Jumamosi, 13 Februari 2016

Umuhimu wa Kutumia Neno la Mungu kwa Halali 1



Ni muhimu kufahamu kuwa ni ujinga kusema kuwa kanisa halijawahi kukutana na changamoto  zinazolilazimisha kujaribu kutunza kweli ya neno la Mungu katika viwango vyake vinavyohitajika, Kwakweli changamoto hizo zimeongezeka sana leo kuliko wakati mwingine wowote, Hata pamoja na ukuaji wa kasi kwa makanisa yanayohubiri injili bado kanisa linakutana na changamoto zinazolipelekea hitaji la kuwepo namna ya kutunza viwango vya kweli vya usafi wa neno na utakatifu unaotokana na mafundisho sahihi ya kibiblia, hili sio jambo jipya kwani tangu wakati wa Kristo kulikuweko na changamoto za falsafa mbalimbali ambazo zilitafuta kuharibu mafundisho ya kanisa, Leo kuna changamoto zaidi kwa sababu kuna televisheni, magazeti, Radio, na vyombo vingine vingi vinavyotumika kueneza mafundisho Lakini mengine ni ya uongo na yako chini ya kiwango cha viwango vilivyokusudiwa na neno la Mungu tutafanyaje? Kanisa linapaswa kuishindania imani somo hili la hermeneutics linasaidia katika kukabiliana na tatizo husika kama linavyoletwa kwako na Mchungaji Innocent Kamote Fuatana naye katika somo hili lenye ufunuo wenye Baraka kwako na kwa yeyote utakaye mfundisha somo hili Mungu na akubariki.

HERMENEUTICS.  ni nini?
*      Hermeneutics  ni sayansi inayohusu namna na kanuni za kuitafasiri Biblia
-          Ni sayansi inayohusu jinsi ya kutafuta maana iliyokusudiwa na Mwandishi maana ya neno au kifungu cha maneno ili uweze kulifafanua neno kwa wengine
-          Ni somo linalohusu kanuni za kutafasiri Maandiko
*      Hermeneutics ni neno lenye asili ya kiyunani Hermeneuo lenye maana ya kutafasiri hivyo ni sayansi inayohusu kanuni za kutafasiri Maandiko. Neno kutafasiri limejitokeza katika agano la kale na agano jipya kama Pathar kiebrania au Pithron yakiwa na maana ya kutafasiri
*      Kutumia neno la Mungu kwa halali ni agizo la kibiblia 2Timotheo 2;15 “Jitahidi kujionyesha kuwa umekubaliwa na Mungu mtenda kazi asiye na sababu ya kutahayari,ukitumia kwa halali neno la kweli
*      Mambo muhimu makuu mawili huzingatiwa katika kuifanya kazi ya kutafasiri Maandiko
i.                     KUGUNDUA maana ya andiko katika maana iliyokusudiwa na Mwandishi kwa watu wake wakati ule tendo hilo kitaalamu huitwa “EXEGESIS” ambalo maana yake kutafuta maana halisi ya andikokwa wakati wa Mwandishi na kisha kuitumia kulingana na wakati wetu tulionao. Kutafuta mawazo yako kisha kuyasingizia Maandiko yamesema tendo hilo huitwa “EISOGESIS”.

                                                                                          
                  EISOGESIS             
                                                                                                EXEGESIS

*      Eisogesis hutokea pale mtafasiri anapoacha  au kudharau kutumia kanuni za kutafasiri Maandiko na kusababisha isiendane na maana iliyokusudiwa na mwandishi ni sawa na kujitafutia maana kisha ukayasingizia Maandiko, Exigesis hutokea pale Mtafasiri anapozingatia kanuni za kutafasiri Maandiko na hivyo kusababisha kupata maana ambayo Mwandishi alikuwa ameikusudia katika kuhubiri jumbe za aina mbalimbali kama Textual. Expository na Topical ujumbe wa somo, Ingawaje Topical ni hatari kama moyo wa muhubiri huyo utakuwa umeharibika kwani ni rahisi kufanya Eisogesis kupitia jumbe hizi kwa hivyo wale wanaohubiri jumbe za Kuchanganua Maandiko Expository huwa salama zaidi ukilinganisha na wale wanaohubiri topical sermon yaani ujumbe wa somo.               
ii). Kuamua namna ya KUTUMIA Maandiko katika wakati wetu baada ya kuwa umepata maana iliyokuwa imekusudiwa au kufanya application kwa msingi huo mpaka mtafasiri awe anauwezo wa kulitumia au kuyatumia Maandiko kwa halali atakuwa amekumbana na vikwazo anavyopaswa kuvibabadua vikwazo hivyo ni tamaduni, lugha zilizotumika, muda na historia hivi vyote vinaweza kuwa vipingamizi vinavyoweza kusababisha mtu kutumia neno la Mungu kwa halali hivyo ni Jukumu la mtafasiri kuchunguza vipingamizi hivyo ili kupata maana iliyokusudiwa na aweze kutumia neno la Mungu kwa halali angalia mfano huu;-

             MTAFASIRI


     MWANDISHI: (PAULO)            KUFANYA TAFASIRI                   WASIKILIZAJI 
 

                                                                                 
                                                 Tamaduni    lugha   muda       historia

                    ENZI HIZO                DARAJA LA VIPINGAMIZI                            LEO HII

Jukumu la mtafasiri
Kutatua lugha, tamaduni, historia na muda.
                                                



UMUHIMU WA KULITUMIA NENO LA MUNGU KWA HALALI

Kuzuia tafasiri zisizo halali katika kanisa
Kulitafasiri Neno la Mungu katika njia sahii kunahitajika sana hususani katika Nyakati tulizo nazo, Kanisa lisipokuwa na kanuni maalumu za kulitafasiri neno kila mtu atalitafasiri kama apendavyo na hivyo hatutakuwa na kweli kamili zinazoweza kutetewa kiimani, kumbuaka kuwa Biblia ni kitabu maarufu sana  cha karibu Nyakati zote huku kinabeba ujumbe wa Muhimu wa wokovu ni kweli ya kimungu inayotufafanulia Mungu ni nani?, anafanya nini kinatuambia pia asili ya vitu vyote, na kinatabiri mambo yajayo, kinabadilisha maisha ya watu na kinafariji kina ushawishi zaidi ya tamaduni yoyote na kimeandikiwa Vitabu vingi kuliko maandishi yoyote ambayo yamepata kuwako duniani.  Hivyo ni kitabu muhimu sana.
Lakini pamoja na umuhimu huo Biblia imetefasiriwa kizembeau vibaya na jamii kubwa ya wahubiri na waalimu kuliko Vitabu vya kawaida vya hadithi. Kwa msingi huu basi kwa kuwa ni kitabu cha kimungu na cha muhimu si vema kutumia kanuni za kawaida za mawasiliano katika kukitafasiri au kukiacha kitafasiriwe kama mtu Fulani anavyofikiri au anavyotaka Biblia ni lazima itafasiriwe katika maongozi ya kimungu yanayokubalika, Na kutokulizingatia hilo tutapata maana mbovu sana zitakazo sababisha madhara.
Mfano;-andiko katika Zaburi 137;9 linasema “Heri yeye atakayewakamata wadogo wako Na kuwaseta wao juu ya Mwamba”. Ukilichukua andiko hili kama lilivyo utauwa watu! Inasemakana kuwa baadhi ya Wanazi wa kijerumani waliwauwa sana wayahudi wakitumia Maandiko katika Mathayo 27;25 kwa kuwa walisema Damu yake mtu huyo na iwe juu yetu sisi na watoto wetu. Katika makanisa pia kunatafasiri nyingi mbovu za kimaandiko ambazo zinapaswa kuwekwa vizuri wako watu wanaamini hata leo kuwa wanaposhiriki meza ya Bwana wanakula mwili wa Yesu na kunywa damu yake kwa kutumia 1 Wakoritho 15;29 au watu wanaojaribu kushika nyoka kwa kufikiri kuwa watalindwa kwa kuwa ni ahadi katika Biblia Marko 16;18, Biblia pia imetumika kuhalalisha zinaa kwa watu kutafasiri vibaya maswala ya malimbuko au Mwanafunzi na amshirikishe mkufunzi katika mema yoote Wagalatia 6;6  ikimaanishwa hata ngono! Au msinyimane 1 Wakoritho 7; 5a na mifano mingine mingi sana kama hivi ndivyo basi  kusipokuwepo na kanuni na Muongozo wa kuitafasiri Biblia tafasiri za Biblia zitaakisi mioyo ya wanadamu na sio kile ambacho Mungu anakitaka kwetu hivyo basi iko haja ya kuwako na Muongozo unaotusaidia ni namna gani tutafasiri Maandiko na kuwa swala hili ni nyeti kuliko tunavyosisitiza.

Kuzuia kutokufikia lengo kuu la kuhubiri kwetu
Historia inaonyesha ya kuwa katika namna ya kushangaza ambayo inakubalika hata kwa watu wasioiamini Biblia ni kuwa watu wa Ninawi ambao walikuwa wakatili sana na wapenda vita walitulia kwa kipindi cha kizazi kimoja bila ya kuwashambulia majirani zao  yaani kulikuwa na mabadiliko makubwa ya kijamii  ambayo yalitokana na ujumbe wa Yona  alipotangaza ujumbe aliokuwa amepewa na Mungu, Leo hii pia ulimwengu unaweza kubadilika na jamii ikawa na maadili mazuri iwapo tutahubiri kile ambacho Mungu amekikusudia kwa watu, Kama injili ya kweli iatahubiriwa matokeo ya kuibadilisha jamii yanawezekana Lakini kama kutakuweko na Tofauti za tafasiri za kiini cha ujumbe ambao Mungu ameukusudia basi ni dhahiri kuwa hatuwezi kufikia lengo katika kuhubiri kwetu.Lengo kubwa la kuhubiri kwetu na kufundisha ni ili watu waishi kama Mungu anavyotaka lakini watu wataishije kama Mungu anavyotaka iwapo neno lake litatafasiriwa kama kila mtu apendavyo? Ni wazi kuwa hatuwezi kufikia lengo

Kuzuia kutofikia lengo la kufundisha Neno la Mungu.
Kama kila mtu atajihubiria ujumbe vyovyote atakavyo ni wazi kuwa na kufundisha pia kutakuwa katika hali kama hiyohiyo na kumbuka kuwa ni rahisi sana kuwaleta watu kwa Yesu Lakini ni vigumu sana kuwafanya watu kuwa wanafunzi Yona alifanya kazi nzuri ya kuwahubiri watu wa Ninawi Lakini hukufanya vizuri kwa kuwanyima mafundisho watu wa Ninawi Mungu anapotuma uamsho mkubwa na kuokoa wengi analitegemea kanisa kuwafundisha wanaookolewa hata hivyo si mafundisho yoyote tu bali ni mafundisho yaliyo ya weli iliyotafasiriwa katika viwango sahii Shetani ni lazima ataendelea kujaribu kuharibu kanisa  Kupitia silaha yake kuu ambayo ni uongo Kupitia mafundisho ya uongo Paulo alifanikiwa sana kuihubiri injili katika Efeso na watu wakaacha kuabudu sanamu Matendo 19;26, Lakini pia alionya sana kuwa mbwa mwitu wakali watainuka wasilihurumie kundi hii ni kwa kufundisha yasiyopasa au yasiyo sahii Matendo 20;27-30.

Kusaidia kujua kwa nini Mungu ametupa Biblia.
     Watu wengi sana wakristo wanaamini kuwa Biblia ni neno la Mungu, Lakini ni muhimu kujiuliza maswali kuwa je Mungu angejenga msingi huu wa Neno katika hali ya Machafuko? Lazima uko msingi wa muhimu sana na msingi huu ni wa zege la ufunuo wa kimungu usiyoweza kutikiswa, Lakini hata hivyo ni wakristo wachache sana  ambao wanavutiwa na kutafasiriwa kwa usahihi kwa neno la Mungu Ni wakristo wachache tena wenye Ufahamu wanaweza kuona jambo hili kuwa ni hatari kutokuweko na mwongozo sahihi au na watu makini ambao wanapaswa kusimamia misingi na kanuni za kuyatafasiri Maandiko katika njia iliyo sahihi Hivi ingekuaje kama tu tungekuwa tunamtumikia Mungu bila hata ya kuwepo Neno lililoandikwa? Watu wangekuwa na maoni Tofauti kuhusu Mungu na wangekuwa na njia Tofauti kuhusu wokovu namna ya kuhubiri au hata kuabudu kwa msingi huo Mungu alitoa neno Lakini hali kadhalika kusipokuwepo na Muongozo katika kutafasiri pia kutakuwa na tatizo linalofanana na kutokuweko kwa Neno la Mungu

Kuzuia hukumu ya Mungu kwa kutumia vibaya Maandiko au kuhubiri kitu kingine.
     Biblia inatutahadharisha kuwa Mungu huliheshimu sana neno lake na hivyo mtu awaye yote mwenye madai kuwa ametumwa na Mungu kufanya kazi ya kufundisha au kuhubiri Maandiko basi ni muhimu kusema kile ambacho Mungu amekusudia kisemwe  Yeremia 23;1-4,15-30, aidha Paulo mtume naye aliwatahadharisha watu watakakohubiri injili ya aina nyingine kuwa walaaniwe Wagalatia 1;8-9, si hivyo tu Yakobo mtume aliyeheshimika na ndugu wa Bwana alitahadharisha kuwa tusiwe waalimu wengi kwani kuna hukumu iliyo kubwa zaidi Yakobo 3;1.kwa msingi huo kuna hukumu ya Mungu pia kwa watu ambao wataongeza au kupunguza katika kile Mungu alicho maanisha Ufunuo 22;18-19 kwa hivyo basi kuna umuhimu wa kuhakikisha kuwa kweli inahubiriwa au neno linahubiriwa kwa kuzingatia misingi yake ili kweli ipatikane kwa kanisa na kuzuia hukumu ya Mungu kwa kuhubiri yale yasiyotupasa hivyo ni muhimu ikafahamika kuwa kuna hukumu ya Mungu kwa kutumia neno lake isivyo halali.

JE KUNA UMUHIMU WA KUWA NA KANUNI ZA KUTAFASIRI MAANDIKO?.

     Kama tulivyoona katika vifungu vilivyotutangulia chukulia kuwa umezungumza jambo na kisha mtu akalipokea vibaya na kwenda kuwaelezea wengine katika namna isiyofaa ni nini kinaweza kutokea? Bila shaka mahusiano ya kirafiki yanaweza kuharibika na hivyo itakupasa kuelezea kwa usahihi mara ya pili kwamba ulikuwa umemaanisha nini? Hiki ndicho humpata Mungu, tunapotafasiri Neno lake katika njia isiyo sahihi, angalia jinsi watu wasiofaa walivyofanya Nyakati za Kanisa la kwanza hata ikampasa Petro kusisitiza jambo kuhusu nyaraka za Paulo Mtume “   Nanyi hesabuni uvumilivu wa Bwana kuwa ni wokovu, kama vile ndugu yetu mpenzi Paulo alivyowaandikia kwa hekima ile aliyopewa na Mungu. Huandika vivyo hivyo katika nyaraka zake zote akizungumzia ndani yake mambo haya. Katika nyaraka zake kuna mambo mengine ambayo ni vigumu kuyaelewa, ambayo watu wajinga na wasio thabiti huyapotosha kwa maangamizi yao wenyewe, kama wapotoshavyo pia Maandiko mengine”. 2Petro 3; 15-16 kwa msingi huo kunahitajika Tafasiri sahihi na kanuni sahihi za kuyatafasiri Maandiko. Ziko sababu maalumu zinazoonyesha kwanini ni muhimu kuwa na tafasiri za Maandiko ikiwemo Tamaduni za wakati ule ni Tofauti na zetu, Lugha zilizotumika ni Tofauti,  Muda wa watu hao walipoishi ni Tofauti historia ya wakati ule ni Tofauti hivyo mtafasiri wa Biblia ili apate maana halisi anapaswa kuruka vikwazo hivyo vyote ili kulileta neno kwetu leo  .
                                                         
Kwa msingi huo utaweza kuona kuwa iko haja ya kujua tamaduni za wakati wa Muandishi, lugha, Historia na nyakati au Muda utahitaji kujua kwa mfano mafarisayo ni akina nani masadukayo, Neno Abba, tamaduni Tofauti na nyakati mfano kitabu cha kutoka kiliandikwa miaka zaidi 3500 iliyopiata Nyakati na lugha na tamaduni kamwe haviwezi kulingana hivyo utaweza kuona kuwa kutafasiri Maandiko kunakuwa kazi ya kitaalamu zaidi na ya uangalifu zaidi kulijko tunavyofikiri

Hakuna maoni: