Alhamisi, 11 Februari 2016

Mfululizo wa Masomo yahusuyo Uongozi wa Kanisa 1



**************************************************************
                                       Somo; Wito wa kuwaongoza Kondoo.
  Leo Tunaanza kujifunza mfululizo wa masomo yahusuyo shule ya uongozi kwa kujifunza somo hili la msingi “Wito wa kuwaongoza kondoo”Tutajifunza Somo hili kwa kuligawa katika vipengele vitano vifuatavyo;-
·         Watu waliookoka huitwa Kondoo
·         Mungu ndiye Mchungaji mkuu wa kondoo
·         Wachungaji wanadamu
·         Jinsi isivyowezekana Mchungaji kuongoza kondoo peke yake
·         Wito wa kuwaongoza kondoo.

 * Watu waliookoka Huitwa Kondoo.
         Watu waliookoka huitwa kondoo (zaburi 79;13;100;3;Yohana10;27-28)Kwanini wanaitwa kondoo,Kondoo ni wanyama wasioweza kufanya lolote bila kuongozwa au kupewa msaada wa Kiroho,wao hutembea wakitazama chini na kuiangalia miguu ya kiongozi wao yaani Mchungaji wao Kondoo wanahitaji Malisho na kunyweshwa maji (Mwanzo 29;7,Yohana 10;2-4).Kondoo watatulia mahali Fulani wakingoja Maelekezo ya Kiongozi wao tofauti na Mbuzi au wanyama wengine  na kutafuta Malisho wenyewe nk.Siyo hilo tu kondoo ni rahisi sana kuvamiwa na wanyama wengine wakali na kuuawa bila kujitetea kwa lolote  hawana mbio kama wengine wala viungo vya kujitetea kama pembe kali nk.hivyo maisha ya kondoo  yanahitaji sana Mchungaji au kiongozi Kadiri mchungaji  wao alivyo shujaa ndivyo wanavyo faidika, mchungaji akiwa mtu mbaya nao pia Hudhurika (1Samuel 17;34-35, Yohana 10;11-12)Hivyo maisha ya watu waliookoka yanatutegemea sana sisi viongozi Tukiwa wema kondoo wataishi maisha Mazuri ya kupendeza(Yeremia 50;6;Ezekiel 34;5-6)
   Kilio cha kondoo wakati woote ni  kupata kiongozi wa kuwaongoza wao
Hulia wakati wote wakisema ni nani atakayeniongoza hata Edom(zaburi108;10)Bila kiongozi  watu waliookoka wanaweza kufanya yaliyo mema machoni pao wenyewe na kumhuzunisha Mungu. (waamuzi 21;25).
 * Mungu ndiye Mchungaji mkuu wa Kondoo.
      Mungu ndiye Mchungaji mkuu wa kondoo ambao pia ndio kanisa ni kondoo zake kanisa ni mali yake (Waebrania 13;20;1Petro 5;4;Zaburi 23;1-3).Mungu kama mchungaji mkuu wa kondoo,Yeye ndie Kiongozi mkuu wa kondoo wake na maongozi yoote ya Kondoo hutokana na neno lake(Kutoka 13;17;Yohana8;47;Zaburi 119;9)hata hivyo ingawa Mungu ndiye Mchungaji mkuu wa kondoo katika mpango wake wa Uongozi ameweka wachungaji wanadamu ambao hufanya kazi pamoja na Mungu(1Koritho 3;9).
* Wachungaji wanadamu.
Katika mpango wake Mungu anawaongoza kondoo wake kwa kuwatumia wachungaji wanadamu(zaburi 78;70-72;2Samuel 5;1-2, Zaburi 77;20 Kutoka 15;22 Hesabu 27;15-21 Yohana 21;15-17).Mungu huwatumia wachungaji wanadamu hawa kufanya kazi ya kuwaongoza kondoo kwa maelekezo ya neno lake(Kutoka 32;34)Hata hivyo uongozi wa wachungaji hao  wanadamu wanadamu hufikia mpaka wanapokuwa na kundi kubwa la kondoo nao huitaji wanadamu hawa wengine wengi wa kutenda kazi pamoja nao
*  Jinsi isivyowezekana Mchungaji kuongoza kondoo Peke yake.
Kadiri kanisa linavyoongezeka kunakuwa na kundi kubwa la kondoo wanahohitaji uongozi.kiongozi mmoja  hata angekuwa na uwezo Mkubwa namna gani huelemewa na kushindwa kukidhi mahitaji ya uongozi wa kondoo wengi, matokeo yake kondoo wengi hujisikia upweke kwa kukosa msaada wa uongozi na matokeo yake hutawanyika na kuliacha kanisa hilo na kutafuta mahali Pengine wanapoweza kupata uongozi wa maisha yao lakini wengine kwa kukosa uongozi  hurudi nyuma na kuacha wokovu(Waamuzi 18;1,30-31). Kiongozi Musa alipokuwa amewaacha kondoo bila kiongozi ,pale alipopanda mlimani Sinai kupokea amri kumi  za Mungu huku nyuma kondoo walipoona  hawana kiongozi maana kiongozi wao amekawia kurudi walirudi nyuma na kuacha wokovu  na kufanya machukizo makubwa mbele za Mungu.(Kutoka 32;1-8,15-24).Ufumbuzi wa Tatizo la watu waliookoka kurudi nyuma na kuacha wokovu ni  kuwa na viongozi wengi wanaomsaidia Mchungaji.Kadiri tunavyokusudia kanisa letu kuwa na watu wengi zaidi ndivyo inavyotupasa kuwa na viongozi wengi zaidi wa kumsaidia Mchungaji kuliongoza kanisa,Viongozi hawa watakuwa wanashughulikia matatizo madogomadogo ya kondoo na kuyapatia ufumbuzi na yale makubwa tu ndiyo yatakuwa yanapelekwa kwa Mchungaji, Bila kufuata mpango huu Kanisa litadumaa na haliwezi kuongezeka kiimani na kiidadi, Hata kama watu wengi watakuwa wanakata shauri,hawataendelea katika zizi la kondoo kwa kukosa uongozi.Musa na watu wake waliukubali na kuufuata mpango huu wa Mungu na matokeo yake walifanikiwa (Kutoka 18;13-26)   Bwana amusaidie kila mmoja wetu ili tusiwe kwazo la kukua na kuongezeka kwa kanisa. 
*Wito wa Kuwaongoza kondoo.
     Kilio cha watu wa Mungu humfikia Mungu (Kutoka 2;23;Mwanzo 18;20-21,Yakobo 5;4) Kondoo wa Mungu  wanaohitaji uongozi wanapolia  wakisema nina atakayetupeleka hata mji wenye Boma?ni nani atakaye tuongoza hata edomu (Zaburi 108;10).Kilio hiki humfikia Mungu,Kondoo hawa wana wasi wasi wa kulala Porini na kuwa katika hali ya kushambuliwa na mbwa mwitu au simba wanataka kiongozi atakaye wapeleka kwenye mji wenye Boma (yaani zizi la kondoo).Kondoo hawa pia wanalia wakihitaji mtu  wa kuwaongoza hata wafike Edomu nchi yenye malisho mengi na maji mengi(Hesabu 20;14-19).Ndivyo kondoo wa Mungu wanavyolia pia,wanahitaji viongozi watakaohakikisha wokovu wao unadumu na hawawezwi na shetani samba aungurumaye na tena wanahitaji viongozi  wa kuwahakikishia wanapata malisho na kuangaliwa na kutunzwa ili wafurahie raha ya Wokovu. Kilio hiki cha kondoo kikimfikia Mungu ,Mungu nae anatoa wito kwa watu wake akitaka wajitoe kuwaongoza Kondoo yaani kiongozi wa kanisa,Mungu anauliza Hapana hata mmoja wa Kumshika mkono? Miongoni mwa wana wote aliowalea(Isaya 51;18) Kwa sababu hiyo mungu anauliza ni nani atakaye kwenda   kwa ajili yetu?-Isaya 6;8 Isaya alisema Mimi hapa, sisi nasi hatupaswi kumuachia mchungaji pekee kuifanya kazi hii peke yake na hivyo tunapaswa kushirikiana nae katika kulitunza Kundi.                   

Hakuna maoni: