Alhamisi, 4 Februari 2016

Kuteswa kwaajili ya Kristo !



Mstari wa Msingi Wafilipi 1;29 “ Maana mmepewa kwa ajili ya Kristo si kumwamini tu ila na kuteswa kwaajili yake “

Kuchukiwa baada ya kuokoka
Baada ya kumuamini bwana Yesu na kuanza kuukiri wokovu ulioupokea hadaharani, kutafuata kila aina ya kebehi kutukanwa na kila namna ya kuchukiwa na ndugu walio karibu ni muhimu kuvumilia mpaka mwisho kwani Yesu alituambia kuwa tukichukiwa kwaajili yake tuna heri Mathayo 10;22.
   Katika hali ya kawaida ungefikiri kuwa ndugu mume au mke au wazazi wangelifurahia uamuzi wako wa kuokoka lakini jambo la kushangaza ni kuwa haitakuwa hivyo wengi wataanza kusema umeiacha imani yako ya kwanza uliyozaliwa nayo? Au dini ya ukoo wako hali inaweza kuvuruga sana hata mahusiano yako na mumeo yanaweza kuingia utata ni muhimu kufahamu kuwa si kila wakati watafurahia watu uamuzi wako ndio maana Yesu alisema hakuja kuleta amani duniani Luka 12;51-53. 

                                                Kwaajili ya Kristo wengine wanakubali kuuawa kinyama


Wakati mwingine kwa sanbabu ya wokovu amani itaondoka utashangaa unaweza kufanyiwa hata vikao  na kuanza kutishwa au kuteswa kwaajili ya bwana na mwokozi wako Yesu Kristo hayo yasikukatishe tamaa fahamu ya kuwa tumepewa si kumwamini tu bali na kuteswa kwaajili yake wanaweza kukupa kila aina ya majina hata kuitwa mchawi isikusumbue kwani hata Yesu aliitwa kuwa anatoa pepo kwa kutumia mkuu wa pepo Mathayo 10;24-25,28 hayo yatatupata mara baada tu ya kulikubali neno la Mungu 

Fahamu kuwa wewe si wa ulimwengu huu na hivyo ndio maana ulimwengu unakuchukia ungelikuwa wa ulimwengu huu ulimwengu ungekupenda  Yohana 17;14 kwa msingi huo ni muhimu kuwa tayari kwa mateso ya namna yoyote ile na kuvumilia huku tukihakikisha kuwa hayatupotezei wokovu wetu Ufunuo 3;11

Biblia inatufundisha kuwa watu wanaokwenda mbinguni ni lazima wapitie dhiki adha  na mateso mengi ndio maana mitume waliwafundisha wanafunzi wao mapema kujua hayo Matendo 14;22 Imetupasa kuingia katika ufalme wa Mungu kwa njia ya dhiki nyingi, aidha katika mafundisho yake Bwana Yesu alisema Heri weri wenye kuudhiwa kwaajili ya haki maana ufalme wa mbinguni ni wao Mathayo 5;10  yeyote ambaye amechagua maisha ya utauwa yaani maisha ya wokovu lazima ataudhiwa soma 2Timotheo 3;12  dhiki hizi tumewekewa na na tusifadhaishwe 1Thesalonike 3;3, Petro anasema katika 1Petro 3;14 Lakini mjapoteswa kwaajili ya haki mna heri kwa hiyo tusiogope kutisha kwao

Mtu anayekata tamaa haraka kwaajili ya dhiki hizi anafananishwa na mbegu zile zilizoangukia juu ya mwamba na kwa kukosa mizizi ikitukia dhiki wanachukizwa soma Mathayo 13; 20-21, tunapaswa kuwa wavumilivu na kamwe hatupaswi kuwajibu vibaya wala kwa hasira  kwa sababu hawajui walitendalo wewe subiri thawabu yako ambayo ni kubwa sana Mbinguni  Mathayo 5;11-12, Ni sifa kubwa mbele za Mungu  kupigwa makofi kwaajili ya wema 1Petro 2;19 dhiki hizi tulizo nazo sisi ni nyepesi na za Muda tu  ukilinganisha na thawabu kubwa ambayo Mungu atakwenda kutulipa huko Mbinguni 2Wakoritho 4;17-18  inatupasa kufurahi tunaposhiriki mateso kama Kristo ili siku akifunuliwa  utukufu mkubwa wa Mungu  na roho wake anatukalia hii ndio maana ulimwengu unatuchukia 1Petro 4;13-14 trukumbuke kuwa yanayotupata yaliwapata pia wale waliokuwa wametutangulia na biblia inatutaka kuchukua manabii waliotutangulia kama mfano wa kustahimili mabaya na wa uvumilivu Yakoboo 5;10, mitume wengi waliuawa kwaajili ya Kristo katika historia za kanisa inaonekana kuwa Petro aliuawa wakati wa mtawala aliyeitwa Nero kwa kusulubiwa kichwa chini miguu juu,huko Roma Andrea alisulubiwa huko Misri na Simon Mkananayo aliyeshurutishwa kuubeba msalaba wa Yesu naye alisulubiwa  na wengine wengi walipata mateso ya namna mbalimbali  kweli ufalme wa Mungu unapatikana kwa njia ya dhiki nyingi nasi inatupasa kuwa wavumilivu sana hata kama kila mtu atatuchukia iwe ni kazini ama popote pale kumbuka kuwa taji kubwa inakungoja 

Kumbuka kuendelea kuwaombea wale wanaotutesa ili kwamba Mungu awaokoe na pia wakati wote huu wa mateso shirikisha wenzako katika Bwana ili mshirikiane katika kuomba kwani kiungo kimoja kikiumia katika Kristo ni viungo vyote Jipe moyo kwani ushindi ni lazima Ubarikiwe sana
Maana mmepewa kwa ajili ya Kristo si kumwamini tu ila na kuteswa kwaajili yake.

Hakuna maoni: