatia unajua kwa nini ugaidi unaruhusu kuua hata waislamu wenzako ambao wanaonekana kuwa na misimamo ya wastani na ndio maana nasema kuwa hata waislamu wana changamoto kubwa la tafasiri sahii isiyo na unafiki kuhusu Quran.

 Nilipotembelea Marekani Mwezi Juni 2014 na wanafunzi wangu Tulifika mahali Yalipokuwepo Magorofa ya World Trade Center Mahali hapa sasa panaitwa Zero Ground na pana visima  na majina ya watu zaidi ya 3000 waliouawa kwa misigi ya tofauti za kiitikadi (Katika picha kutoka Kushoto Yohana Komba, Onstard Mashauri, Herbeth Gumbo, Imani Peter Mngazija, Willium Biniventure Kifutumo, Mimi Rev. Innocent Kamote na Author Chikoka Picha na Maelezo kwa Hisani ya Mwandishi wa Makala hii Rev. Innocent Kamote)

Hakuna maoni: