Alhamisi, 4 Februari 2016

Umuhimu wa Kuhudhuria Ibada!



Mstari wa msingi Matendo 2; 46 “Na sikuzote kwa moyo mmoja walidumu ndani ya Hekalu…….”
Somo la umuhimu wa kuhudhuria ibada zote ni moja ya masomo muhimu sana , ufahamu kuhusu somo hili kunamfanya mtu aliyeokoka kupiga hatua kubwa sana katika kukua kiroho  na hatimaye yeye naye kuwa mwalimu wa wengine kwa upesi zaidi,Tutajifunza somo hili kwa kuzingatia vipengele vitatu vifuatavyo;-
Kanisa Mjini Dubai wakristo wanaruhusiwa kuabudu na kujenga makanisa bila kuweka alama ya msalaba juu ya Majengo yao


·         Umuhimu wa kuhudhuria ibada zote
·         Kwanini inatupasa kuhudhuria ibada zote
·         Tuhudhurie ibada katika kanisa lipi?

Umuhimu wa kuhudhuria ibada zote
Moja ya ishara ya muhimu inayoonyesha kuwa mtu ameokoka ni kuwa na shauku ya kumtafuta Mungu kilka siku Isaya 58;2 mtu aliyeokoka atapenda kujisomea Biblia  na kufanya maombi binafsi nyumbani  kila mara anapopata nafasi  atakuwa akitafakari na kujifunza neno la Mungu lakini pia atakuwa akihudhuria ibada 

Kuhudhuria Ibada ni amri ya Mungu kwa kila mtu aliyeokoka Biblia inasema katika Kumbukumbu 12;5 “Lakini mahali atakapopachagua Bwana Mungu  wenu …..Apaweke jina lake maana ni makao yake, elekezeni nyuso zenu hapo nawe wende huko” Maneno nawe wende huko katika Biblia ya kiingereza ya New International Version yanasomeka “To that place you must go” kwa msingi huo kwa tafasiri rahisi tunaweza kusema mahali hapo ni lazima uende unaona kwa hiyo kuhudhuria ibada ni swala la lazima Mungu anasema lazima uende kanisani Biblia inaagiza kutokuacha kukusanyika Waebrania 10;25. 

Yesu kristo mwenyewe alionyesha wazi jinsi ilivyo lazima kuwako nyumbani mwa Mungu Luka 2;49 Akawaambia kwani kunitafuta ? Hamkujua ya kuwa imenipasa kuwamo nyumbani mwa baba yangu? Yaani imenilazimu  Kama kwa Yesu ilikuwa ni lazima basi sisi ni zaidi sana  Biblia inasema Yeye asemaye ya kuwa anakaandani yake imempasa kuenenda vilevile kama Yeye alivyoenenda  1Yohana 2;6, Watakatifu waliotutangulia kwao ilikuwa ni furaha walipoambiwa kwenda nyumbani mwa Bwana  na waliona siku moja ya kuwamo nyumbani mwa Bwana ni bora kuliko siku elfu za shughuli za dunia soma Zaburi 122;1,84;1-2,10, ilikuwa ni kawaida kwa manabii na mitume kutunza muda wa kwenda kusali soma Luka 2;36-37,24;53 Matendo 3;1 sisi nasi kama tunataka kutumiwa sana na Mungu inatupasa kuiga mfano wao
Watu waliookoka nyakati za kanisa la kwanza siku zote walidumu kwa moyo mmoja ndani ya hekalu Matendo 2;46 hii ndio siri kubwa ya mafanikio yao  tusikubali kamwe kwa namna yoyote ile masumbufu ya dunia hii kutunyima muda wa kwenda kuabudu.

Kwanini inatupasa kuhudhuria ibada zote
Tukiisha kujifunza kuwa neno la Mungu ni nini na sisi tuliookolewa ni akina nani ufahamu huu utatupa kuelewa vizuri umuhimu wa kuhudhuria ibada zote
1.       Neno la Mungu ni chakula cha kiroho Yeremia 15;16, Mathayo 4;4, Yohana 6;48-49,57-58, Kumbukumbu 8;3  Ili mtu apige hatua kubwa ya kiroho katika wokovu inampasa kulipenda Neno la Mungu kuliko hata chakula cha kimwili  Ayubu 23;12 watu wanaokula mara tatu kwa siku pamoja na mapochopocho mengine kwa wiki wana kula zaidi ya mara 21 kuulisha mwili maana yake na sisi ni muhimu kuhakikisha kuwa tunazilisha roho zetu kwa kuhudhuria ibada na kuomba na kuabudu na kujisomea neno n.k.
2.       Sisi ni wanafunzi wa Yesu Baada ya kuwa tumeokolewa tunageuka kuwa wanafunzi wa Bwana Yesu Mathayo 27;57, Yesu Kristo anakuwa ni mwalimu wetu  Yohana 13;13, Naye amelipa kanisa wasaidizi wa kutusaidia kufundisha neno la Mungu Waefeso 4;11-12 , Mathayo 28;19-20 kwa msingi huo waliookolewa ni wanafunzi wa Yesu na ili mwanafunzi aweze kufanikiwa anapaswa kuhudhuria darasani vipindi vyote bila kukosa  kama tutalizingatia hili ndipo tutakapokuwa miongoni mwa hao washindao Ufunuo 2;11.
3.       Tuhudhurie ibada katika kanisa lipi?
Baada ya kuokolewa Biblia inatupa muongozo wa dhahiri juu ya mahali sahii pa kuabudu Biblia inasema hatupaswi tena kuyarudia mafundisho yaliyo manyonge Wagalatia 4;9 sasa tunawezaje kujua kuwa mahali hapa ni penye mafundisho manyonge? Tutachunguza alama zifuatazo na ukigundua moja kati ya hizo basi mahali hapo hapafai kwa kuabudu

§  Mahali ambapo pana viongozi vipofu Luka 6;39, Mathayo 15;14 yaani mahali ambapo kuna wachungaji au wainjilisti au wazee wa kanisa wa dhehebu lolote ambao ulevi, zinaa na uasherati na kila aina ya dhambi inawatawala hao hawawezi kuwa msaada wa mtu wa kiroho kwa sababu mtu aliyeokoka amepewa kuona Yohana 9;39-41 hivyo hupaswi kuongozwa na kipofu
§  Mahali ambapo matendo ya giza hayakemewi Waefeso 5;11
§  Mahali ambapo sanamu zinashirikishwa katika Ibada  Isaya 31;7,1Wakoritho 10;14, 1Yohana 5;21
§  Mahali ambapo wanafuata maneno yaliyotungwa na wanadamu na sio neno la Mungu 2Petro 2;1-3
§  Mahali ambapo hawaamini kuwa Yesu ni mwana wa Mungu 1Yohana 4;15,5;10-12,Yohana 3;36 .
§  Mahali ambapo Neno la Mungu halihubiriwi bali zina hubiriwa hadithi  tu na hakuna kukaripiwa kukemewa wala kuonywa Neno siku zote linakuwa ni kufariji tu 2Timotheo 4;1-2,Ayubu 16;1-2,Waebrania 12;5-8.
§  Mahali ambapo kila mtu hata mtoto mchanga anapewa zamu ya kutoa neno badala ya kukaa chini  na kujifunza neno kwanza kwa kukaa chini ya waalimu 1Koritho 12;28-29 Waebrania 5;11-12
§  Mahali ambapo watu wanafundishwa kushika sheria ya Musa kwa kutokula aina Fulani ya vyakula kushika sabato n.k. Wakolosai 2;16-17,1wakoritho 10;25-27
§  Mahali ambapo hakuna changamoto bali unakaa tu na hakuna jipya unaingia ukiwa na kiu ya kujifunza na unatoka ukiwa hajapata kitu Yohana 7;46
§  Mahali ambapo wanakwepa kuwafundisha watu maneno magumu ya uzima wa milele Yohana 6;60-61,66-68

Baada ya kuokoka kama utakaa mahali pa namna hii kwenye mafundisho manyonge ni muhimu kufahamu kuwa wewe nawe utakuwa mnyonge na hutaweza kuingia mbinguni kwani hakuna kinyonge kitakachoingia huko Ufunuo 21;27 wala usikubali vyeo au namna yoyote ya kuwapendeza wanadamu na kukubali kukaa katika unyonge kwa sababu hizo Yeremia 45;5,Wagalatia 1;10, baada ya kuchagua kanisa lisilo na mafundisho manyonge  sasa kaa hapo na uabudu na kumtumikia Mungu. Mungu akubariki sana   

Hakuna maoni: