Jumapili, 7 Februari 2016

UPI NI MUONGOZO WA MUNGU WA KWELI QURAN AU BIBLIA?



      Kabla ya Kushughulika na jambo lolote ni muhimu tukafahamu upi ni muongozo kamili wa Mungu,kila dini duniani ina Muongozo wake,lakini sihitaji kupoteza muda kushughulika na miongozo ya watu wengine kwani wao wameridhika na miongozo yao na huwa hawana habari na miongozo ya watu wengine lakini Nitazungumzia zaidi Quran kwani waislamu wana chokochoko hawajatulia na kuridhika na Muongozo wao kama ilivyo kwa Wahindi,Buddha,Shinto,nk. Wala sina shaka na Muongozo wangu yaani Biblia kwa sababu ni Muongozo kamili unaojitegemea na ambao mtu akiufuata atafanikiwa tu ndivyo Mungu alivyomhakikishia Yoshua soma Yoshua (Yoshua 1:7-8)pia Daud alimuhusia Suleman (Ifalme 2;2-3) wala sina wasiwasi na injili kwani ni uongozi kamili wa Mungu kupitia Masihi Yesu hakuna mtu mwenye shaka na Yesu ni mtakatifu na muadilifu alipewa kitabu Ndiyo injili hakuna maswali injili inatosha kabisa kumpeleka mtu mbingini huwezi kutenganisha injili na Yesu yeye ni njia kweli na uzima!


 Lakini nina mashaka na qurani kuwa ni kitabu kisicho jitosheleza kabisa hakiongozi mbinguni hakina nguvu ya kutuokoa na dhambi kuondoa hatia au kutia matumaini ndani ya kurani utakutana na aya zinazo kutia moyo kuendelea kuangalia torati na injili kama Muongozo wa kweli wa Mungu kwa vipi?Quran huiita Tourat na injili “Vitabu vyenye nuru” soma (al Imran 3:184,Fatir 35:25)Aya nyingi za Qurani zinatuambia kwamba torati na injili zimetoka kwa Mungu soma (al-Baqara 2;89 al anam 6:92) humo kuna uongozi na Nuru(al-maida 5;44,46) Wengi wa wafasiri maarufu wa Quran kama Al-Jalalayn,Al-Fakhr,Al-Razi,Al-Tabari na Al-Baydawi woote wanakiri kuwa kulingana na Qurani Torati inaitwa kitabu cha Mwenyezi Mungu (al Imran 3;23)na kitabu kibainishacho kila linalohitajiwa(as saafat 37;117).Hata hivyo tunajua kuwa baadhi ya wanaharakati wa kiislamu wanaamini kuwa Torati na injili zimepotoshwa na zimetiwa mkono hivyo haziaminiki kama hivyo ni kweli uongo huu uliingizwa lini? Quran  inataka watu waiamini torati na injili iweje watu waamini vitu vilivyopotoshwa?hii ina maana mpaka quran inaandikwa vitabu hivyo vilikuwepo na vinaaminika  quran inazidi kutia moyo tuviamini vitabu hivyo ona (al-baqara 2;136,al Imran3;84 an nisaa4;136  )Qurani inawaagiza waislamu kututafuta sisi wenye ujuzi wa torati na injili ikisema hivi Waulizeni wenye kumbukumbu (za vitabu vya mwenyezi Mungu vya kale )ikiwa ninyi hamjui (an nahil 16;43,al-Anbiyaa 21;7) sasa hebu tujiulize Quran ingeelekeza hayo kama vitabu hivi vimepotoshwa?kama haitoshi quran inatuomba sisi watu wa kitabu torati na injili kuvirudia vitabu vyetu soma( al-maida 5;47,68)Kama vitabu hivi vimepotoshwa huoni kuwa kuran inatupoteza zaidi kama inaagiza kuvirudia?Hivyo Vitabu hivi havingeweza kupotoshwa kamwe  baada ya kuandikwa quran,Kuna uthibitisho jinsi maandiko matakatifu  ya siku zetu yanapolinganishwa na torati na injili zilizoandikwa karne nyingi kabla ya Quran zinaonyesha hakuna tofauti wala badiliko wala upotovu na kwabahati nzuri hati hizi za mkono zinapatikana katika maktaba za umma na majumba ya makumbusho,Mtu yeyote anayeamini quran ni lazima akubali kwamba maandiko matakatifu hayajapotoshwa.

 Baadhi ya watu wanaweza kuendelea kupinga wakidai kuwa quran inaonyesha upotovu huo yaani Tahrif kwa kiarabu lakini maulamaa au wasomi wa kiislamu wanasemaje kuhusu hilo? Wanasema hivi upotovu uko wa aina mbili 1. Kuingiza uongo katika maandiko na 2. kupinda au kupotosha maana ya maandishi, Maulamaa hawakubaliani na lile la kwanza ila hili la pili ambalo hata wanaharakati wa kiislamu wanalifanya sana na hukumu yao inawangoja, katika kitabu kinachohusu imani ya Mungu mmoja ambacho ni sehemu ya Sahih, imamAl-bukhari anaeleza maana ya neno tahrif humaanisha ubadilishaji,Hata hivyo hakuna awezaye kubadili herufi yoyote katika kitabu cha Mungu, Katika kitabu chake cha maelezo juu ya an-Nisaa4;46,Imam al-Fakhr Al-raz anasema hivi…. “Maana ya upotovu Tahrif ni kuingiza shaka la kipuuzi na maelezo yenye makosa na kubadili neno liache maanayake ya kweli ili ilete maana isiyo na msingi kwa kutumia hadaa za kimaneno kama vile wazushi wanavyofanya  sasa na zile aya zinazopingana na mafundisho ya madhehebu yao wenyewe hayo ndiyo maoni yalito hakika zaidi” na hiki ndicho wanaharakati wa kiislamu wanavyoifanyia biblia  hii ndiyo Tahrif  hivyo hakuna abadilishaye maneno ya (waadi wa )Mwenyezi Mungu (Surat al anam 6;34),Hivyo quran inathibitisha kuwa Torat na injili (Biblia) ni mwongozo na Nuru, upi ni muongozo wa Mungu wa kweli ni Biblia bila shaka Maswali?................

Hakuna maoni: