Alhamisi, 11 Februari 2016

Mfululizo wa Masomo yahusuyo Uongozi wa Kanisa 7



*******************************************************************
                                           Somo; Majukumu ya kiongozi wa kanisa
Kufahamu majukumu ya kazi za kiongozi katika kanisa ni mojawapo ya Jukumu muhimu kwa kiongozi wa kanisa, Mara nyingi imetokea Viongozi wengi wa makanisa ya kiroho hawajui majukumu yao na hii inachangia kwa kiasi Fulani kutokuyafikia malengo. Tutajifunza somo hili kwa kuzingatia mambo mawili yafuatayo

*      Viongozi wa kanisa ni wachungaji.
*      Majukumu ya kichungaji ya kiongozi wa kanisa

Viongozi wa kanisa ni wachungaji.
     Viongozi wa makanisa ya nyumbani au cells na Viongozi wengine woote na wasaidizi wao woote ni wachungaji wa kondoo wa Mungu, Hawa ni wachungaji wanaotenda kazi chini ya Mchungaji hata ingawa hawaitwi kwa jina hili, lakini majukumu yao wanayoyafanya ni ya kichungaji, katika mpango wa Mungu kila mtu ana husika katika utendaji kama makuhani wa Mungu Ufunuo 1;5-6, 1Petro 2;5,9 kama ikiwa kila mtu aliyeokoka Maandiko yanamuita kuhani ni zaidi sana mtu anapokuwa kiongozi katika kanisa Viongozi katika kanisa ni wachungaji wanaotenda kazi chini ya Mchungaji na kumsaidia katika huduma za kichungaji

Majukumu ya kichungaji ya kiongozi wa kanisa.
    Viongozi wa kanisa kama ilivyo kwa Mchungaji wana wajibika kufanya kazi ya uiunjilisti uchungaji na ualimu katika eneo lao walilopewa na Mungu leo tutachukua Muda kujifunza majukumu  mbalimbali ya kiongozi wa  yanayohusiana na uinjilisti na ualimu na uongozi kwa ujumla wake
  1. Kuwafahamu Kondoo kwa sura na majina Yohana 10; 2-3.
Ni wajibu wa kiongozi katika kanisa kuwafahamu kondoo wake kwa majina na sura, kadiri kanisa linavyokua na kuongezeka lazima kanisa liwe na mfumo unaoruhusu watu kujulikana kama kuwa na makanisa ya nyumbani ambapo kiongozi anapaswa kuwatambua kwa sura na majina ,watu hupenda kutambulika na hujisikia salama pale  anapokuwa anatambukiwa Kanisani hivyo ni wajibu wa kiongozi kuwatambua watu wake, na kutokana na kuwafahamu kwa majina na sura  inakuwa rahisi kuwaombea kwa kuwataja majina yao Viongozi wanapaswa kuwafahamu wale Viongozi wengine walio chini yao  pia tunapaswa kujua mahudhurio yao katika ibada zote za mafundisho siku ya bwana na kadhalika 

  1. Kuhubiri na kufanya uinjilisti Marko 1;38-39;Matendo 20;27.
Kiongozi yeyote wa kanisa kwa ngazi yoyote ni lazima awe muhubiri  na anawajibika kuwahamasisha watu walio chini yake kuwa na furaha ya kuona watu wakiokolewa na kuongezeka katika kanisa  tuhakikishe kuwa tunawahubiri watu na wageni wanaokuja katika kanisa letu na kuwaaalika katika ibada mbalimbali za kanisa ,aidha kama ni kuiongozi wa cell au kanisa la nyumbani hakikisha kuwa unalihubiri eneo lote linalokuzunguka na kuhamasisha watu kuhudhuria ibada zote  aidha tunapofahamu kuwa Fulani na Fulani hawakuhudhuria ibada ni muhimu kuwatembelea na kujua ni kwanini hakuhudhuria  na kutoa msaada unao hitajika kwa  pia kufanya ufuatiliaji kwa washirika wachanga kiroho na kuwalisha kwa neno na mafundisho,kiongozi anapaswa kukumbuka kuwa mfano au kielelezo kwa watu aliopewa kuwaongoza.

  1. Kufundisha au kulilisha kanisa. Matendo 20;28.
   Lisha kondoo zangu huu ni wito kwa kila kiongozi wa kanisa kwa msingi huo ni wajibu wa kiongozi wa kanisa la nyumbani n.k kujiandaa na kujitayarisha mapema kwa habari ya somo atakalolifundisha  kila siku ya ibada za makanisa ya nyumbani au katika vipindi vya ibada za idara n.k. Masomo yanayopaswa kufundishwa ni yale yaliyo maalumu kwa ajili hiyo au yale yanayofundishwa Kanisani ni hatia kuleta mafundisho mageni 2Yohana 1;9-11,Tito 1;9 kufundisha kwetu hakuna budi kuwe na malengo ya kuondoa au kurekebisha  matatizo yaliyopo katika sehemu zetu za maongozi tabia kama masengenyo, kuchelewa ibada au kutohudhuria n.k kumbuyjka kuwa inahitaji maombi na maandalizi ya kutosha  kabla ya kufundisha somo au siyo kondoo watajkuwa  hawashibi na matokeo yake hawatavutiwa kuendelea kuja katika  katika kipindi husika.

  1. Kuwatunza kondoo.
Ni wajibu wa kiongozi kufanya kazi ya msamaria katika kutunza kondoo wake Luka 10;30-37 ni lazima kuwatafuta waliopetea na kujua kuwa ni kwanini hawaji katika ibada,lazima tumuombe Mungu atupe karama na vipawa  ili kuwahudumia watu wake kuomba kwa ajili ya uponyaji kwa ajili ya wote wenye shida za magonjwa na kuwafungua waliovunjika moyo kwa kuwapa neno la Mungu la kuwaita moyo Ezekiel 34;1-2,4-6.

  1. Kuwatembelea washirika na kujua hali zao za kimwili na kiroho.
    Yeremia 23;1-2 matendo 15;36.  Kiongozi yeyote wa kanisa anatakiwa kuifahamu kila nyumbay a mshirika wake  na kuwatembelea mara kwa mara na waqkati mwingine kwa kushtukiza ili ajue hali ya kimwili na kiroho ya washirika, bila matembezi ya jinsi hii  ni rahisi kumkuta kondoo amejerihiwa  iwapo kuna taarifa ya tabia mbaya ya mshirika awaye yoote  zifanyiwe uchunguzi wa kina na wa haki kisha zitafutwe njia za kumsaidia kiroho endapo liko juu ya uwezo wako likabidhio kwa Mchungaji kumbuka katika kuwatembelea washirika pia ni muhimu kuweka kipaumbele kwa wale walio wachanga ,wageni na wenye kuugua au waliopatwa na misiba na matatizo mbalimbali haita kuwa busara sana kwa mshirika aliyekomaa kiriho kuwa na madai ya kutembelewa na badala yake wao nao washirikiane na Viongozi katika kuifanya kazi ya kuwatenbelea washirika na kuwaita moyo.

  1. Kutoa ushauri kwa kondoo. Mithali 20;18;12;15.
Mengi tunayoletewa na kondoo kutaka ushauri mara nyingi ni yale yaliyo mepesi kuyatolea ushauri hata hivyo Mengine huwa magumu na mtu unapoletewa tu ni rahisi kuona moyoni kuwa hili limenizidi kimo  katika mazingira kama hayo hilo lipeleke kwa kiongozi wako wa juu na katika kanuni za kutoa ushauri ni vizuri uwe mwepesi wa kusikia kuliko kusema Yakobo 1;19 Roho wa Mungu hudondosha ushauri kwetu tunapokuwa watu wa kusikia au katika hali hii ya utulivu,  na wakati huo huo zingatia kuwa ni Kinyume na mapenzi ya Mungu kutoa siri za matatizo ya mtu aliyekuomba umpe ushauri Mithali 25;2,9.

  1. Kumlinda Mchungaji 1 Samuel 26;16
Viongozi katika kanisa  ni wawakilishi wa Mchungaji na wana wajibu wa kumlinda Mchungaji na kuhakikisha kuwa kila roho ya uasi  inayoinuka kinyume na Mchungaji inashughulikiwa ipaswavyo na kuitolea taarifa lazima kiongozi wa kanisa awe na moyo wa kiuchungaji Isaya 40;11,1Thesalonike 2;7 Bila moyo huu utendaji wetu wa kazi utaingia dosari.lolote linalopungua katika karama hii ya kumtumikia Mungu tumuombe Mungu atupe karama hizo za kutuwezesha kuifanya kazi yake  aidha sivibaya kuwatumia wale ambao Mungu amewapa karama hizo kutusaidia  katika kuwahudumia wale tunao waongoza.

Hakuna maoni: