Jumatatu, 15 Februari 2016

FREEMASONS NA ILLUMINANT



Hiki ni kitabu chenye siri nzito za Freemasons na Illuminant

UTANGULIZI.

 
Ni mpango wa Shetani kuangamiza sheria ya Mungu tangu mwanzo. Shetani amekuwa akifanya vita dhidi ya amri 10 za Mungu ambazo ndicho kipimo pekee cha utii kwa Mungu. Katika vita hiyo, Shetani amekuwa akitumia mawakala wa aina mbalimbali kiasi cha kufanikiwa kuwadanganya mamilioni ya watu duniani nao wakaiacha sheria ya Mungu na kufuata mafundisho yaliyo maagizo ya wanadamu. Shetani ameanzisha kanisa lake na kuweka amri 11 kinyume cha amri 10 za Mungu. Mbeleni tutaona jinsi waumini wa Shetani kwa dini la Freemasons na Illuminati wanavyotumia namba na ishara katika kazi zao duniani kiasi cha kuwapofusha watu huku wakidhani kwamba wanamuabudu Mungu wa mbinguni kumbe wanamuabudu Shetani mwenyewe.

Tunaishi katika nyakati za hatari. Majanga yameenea kila mahali. Machafuko ya kila aina yameenea ulimwenguni kote. Ubakaji, matetemeko ya ardhi, moto usiowezekana kuzimwa, mafuriko wakati wa kiangazi, migomo ya wafanyakazi, maporomoko ya ardhi, kuyumba kwa uchumi, milipuko ya Volkano na mengine mengi yanazidi kutokea kila kukicha, tena katika mataifa makubwa yaliyoendelea na hata kuitwa ‘mataifa ya ulimwengu wa kwanza’.

Kuongezeka kwa machafuko haya ya asili na kisiasa yanawafanya wanadamu wawe na hofu kuhusu maisha yao ya baadae. Inaonekana kana kwamba tupo katika ncha ya mwisho mbele yetu kukiwa na shimo kubwa tayari kuangukia shimoni. Yote haya ni dalili za mwisho wa wakati kwa wale walio na masikio ya kusikia na macho ya kuona, kwamba ulimwengu hautaendelea kwa muda mrefu ukiwa katika hali hii. Mioyo ya watu inajawa na hofu kwa haya yanayotokea (Luka 21:26). Na watu wanajiuliza maswali:

“kwa nini haya yanatokea?” “Je, Shetani ametawala kikamilifu?”

Hapana, Mungu hajawaacha watu wake waaminifu, lakini maswali hayo yote yanaonyesha kwamba  kuna kitu nyuma ya matukio haya kuliko wengi wanavyoweza kuelewa. Kuna vita kali inayoendelea kati ya nguvu za nuru na nguvu za giza —-vita kali kati ya Yesu na Shetani— na matokeo yake ndiyo yanayoonekana kwa wanadamu ikiwa ni matukio hayo. Hata hivyo Mungu wa mbinguni amewaambia watu wake kwamba “muda ubakio si mwingi.” Na anaendelea kusema “Tukijua ya kwamba saa ya kuamka katika usingizi imewadia, kwa maana sasa wokovu wetu u karibu nasi kuliko tulipoanza kuamini. Usiku umeenda sana, mchana umekaribia, basi, na tuyavue matendo ya giza, na kuzivaa silaha za nuru.” 1 Wakor 7:29; Warumi 13:11-13. aulo anatueleza kwamba “Tuvae silaha za  Mungu,”  ndipo tutakapoweza kusimamadhidi ya madanganyo ya Mwovu (Waefeso 6:11). Nilipokuwa nasoma unabii wa Danieli, Ezekieli, Ufunuo nk sikujua jinsi unabii huu utakavyotimia na kwamba kumbe kundi linalofanya kazi zake kwa siri kubwa ndilo linalotimiza unabii huu kwa kiasi kikubwa sana. Wengi hawana habari na madanganyo haya ya Shetani na Mungu ametuagiza kwamba tusiwe wajinga kiasi cha kutotambua mbinu za Shetani na hivyo “Shetani akapata kutushinda” 2 Wakorintho 2:11.

Mafanikio makubwa ya Shetani katika udanganyifu yamepatikana kwa njia ya kuwafanya watu wawe  wajinga wa mbinu anazotumia katika kazi yake. Wakati tunapokuwa wajinga au kuchanganyikiwa, ndipo Shetani anapotushinda na amefanikiwa kwa kiasi kikubwa kuwashinda wanaume na wanawake wengiulimwenguni. Hivyo hatupaswi kulala usingizi na kushindwa kutambua kile kinachoendelea katika
ulimwengu wa giza. Kwa nini? Kwasababu “Mshitaki wenu, kama simba angurumaye, huzunguka zunguka, akitafuta mtu ammeze.” 1 Petro 5:8; Ufunuo 12:12. Mwovu anajua kwamba muda wake ni mchache na hivyo halali akiwa anafanya kazi ya kuuongoza ulimwengu kuelekea katika uangamivu wa mwisho. Watu wa Mungu karibu watajaribiwa. Wale wasioshinda kwa damu ya mwana kondoo watapata hofu ya majaribu na hivyo kushindwa.

Lakini ni kwa njia gani Shetani anafanya kazi yake? Anafanya kazi kupitia mawakala gani? Jibu linatolewa na Mungu. kwa upendo mwingi Mungu anatufunulia wahusika wakuu katika mchakato huu wa vita ya mwisho kati ya Kristo na Shetani. Wahusika hawa ndio wanaostahili kulaumiwa kutokana na matokeo tunayoyaona katika ulimwengu wote kama yalivyotajwa hapo juu. Katika kitabu cha Ufunuo, Mungu anatufunuliwa wahusika au mawakala watano ambao ni:

1—Mnyama mwekundu wa Ufunuo 12—Shetani mwenyewe
2—Mnyama mfano wa chui wa Ufunuo 13—Rumi ya kidini
3—Mnyama mfano wa mwana kondoo wa Ufunuo 13:11—Taifa la Marekani
4—Sanamu ya Mnyama Ufunuo 13—Umoja wa makanisa —WCC
5—Mnyama wa rangi nyekundu sana na mwanamke wa Ufunuo 17—-Illuminati, freemason wakiwa wameungana na kanisa la Rumi..

Wengi hawakuwa wanatofautisha wanyama hao lakini utakapojifunza kwa undani zaidi utagundua kwamba mnyama wa Ufunuo 17 ambaye ni mwekundu sana mwenye pembe kumi na vichwa saba ambaye amembeba mwanamke inamaanisha muungano wa Illuminati wakiwa wameunda majimbo kumi katika dunia nzima pamoja na kanisa la Rumi likiwa na watawala saba tangu kuanza kazi yake baada ya kupata jeraha la mauti. Biblia inapotumia neno mwanamke kiunabii humaanisha kanisa (Ufunuo 21:2) na neno‘kichwa’ humaanisha kiongozi wa kanisa ambapo kwa kanisa la Mungu, kichwa ni Kristo lakini kwa kanisa la uongo, kichwa ni mwanadamu aliyechukua nafasi ya Yesu duniani, (Wakolosai 1:18; 2Wathesalonike 2:4). Biblia kamwe haijawahi kutumia neno ‘kichwa’ kumaanisha kiongozi wa kiserikali ila hutumia neno ‘watawala au wafalme’. Ndio maana vichwa saba inamaanisha vipindi saba vya viongozi saba wa kanisa. Ufunuo 17:8 anasema kwamba mnyama huyo yuko tayari kupanda kutoka kuzimu na katika Ufunuo 9:11 tunasoma kwamba “Na juu yao wanaye mfalme, naye ni malaika wa kuzimu…”. Mafungu yote hayo yanamaanisha umizimu (spiritualism) ambayo ni imani ya Illuminati. Imani hii inamfanya muumini aamini kwamba hakuna kifo na mtu anapokufa anakuwa amebadilisha mahali kwa kuhama duniani na kwenda mahali pengine akiendelea kuishi na kwamba hiyo ndiyo mbingu yake maana hawaamini kama kuna ufufuo. Chanzo cha fundisho hili ni Shetani alipomfundisha Hawa kwamba “Hakika hamtakufa” Mwanzo 3:4. Hivyo tutajifunza na kuona ukweli huu wa Illuminati kwa kujiunga na kanisa ili kutimiza malengo yao.

Je, kuna watu au kitu kinachoitwa Illuminati? Inaweza kuwa katika kizazi chetu hiki? Baadhi wamekuwa wakidhihaki kuhusu swala zima la Illuminati. Hata hivyo katika kitabu hiki unaweza kupata ufahamu wa kina kuhusu Illuminati na Freemason ndani ya jamii tunayoishi. Je, maneno kama Illuminati au Freemason ni mapya kwako? Hilo linawezekana maana maneno hayo hayafahamiki kwa watu wengi, hata kwa wasomi wakubwa wa elimu ya duniani. Hii ni kutokana na ukweli kwamba wahusika wa maneno hayo wamekuwa wakifanya kazi zao kwa siri kubwa kiasi cha kuwafanya watu mamilioni wasielewe kinachoendelea na hivyo maneno hayo kuendelea kuwa siri kubwa.

“The great strength of our order lies in its concealment,” yaani “nguvu kubwa ya utaratibu wetu iko katika kuficha na kufanya kazi zetu kwa siri kubwa” ni maneno ya Adam Weishaupt, mwanzilishi wa Illuminati mwaka 1776. Akaendelea kusema, “Let it never appear in any place in its own name, but always covered by another name and another occupation” yaani “Hebu isionekane mahali popote kwa jina lake, lakini daima ifanyike kwa jina lingine na kwa namna nyingine.” (Kutoka kwa Robin’s Proofs of a Conspiracy, p. 195.)

Kazi hizi za Illuminati zimekuwa zikifanyika duniani kote kwa karne nyingi kiasi kwamba watu wengi hawajui hata kuwepo kwa watu kama hao. Njama hizi za siri zinaweza kuwa na msingi wake tangu wakati wa Nimrodi, mtu yule muovu aliyeanza kazi zake za uasi huko Mesopotamia. Wakati kila mwalimu wa dini anajua kuhusu mnara wa Babeli, ni wachache wanaojua kwamba kanuni za mchakato huo wa zamani wa kujenga mnara wa Babeli ndizo zinazofanya kazi hadi leo katika nyanja za Siasa na Dini.

Kitabu hiki kiitwacho ‘Illuminati na Freemason katika mnyama wa namba 666’, kitakupa ukweli wa leo na wa ajabu na ukiondoa Biblia, ni vitabu vichache vinavyoweza kukupatia habari za uhakika na muhimu kwa ajili ya wokovu wa maisha yako. Sio lengo la mwandishi wa kitabu hiki kushabikia dini fulani au kuanzisha kanisa na kupata waumini kama wafanyavyo walio wengi, bali lengo ni kutoa bila woga wala upendeleo ukweli halisi kama ulivyotolewa na Mungu mwenyewe. Hivyo kama utakutana na habari zinazopingana na imani yako ni vema basi kutulia na usikasirike maana hasira ya mwanadamu haitendi haki ya Mungu (Yakobo 1:20), ni vema kumuuliza Mungu kwa unyenyekevu ili akuhakikishie kama habari hizi zinatoka kwake na uwe tayari kupokea lolote atakalokujibu. Mungu ni mwaminifu na hakika atakujibu kama utamwendea kwa nia ya kutaka kufuata ukweli wake. Lengo la mwandishi wa kitabu hiki ni kuwapeleka wasomaji kwa Mungu mwenyewe na sio kuwapeleka kwa mwandishi. Kabla ya kuanza kujifunza kwa undani, hebu tuone vyanzo vya habari hizi nzito. Ninatoa shukrani kubwa kwa ajili ya vitabu hata vile ambavyo hatuvikubali, maana vinatuonyesha mawazo ya waandishi wengine. Vipo vitabu vingi ambavyo vimetumika katika kuandaa kitabu hiki, vitabu hivyo baadhi ni pamoja na “The Illuminati 666” cha ndugu Roy Allan Anderson; “The broken Cross” cha Padre Peirs Compton wa kanisa katoliki; “The Two Babylonians” cha ndugu Alexander Hislop, “Freemasonry encyclopedia”, “Morals and Dogma” cha Dr. Albert Pike; “To be God of One World” cha Robert Sessler; “The Keys of this Blood” cha Padre Malachi Martin wa kanisa katoliki, “The Secrets of The Illuminati” cha ndugu Mac Marquis aliyewahi kuwa freemason na akajitoa, mtandao wa Wikipedia na mitandao mingine mingi ikiwa ni pamoja na vyanzo vya kuaminika kutoka kwa Illuminati na Freemason wenyewe; pamoja na vitabu vingine vingi utakavyoviona kama rejea ya kila nukuu utakayoisoma. Hata hivyo kitabu ambacho tumekitegemea sana katika kuandika kitabu hiki, ni kitabu cha vitabu vyote, kitabu ambacho ni zaidi ya vitabu vyote, kitabu ambacho ni tofauti na vitabu vingine vyote duniani kilichoandikwa na zaidi ya watu 30 walioishi wakati na mahali tofauti tena kwa tofauti ya maelfu ya miaka, wengi wao bila kukutana wala kufahamiana huku muasisi akiwa ni Mungu Mwenyewe, kitabu hicho ni “Biblia Takatifu” ambayo pamoja na kuandikwa na watu zaidi ya 30, hawakutofautina hata katika neno moja. Wakati tumetumia nukuu kutoka katika vitabu vingine, lakini bado tumechukulia kwamba neno la Mungu ndani ya Biblia ndilo lenye nuru na ukweli wa mwisho na hivyo limetumika hata kupima maandishi ya vitabu vingine. Kwa muda wa miaka zaidi ya kumi na mbili sasa tangu nianze kufanya uchunguzi kuhusu vyama vya siri, kamwe sijawahi kufundisha bila kupima mafundisho ya vyama hivi kwa kutumia Biblia. Kila mipango na matukio yanayofanywa na Illuminati nimekuwa nikiyapima kwa Biblia katika unabii ili niwe na uhakika kama mipango yao iko sawa na unabii alioutoa Mungu kupitia Biblia.

Tunaweza kusoma katika Ufunuo 17:17 nabii Yohana anasema: “Maana Mungu ametia mioyoni mwao kufanya shauri lake, na kufanya shauri moja na kumpa Yule mnyama ufalme wao, hata maneno ya Mungu yatimie” ikiwa na maana kwamba Mungu ametia shauri lake mioyoni mwa Illuminati ili wapange mipango yao ya kumpa ufalme wao mnyama wa namba 666 kusudi maneno ya Mungu—yaani unabii wa Mungu utimie. Hapa tunaweza kutambua kwamba mipango ya Illuminati inakwenda sawa na unabii wa Mungu. Kitabu hiki kitakupa habari za uhakika jinsi mipango ya Illuminati ilivyowekwa kwa ajili ya kumpa utawala wao na nguvu zao mnyama wa namba 666 ili apate kutawala dunia kama Mungu alivyotufunulia katika unabii wa Biblia. Mipango hiyo ni ya siri ikiwa ni pamoja na kuweka ratiba ya vita kuu tatu (3) za dunia ambapo tayari vita kuu mbili za dunia zimeshatekelezwa wakati vita kuu ya tatu ya dunia itatekelezwa muda simrefu.

Katika agano la kale na agano jipya ndani ya Biblia ndipo tumeweza kupata mwanga wa kuelezea siri hizi za Illuminati na Freemason, ambalo ndilo kusudi la kitabu hiki ili watu wajue ukweli na kisha wawe huru kutoka utumwani mwa shetani. Mtume Paulo katika barua zake kwa kanisa ameelezea kuhusu “Siri ya Mungu” ambayo katika neno la Mungu ni “Mungu kufunuliwa katika mwili,” na “Kristo ndani yetu, tumaini la utukufu wetu” (1Timotheo 3:16; Wakolosai 1:26,27). Katika barua yake ya pili kwa Wathesalonike anaelezea kuhusu “Siri ya kuasi” ambayo anaiita “Mtu wa dhambi,” maana yake mnyama wa namba 666, anayejifanya kuwa ni Mungu akitaka aabudiwe kama Mungu (2Wathesalonike 2:7; 3 na 4). Mtume anasema kwamba siri hiyo ilikuwa inatenda kazi tangu wakati wake lakini akaelezea kwamba siri hiyo itafanya kazi kubwa zaidi wakati wa mwisho kwa kutumia ishara na maajabu mengi. Hivyo tunakuta aina mbili za siri, yaani “Siri ya Mungu” na Siri ya kuasi”. Siri ya kuasi inatokana na uasi wa Shetani na kisha kuendelea kufanya kazi zake kwa siri kubwa ili kuwafanya watu wasielewe kinachoendelea katika ulimwengu wa siasa, uchumi, elimu na dini na hivyo watu wengi wanakuwa watumwa wa freemason bila wao kujua kama ni watumwa.

Kwa nini nimehusisha mnyama wa namba 666, Illuminati, freemason na maswala ya ibada na imani? Ukweli ni kwamba unapoongelea Illuminati, Freemason na mnyama wa  namba 666 unaongelea kuhusu mambo ya imani, ibada na utawala kama anavyosema mmoja wa Illuminati mwenye digrii 33 Bw. Albert Pike, namnukuu: “Every Masonic Lodge is a temple of religion, and its teachings are instruction in religion” (Albert PikeMorals and Dogma, P. 213.) Kwamba “kila Loji (Jumba au kituo) ya Freemason ni hekalu la mambo ya dini, na mafundisho yake ni maagizo katika dini.” Bw. Albert anaendelea kusema kwamba: “Freemasonry is a search for Light. That search leads us directly back, as you see, to the Kabalah.” [Albert Pike, Morals and Dogma, p. 741]

Kwamba “Freemason ni kutafuta nuru. Na kutafuta huko kunatufanya, kama unavyoona, tujielekeze Kabalah.” Kama Freemason wana kazi ya kutafuta nuru, ambayo kwa kweli siyo nuru ya kweli, basi watu wanaotafuta wokovu wanapaswa kutafuta nuru ya kweli. Yesu alisema, “Ninyi ni nuru ya ulimwengu.” Mathayo 5:14 Hivyo tutakuwa tukichunguza mambo ya imani, ibada na utawala ambavyo ni vitu muhimu zaidi kuliko kitu kingine katika maisha ya mwanadamu maana ndivyo vitakavyotoa taswira ya hatima ya kila mmoja wetu, ama ni uzima wa milele au kupotea milele. Mibaraka ya kujifunza neno la Mungu ni kwamba unapoona dalili fulani zikitokea, hazikustui wala kukutia hofu. Dalili hizo badala yake zinakufanya usonge mbele katika kufanya kile ambacho Mungu amekiagiza ili kushiriki na wengine mibaraka hiyo ya ukweli kadri wengi wanavyoweza kuwa na masikio na kusikia. Lakini pia kushiriki huku kwa mibaraka na wengine si kwa lengo la kuwafanya wawe na hofu, bali kuwafanya wajiandae kutokana na kile kitakachoupata ulimwengu kadri tunavyoishi. Kwa kufanya hivyo mara kwa mara huwafanya wasikilizaji na wasomaji watafute kutembea na Mungu kwa ukaribu zaidi ili kwamba wawe tayari kwa lolote atakalowaambia kulifanya katika siku hizi za mwisho. “Yaliyokuwako ndiyo yatakayokuwako; na yaliyotendeka ndiyo yatakayotendeka; wala hakuna jambo jipya chini ya jua.” Mhubiri 1:9.

Kujifunza unabii kunaweza kuwa ni jambo muhimu na zuri ambalo kamwe haliwezi kushindwa katika kuamsha roho ya kumtafuta Mungu. Kila siku mtu anapojifunza ukweli wa leo kutoka kwa Mungu, ndipo anapoanza kuona zaidi na zaidi unabii unavyotimia mbele yake. Wakati watu wengi wanashindwa kuona hatari inayowakabili, msomaji wa neno la Mungu anapata mbaraka wa kujua maonyo na hivyo kuweza kujiandaa yeye na nyumba yake kwa ajili ya kurudi kwa Yesu mara ya pili. Na hii ndio sababu kwamba Yesu hatakuja kama mwivi kwa yeye aaminiye, maana anaweza kujua unabii na kujiweka tayari kwa ujio wa Yesu. Ndio maana Paulo anasema, “Bali ninyi ndugu, hammo gizani, hata siku ile iwapate kama mwivi.” 1 Wathesalonike 5:4.

Mara nyingi wahubiri huhubiri kuhusu mafungu mawili yanayofuatia katika nukuu hiyo ya Paulo na kisha wanasimamia hapo tu. sababu ni kwamba, kama watalihubiri fungu hilo hapo juu, kondoo wao watahitaji kufahamu ni jinsi gani Wakristo baadhi watakutwa hawako tayari au wako gizani wakati Yesu anarudi. Lakini mhubiri huyo kwa vile hajifunzi unabii na wala hajui unabii vya kutosha ili aweze kuwasaidia wasikilizaji wake, hivyo anakwepa kusoma fungu hilo ili kuepuka maswali atakayoulizwa kutokanana fungu hilo.

Kuna matukio mengi ya kiunabii ambayo yameshatimia katika siku zetu hizi kiasi kwamba sina nafasi ya kuyaelezea maana kila mtu anaona hali ilivyo. Moja ya unabii muhimu sana katika siku hizi za mwisho ni ule wa mnyama wa namba mia sita sitini na sita. Baadhi ya matukio ya kiunabii hayaonekani kuwa ni unabii na watu wengi wamechukulia kuwa ni hali ya kawaida ya asili kutokea. Wakati tunaamini kwamba Yesu aliahidi kwamba atarudi tena kuwachukua walio wake, baadhi wameifanya hiyo ahadi kuwa mzaha na hilo lilielezwa na mtume Petro, akasema,“…..Mkijua kwanza neno hili ya kwamba katika siku za mwisho watakuja na dhihaka zao watu wenye kudhihaki, wafuatao tamaa zao wenyewe, na kusema, Iko wapi ahadi ile ya kuja kwake? Kwa maana tangu hapo babu zetu walipolala, vitu vyote vinakaa hali iyo hiyo, tangu mwanzo wa kuumbwa.” “Watayakataa mafundisho yenye uzima; ila kwa kuzifuata nia zao wenyewe watajipatia waalimu makundi makundi, kwa kuwa wana masikio ya utafiti, nao watajiepusha wasisikie yaliyo ya kweli, na kuzigeukia hadithi za uongo.” 2 Petro 3:3,4; 2 Timotheo 4:3,4. Hili nalo ni tukio la kiunabii maana limetimia. Utakuta ukimwambia mtu akusubiri utarudi muda si mrefu, anakuambia “Umekuwa Yesu?” Akimaanisha kwamba Yesu alisema atarudi lakini hajarudi na hatarudi hivi karibuni. Bahati mbaya wengi wa watu hawa, wenye dhihaka, ni wale wanaodai kuamini mamlaka kuu ya Biblia.

Wanaamini kwamba Yesu atarudi lakini sio sasa ila ni miaka mamia ijayo. Sasa hapa Mungu anatupatia unabii wa siku za mwisho kuhusu mnyama wa ajabu ambaye anatambulika kwa hesabu ya kibinadamu. Wakati Mungu anatumia wanadamu kama wakala wake katika kupeleka nuru ulimwenguni, Shetani naye anatumia wanadamu kama wakala wake wa kueneza dini ya Shetani. Mungu anawaita mawakala wake kuwa ni Wachungaji, Wainjilisti, Mitume, Manabii na watu mmoja mmoja kama washiriki wa upande wa Mungu. Shetani amekuwa akiwaita mawakala wake kuwa ni Illuminati na Freemason ambao hata hivyo hujigeuza na kujiita kama wachungaji, Wainjilisti, Mitume Manabii kumbe kwa ndani ni mbwa mwitu wakali. Nitapaje kuwatambua Freemason na Illuminati hata kama wanajiita majina ya wakala wa Mungu? kitabu hiki kitatoa majibu mengi ya maswali yako. Napenda pia kuomba radhi mapema kwa kutokutafsiri baadhi ya maneno yaliyoandikwa kwa lugha ya Kingereza; hii ni kutokana na umuhimu wa maneno hayo kuwa katika lugha iliyotumika kuyaandika na pia kubana nafasi ili kitabu kisiwe kikubwa. Naamini kwa wale wasiojua lugha ya Kingereza watapata watu wa kuwasaidia kujua maana ya maandishi hayo kwa kuwa ni ya muhimu pia. Baada ya kujifunza yote yaliyoandikwa katika kitabu hiki utaweza kutambua yafuatayo:

1. Malengo na matukio ya Mpango Mpya wa Ulimwengu—-New World Order.
2. Madhara yatokanayo na mpango huo kwa kila mtu duniani.
3. Jinsi mpango huo unavyoathiri hata sasa kila mtu, kila familia na kila dini hata kabla ya hitimisho la mpango huo. Ukiwa umeshapata ujuzi na ukweli huu utaweza kujua jinsi ya:

1. Kujilinda wewe mwenyewe dhidi ya mpango huu, kuwalinda watoto wako, kuilinda familia yako na wote uwapendao.
2. Kuishi maisha ya Kikristo huku ukiwa ni mshindi ndani ya ulimwengu huu wa giza kuu la kiroho kwa sababu utaijua kweli nayo kweli itakuweka huru. Tutaanza kuona katika sura ya kwanza jinsi Shetani anavyofanya kazi kwa siri kubwa chini ya utambulisho wa namba 666 na katika sura zitakazofuatia za kitabu hiki tutaona msingi wa uasi mkuu na matokeo yake, tutaona pia baadhi ya matukio ndani ya jamaii, kiuchumi, kiutamaduni na kidini yaliyo na muhuri wa Illuminati, na hatimaye tutapata wito kutoka mbinguni ili kama tutaitikia wito huo tuweze kurejea katika kanisa la mitume kama lilivyokuwa kabla ya ukengeufu kisha Yesu atakaporudi hivi punde, atukute tuko tayari kumlaki mawinguni.

Kwa nini ni muhimu kumjua Mnyama wa namba 666? Umoja wa mataifa na namba 666

Katika picha hapo juu unaweza kuona umuhimu wa kujua asili ya namba 666 na kwa nini namba hiyo inatumiwa na viongozi wakuu wa umoja wa mataifa. Kwa kifupi kwenye picha hiyo wapo watu 6 wakiongoza mkutano wa umoja wa mataifa na nyuma yao kuna kitambaa kilichoandikwa ‘United Nations 666’ kumaanisha kwamba umoja wa mataifa unaandaa njia ya utawala wa mnyama wa namba 666.

Je, asili ya namba 666 ni nini? Namba 666 inatoka wapi? Wengi wanasoma Biblia au kusikia kutoka kwenye Biblia watu wakitaja namba 666 lakini ni wachache sana wanafahamu kwamba namba 666 ilitoka wapi au kwa nini kitabu cha Ufunuo kinazungumzia kuhusu namba hiyo na kwamba iko kinyume na Mungu. Lakini pia nini maana ya namba 666? Watu wengi wanafikiri kwamba namba hiyo ni ya shetani, Je ni kweli? Hebu tuangalie kwa ufupi historia ya namba hii kwamba ilitoka wapi.

Namba 666 inatokana na ibada zilizokuwa zikifanywa na watu wa Babeli wakati wa kipindi cha nabii Ibrahimu na nabii Danieli. Babeli ni mji na mnara uliojengwa na Nimrodi mara baada ya gharika akiwa na makusudi makubwa mawili. Kusudi la kwanza ilikuwa ni kuwalinda watu wa Babeli na gharika kwa kutumia mnara uliokusudiwa kufika mbinguni kwenye miungu wa angani. Kusudi la pili lilikuwa ni kuwakusanya watu wote wakae mahali pamoja na kuwa na serikali na dini moja kinyume na mpango wa Mungu wa kuijaza nchi. Mungu aliingilia kati na kukwamisha ujenzi wa mnara wa Babeli ingawa Nimrodi alifanikiwa kufika mbinguni kimawazo na kupata miungu 36 ambazo ni sayari na nyota. Makusudi hayo mawili yameendelea kufanya kazi hadi leo na hivi karibuni ulimwengu wote utashuhudia serikali na dini moja ikimuabudu mungu jua ambaye alikuwa ni mungu baba wa Wababeli. Watu wa Babeli waliabudu miungu iliyotokana na utafiti wa nyota—yaani unajimu (astrology). Hivyo watu wa Babeli wakawa na miungu ambayo ni jua, mwezi, sayari zinazoonekana pamoja na nyota walizozigundua wakati wa utafiti wa nyota. Watu wa Babeli ndio chimbuko la mwanzo wa unajimu wa nyota ambapo hata leo tunaona wanajimu wakitabiri kwa kutumia nyota. Wababeli walitumia hesabu pia katika shughuli zao za kila siku ikiwa ni pamoja na ibada zao.

Kulikuwa na jumla ya miungu 36 na mungu aliyekuwa mkuu alikuwa ni mungu jua kwa sababu alichukuliwa kuwa ndiye baba wa mimgu wote. Wapagani wa Babeli walikuwa wakiwaabudu miungu hao kwa sababu mbalimbali kama vile kupiga ramuli, kuomba kinga na hata kutoa utabiri wa wakati ujao kwa sababu waliamini kwamba wote walikuwa ni waovu hivyo waliwaogopa miungu wao.

Watu wa Babeli waliamini kwamba namba zina nguvu kwa miungu waliokuwa wanaabudiwa. Kila mungu kati ya miungu 36 alipewa namba yake iliyotumika kumuwalisha mungu na mahali pake (Rejea Murl Vance, Trail of the Serpent, uk. 26, 27, 72). Namba aliyopewa mungu iliwakilisha nguvu aliyonayo mungu huyo. Kwa hiyo namba husika kwa mungu iliwakilisha ukuu wake ikimaanisha kwamba mungu aliyepewa namba za awali alikuwa na nguvu kubwa kuliko aliyepewa namba za mbele.

Kwa nini kulikuwa na miungu 36? Je, namba 36 ilitokana na nini? Wababeli walipata idadi ya miungu wao kuwa 36 kwa sababu kila mungu alitakiwa kuheshimiwa au kutawala kwa mzunguko wa nyuzi 10 au digrii 10 kwa mwaka na kwa vile mwaka una siku 360 waligawa kwa 10 na kisha ikawa sababu ya kwanza kupata idadi ya miungu wao 36. Lakini pia wanajimu au watafiti wa sayari na nyota waligundua jumla ya sayari na nyota 36 na kwa vile walikuwa wakiziabudu wakazifanya kuwa miungu wao. Ni kutokana na miungu hao 36 Wababeli walifanya hesabu na kupata namba 666 ikimaanisha mamlaka, nguvu na ukuu wa miungu wote 36.

Watu wa Babeli walihesabu miungu wao kuanzia namba 1 hadi 36 na kasha kujumlisha. Mungu wa kwanza alipewa namba 1 na mungu wa pili alipewa namba 2 na kuendelea. Mungu wa namba 1 alikuwa ni mungu jua na mungu namba 2 alikuwa ni mungu mwezi. Miungu kuanzia namba 3 hadi 36 walikuwa ni watoto wa mungu jua ambao walikuwa ni sayari na nyota zilizogunduliwa na wanajimu wa Babeli. Ndipo wakajumlisha namba 1 hadi 36 na kupata namba 666. tazama hesabu hii kuhusu asili ya namba 666:

1 + 2 + 3 + 4 + 5 + 6 + 7 + 8 + 9 + 10 + 11 + 1
2
+ 13 + 14 + 15 + 16 + 17 + 18 + 19 + 20 + 21 + 2
2
+ 23 + 24 + 25 + 26 + 27 + 28 + 29 + 30 + 31 + 3
2
+ 33 + 34 + 35 + 36 = 666

Umuhimu wa namba 36 kwa Wababeli ulisababishwa na mgawanyo wa ishara 12 zinazoitwa ‘12 Zodiac signs’ sawa na miezi 12 kwa mwaka na ishara hizo zilitokana na unajimu wa nyota na waligawa namba 36 katika mafungu matatu ya 12 Zodiac signs—12 x 3 = 36. Wababeli waliamini kwamba mtu anapokufa anakwenda kwa mungu wake. Miungu hawa 36 waliitwa kwa jina la ‘Decans’ kwa pamoja kwa sababu kila mmoja alitakiwa kufanya kazi kwa digrii 10 katika mzunguko wa Zodiac kwa siku 10 katika siku 360 za mwaka. Kila mtu alipewa kundi lake katika ishara 12 kutegemeana na mwezi aliozaliwa na huo ukawa mwanzo wa utabiri wa maisha ya mtu kwa kutumia nyota zilizokuwa katika mafungu matatu (3) ya miezi 12 katika jumla ya miungu 36.

Sayari 7 au joka lenye vichwa 7 ndilo lililotawala miungu hawa wote 36 walioitwa Decans na kati ya miungu hao aliyekuwa mtawala wa wote alikuwa ni mungu jua. Jumla ya namba 1 hadi 36 sawa na 666 iliitwa “The Grand Number of the Sun” yaani jumla kuu ya hesabu ya jua.

Kila mungu aliwakilishwa kwa alama na wakati wa ibada kila muumini alitakiwa kuvaa hirizi inayomuwakilisha mungu wake kati ya miungu 36. Hivyo kulikuwa na aina 36 za hirizi zilizowakilisha miungu 36. Hirizi hizo zilitengenezwa kwa mfumo wa hesabu uitwao ‘6×6 Matrix’ na mtu ambaye alikataa kuvaa hirizi iliaminiwa kuwa angepata majanga ya ugonjwa, njaa, mateso na kisha kifo.

Wapagani wa Babeli walitakiwa kuvaa hirizi yenye namba na alama ya mungu mhusika. Wakristo wachukua desturi hii kwa kuendelea kuvaa msalaba shingoni ukiwakilisha alama ya mungu Ishtar. Unaweza kuangalia picha hii mwanamke akiwa amevaa sura ya simba kichwani kumaanisha utawala wa Babeli uliowakilishwa na simba (Danieli 7:4) na amevaa hirizi shingoni yenye namba tofauti pamoja na mduara wenye jicho kifuani mwake uliowakilisha mungu jua aonaye kila mahali.

Hirizi na alama ya mungu mhusika

Hirizi hizo zilitengenezwa kwa mfumo wa hesabu uitwao ‘6×6 Matrix’ (rejea jedwali la hesabu za Illuminati) na mtu ambaye alikataa kuvaa hirizi na alama ya mungu wake iliaminiwa kuwa angepata majanga ya ugonjwa, njaa, mateso na kisha kifo. Je, mtu alipata kujua vipi kwamba mungu fulani ni mungu wake? Watu wote waliwekwa kwenye mafungu matatu (3) ya ’12 Zodiac Signs’ kufuata mwezi aliozaliwa mtu husika na hivyo kulikuwa na makundi matatu (3) yaani kundi la kwanza watu wote waliozaliwa mwezi wa kwanza  Hadi wa nne, kundi la pili waliozaliwa mwezi wa tano hadi wa nane, la tatu mwezi wa tisa hadi wa kumi na mbili. Kila kundi likiwa na miezi mitatu lilileta namba 6, yaani 1+2+3 =6 na wakaweka makundi yote matatu pamoja na kupata 666 ikimaanisha namba iliyowahusu watu wote kutokana na kuzaliwa kwao ndani ya miezi 12  Ya mwaka. Unaweza kuchunguza alama zinazotumika kwenye utabiri wa nyota utaziona zikiwakilisha  ng`ombe, nge, samaki na kadhalika. Elimu hiyo ilitokana na miungu wa Babeli waliowakilishwa kwa alama na namba.

Sayari 7 au joka lenye vichwa 7 ndilo lililotawala miungu hawa wote 36 walioitwa ‘Decans’ na kati ya miungu hao aliyekuwa mtawala wa wote alikuwa ni mungu jua. Kwa mfano kama mtu alivaa hirizi yenye namba 2 ilimaanisha kuwa mungu wake ni mungu mwezi na hivyo alitakiwa awe na alama ya mungu mwezi akiwa amevaa shingoni mwake pamoja na hirizi na kama mtu alivaa hirizi namba 1 alitakiwa kuvaa alama ya mduara iliyowakilisha mungu jua huku aliyevaa hiziri namba 6 alivaa pamoja na alama ya msalaba ikiwakilisha mungu Ishtar.Kwa kutumia hesabu, Wababeli walifanikiwa kutengeneza jedwali lenye namba 1 hadi 36 ambapo namba hizo zikijumlishwa kwa pamoja katika kila msitari wowote unapata jumla ya 111 na kwa vile jedwali lina misitari 6 walizidisha 111 x 6 = 666.

Namba iliyoandikwa kwenye hirizi ilimpa nguvu mvaaji zilizotoka kwa mungu aliyepewa namba hiyo. Nguvu ya mungu iliweza kuongezeka kwa kujumlisha namba ya mungu huyo na namba zingine katika msitari na kupata namba 111 na mungu alizidi kupata nguvu zaidi kwa kuzidisha 111 x 6. Namba 666 ilikuwa ni alama ya mamlaka ya miungu wote hivyo ilimaanisha kwamba ilikuwa na nguvu kwa miungu
wote.Hapa chini ni jedwali lenye namba za miungu 36 wa Babeli.

Kumbuka kwamba Wababeli walikuwa ni waabudu sanamu na hawakumuabudu Mungu wa kweli. Hata
hivyo leo pia kuna ibada nyingi ambazo chimbuko lake ni ibada za sanamu kutoka Babeli. Jedwali la miungu 36 wa Babeli.

6 32 3 34 35 1
7 11 27 28 8 30
19 14 16 15 23 24
18 20 22 21 17 13
25 29 10 9 26 12
36 5 33 4 2 31

Zingatia kwamba namba 666 haiwezi kusimama peke yake bila kuhesabu miungu maana bila kuhesabu huwezi kupata jumla ya namba 666. Hivyo unapotaka kuielezea namba 666 lazima ufanye hesabu na kisha upate jumla yake iwe 666. Hata hivyo haimzuii mtu kutumia njia nyingine ili kupata jumla ya 666, ila jambo muhimu ni kwamba unatakiwa ujue asili ya namba 666 na kwamba ilipatikana kwa kujumlisha miungu wa Babeli na ndio maana Mungu wa Mbinguni anaihusisha namba 666 na Babeli maana chimbuko lake ni Babeli. Kwa watu wa Babeli, mungu aliyehitimisha hesabu na kufanya jumla iwe namba 666 ndiye aliyekuwa na nguvu hata kumshinda mungu jua ambaye alikuwa ni baba wa miungu wote. Wakati Biblia inapotuambia kwamba mnyama ana namba 666 inatuambia kwamba namba 666 ilipatikana kwa kuhesabu na kujumlisha miungu na haimaanishi kwamba namba 666 inasimama peke yake. Kama hakuna miungu itakayohesabiwa, isingewezekana kupata jumla ya namba 666. Biblia inatuambia pia kwamba hesabu inaanzia kwa mungu wa kwanza na kujumlisha namba ya miungu wanaofuatia na mungu ambaye angehitimisha hesabu kwa kufanya jumla iwe 666 mungu huyo angeweza kuwa na nguvu zaidi hata ya mungu wa kwanza maana yeye angetumia namba 666 yenye nguvu za miungu wote.

Wababeli pia walikuwa na miungu saba (7—sayari 7) wa kwanza ambao ndio walikuwa maarufu na ndio waliotumia majina ya siku kwa wiki kama ifuatavyo:

JEDWALI LA SAYARI 7 SAWA NA MIUNGU 7 YA BABELI.

Miungu Sayari/vichwa vya Joka/majina ya siku katika wiki Jina la Sayari Jina la mungu wa Babeli Jina la siku kwa leo

Jua Shamash—namba 1 Sunday – jumapili
Mwezi Sin—namba 2 Monday- jumatatu
Mars Nergal—namba3 Tuesday- jumanne
Mercury Nabu—namba 4 Wednesday- jumatano
Jupiter Marduk—namba 5 Thursday- alihamisi
Venus Ishtar—namba 6 Friday- ijumaa
Saturn Ninib—namba 7 Saturday- jumamosi

Unaweza kuona jinsi miungu hawa wa Babeli walivyoendelea kuabudiwa hata wakati wa Ukristo maana baada ya karne nyingi kupita, wakati mtume Paulo na Barnaba walipotembelea Listra, walifanya muujiza wa kumponya mtu aliyekuwa kiwete. Watu wa mji huo walikuwa waabudu miungu wa Babeli na mara baada ya kufanyika kwa muujiza huo, watu “wakapaza sauti zao wakisema kwa Kilikaonia, Miungu wametushukia kwa mfano wa wanadamu. Wakamwita Barnaba, Zeu, na Paulo, Herme, kwa sababu ndiye aliyekuwa mnenaji”. Matendo 14:12. Unaposoma Biblia ya King James, jina Zeu ni sawa na Jupiter, na Herme ni sawa na Mercury. Leo sayari au madini ya Mercury yanatumiwa sana kwa ajili ya mawasiliano na ndio maana wapagani hao walimuita Paulo jina la Mercury kwa sababu yeye ndiye alikuwa mnenaji. Ni kwa njia hiyo hata leo ibada za miungu wa Babeli zinatawala ndani ya dini nyingi na waumini wengi hawajui kwamba wanaabudu wasichokijua kama Yesu alivyomwambia yule mwanamke msamaria

(Yohana 4:19-24). Sasa, utakapofahamu kweli hii, tafadhali itikia wito wa Mungu anaposema, “Umeanguka, umeanguka Babeli….Tokeni kati yake enyi watu wangu”.

Ufunuo 18:4.

Unaweza kuangalia jinsi joka mwenye vichwa saba alivyoaminiwa na Wababeli kuwa ni miungu saba, kitu ambacho ni kweli ukilinganisha na Ufunuo 13na Ufunuo 17. Wababeli waliendelea na hesabu, wakajumlisha namba 1 hadi 3 yaani 1+2+3 = 6 na kuhitimisha kwamba namba 6 inawakilisha nguvu ya mungu baba (jua), mungu mama (mwezi) na mungu mwana (sayari ya mars). Kisha wakatumia namba 11 kujumlisha miungu namba 1 hadi 11 yaani 1+2+3+4…..+11 = 66 wakamaanisha kwamba namba 66 ina nguvu za miungu 11 wa kuanzia namba 1 hadi 11 na kisha wakajumlisha namba 1 hadi 36 wakapata namba 666 ikimaanisha mamlaka na nguvu za miungu wote. Hapa walichukua namba 3, 11 na 36 na kuzifanya kuwa namba muhimu kwao. Biblia inatuambia kuhusu mfalme Nebukadneza wa Babeli kwamba “alifanya sanamu ya dhahabu ambayo urefu wake ulikuwa ni dhiraa 60 na upana wake dhiraa 6…” Danieli

3:1. Nebukadneza alitumia hesanu za miungu wa Babeli ili kutengeneza sanamu ikimaanisha kwamba alichukua miungu watatu yaani 1+2+3 = 6 kwa upana wa sanamu hiyo na kisha akazidisha kwa nyuzi 10 ya kila mungu katika mzunguko wa Zodiac signs na kisha kupata 6×10 = 60 kwa vipimo vya urefu wa sanamu hiyo. Kwa kifupi hiyo ndiyo asili ya namba 666 ikiwa inatokana na jumla ya miungu wa

Wababeli ambao walikuwa miungu 36 na ukijulisha namba zote kuanzia 1 hadi 36 = 666. Kazi iliyopo sasa ni kutumia kanuni ya Wababeli ili tuweze kumjua mnyama anayewakilishwa na namba 666 kwa leo maana hatimaye ulimwengu wote utamsujudia mnyama huyo badala ya kumuabudu Mungu. Tutaanza kwa kujifunza katika kitabu cha Ufunuo na Danieli ili kuona ujumla wa jinsi ya kumtambua mnyama huyo.

Tunasoma kwamba “Na watu wote wakaao juu ya nchi wakamsujudu, kila ambaye jina lake halikuandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-kondoo aliyechinjwa tangu kuwekwa misingi ya dunia. Mtu akiwa na sikio na asikie. Hapa ndipo penye hekima. Yeye aliye na akili, na aihesabu hesabu ya mnyama huyo; maana ni hesabu ya kibinadamu.

Na hesabu yake ni mia sita, sitini na sita.” Ufunuo 13: 8,9; 18. Jambo muhimu ni kwamba heasabu ya mnyama huyu inapatikana kwa kuhesabu, yaani 1, 2, 3, …na kadhalika na kwamba mnyama huyu ataabudiwa, lakini watakaomwabudu ni wale ambao majina yao hayakuandikwa kwenye kitabu cha Mwana-kondoo, kwa maana nyingine ni wale ambao hawatakwenda mbinguni, wale ambao hawakukubali kafara ya Mwanakondoo.

Watu wengi leo wanaridhika kuandikwa majina yao kwenye vitabu vya makanisa yao badala ya kujitahidi ili majina yao yaandikwe kwenye kitabu cha uzima cha Mwana-kondoo.

Sasa ni jukumu na muhimu kwa kila mmoja wetu anayetaka jina lake liandikwe katika kitabu cha Mwana-kondoo kutambua kwamba jina lake litaandikwa kweny kitabu hicho kwa masharti ya kutokumsujudia mnyama wa namba 666. Tunapaswa kujiuliza swali moja muhimu, kwamba, nitawezaje kutokumsujudia mnyama huyo kama mimi mwenyewe sijamfahamu jinsi anavyofanana, jinsi anavyofanya kazi yake na hata kufahamu mahali alipo? Jibu ni kwamba ni lazima umtambue huyo mnyama na kutambua kazi zake ndipo utafanikiwa kutokumsujudia na hivyo jina lako kuandikwa kwenye kitabu cha Mwana-kondoo.

Lakini pia “Mtu awaye yote akimsujudu huyo mnyama na sanamu yake, na kuipokea chapa katika kipaji cha uso wake, yeye naye atakunywa katika mvinyo ya ghadhabu ya Mungu iliyotengenezwa pasipo kuchanganywa na maji, katika kikombe cha hasira yake; naye atateswa kwa moto na kiberiti mbele ya malaika watakatifu, na mbele ya Mwanakondoo.”

Ufunuo 14:9,10. Je, ni muhimu kweyu kujifunza ili tumtambue huyu mnyama mwenye namba 666? Kwa wale wanaotaka majina yao yaandikwe kwenye kitabu cha

Mwana-kondoo wataona umuhimu huo. Shetani amekuwa akitumia namba sita kuonyesha utawala wake maana katika viumbe vyote vilivyoumbwa na Mungu hapa duniani, ni Adamu peke yake ndiye aliyeasi sheria ya Mungu na Adamu huyo aliumbwa katika siku ya sita. Hivyo Shetani akapata utawala wa dunia hii kupitia kiumbe aliyeumbwa siku ya sita (Mwanzo 2:26-31). Tangu alipofukuzwa kutoka mbinguni Shetani amekuwa akimtumia mwanadamu kama wakala wake wa kufanya kazi ya kupotosha kazi ya Mungu. Wakati wa utawala wa Babeli

Shetani alimtumia mfalme wa Babeli kama wakala wake na akamuagiza atengeneze sanamu yenye vipimo vya namba sita: “Nebukadreza, mfalme, alifanya sanamu ya dhahabu, ambayo urefu wake ulikuwa ni dhiraa sitini, na upana wake dhiraa sita, akaisimamisha katika uwanda wa Dura, katika wilaya ya Babeli.” Danieli 3:1. Baada ya kutengeneza sanamu hiyo, iliamuriwa kwamba watu wote waisujudu na kuiabudu sanamu hiyo atakayekataa sharti auwawe. Lakini walikuwepo vijana watatu ambao walikubali kufa kuliko kuisujudu sanamu hiyo. Vijana hao walikataa kwa sababu majina yao yalikuwa yameandikwa kwenye kitabu cha Mwana-kondoo. Ndivyo itakavyokuwa hivi karibuni watu wote ambao majina yao hayakuandikwa kwenye kitabu cha Mwanakondoo watamsujudia mnyama wa namba 666, na kwa kweli wengi wanamsujudia mnyama huyo, wengine wakiwa wanajua na wengine wakiwa hawajui. Hata hivyo uwe unajua au hujui kitu muhimu ni kwamba wote wanaomsujudu huyo mnyama majina yao hayakuandikwa kwenye kitabu cha Mwana-kondoo.

Hivyo basi limekuwa kusudi la Shetani kuuangamiza ulimwengu kupitia mnyama wa namba 666 na ni jambo muhimu kwetu kumfahamu mnyama huyo maana bila kumfahamu tutaangamizwa na Shetani kama Mungu anavyosema “Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa…..” Hosea 4:6. Haya si maarifa mengine bali yale ya kuweza kuihesabu hesabu ya mnyama, yaani mia sita sitini na sita maana Yohana anatuambia pia kwamba, “Hapa ndipo penye hekima. Yeye aliye na akili, na aihesabu hesabu ya mnyama huyo…”
Napenda tuelewe kwamba tunapojifunza habari za mnyama huyu tunajifunza habari za ibada ya kweli na ibada ya uongo maana mnyama huyu anaabudiwa pia. Hebu tuiruhusu sasa Biblia iweze kutuelezea habari zaidi za mnyama huyu. Tutaanza kwa kuchunguza mambo yanayokwenda sambamba na mnyama huyu kisha tutahakikisha kama tuko sawa kwa kuihesabu hesabu ya mnyama. Biblia inasema:

“Kisha nikaona mnyama akitoka katika bahari, mwenye pembe kumi na vichwa saba, na juu ya vichwa vyake ana vilemba kumi, na juu ya vichwa vyake majina ya makufuru. 2.

Na yule mnyama niliyemwona alikuwa mfano wa chui, na miguu yake ilikuwa kama miguu ya dubu, na kinywa chake kama kinywa cha simba; yule joka akampa nguvu zake na kiti chake cha enzi na uwezo mwingi. 3. Nikaona kimoja cha vichwa vyake kana kwamba kimetiwa jeraha la mauti, na pigo lake la mauti likapona. Dunia yote ikamstajabia mnyama yule. 4. Wakamsujudu yule joka kwa sababu alimpa huyo mnyama uwezo wake; nao wakamsujudu yule mnyama, wakisema, Ni nani afananaye na mnyama
huyu? Tena ni nani awezaye kufanya vita naye? 5. Naye akapewa kinywa cha kunena maneno makuu ya makufuru. Akapewa uwezo wa kufanya kazi yake miezi arobaini na miwili. 6. Akafunua kinywa chake amtukane Mungu, na kulitukana jina lake, na maskani yake, nao wakaao mbinguni. 7. Tena akapewa kufanya vita na watakatifu na kuwashinda, akapewa uwezo juu ya kila kabila na jamaa na lugha na taifa. 8. Na watu wote wakaao juu ya nchi wakamsujudu, kila ambaye jina lake halikuandikwa katika kitabu cha uzima cha mwanakondoo, aliyechinjwa tangu kuwekwa misingi ya dunia” Ufunuo 13: 1-8.

a) Maelezo hayo yamejaa mafumbo au alama, je nitafahamuje mafumbo na alama hizo? Tunahitaji kuiruhusu Biblia itafsiri mafumbo na alama ilizozisema. Tungetegemea kwamba, Mungu, kwa faida yetu, alifunua ndani ya Biblia maana ya mafumbo na alama hizi. Kwa hiyo, kile tunachohitaji ni usomaji makini ili tupate tafsiri ndani ya Biblia. Kwa njia hiyo, tunaepuka kukisia na ubahatishaji wa kibinadamu. Kwa hakika, Biblia inabatilisha kukisia na ubahatishaji wa kibinadamu kwa sababu “hakuna unabii …….upatao kutafsiriwa kama apendavyo mtu fulani tu” 2Petro 1:20.
Biblia inajitafsiri yenyewe. Kwa mfano, kitabu cha Ufunuo kina jumla ya mafungu 404. Kati ya hayo, mafungu 278 yanapatikana neno kwa neno katika vitabu vingine vya Biblia, ambapo maana yake inajieleza wazi zaidi.
Kwa hiyo, tunakutia moyo kufanya kile Biblia inachotaka ufanye unapojifunza (Angalia Matendo17:10,11 watu wa Thesalonike “…walilipokea neno kwa usikivu, wakayachunguza Maandiko kila siku, waone kwamba mambo hayo ndivyo yalivyo”), na weka kila fundisho lipimwe na maandiko. Kwa vile, kila atakayejifunza Biblia kwa kuomba, akitamani kufahamu kweli, ili aitii kweli hiyo, atafahamu maandiko. “Mtu akipenda kuyatenda mapenzi yake, atajua habari ya yale mafunzo, kwamba yatoka kwa Mungu, au mimi nanena kwa nafsi yangu tu” Yohana 7:17

b) Ni alama (au mafumbo) gani tunazohitaji kuzifunua? Kuna alama nyingi kwa ajili ya mnyama, hata hivyo, tutajikita zaidi kwenye zile ambazo ni muhimu kwa ajili ya fundisho hili ili kumtambua mnyama, sanamu ya mnyama na alama ya mnyama. Alama hizi ni ‘mnyama’, ‘joka’, ‘bahari’, ‘miezi 42’, na ‘makufuru’. Mnyama: Katika unabii wa Biblia, mnyama ni alama ya mfalme au ufalme. “wanyama hao wakubwa, walio wanne, ni wafalme wanne….mnyama wa nne atakuwa ufalme wa nne…”: Dan. 7:17,23. Kuhusu mnyama huyu, tunajifunza mnyama wa pekee kwa sababu siyo tu nguvu ya kisiasa, bali pia ni mnyama mwenye dini, maana watu “walimsujudu huyo mnyama”. Ufunuo 13:4.

Joka: Katika unabii wa Biblia, Joka ni jina jingine la shetani, baba wa uongo na machafuko. “yule joka akatupwa, yule mkubwa,….aitwaye ibilisi na shetani, audanganyae ulimwengu wote.” Hii ingemaanisha kwamba wakati shetani alipotoa “nguvu zake, kiti chake cha enzi, na uwezo mwingi” kwa mnyama, tunaweza kumtarajia mnyama akiwa na tabia ile ile ya shetani au joka, ya udanganyifu. Hivyo basi, udanganyifu mkubwa utaonekana katika tabia ya mnyama. Ufunuo 12:9; 13:2.

Bahari: Katika unabii wa Biblia, bahari ni alama au kielelezo cha wingi wa watu tofauti au wingi wa watu mbalimbali. “….Maji ni jamaa, na makutano, na mataifa, na lugha” Ufunuo 17:15. Vilevile, ufalme huu wa pekee uliinuka kutoka baharini, ikimaanisha kwamba ulitoka katika eneo la dunia ambalo lilikuwa na watu wengi wa mataifa mbalimbali.

Miezi Arobaini na miwili: Kipindi hiki ni sawa sawa na miaka mitatu na nusu (42 gawanya kwa miezi 12). Na Biblia iliandikwa kwa mujibu wa kalenda ya Kiyahudi ambapo kila mwaka wa kiyahudi una siku 360 (yaani siku 30 kwa kila mwezi). Kwa hiyo, miaka mitatu na nusu na miezi arobaini na miwili vyote ni sawa na siku 1260. Sababu inayotufanya tubadili miezi kwenda sambamba na siku zake ni kwamba, wakati Mungu alipotoa unabii, mara nyingi Amekuwa akilinganisha siku moja kwa mwaka mmoja. “….yaani, siku arobaini, kila siku kuhesabiwa mwaka, mtayachukua maovu yenu, ndiyo miaka arobaini…..” “…..siku arobaini, siku moja kwa mwaka mmoja, nimekuagizia.” Hesabu14:34, Ezekieli 4:6. Kwa hiyo, miezi arobaini na miwili ya kiunabii inamaanisha miaka 1260 ambayo mnyama alipewa “kinywa kunena maneno makuu, ya makufuru” na atafanya “vita na watakatifu na kuwashinda: na akapewa uwezo kwa kila kabila, na jamaa, na lugha, na taifa.” Ufunuo 13:5,7… Ikimaanisha kwamba katika kipindi hiki cha miaka 1260, mnyama atakufuru, atatesa wakristo, na atakuwa na uwezo mkuu.

Makufuru: Katika Biblia, makufuru yameelezewa katika namna mbili, ya kwanza ni pale mtu anapodai kuwa yeye ni Mungu au muwakilishi wake. “…kwa ajili ya kazi njema, hatukupigi mawe; bali kwa kukufuru, na kwa sababu wewe uliye mwanadamu wajifanya mwenyewe u Mungu.” Yohana 10:33. Kwa hiyo, mnyama, ambaye ni mwenye mamlaka ya kisiasa na kidini, anamkufuru Mungu kwa kujiweka mahali pa Mungu hapa Duniani. Hata hivyo, wayahudi hawakumwelewa Yesu kuwa ndiye masihi, mwana wa Mungu, sawa na Mungu, ambaye ni Mungu, tofauti na mwanadamu mwingine yeyote asiye sawa na Mungu, na hivyo Yesu hakukufuru. Namna ya pili ya kukufuru, ni kujipa uwezo wa kusamehe dhambi za watu. “Mbona huyu anasema hivi? Anakufuru. Ni nani awezaye kusamehe dhambi isipokuwa mmoja, ndiye Mungu?” Marko 2:7 Hata hivyo, Yesu alikuwa na uwezo wa kusamehe dhambi maana Yeye ni Mungu.

Mnyama huyu, mwenye nguvu za kisiasa na kidini, amemkufuru Mungu, sio tu kwa kuchukua mahali pa Mungu hapa duniani, lakini pia kwa kudai kuwa na uwezo na haki ya kusamehe dhambi. Hivyo si ajabu kuwa mnyama ana “majina ya makufuru” na ananena “makufuru dhidi ya Mungu na jina lake” . Hii ni kwa sababu mnyama anadai kuwa na nguvu ambayo ni haki ya pekee ya Mungu tu. Ufunuo 13:1,6.

Baada ya kuiruhusu Biblia ijitafsiri yenyewe, tunaweza sasa kuwa na funguo tisa zitakazotusaidia kumtambua mnyama. Hata hivyo, hizi si funguo pekee za kumtambua mnyama, zipo nyingi zaidi ndani ya Biblia. Tunatumaini muungano huu wa funguo za utambuzi zitakuongoza kusoma na kujifunza zaidi Biblia ili uweze kupata funguo zaidi.

(1) Mnyama ana mamlaka ya kisiasa na kidini kwa wakati mmoja, “wakamsujudu Yule mnyama…..” Ufu. 13:4 (2) Mnyama alitoka kwenye eneo hapa duniani lenye watu wengi wa mataifa “ …nikaona mnyama akitoka katika bahari.” Ufu.13:1 (3) Mnyama alipata nguvu na mamlaka yake kutoka kwa shetani. “…yule joka akampa nguvu zake na kiti chake cha enzi na uwezo mwingi.” (4) Mnyama alitawala kwa mateso makali kwa mda wa miaka 1260. “…akapewa kinywa kunena maneno ya makufuru. Akapewa uwezo kufanya kazi yake miezi arobaini na miwili.” Ufu.13:5. (5) Mnyama aliwatesa watakatifu kwa miaka 1260 na kuwashinda. Ufu. 13:7 (6) Mnyama atapona jeraha lake la mauti “…na pigo lake la mauti likapona.” Ufu. 13:3 (7) Mnyama ana hesabu ya kibinadamu 666 inayotambulisha ofisi yake. “…na aihesabu hesabu ya mnyama huyo. Na hesabu yake ni mia sita, sitini na sita.” Ufu.13:18 (8) Mnyama anakufuru kwa kudai
anasamehe dhambi na kuchukua nafasi ya Mungu hapa duniani. (9) Mnyama amefanya makufuru mengine kwa vitendo vyake dhidi ya Mungu. “naye akapewa kinywa cha kunena maneno makuu, ya makufuru.” Ufu.13:5. Hizo ndizo sifa za mnyama wa ajabu mwenye namba 666. Sasa tunaweza kumtambua mnyama huyo kutokana na sifa zake kwamba ni taifa ambalo lina utawala wa kisiasa na kidini pia. Haishangazi leo pia kuona nchi nyingi zikitambuliwa kutokana na kuwakilishwa na wanyama. Kwa mfano Tanzania inawakilishwa na mnyama aitwaye Twiga, Marekani inawakilishwa na ndege aitwaye Tai, Urusi inawakilishwa na Dubu, China inawakilishwa na Joka (Dragon), Kenya inawakilishwa na Jogoo nk.

Kwa nini mataifa huwakilishwa na wanyama? Maana yake ni nini? Tunasoma kwamba “Naliona katika maono yangu wakati wa usiku; na tazama, hizo pepo nne za mbinguni zikavuma kwa nguvu juu ya bahari kubwa. Ndipo wanyama wakubwa wane wakatokea baharini, wote wa namna mbalimbali. Wa kwanza alikuwa kama Simba…wa pili kama dubu, ….mwingine kama chui….mnyama wa nne mwenye kutisha.”Danieli

7:2-7. Pia tunasoma “Na yule mnyama niliyemuona alikuwa mfano wa chui, na miguu yake ilikuwa kama miguu ya dubu, na kinywa chake kama kinywa cha Simba….” Ufunuo 13:2. Sababu ya kusoma mafungu hayo mawili ni kwamba katika Danieli tunakuta wanyama wanne tofauti wakati katika Ufunuo tunakuta mnyama mmoja mwenye alama za wanyama wanne wa Danieli. Huyu mnyama wa Ufunuo ni sawa na mnyama wa nne katika Daniel ambaye anatamkwa kuwa ni mwenye kutisha, maana yake ni kwa sababu alikuwa na tabia za wanyama watatu waliomtangulia kutokea.

Ukweli ni kwamba wanyama wa Danieli 7 ni falme nne kama inavyojitafsiri, yaani Babeli, Uyunani au Greece, Umedi na Uajemi na Rumi au Roman Empire. Hizo ni tawala zilizowahi kutawala dunia nzima. Baada ya Roman Empire alifuatia mnyama wa ufunuo 13:1-10 ambao ni utawala wa Rumi ya kidini iliyotawala kwa miaka 1260 kuanzia mwaka 538-1798. Utawala huo ulikuwa na tabia ya tawala zilizoutangulia. i) Simba: utawala unaowakilishwa na simba humaanisha kuwa na ujasiri mkubwa; “Simba aliye hodari kupita wanyama wote; wala hajiepushi na aliye yote.” Mithali 30:30. ii) Dubu: Utawala unaowakilishwa na Dubu hufanana kwa kiasi fulani na utawala unaowakilishwa na Simba; “Bwana aliyeniokoa katika makucha ya simba na makucha ya dubu ataniokoa…” 1 Samweli 17:37. Pia soma Isaya 11:7. iii) Chui: Utawala unaowakilishwa na mnyama chui humaanisha utawala wa kuvizia na unaopenda vita kama vile simba na dubu; “Basi nimekuwa kama simba kwao; kama chui nitavizia njiani; nitakuwa nao kama dubu aliyenyang`wanywa watoto wake; name nitararua nyama ya mioyo yao, na huko nitawala kama simba; huyo mnyama mkali atawararua.” Hosea 13:7-8. Hizo ndizo zilikuwa tabia za falme nne zilizotawala dunia yote. Sasa unaweza kuona kuwa Marekani kuwakilishwa na tai inamaanisha kuwa na tabia ya tai; “Farasi zao ni wepesi kuliko chui, ni wakali kuliko mbwa-mwitu wa jioni; na wapanda farasi wao hujitupa naam, wapanda farasi wao watoka mbali sana; huruka kama tai afanyaye haraka.” Habakuki 1:8. Taifa la Marekani lilianzishwa katika karne ya 18 wakati wa kipindi cha utawala wa mnyama wa 666 ambapo tunasoma kwamba mnyama huyo (Marekani) alitokea katika nchi ikimaanisha kuwa katika eneo ambalo halikuwa na watu. Wakati wa mateso ya mnyama wa 666 ndipo watu walipokimbilia katika bara la Amerika wakitoka ulaya na mabara mengine na mnamo July 4, 1776 Marekani ikapata uhuru chini ya Rais wa tatu aliyeitwa Thomas Jafferson. Marekani kuwakilishwa na tai inamaanisha kwamba ni taifa linalofanya haraka kuruka kama tai na kwenda mbali zaidi lengo likiwa ni kushambulia. Tai ni ndege mkubwa anayekula nyama; hivyo ndio maana tunashuhudia tukiona taifa la Marekani likivamia nchi yoyote duniani na hivi karibuni tutaona Marekani ikiishambulia Iran baada ya kuipiga Iraq. Kumbuka kuwa utawala wa Umedi na Uajemi  ulikuwa katika maeneo ambayo leo kuna nchi za Iraq na Iran. Tanzania kuwakilishwa na twiga; tunafahamu tabia ya twiga alivyo mpole, mnyama asiyependa makuu tena anayependa kula majani ya juu kabisa ambayo hayajaguswa tena yaliyo laini. Je, si kweli kwamba watanzania pia hawapendi ugomvi na ndio maana kuna amani? Maana kila nchi inayowakilishwa na mnyama ina tabia ya huyo mnyama; kwa mfano jirani zetu Kenya wanawakilishwa na jogoo, tunafahamu tabia ya jogoo kwamba hapendi kushindwa na jogoo mwenzake, huoni chaguzi za Kenya hutawaliwa na fujo na kutokukubali kushindwa(?). China inawakilishwa na dragon au joka. Joka katika Biblia ni ibilisi na shetani; ukweli ni kwamba China ni nchi isiyotambua uwepo wa Mungu, kumbuka enzi za Mao na siasa za Ukomunist, na ndiyo sababu iliyomfanyaShetani afukuzwe mbinguni. Wachambuzi wa habari wanasema kuwa China na Asia kwa ujumla ndiko wanakopatikana Freemason wengi kuliko maeneo mengine duniani, haishangazi kuona uchumi wa China unakua kwa kasi maana kila anayemkubali mnyama wa 666 atapata utajiri mkubwa. Tena inasemekana kuwa China ndiyo nchi inayayoongoza katika ulimwengu kwa kunyonga raia wake – na hiyo kwa kifupi ni tabia ya joka – ibilisi na Shetani. Hivyo nchi huwakilishwa na wanyama kutokana na tabia ya wanyama hao na nchi husika huwa na tabia hiyo. Sasa tutatumia kanuni asili kutoka kwa Wababeli jinsi ya kuipata namba 666 ili tulinganishe na maelezo hapo juu tuone kama tuko sawa au la. Biblia inasema “Hapa ndipo penye hekima. Yeye aliye na akili, na aihesabu hesabu ya mnyama huyo; maana ni hesabu ya kibinadamu. Na hesabu yake ni mia sita, sitini na sita.” Ufunuo 13:18.

Nini Na ni Nani Illuminati?

Dr. Adam Weishaupt (1748 – 1830) Baada ya kumuona mnyama anayetambulika kwa namba 666, sura hii inaanza kwa kuwaelezea THE ILLUMINATI, kundi ambalo ni hatari zaidi katika mchakato mzima wa kuharibu maadili na kuwafanya watu wamwabudu Lucifer – yaani Shetani aliye baba wa uongo katika ulimwengu huu – Yohana 8:44. Kuna wakati ambapo Mungu alimtoa mwokozi wa taifa la Israeli kwa kuwapa mtu mwenye nguvu nyingi kuliko watu wote duniani. Mungu alimwambia mnadhiri wake Samson kwamba asiseme na iwe siri kwake kuhusu asili ya nguvu zake. Ni kwa njia hiyo hiyo ya kuficha asili ya nguvu zao, Illuminati wamefanikiwa kuutawala ulimwengu. Wao wanasema kwamba:

“The great strength of our Order lies in its concealment; let it never appear in any place in its own name, but always concealed by another name, and another occupation. None is fitter than the lower degrees of Freemasonry; the public is accustomed to it, expects little from it, and therefore takes little notice of it. Next to this, the form of a learned or literary society is best suited to our purpose, and had Freemasonry not existed, this cover wouldn’t have been employed; and it may be much more than a cover, it may be a powerful engine in our hands… A Literary Society is the most proper form for the introduction of our Order into any state where we are yet strangers.” (John Robinson’s “Proofs of a Conspiracy” 1798, Boston, 1967, p. 112)

“Nguvu kubwa ya utaratibu wetu inapatikana kwa kuuficha utaratibu huo, hebu isionekane mahali popote kwa jina lake, lakini daima ifichwe kwa jina lingine, na kazi nyingine. Hakuna anayefaa kama Freemason wa digrii za chini; jamii inafanya kazi pamoja na hao, ina matarajio kidogo kutoka kwao, na kwa hiyo haina habari nao.

Wanaofuatia kwa hawa ni jamii ya watu waliosoma maana wanafaa kwa ajili ya malengo yetu, na kama Freemason isingekuwepo, njia hii ya kujificha isingetumika; na ingekuwa ni zaidi ya kujificha, ingekuwa ni injini yenye nguvu mikononi mwetu…jamii ya wasomi ni njia inayofaa zaidi kwa kuelezea taratibu zetu katika taifa lolote mahali ambapo sisi bado tu wageni.” (John Robinson’s “Proofs of a Conspiracy” 1798, Boston, 1967, p. 112)

Hivyo unaweza ukawa na jamii ya Illuminati na freemason wakiwa wanafanya kazi kwa majina mengine na sio majina ya Illuminati na Freemason na hapo ndipo nguvu yao ilipo. Watu wengi wameshindwa kuwatambua kwa sababu ya kujificha kwao. Kwa nini wanajificha? Kwa sababu wanajua kwamba wanachokifanya si halali na wala hakitokani na mapenzi ya Mungu. wanatumia jamii ya watu wasomi ili kufanikisha malengo yao.

Huwezi kuwazungumzia Illuminati bila kumfahamu Dr. Adam Weishaupt na huwezi kuwazungumzia freemasons bila kumfahamu na kumtaja Dr. Albert Pike.

Unapofanya utafiti wa Illuminati na freemason katika mtazamo mzima wa ‘New World Order’, unapaswa kujua kanuni tatu ( 3) muhimu ambazo ndizo msingi wa freemason/illuminati: 1)Thesis x Antithesis = Synthesis; 2) Hesabu na namba za freemason; na 3)Alama na ishara za freemason. Huwezi kuelezea freemason kwa ufasaha kama hutazingatia kanuni hizo tatu. ‘Thesis x Antithesis = Synthesis’ ndiyo kanuni inayotawala kwa freemason na kutekelezeka kwake kunategemea hesabu na namba pamoja na alama na ishara za freemason. Kwa nini wanatumia kanuni ya alama na ishara? wanasema “By symbols…is a man guided and commanded… ” wakimaanisha kuwa “watu huamrishwa na kuongozwa kwa kutumia alama”. Ndio maana hata waumini wengi wanaongozwa kwa kutumia alama ama ya nyota ya pentagram, jua, mwezi au msalaba. Kwa nini wanatumia kanuni ya namba? Kwa sababu “Occultists Worship Numbers and numbers have power”. Hivyo kama umepungukiwa na moja ya kanuni hizo ni wazi kwamba utafiti wako utapungua pia.

Dr. Adam Weishaupt alikuwa ni Profesor wa somo linaloitwa ‘cannon law’ katika Chuo Kikuu cha Ingolstadt huko Bavari. Alipata elimu yake kutoka katika shirika liitwalo ‘Jesuit Society’ na akawa Padre wa shirika hilo. Baadaye alitoka katika shirika hilo na akajiunga na chama cha siri kiitwacho Rosicrucian na akajifunza uchawi wa wayahudi uitwao Qabbala na ndipo alipoanzisha mpango wake uitwao ‘Order of the Illuminati’ mnamo tarehe 01/05/1776 huko Bavaria. (Rejea, John Robison, A.M., Proofs of a Conspiracy, p 63; Nesta H. Webster, The French Revolution, p 20). Weishaupt alianzisha kikundi cha Illuminati kwa misingi ya utaratibu wa Jesuit (Jesuit order). Illuminati ni chama cha siri na kina mpango wa kuangusha serikali na dini zote ulimwengu kisha kuanzisha serikali na dini moja wanayoiita ‘New World Order’.

Weishaupt alianzisha chama cha Illuminati akiwa na wenzake wakiwa watano, Weishaupt, Kollmer, Francis Dashwood, Alphonse Donatien DeSade na Meyer Amschel Rothschild. Illuminati iliundwa kwa kusomea digrii tatu za awali ambazo ni Novice, Minerval, na Illuminated Minerval; zikifuata utaratibu wa chama cha Jesuits na freemasons. Wanachama wote walitakiwa kubadili majina yao na kutuma majina ya dini yao ambapo Weishaupt aliitwa “Spartacus” msaidizi wake, Xavier von Zwack, aliitwa “Cato”; Nicolai, akaitwa “Lucian”; Professor Westenreider akaitwa “Pythagoras”; Canon Hertel akaitwa “Marius”; Marquis di Constanza akaitwa “Diomedes”; Massenhausen akaitwa “Ajar”; Baron von Schroeckenstein akaitwa “Mohomed”; na Baron von Mengenhofen “Sylla.” Makao makuu yalikuwa huko Munich, Ujerumani, yakijulikana kama ‘the Grand Lodge of the Illuminati’ (au Lodge of the Grand Orient), na kupewa jina la “Athens.” Vituo vingine vilikuwa huko Ingolstadt pakipewa jina la “Ephesus,”

Heidelberg jina la “Utica,” Bavaria kama “Achaia,” na Frankfurt pakajulikana kama “Thebes.”Ili kufanikisha lengo lao, waliweka mkakati ufuatao kama ilivyoandikwa na Nesta Webster kwenye kitabu kiitwacho “World Revolution” uk. 22, wakiwa na malengo sita:

1. Kukomesha utawala wa kifalme
2. Kukomesha umiliki wa mtu binafsi
3. Kukomesha urithi
4. Kukomesha utawala na utumishi wa serikali za nchi
5. Kukomesha ndoa na familia kwa kuweka ndoa za mikataba na kuanzisha elimu ya watoto kwa wote itakayosimamiwa na serikali moja.
6. Kukomesha dini na kuanzisha dini moja yenye mchanganyiko wa imani.

Ili kutekeleza mpango huu na kisha kutimiza malengo hayo, Weishaupt alitambua kwamba anahitaji nguvu zisizo za kawaida ili kufanikiwa kuharibu ustaraabu wa nchi za magharibi, ambapo nchi hizo zilikuwa na imani ya Kikristo. Hatua ya kwanza ilikuwa ni kutengeneza alama ya utambulisho wa Illuminati na akabuni Piramidi likiwa na jicho na kuweka maneno ya kilatini juu yake “Annuit Coeptus” yakimaanisha “kutangaza kuzaliwa kwa” na chini ya Piramidi akaweka maneno “Novus Ordo Seclorum”
yakimaanisha “Mpango mpya wa Ulimwengu” (Rejea “The New World Order”, A. Ralph Epperson, p. 108-112). Kisha akafanikiwa kuweka umbo hilo la Piramidi nyuma ya Dolla moja ya Kimarekani.

Weishaupt alitambua kwamba ingekuwa vigumu kufanikisha mipango yake ikiwa ulimwengu utaendelea kuwa na amani na hivyo akaamua kuanzisha utaratibu utakaopingana na imani ya wakati huo kwa kanuni ya “Ordo ab chao” yaani “Order Out of Chaos” ikimaanisha kuanzisha “machafuko yaliyopangiliwa”. Mataifa ya magharibi wakati huo yalitawaliwa na serikali katika mfumo wa Thesis. Weishaupt aliamua kuanzisha mfumo pinzani na Thesis ambao ni Antithesis. Mifumo hii miwili ilianza kupingana (kupigana vita) na hili lilipelekea kuzaliwa kwa ya mfumo mpya (hybrid) unaoitwa Synthesis ambalo ndilo lengo la Illuminati. Weishaupt akaweka kanuni ya ‘Order out of Chaos’. Hebu tuangalie maana ya maneno hayo:

•  Thesis – Ni mfumo uliotawala Ulaya miaka ya 1700. Mfumo huu ulikuwa hivi: Kiuchumi umiliki wa mali ulikuwa wa mtu au ubepari (economically Private Enterprise), Kisiasa ulikuwa wa kifalme au demokrasia (politically either Monarchy or Democracy), na kidini ulifuata Ukristo (religiously Judeo-Christian)

•  Anti-Thesis – Huu ni mfumo kinyume na Thesis na ndio unaopelekea kuzaliwa kwa mfumo unaoitwa Synthesis kutokana na kupinga mfumo wa Thesis. Kiuchumi ulitawaliwa na Ujamaa (Communism), Kisiasa ulitawaliwa na Udikteta na kidini ulitawaliwa na kutokuamini uwepo wa Mungu (Ukomunist). Mfumo wa Thesis ulikuwa na nguvu nchini Marekani na ndipo Illuminati waliona ni vema kuanzisha taifa lenye mfumo wa Antithesis litakalokuwa na nguvu kubwa na kupingana na taifa la Marekani. Ndipo taifa la Urusi likaanzishwa kwa kupewa nguvu baada ya vita kuu ya kwanza ya dunia na ya pili. Wakati Marekani ilifuata mfumo wa Kibepari kiuchumi, Ukristo kidini na demokrasia kisiasa, Urusi ilifuata mfumo wa Kijamaa kiuchumi, aethitic kidini na Udikteta kisiasa. Mwaka mmoja kabla ya kumalizika vita kuu ya pili ya dunia ulifanyika mkutano wa viongozi wakuu watatu mwaka 1944 huko Yalta. Viongozi hao waliunda pembe tatu (Piramidi) na walikuwa ni rais wa Marekani Franklin Roosevelt, waziri mkuu wa Uingereza Winston Churchill na Dikteta wa Kikomunist Josef Stalin wa Urusi. Viongozi hao walikutana ili kuweka utaratibu wa utekelezwaji wa mipango ya ulimwengu kuhusu serikali na dini zote. Kila mmoja anakumbuka vita baridi kati ya Marekani na Urusi ambapo hadi sasa vita hiyo imemalizika kwa hesabu hii: Thesis x Antithesis = Synthesis. Moja ya kanuni za ‘Order of the Illuminati’ inatokana na uchawi wa wa Simon Magus uliochanganywa na Ukristo. Lakini pia kanuni hiyo ilitoka katika kundi moja liitwalo ‘Wanikolai’ ambao walikuwa wafuasi wa mmoja wa mashemasi saba aitwaye Nikolai wa kanisa la awali la Kikristo (Ufunuo 2:14,15), [Rejea Grolier's Encyclopedia, vol 9, p 374 (1944). The New Age Movement and the Illuminati--666, p 94-95, published by The Institute of Religious Knowledge].

Illuminati wanapata wapi nuru yao? Wanapata nuru kutoka katika Filosofia ya Ugiriki. Na je filosofia ya Ugiriki inapata wapi nuru hiyo? “The individual who became spiritually or intellectually enlightened in the ancient Babylonian Mysteries was…called an Illuminated.” [Institute, 666, p 92]

Kwamba mtu aliyepata ujuzi wa kiroho huko Babeli aliitwa “an Illuminated” yaani aliyevuviwa nuru.

Neno Lucifer kwa Kilatin linamaanisha “Light –Bearer” yaani mwenye nuru; neno Titan kwa Kigiriki lina maanisha “mungu Jua” na katika kitabu kiitwacho young`s Concordance to the Bible” ukurasa wa 806, neno Lucifer limetafsiriwa kama “Illuminated One” au “Shining One” yaani aliyevuviwa nuru. Hivyo Illuminati wanapata nuru yao kutoka kwa shetani au mungu jua.

Weishaupt anakubaliana na hili ndio maana akaandika kwamba:

“This is the great object [uniting all the world into one] held out by this Association: and the means of attaining it is Illumination, enlightening the understanding by the sun of reason….The Flaming Star is the Torch of Reason. Those who possess this knowledge are indeed Illuminati.” [Robison, Proofs, p 64, 93.]

Hebu tusitishe kwa muda mfupi kuwatazama Illuminati ili tupate nafasi ya kuliangalia kundi la ‘Jesuit Society’ maana wao ndio waliomfundisha Adam Weishaupt ambaye ni muasisi wa Illuminati.

Shirika la Jesuits lilianzishwa na Ignatius Loyola aliyezaliwa mwaka 1491 na kufariki Julai 31, 1556. Sherehe ya Ignatius Loyola hufanyika kila ifikapo Julai 31 ya kila mwaka, siku aliyokufa. Mkuu wa shirika la Jesuit anaitwa “Black Pope” yaani “Papa Mweusi.” Hapa haimaanishi kuwa mkuu huyo anatakiwa awe wa rangi nyeusi yaani mwafrika bali neno ‘black’ linamaanisha ‘asiyeonekana,’ na kwa maana hiyo Jesuit

Society wanafanya kazi za siri, zisizoonekana, tena za giza ambazo ni kinyume na nuru ya neno la Mungu.
Shirika hili lilianzishwa ikiwa ni matokeo ya kanisa Katoliki kupiga vita uprotestant. Kujitoa kwa Loyola katika kulitumika kanisa kunaweza kuonekana kwenye kanuni 13 za shirika la Jesuits zinazolihusu kanisa; “Rules for thinking with the church” anaposema “I will believe that the white that I see is black if the hierarchical Church so defines it”.

Kwamba “nitaamini rangi nyeupe ninayoina kuwa ni nyeusi kama mfumo wa uongozi wa kanisa utatafsri hivyo.” Na ndivyo ilivyo katika shirika hili ya kwamba mtu anapaswa kuamini na kufanyia kazi kile anachofundishwa na kanisa hata kama dhamira yake inamwambia kuwa hicho si sahihi. Hebu soma nukuu hizi ili tuone chanzo cha chama cha Jesuits“Kuinuka kwa dhama za giza kulitokana na kuruhusu Biblia ipatikane kwa urahisi hata kwa watu wa kawaida na mafundisho ya waprotestant wanamatengenzo. Mafundisho haya yalikuwa na msingi wa kutafsiri unabii kutokana na historia; yaani kuwakilisha siku 1260 za Danieli na Ufunuo kuwa miaka 1260. Viongozi wa matengenezo kama Luther,

Calvin, Huss, Wycliff, Knox, Latimer, Cranmer, Ridley, Hooker, Newton na wengine waliamini hivyo na kufundisha.” Ibid p 7. “Kwa kutumia mbinu hii ya kutafsiri unabii, kanisa la Roma lilionekana wazi kuhusika na unabii huu wa pembe ndogo katika Daniel 7, na mnyama wa Ufunuo 13:1, mwanamke wa Ufunuo 17, ikiwa ni pamoja na kichwa cha kanisa kuwakilisha Mtu wa Kuasi wa 2 Wathesalonike 2. Kadri mafundisho haya yalivyozidi, kanisa la Roma lililazimika kujilinda dhidi ya kuongezeka kwa ushahidi wa unabii wa Biblia kulihusisha kanisa hilo.

Hivyo upapa ukaanza kuweka mipango ya kuwapinga waprotestant kwa kuanzisha ‘Jesuit society’ ili kisaidie kufundisha mafundisho ya kanisa na kuharibu mafundisho na vitabu vyote vilivyokuwa kinyume na kanisa na kuanzisha “Holy Office of the Inquisition” maalumu kwa ajili ya kuwatesa hata kuwaua wapinzani wa kanisa.” Ibid. pp 126, 127.

Kati ya mwaka 1524 na mwaka 1537 Loyola alisomea Theology huko Hispania na Ufaransa. Mwaka 1534 alifika Ufaransa wakati wa kipindi cha mapambano dhidi ya uprotestant, mapambano ambayo yalimfanya John Calvin akimbie kutoka Ufaransa.

Mwaka 1539, Loyola akiwa na wenzake walifanikiwa kuanzisha muungano na kuuita ‘Society of Jesus’. Mwaka uliofuata yaani 1540 chama hicho kikapewa baraka na Papa Yohana III na ilipofika mwaka 1548 Papa huyo akatoa kibali kwa Society of Jesus ili kiweze kushughulika na maswala ya kiroho. Loyola alikufa mnamo Julai 31, 1556 na akabarikiwa na Papa Paul V mwaka Julai 27, 1609, akapewa hadhi ya utakatifu Machi 12, 1622 na Papa Gregory XV na akatangazwa kuwa kiongozi wa maswala la kiroho mwaka 1922 na Papa Pius XI. Jina kamili la Loyola lilikuwa ni Íñigo akiwa ni mtoto wa mwisho kati ya watoto 13.

Baada ya kifo cha mama yake mwaka 1506 Íñigo alichukua jina la mwisho “de Loyola” kutokana na jina la mji ulioitwa Loyola ambako alizaliwa. Akaamua kutumia jina la “Ignatius of Loyola” yaani Ignatius anayetokea mji wa Loyola.

Mwaka 1534 aliwakusanya marafiki zake sita ambao alikutana nao chuo kikuu wakiwa ni wanafunzi wenzake ambao ni Francis Xavier, Alfonso Salmeron, Diego Laynez na Nicholas Bobadilla wote wakiwa ni Wahispania; Peter Faber akiwa ni Mfaransa; na Simao Rodrigues aliyekuwa Mreno. Asubuhi ya tarehe 15 Agust 1534, katika kanisa la Our Lady of the Martyrs huko Montmartre, Loyola akiwa na wenzake sita ambapo mmoja wa marafiki hao alikuwa ni padre, waliapa kutumika maisha yao yote. Ignatius akawa ndiye kiongozi mkuu (Superior General) wa chama cha Yesu – Society of Jesus.

Yeye ndiye aliyetunga katiba ya chama hicho mwaka 1540. Nukuu muhimu tunayoweza kuichukua kutoka kwa Ignatius wa Loyola ni hii: “That we may be altogether of the same mind and in conformity with the Church herself, if she shall have defined anything to be black which appears to our eyes to be white, we ought in like manner to pronounce it to be black. For we must undoubtingly believe, that the Spirit of our Lord Jesus Christ, and the Spirit of the Orthodox Church His Spouse, by which Spirit we are governed and directed to Salvation, is the same.” [Ignatius Loyola, Spiritual Exercises, Rule 13 Henry Bettenson, ed., Documents of the Christian Church, 2nd ed. (London: Oxford University Press, 1963), p. 260.]

“Kwamba wote tuwe na nia moja na kukubaliana na kanisa, kama limetafsiri kitu chochote kuwa ni cheusi wakati kinaonekana machoni mwetu kuwa ni cheupe, tunapaswa kukitangaza kuwa ni cheusi. Maana bila shaka tunapaswa kuamini, kwamba roho wa bwana wetu Yesu kristo, na roho wa kanisa la Orthodox ndugu yake, roho ambaye anatuongoza katika wokovu, ni yule yule.” [Ignatius Loyola, Spiritual Exercises, Rule 13 Henry Bettenson, ed., Documents of the Christian Church, 2nd ed. (London: Oxford University Press, 1963), p. 260.]

Kwa mujibu wa Ignatius Loyola, kanisa Katoliki na kanisa la Orthodox ni ndugu mmoja na wote wanaongozwa na roho mmoja. Lakini pia tunaweza kujiuliza kwa nini Loyola atumie rangi nyeusi hata kama ni nyeupe? Jibu ni kwamba alikuwa anaongelea kiongozi mkuu wa chama hicho cha Jesuits ambaye anaitwa ‘black Pope’ yaani Papa mweusi. Lakini pia Loyola aliweka kanuni 13 za kuongoza chama cha Jesuits. Katika sura zitakazofuatia tutaona jinsi Illuminati wanavyoabudu namba ikiwepo namba 13 na kuna uhusiano mkuwa sana kati ya Jesuits, Illuminati na Freemasons, wote wakiwa ni watumishi wa mnyama wa namba 666.

Ni utaratibu gani unafanyika wakati mtu anapotaka kuwa mwanachama wa “Jesuit Society?” Kama tutakavyoona, utaratibu wa kujiunga na chama cha Jesuits unafanana na utaratibu wa kujiunga na freemason. Cha ajabu ni kwamba baadhi ya madhehebu na makanisa yanafuata utaratibu huo wakati waumini, na hasa viongozi kama watawa, wachugaji, maaskofu nk wanapopewa nafasi hizo kwa mara ya kwanza japo Biblia inakataza wazi kutumia utaratibu kama huo.

Wakati mtu anapotaka kujiunga na chama cha Jesuits anatakiwa, pamoja na mambo mengine, kutoa viapo vya utii katika chama hicho, kiongozi wa chama hicho na kiongozi wa kanisa. Kabla ya kusoma viapo vya Jesuits, hebu tuiulize Biblia kuhusu viapo. “Tena mmesikia watu wa kale walivyoambiwa, Usiape uongo, ila mtimizie Bwana nyapo zako; lakini mimi nawaambia, Usiape kabisa; hata kwa mbingu, kwa maana ndicho kiti cha enzi cha Mungu; wala kwa nchi, kwa maana ndiyo pa kuweka miguu yake…wala usiape kwa kichwa chako, maana huwezi kufanya unywele mmoja kuwa mweupe au mweusi…..kwa kuwa yazidiyo hayo yatoka kwa yule mwovu.” Mathayo 5:33-37. “Lakini zaidi ya yote, ndugu zangu, msiape….msije mkaangukia hukumu.” Yakobo 5:12.

Biblia inakataza kuapa kwa aina yoyote ile, hivyo kama Jesuits wanaapa wanafanya hivyo kwa sababu wako kinyume na Biblia. Hata hivyo yapo madhehebu mengi yaliyo na utaratibu wa kuapisha viongozi wao ikiwa ni wachungaji, maaskofu, mapadri kila wanapowekwa wakfu kwa ajili ya kazi za kanisa husika. Chunguza ndani ya kanisa lako huenda likawa moja ya wahusika wa viapo.

Sasa tuangalie viapo vya Jesuits. Naomba niweke maelezo haya katika lugha ya Kingereza maana ndiyo iliyotumika kuandika viapo hivi, naamini kama hujui lugha hii unaweza kupata mtu wa karibu akakupa tafsiri fasaha. “When a Jesuit of the minor rank is to be elevated to command, he is conducted into the Chapel of the Convent of the Order, where there are only three others present, the principal or Superior standing in front of the altar. On either side stands a monk, one of whom holds a banner of yellow and white, which are the Papal colors, and the other a black banner with a dagger and red cross above a skull and crossbones, with the word INRI, and below them the words IUSTUM, NECAR, REGES, IMPIOUS. The meaning ofwhich is: It is just to exterminate or annihilate impious or heretical Kings, Governments, or Rulers. Upon the floor is a red cross at which the postulant or candidate kneels. The Superior hands him a small black crucifix, which he takes in his left hand and presses to his heart, and the Superior at the same time presents to him a dagger, which he grasps by the blade and holds the point against his heart, the Superior still holding it by the hilt, and thus addresses the postulant:” Kabla ya viapo, maneno yafuatayo yatasemwa na kiongozi wa ngazi ya juu kwa Jesuits anayeitwa “Superior”

Superior speaks: “My son, heretofore you have been taught to act the dissembler: among Roman Catholics to be a Roman Catholic, and to be a spy even among your own brethren; to believe no man, to trust no man. Among the Reformers, to be a reformer; among the Huguenots, to be a Huguenot; among the Calvinists, to be a Calvinist; among other Protestants, generally to be a Protestant, and obtaining their confidence, to seek even to preach from their pulpits, and to denounce with all the vehemence in your nature our Holy Religion and the Pope; and even to descend so low as to become a Jew among Jews, that you might be enabled to gather together all information for the benefit of your Order as a faithful soldier of the Pope.

Nimefupisha maelezo hayo na baada ya hapo ndipo viapo sasa vinaanza wakati muapaji akiwa amelala chini kifudifudi:

The Extreme Oath of the Jesuits:

—-”I, _ now, in the presence of Almighty God, the Blessed Virgin Mary, the blessed Michael the Archangel, the blessed St. John the Baptist, the holy Apostles St. Peter and St. Paul and all the saints and sacred hosts of heaven, and to you, my ghostly father, the Superior General of the Society of Jesus, founded by St. Ignatius Loyola in the Pontificate of Paul the Third, and continued to the present, do by the womb of the virgin, the matrix of God, and the rod of Jesus Christ, declare and swear, that his holiness the Pope is Christ’s Vice-regent and is the true and only head of the Catholic or Universal Church throughout the earth; and that by virtue of the keys of binding and loosing, given to his Holiness by my Savior, Jesus Christ, he hath power to depose heretical kings, princes, states, commonwealths and governments, all being illegal without his sacred confirmation and that they may safely be destroyed. Therefore, to the utmost of my power I shall and will defend this doctrine of his Holiness’ right and custom against all usurpers of the heretical or Protestant authority whatever, especially the Lutheran of Germany, Holland, Denmark, Sweden, Norway, and the now pretended authority and churches of England and Scotland, and branches of the same now established in Ireland and on the Continent of America and elsewhere; and all adherents in regard that they be usurped and heretical, opposing the sacred Mother Church of Rome. I do now renounce and disown any allegiance as due to any heretical
king, prince or state named Protestants or Liberals, or obedience to any of the laws, magistrates orofficers.
—–I do further promise and declare, that I will have no opinion or will of my own, or any mental reservation whatever, even as a corpse or cadaver (perinde ac cadaver), but will unhesitatingly obey each and every command that I may receive from my superiors in the Militia of the Pope and of Jesus Christ.
—–That I may go to any part of the world withersoever I may be sent, to the frozen regions of the North, the burning sands of the desert of Africa, or the jungles of India, to the centers of civilization of Europe, or to the wild haunts of the barbarous savages of America, without murmuring or repining, and will be submissive in all things whatsoever communicated to me.
—– I furthermore promise and declare that I will, when opportunity present, make and wage relentless war, secretly or openly, against all heretics, Protestants and Liberals, as I am directed to do, to extirpate and exterminate them from the face of the whole earth; and that I will spare neither age, sex or condition; and that I will hang, waste, boil, flay, strangle and bury alive these infamous heretics, rip up the stomachs and wombs of their women and crush their infants’ heads against the walls, in order to annihilate forever their execrable race. That when the same cannot be done openly, I will secretly use the poisoned cup, the strangulating cord, the steel of the poniard or the leaden bullet, regardless of the honor, rank, dignity, or authority of the person or persons, whatever may be their condition in life, either public or private, as I at any time may be directed so to do by any agent of the Pope or Superior of the Brotherhood of the Holy Faith, of the Society of Jesus.

Baada ya kumaliza viapo hivyo muapaji anatakiwa kuandika jina lake kwa kutumia kifaa chakuandikia kilichochovywa damu yake iliyotolewa kifuani upande ulipo moyo wake.

Kisha Superior anauliza maswali yenye majibu kama ifuatavyo:
Question —From whither do you come? Answer — The Holy faith.
Q. —Whom do you serve? A. —The Holy Father at Rome, the Pope, and the Roman Catholic Church Universal throughout the world.
Q. —Who commands you? A. —The Successor of St. Ignatius Loyola, the founder of the Society of Jesus or the Soldiers of Jesus Christ.
Q. —Who received you? A. —A venerable man in white hair.
Q. —How? A. —With a naked dagger, I kneeling upon the cross beneath the banners of the Pope and of our sacred order.
Q. —Did you take an oath? A. —I did, to destroy heretics and their governments and rulers, and to spare neither age, sex nor condition. To be as a corpse without any opinion or will of my own, but to implicitly obey my Superiors in all things without hesitation of murmuring.
Q. —Will you do that? A. —I will.
Q. —How do you travel? A. —In the bark of Peter the fisherman.
Q. —Whither do you travel? A. —To the four quarters of the globe.
Q. —For what purpose? A. —To obey the orders of my general and Superiors and execute the will of the Pope and faithfully fulfill the conditions of my oaths.
Q. —Go ye, then, into all the world and take possession of all lands in the name of the Pope. He who will not accept him as the Vicar of Jesus and his Vice-regent on earth, let him be accursed and exterminated.”

The Jesuit Oath of Induction is also recorded in the Congressional Record of the U.S.A. (House Bill 1523, Contested election case of Eugene C. Bonniwell, against Thos. S. Butler, Feb. 15, 1913, pp. 3215-3216) It can also be found in the book entitled, “Subterranean Rome” by Charles Didier translated from the French and published in New York in 1843. Dr.

Hivyo ndivyo viapo kwa kifupi vya wanachama wa Jesuits na unaweza pia kuvipata kwenye mtandao huu:
http://www.zenit.org Ukweli ni kwamba viapo hivyo vinamfanya muapaji awe tayari kuua ikiwa ni kwa siri au kwa uwazi mtu yeyote atakayekuwa kinyume na kanisa. Tunajua kwamba ulimwengu wote hatimaye utakuwa chini ya dini na serikali moja kama anavyosema Padre Malachi Martin wa kanisa Katoliki katika kitabu chake kiitwacho “The Keys of this blood”, anasema “He is as determined to be world ruler as was Constatine in his day.” p. 49. Akimaanisha kwamba Papa wa kanisa Katoliki atakuwa kiongozi wa dunia nzima kama alivyokuwa Constatine wakati wake. Hili pia linathibitishwa na Mungu kama tunavyosoma kwamba “….akapewa uwezo juu ya kila kabila na jamaa na lugha na taifa.” Ufunuo 13:7. Wale watakaokataa kutawaliwa na mnyama huyo watakabiliwa na kifo maana tayari sheria imetungwa katika mahaka ya kimataifa inayoitwa “The Rome statute of International Criminal Court.”

Hebu tumsikilize mkuu wa shirika la Jesuits anavyosema: “See, sir, from this Chamber, I govern, not only to Paris, but to China; not only to China, but to all the world, without anyone knowing how i do it.” (Tamburini, General of the Jesuits.) Yeye anasema kwamba “kutoka ndani ya ofisi hii, ninatawala, sio tu hata Paris, bali hadi China, sio tu hadi China bali katika ulimwengu wote, bila mtu yeyote kujua jinsi ninavyofanya.” “In these last days God hath spoken to us by his son Ignatius, (Jesuit founder) whom he hast appointed Heir of all thing, by whom also he made the world”. – Preached by F. Doza J.S., “The Firey Jesuits,” p, 66

“Katika siku hizi za mwisho Mungu amezunguza nasi kupitia kwa mwanae Ignatius, (mwanzilishi wa Jesuits) ambaye amemchakuwa kuwa mrithi wa vitu vyote, ambapo kwa yeye aliumba ulimwengu”. “The Grand Rule For an inferiro readily to declare his assent and consent to his Superiror in active obediance when he says, the snow is black, or the crow is white…we should always be ready to accept this principal: I will believe that the white that I see is black, if the hierarchical Church defines it as such.” -The Spirit Exercies of St. Ignatius, p. 141, -By Ignatius de Loyola.

Naye rais wa Marekani Abraham Lincoln akiwa anakifahamu chama cha Jesuits na kazi zao alisema kwamba:

“This War (Civil war) would never have been possible without the sinister influence of the Jesuits. We owe it to popery that we now see our land reddened with the blood of her noblest sons”…. “The mormon and the Jesuit priests are equally the uncompromising

ENEMIES of our Constitution and our laws; but the more dangerous of the two is the Jesuit- the romish priest, for he knows better how to conceal his hatred under the mask of friendship and public deeds for the glory of God…. So many plots have already been made against my life, that it is a real miracle that they have all failed, when we consider that the great majority of them were in the hands of the skillful Roman Catholic murderers, evidently trained by Jesuits. But Can we expect that God will make a perpetual miracle to save my life? I believe not. ..My escape from their hands, since the letter of the pope to Jeff Davis has sharpened a million of daggers to pierce my breast, would be more than a miracle. But just as the Lord heard no murmur from the lips of Moses when he told him that he had to die, before crossing the Jordan, for the sins of his people; so i hope and pray that he will hear no murmur from me when i fall for my nations sake. ..” (Abraham Lincoln)

“Vita hii isingewezekana kuwepo kama isingesababishwa na Jesuits. Tunamdai Papa sasa kwa kuona ardhi yetu ikienea damu za watu wake…” “Watu jamii ya mormon na makasisi wa shirika la Jesuit ni maadui wa katiba na sheria zetu; lakini kati ya hao wawili Jesuits ndio kundi hatari zaidi – kasisi wa rumi, maana anajua vizuri jinsi ya kuficha chuki yake katika mavazi ya urafiki na kufanya kazi za jamii kwa ajili ya utukufu wa Mungu….hivyo njama nyingi zimewekwa dhidi ya maisha yangu, ambapo ni muujiza kwamba wameshindwa, maana tunajua kwamba wengi wao walikuwa miongoni mwa wauaji wa Roman Catholic waliotumia akili nyingi, bila shaka wakiwa wamefundishwa na Majesuits. Lakini tutarajie kwamba Mungu ataendelea kufanya muujiza ili kuokoa maisha yangu? Siamini hivyo…kutoka kwangu mikononi mwao, tangu barua ya papa kwenda kwa Jeff Davis imenoa makali ya mamilioni ya watesaji ili kupasua kifua changu, itakuwa zaidi ya muujiza nikitoka mikononi mwao. Lakini kama vile Bwana ambapo hakusikiliza manung`uniko ya Musa wakati alipomuambia kwamba atakufa kabla ya kuvuka mto Yordani, kutokana na dhambi za watu wake; ndivyo nilivyo na matumaini na kuomba kwamba asisikie manung`uniko yangu nitakapoanguka kwa ajili ya taifa langu”.

(Abraham Lincoln) Yapata mwaka 1865, Abraham Lincoln aliuawa baada ya kuonekana kuwa anapiga vita vyama vya siri. Katika historia ya taifa la Marekani wapo marais wachache sana ambao walipinga uwepo wa vyama vya siri mmoja wao alikuwa Abrahm Lincoln. Hata hivyo wapinzani wa vyama hivi wamekuwa wakikutana na vikwazo na hata kuuawa. Baada ya kugusia chama cha Jesuits sasa tuendelee na kuwaona Illuminati ambao chimbuko lao ni Jesuit Society. Ielewe kwamba unapozungumzia Illuminati, unazungumzia ibada na utawala katika jamii, kama vile mnyama wa namba 666 anavyojishughulisha na ibada na utawala.

Mmoja wa waumini wa Illuminati mwenye digrii 33 ambaye aliwahi kuwa kiongozi mkuu wa Illuminati nchini Marekani Dr. Albert Pike, anasema, namnukuu: “Every Masonic Lodge is a temple of religion, and its teachings are instruction in religion”
(Albert Pike, Morals and Dogma, P. 213.) Kwamba “kila Loji (Jumba au kituo) ya Freemason ni hekalu la mambo ya dini, na mafundisho yake ni maagizo katika dini.” Unapoingia kwenye Loji za Freemason utakuta kuna Biblia ya toleo la King James ikiwa imewekwa juu ya madhabahu (Altare) ya Loji hiyo. Bw. Albert anaendelea kusema kwamba: “Freemasonry is a search for Light. That search leads us directly back, as yous ee, to the Kabalah.” [Albert Pike, Morals and Dogma, p. 741] Kwamba “Kazi ya Freemason ni kutafuta nuru. Na kutafuta huko kunatufanya, kama unavyoona, tujielekeze Kabalah.” Katika dini ya Uislamu kuna kitu kinachoitwa الكعبة yaani al-Kabah huko

Mecca Saud Arabia. Illuminati nao wana kitu kinachoitwa Kabalah. Nitaelezea zaidi katika sura zinazofuata.

Wakati Jesuits wanayaita majumba yao ya kufundishia kwa jina la ‘Convent’ na wanaojiunga kuitwa ‘Novice’ Illuminati na freemason wanayaita majumba yao ‘Lodge’ na wanaojiunga katika digrii tatu za awali hutumia majengo yanayoitwa ‘Blue Lodge’. Maana ya Illuminati ni “aliyepewa nuru” au kwa lugha ya kigeni “one who is illuminated” au “the enlightened ones,” ikimaanisha “mtu aliyepokea nuru au ujuzi mkubwa.” Umewahi kusikia watu wanaoitwa “Jesuits”? Kama umewahi kuwasikia, tambua kwamba hao ndio waliomfundisha Adam Weishaupt, ambaye ndiye mwanzilishi wa The Illuminati. Kwa maana nyingine, Illuminati ni mwanafunzi wa Jesuits.

Baada ya Adam Weishaupt kupata elimu yake kutoka kwa Jesuits, mwaka 1785 serikali ya Bavaria ikafunua mpango wa Weishaupt wa kuangamiza Ukristo na kutawala serikali zote duniani. Mpango huo ulipingwa vikali na serikali ya Bavaria na kulifukuza kundi la Illuminati nchini humo. Hata hivyo huu haukuwa mwisho wa Illuminati, kama] wanahistoria wengi walivyoandika. Mipango ya Weishaupt ilichukuliwa na kushughulikiwa kama mapinduzi yaliyo hatari katika nchi ya Ujerumani (Bavaria) peke yake. Lakini kuna mataifa mengi ambayo Illuminati walikuwa wanafanya kazi na hivyo serikali za mataifa hayo hazikujali tahadhari ya serikali ya Bavaria kuhusu Illuminati. Baada ya miaka michache mpango wa kuangamiza Ukristo na kisha kutawala serikali zote ulionekana kwa mara ya kwanza wakati wa mapinduzi ya Ufaransa. Nguvu kama hiyo ya mapinduzi ilionekana tena huko Ujerumani ikiitwa “The Legue of the Just” kukiwa na matawi yake huko London, Brusses, Paris na Switzerland. Wakati Napoleon alipoingia madarakani, hakuvumilia vitendo vya Jacobin Clubs vilivyokuwa chini ya Illuminati hivyo akavifutilia mbali. Hata hivyo Illuminati waliendelea kufanya kazi kwa jina lingine. Walifanya kazi kwa jina la “The Legue of the Just” ambapo “Karl Marx” alikuwa mfuasi. Alipewa kazi ya kurudia kwa kuandika kwa kina kile kilichoandikwa na Adam Weishaupt miaka sabini iliyopita.

Weishaupt alikufa mwaka 1830, lakini mipango yake ya mapinduzi iliendelezwa na wafuasi wake ambao hadi leo wako kwenye hatua za mwisho za kukamilisha mipango hiyo ya kuhakikisha kwamba dunia yote inarudia imani ya kipagani na kumuabudu shetani.

Mwaka 1842 Karl Marx alianza kuandika propaganda za mapinduzi kwa ajili ya “League of the Just”, akitumaini kusababisha machafuko. Mwaka 1844, akishirikiana na Friedrich Engels, wakiwa chini ya usimamizi wa “The League of the Just”, Marx alianza kuandika “Manifest der Kommunistichen Partei,” kinachojulikana kama “The Communist Manifesto,” yaani “Ilani ya Ukomunist” iliyotolewa mwanzoni mwa mwaka 1848. Baadaye, Illuminati wakiwa wanafanya kazi chini ya “The League of the Just,” walibadilisha jina lao na kuitwa “The League of Communists”.
Wakomunist husherehekea May Mosi ikiwa ni kuzaliwa kwa harakati za mapinduzi yao kwa sababu ilikuwa ni tarehe ya kuanzishwa kwa Illuminati iliyoanzishwa na Adam Weishaupt. Wasomi wengi wanajua kwamba Ukomunist ni dhana ambayo haikubali uwepo wa Mungu kama Biblia inavyoelezea. Vivyo hivyo Illuminati ni wapinzani wakubwa wa Biblia maana wanatumiwa na Shetani ambaye ni adui wa Mungu na watu wake. Na sio kwa kubahatisha kwamba Wakomunist wote hutumia umbo la pentagram (umbo la nyota yenye pembe tano) kama moja ya nembo yao. Pia sio kwa kubahatisha kwamba Wakomunist hutumia neno RED katika kuelezea harakati za mapinduzi yao.

Familia ya “The Rothschild international banking” ambayo kwa takribani miaka 200 imekuwa na mafanikio huko Ulaya katika nyanja za uchumi na siasa, ilianzishwa na Mayer Amschel Rothschild mnamo Feb. 23, 1744 huko Frankfurt Ujerumani. Alikuwa na watoto watano na jina la familia lilitokana na RED SHIELD. Ni Adam Weishaupt pamoja na familia ya “the House of Rothschild” ndio walioanzisha harakati hizi kwa sehemu zikiwa za kidini na kwa sehemu zikiwa ni za kisiasa kama zilivyotabiriwa katika unabii wa Yohana kuwa ni mnyama mwekundu sana atakayetoka katika shimo la kuzimu (yaani umizimu) Ufunuo 17:3,8. Inaaminiwa kwamba Illuminati ni sehemu ya Freemason. Hawa Freemason, ambao ni Illuminati, walichukua imani yao kutoka kwa “The Knights Templar”. “The Knights Templar” kilikuwa ni kikosi cha kidini ambapo wafuasi wake walipata kuwa matajiri wakubwa kutokana ka kupewa ardhi na zawadi kutoka kwa wafalme wa nchi za Ulaya. Kufikia miaka ya 1300 kikosi hiki cha Templars kilijiita kuwa ndio wamiliki wa Benki za Ulaya kutokana na utajiri mkubwa waliokuwa nao. Walikuwa na ndoto za kuwa matajiri wakubwa kiasi cha kuununua ulimwengu. Mfalme wa Ufaransa na Papa walianzisha msako wa kuwakamata The Knights Templar lakini Papa akawa na mashaka kutokana na jinsi mfalme alivyokuwa anaendesha msako ndipo Papa akaendelea kufanya msako bila kushirikiana na mfalme. Wakati wa msako huu kikosi hiki cha Templars kikaungama kosa lao kwa Papa na kujifanya kuwa Templars sasa wamekuwa Wakristo huku wafuasi wake wakificha imani yao ya kumuabudu Lucifa kama mungu wao.

Papa akawa amefanikiwa kukikomesha kikosi hiki lakini hakuwa amekikomesha kabisa kwani hatimaye kiligeuka na kuwa Freemason huku jamii ikiwa inawaona Freemason kuwa ni chama kizuri chenye malengo mazuri tu. ni kwa njia hii Adam Weishaupt aliyekuwa mwanachama wa Freemason alifanikiwa kuanzisha imani ya chama cha siri cha Illuminati ndani ya chama cha siri cha Freemason.
Freemason ni chama cha siri ambacho kipo hata leo kikiwa kinafanya kazi kwa kisingizio cha kuleta usawa na amani kwa watu wote. Kuna mtazamo mwingine kuhusu Illuminati, kwamba mwanzo wao unaanzia miaka 4000 iliyopita huko Mesopotamia, katika zama za kipindi cha Sumeria. Mfalme aliyekuwa mtawala kipindi hicho aliitwa mfalme Uru-Nammu. Habari za Uru zinapatikana pia ndani ya Biblia wakati wa utawala wa Babeli ikiwa ni Ur ya wakaldayo. Lakini zaidi Freemason wakiwa ni waabudu Shetani, tunaweza kupata chimbuko lao muda mrefu sana tangu wakati wa Habili na Kaini ambapo Kaini alimuasi Mungu. Mafundisho ya Illuminati yana mchanganyiko wa siri za Mason (Masonic secrets) yaani (Luciferian Doctrines), Islamic mysticism (Sufism), na Jesuit mental discipline (Hatha Yoga). Nitaelezea zaidi kuhusu Freemason katika sura za mbele.

Luciferian wao wanaunda makundi ya Freemason maana wao wanakubali moja kwa moja kwamba wanamwabudu Shetani. Islamic mysticism ni imani ambayo imo ndani ya dini ya kiislamu, kihindu, budha, nk lakini ikiwa inatokana na imani ya Illuminati, hivyo waislamu, wahindu na wabudha wengi wametekwa bila kujua na hivyo wanamwabudu Lucifer pasipo kujua. Jesuit mental displine, yaani Hatha Yoga, ni mbinu ya Illuminati inayotumiwa katika madhehebu ya Kikristo na kuwafanya waumini wao kumwabudu shetani pasipo kujua, na hivyo wote wanajikuta wakiwa kinyume na Mungu wa mbinguni. Kumbuka kwamba Shetani anatumia wakala anayeitwa Mnyama wa namba 666 maana mnyama huyo alipewa kiti cha enzi cha Shetani (Ufunuo 12:9; 13:2). Lakini sasa tunaona pia mnyama huyo naye akitumia mawakala wake ambao wanaitwa Illuminati. Tutaona pia kuwa Illuminati nao wanatumia mawakala wanaoitwa Freemason na vyama vingine vya siri pamoja na taasisi kubwa zisizo za siri. Kwa ujumla, Illuminati wanatumia mbinu ya “Divide and Rule” iliyotumiwa wakati wa ukoloni katika kulitawala bara la Africa. Kwa nje Illuminati wanajionyesha kuwa na nia ya kuifanya jamii iwe nzuri na safi lakini kwa ndani lengo lao kubwa ni kujikweza na hatimaye kuweza kuitawala jamii yote ya ulimwengu. Wafuasi wa Islamic mysticism (Sufism) wanaamini kwamba wao wako kwenye safari ya kiroho kwenda kwa Mungu na kwamba inawezekana kuwa karibu sana na Mungu wakati mtu akiwa hai – hapa kuwa karibu na Mungu wanamaanisha kumsogelea Mungu kimwili na sio kimaadili – Katika imani ya Sufism, mtu akiwa katika hali ya utambuzi – mawazo, hisia, mitazamo nk, wanaamini kwamba yote yanatoka kwa mungu au ni zawadi kutoka kwa mungu. Rejea Septemba 11 kule World Trade Center, waendesha ndege zilizogonga yale majengo marefu walikuwa na imani ya Sufism. Sufis wanaamini kwamba wao wanajitahidi kuwa mungu na mungu anajitahidi kuwa wao, yaani wanajitahidi kufanana na shetani na shetani anajitahidi kufanana na wao, na hivyo siku moja watakutana na kufikia utimilifu wa kufanana wote. Lakini pia Illuminati katika imani ya Jesuit mental displine (Hatha Yoga) wanajitahidi kuwafanya watu wa imani ya Kikristo kuamini kwamba kwa juhudi zao wenyewe wanaweza kufikia ukamilifu wa kufanana na Mungu. Hapa bwana J.D Buck, katika kitabu chake kiitwacho Mystic Masonry anasema: “It is far more important that men should strive to become Christs than that they should believe that Jesus was Christ…all men may reach the same Divine perfection.” – J.D. Buck, Mystic Masonry. “Ni muhimu kwamba watu wanapashwa kujitahidi kuwa Wakristo kuliko kuamini kwamba Yesu alikuwa ni Kristo….watu wote wanaweza kufikia ukamilifu ule ule wa kimbingu.” – J.D. Buck, Mystic Masonry. Ndio maana katika dini ya Waislamu utakutana na mafundisho mengi sana yanayomshambulia Yesu na kumshusha hadhi aliyonayo - hiyo inatokana na The Illuminati Doctrines katika imani ya Islamic mysticism (Sufism). Hata hivyo Biblia inatuambia vizuri kwamba hiyo ilikuwa roho na nia ya Lucifer aliposema kwamba: “…Nitapanda mpaka mbinguni, nitakiinua kiti changu juu kuliko nyota za Mungu; nami nitaketi juu ya mlima wa mkutano, Katika pande za mwisho za Kaskazini. Nitapaa kupita vimo vya mawingu, Nitafanana na yeye Aliye Juu.” Isaya 14:13. Lucifer aliapa kukiweka kiti chake juu na hatimaye kufanana na Aliye juu – yaani Mungu. Maana ya mlima wa mkutano ni kanisa la Mungu. Kama umo ndani ya kanisa linalojiita kuwa ni kanisa la Mungu – najua kwamba makanisa yote yanajiita kuwa ni makanisa ya Mungu – sasa muelewe kwamba Lucifer aliapa kuketi juu ya mlima wa mkutano. Kuhusu Pande za Kaskazini katika unabii Kaskazini ni upande wa mlima Sayuni – yaani upande wa kanisa la Mungu; Soma Zaburi 48:2 “Kuinuka kwake ni mzuri sana, Ni furaha ya dunia yote, Mlima Sayuni pande za Kaskazini, Mji wa Mfalme Mkuu.” Hivyo shetani amefanikiwa kuuteka ulimwengu wa kiroho kwa kutumia mnyama wa namba 666 na Illuminati katika Islamic mysticism, na Jesuit mental displine – yaani Hatha Yoga.Illuminati na taifa la Marekani:
Tutaanza kuangalia muhuri wa taifa la Marekani na alama zilizotumika kutengeneza muhuri huo unaoonekana kwenye noti ya dola moja ya Marekani. Unapotazama dola moja ya marekani utakuta kuna alama ya Piramidi upande mmoja na alama ya tai upande wa pili. Kama hujawahi kuona noti hiyo unaweza kuangalia kwenye picha hapa chini. “Our beautiful seal is an expression of Freemasonry, an expression of occult ideas.” (Wyckoff, H. S. The Great American Seal. The Mystic Light, the Rosicrucian Magazine,p.56).

Maelezo hayo yanajitosheleza kutuonyesha kwamba alama zilizotumika kubuni muhuri huo wa marekani zinatokana na Freemason. Noti ya Dola Moja ya Marekani. Piramidi likiwa na jicho. Tai akiwa amevalishwa bendera ya Marekani Hapa ndipo penye nguvu ya Illuminati. Katika dola moja ya Marekani ndipo tunakuta kile kinachoitwa “Great Seal of The United States of America”. Kuna vitu vingi vinavyoelezea jinsi Illuminati walivyohusika katika ubunifu wa muhuri huo wa taifa lenye nguvu kubwa duniani. Ubunifu huo wal iupata kutoka kwa mungu wanayemwabudu. Mungu huyo anaitwa GAOTU – Great Architect Of The Universe.
Yeye ndiye mwenye jicho katika Piramidi lililoko kwenye muhuri huo na kwenye dola moja ya Marekani. Wabunifu wa muhuri huu walikuwa ni watu sita ikiwa ni ishara ya kwamba walikuwa chini ya utawala wa Shetani maana namba sita kama tulivyoona hutumiwa na Shetani ikimaanisha utawala wa Shetani. Watu hao walikuwa kama ifuatavyo: 1) Benjamin Frankline, 2) John Adams, 3) Tomas Jeffeson, 4) Francis Hopkinson, 5) Charles Thomson ambaye alibuni pia bendera ya Marekani, na 6)William Burton. Kwa maelezo zaidi soma kitabu kiitwachwo “Illuminati 666” Uk. 232-234.

Hebu tuchunguze kwa makini kila tunachoweza kukiona kwenye muhuri huo. Tuanze na Piramidi……… Katika Piramidi iliyopo kwenye dola moja ya Marekani chini kabisa utakuta maneno haya: MDCCLXXVI na kisha kuanza kozi za tofali hadi kozi 33 ikimaanisha degree ya juu kabisa ya Illuminati. Kwa nini ziwepo degree 33? Swali hili litajibiwa kwa undani katika sura zinazofuata mbele. Wengi wamekuwa wakitafsiri maneno MDCCLXXVI kuwa ni mwaka 1776 ambapo Marekani ilipata uhuru wake, lakini ukweli ni kwamba yana maana ya May 1, 1776, tarehe ya kuanzishwa kwa Illuminati. Pia kwenye Piramidi lililoko kwenye dola moja ya kimarekani kuna maneno “Annuit Coeptis” juu ya piramidi yakimaanisha “Our enterprise (conspiracy) has been crowned with success” yaani “njama zetu zimepata mafanikio”. Na

chini kabisa ya piramidi kuna maneno “Novus Ordo Seclorum” yakielezea asili na lengo la njama hizo “new order of the ages” yaani “mpango mpya wa vizazi”. Sasa ukiyaweka pamoja maneno hayo yanamaanisha kwamba Illuminati “wanatangaza Kuzaliwa kwa mpango mpya wa kipagani”. Kwa mujibu wa kitengo cha hazina cha serikali ya Marekani tamko lililotolewa August 15, 1953, ambapo kulitolewa maana halisi ya alama zilizowekwa nyuma ya dola moja: “Jicho na umbo la pembe tatu lilimaanisha mungu aonaye yote. Piramidi ni alama ya kuwa na nguvu na uwezo na kwa vile piramidi hilo linaonekana kutokukamilika, ina maana kwamba kuna kazi bado ya kufanywa.” “Mungu aliyetajwa hapo ni mungu wa Misri na anaitwa Horus ambaye jicho lake kamwe halifumbwi wala halisinzii.”

Kwa upande mwingine tunamkuta Tai akiwa ameshikilia vitu miguuni mwake. Kwenye mguu wa kulia (Right Talon) Tai huyo amebeba tawi lenye majani kumi na tatu (13) yenye matunda ya mizeituni (Berries) kumi na tatu (13). Maana ya namba 13 inawakilisha familia kumi na tatu za Illuminati (Illuminati bloodline) na maana ya matunda ni jinsi taifa la Marekani linavyotoa misaada ya hali na mali duniani, maana ya majani ni jinsi Marekani inavyojishughulisha na kutafuta kile kinachoitwa amani duniani.

Inadaiwa kwamba Marekani ndiyo inayoongoza katika kutoa misaada kwa wakimbizi kwenye shirika la wakimbizi la umoja wa mataifa – UNHCR. Inashangaza kwamba hata nembo ya UN na UNHCR ina tawi lenye majani kumi na tatu kama lile aliloshikilia Tai anayewakilisha Marekani. Juu ya kichwa cha Tai kuna nyota kumi na tatu (13) ambazo zinatengeneza umbo lenye pembe sita (6) ‘hexagon’. Hapa namba 6 inawakilisha alama ya utawala wa Illuminati na mnyama wa namba 666 ikiwa ni idadi ya waliohusika kubuni muhuri huo wa Marekani. Katika mguu wa kushoto Tai huyo amebeba mishale kumi na tatu (13). Mishale kumi na tatu maana yake ni kwamba familia hizo kumi na tatu za Illuminati ambazo ndizo zinazotawala Marekani ziko tayari kufanya vita na taifa lolote lile linalotishia amani (majani 13) duniani. Taifa hilo litakuwa tayari kufanya vita kwa jinsi ya Tai arukaye na kushambulia popote duniani.

Kwa hatua hii, inatupasa kuchunguza njama zinazotumika katika matukio duniani. Ukweli ni kwamba watu wengi wanadhihaki juu ya matukio kama hayo. Hata hivyo napenda niwakumbushe wasomaji ukweli huu:

I) Biblia inaelezea wazi kwamba Shetani amekuwa mpinzani wa Mungu tangu mwanzo wa historia ya ulimwengu huu akijaribu kuutawala ulimwengu kutoka mikononi mwa Mungu. Wote wawili, Shetani na Mungu hutenda kazi kwa kutumia mawakala ambao ni binadamu ili watawale dunia hii. Tunaona hali kama hii katika kitabu cha Danieli 10 wakati Danieli alipokuwa akiomba kwa muda wa siku ishirini na moja katika ombi lililopata majibu. Wakati malaika wa Mungu alipomwendea Danieli, alimwambia Danieli kwamba Mungu alikuwa amesikia ombi lake na kujibu tangu siku ya kwanza alipoanza kuomba na alimtuma malaika huyo ili aende kumpa jibu. Hata hivyo, malaika huyo alicheleweshwa na mapepo wa shetani ambao walikuwa wanapigana na malaika wa Mungu. Vita hiyo ilikuwa kwa ajili ya nini? Ilikuwa ni kwa ajili ya kuona ni nani haswa anayewatawala wafalme wa dunia hii, maana wao ndio wanaofanya maamuzi kila siku ambayo yataadhiri historia ya mwanadamu. Biblia inafundisha juu ya njama za Shetani na wafuasi wake hapa duniani dhidi ya Mungu na watakatifu Wake.

2) Mwanahistoria aitwaye Edward Gibbons aliandika katika kitabu chake kiitwacho “The History of the Decline and Fall of the Roman Empire”, kwamba sababu kubwa iliyosababisha kuanguka kwa dola ya Rumi iliyotawala takribani miaka 1200 ilikuwa ni njama za siri ndani ya serikali yenyewe. Wakati huo huo waliofanya njama hizo walikuwa wakifanya kazi ya kujiangamiza wao wenyewe, walifanikiwa kuwadanganya wakazi katika Dola hiyo. Mtu yeyote asiyejifunza historia yuko tayari kuirudia, kwa hiyo tunapaswa kuamka na kuwa na tahadhari ya njama zinazotukabili za mpango mpya wa ulimwengu (NWO) kutoka kwa Illuminati.

Illuminati na Freemason walifanikiwa kubuni ramani ya jiji la Washington DC huko marekani katika maumbo ya Freemason. Hapa chini ni picha ya ramani ya jiji la Washington DC ikiwa na umbo la Pentagram linalotumiwa na waabudu wa Shetani ikiwa ni sharti ya kupata nguvu kutoka kwa Shetani..

JIJI la Washington DC Jiji la Washington DC. Ramani ya jiji la Washington ambayo ni makao makuu ya Marekani ikiwa imebuniwa katika mtindo wa umbo la Pentagram ambalo ni umbo la kishetani pamoja na umbo la Piramidi. Maeneo muhimu ya jiji la Washington, kama White House, US Capitol, sanamu za makumbusho ya marais wa Marekani yalibuniwa na Freemasons na kujengwa katika mitindo ya Freemason. Utakumbuka pia kwamba makao makuu ya wizara ya ulinzi yamejengwa katika muundo wa pembe tano (Pentagon) ikiwa ni kwa ajili ya matumizi ya namba tano katika Freemason. Je, nini maana ya umbo hilo? Jibu litapatikana kwenye sura inayofuata katika kipengele cha ishara za vidole viwili na vidole vitatu.

Malengo ya Illuminati ni yapi?

Katika kitabu chake kiitwacho “The broken Cross” Bw. Peirs Compton ambaye ni kasisi wa kanisa Katoliki na aliwahi kuwa mhariri wa gazeti la “The Universe” la kanisa Katoliki, anasema kwamba: “The Illuminati had …a plan …they decided on a most ambitious line of conduct. It would form and control public opinion. It would amalgamate religions by dissolving all the differences of belief and ritual that had kept them apart; and it would take over the Papacy and place an agent of its own in the Chair of Peter.” (“The Broken Cross”, by Peirs Compton, 1981. p. 7-8) Lengo kubwa la Illuminati ni kuhakikisha kwamba wanafutilia mbali imani za dini zote, kutawala mawazo ya watu, na kisha wanakalia kiti cha Petro huko St. Peters Vatican. Mipango hiyo iliandaliwa tangu mwaka 1776 wakati mwanzilishi wa Illuminati Adam Weishaupt alipopata ufadhili wa fedha kutoka taasisi za kifedha zinazotawaliwa nafamilia ya Kifreemason ya Rothschilds.

Baadae mtu mmoja ambaye alikuwa muumini wa Illuminati bw. Nubius, mwaka 1818 aliandika akiwa anaelezea malengo ya Illuminati kwamba ni kuhakikisha wanatawala katika dini zote ulimwenguni. Hata hivyo Biblia inatuambia kwamba hilo limekuwa ni lengo la Shetani tangu mwanzo maana alisema kwamba, “…Nitapanda mpaka mbinguni, nitakiinua kiti changu juu kuliko nyota za Mungu; nami nitaketi juu ya mlima wa mkutano, Katika pande za mwisho za Kaskazini. Nitapaa kupita vimo vya mawingu,

Nitafanana na yeye Aliye Juu.” Isaya 14:13. Compton anamnukuu Nubius akisema kwamba:
“The Papacy has been for seventeen hundred years interwoven with the history of Italy. Italy can neither breathe nor move without the leave of the Supreme Pontiff…It is necessary to seek a remedy. Very well, a remedy is at hand. The Pope…will never enter into a secret society. It therefore becomes the duty of the secret societies to make the first advance to the Church and the Pope, with the object of conquering both.” Peirs Compton, The Broken Cross p. 13.)

Illuminati walijua kwamba watakapofanikiwa kutawala katika kanisa la Roma itawawia rahisi kutawala katika dini zote wakiwa wanatokea Vatican. Lakini pia Illuminati walijua kwamba Papa hawezi kujiingiza kwenye vyama vya siri na hivyo wakawa na lengo la wao kuingia kwenye kanisa na kwa Papa wakikusudia kuwatawala wote, kanisa na Papa.

Ni kwa jinsi gani Weishaupt alifanikiwa kupata fedha kutoka kwa Benki iliyo chini ya Rothschilds (House of Rothchilds)? Compton anaelezea kwamba “He (Weishaupt) was backed financially,…by a group of bankers under the House of Rothschild. It was under their direction that the long-range and worldwide plans of the Illuminati were drawn up…” p. 8-9.

Hivyo ikaandaliwa mipango ya muda mrefu (long term and worldwide plans) kwa ajili ya kufanikisha malengo ya Illuminati katika kile kinachoitwa ‘New World Order’. Katika kutekeleza mipango yao, Illuminati walibuni matumizi ya namba, ishara na maumbo katika kutoa amri zao. Ishara hizo zinatokana na nguvu za Shetani. Bwana Compton anasema: “By symbols…is a man guided and commanded…The Illuminati made use of … a pyramid, or triangle, which has been long known to initiates as a sign of mystic or solar faith. At the top of that pyramid, or sometimes at its base, was, and in fact, still is, the image of a separate human Eye, which has been variously referred to as the open eye of

Lucifer…or the eternal watcher of the world and the human scene.” “The pyramid was one of the symbols that represented the unknown and nameless deity in pre-Christian cults. Centuries later, it was resurrected as a symbol of the destruction of the Catholic Church; and when the first phase of that destruction had been brought about…by those who had infiltrated and since occupied some of the highest places in the Church, they reproduced it as a sign of their success.”

Kisha Compton anatustua kwa kutufunulia siri hii: “It (this All-Seeing Eye) overlooked the crowds who gathered for the Philadelphia Eucharistic Congress in 1976. It was taken up by the Jesuits who edited the Society’s year book; and it appeared on a series of Vatican stamps issued in 1978.” (p. 10-11). Compton more specifically identifies the true meaning of this All-Seeing Eye: “The Eye, which can be traced back to the Babylonian moon worshippers, or astrologers, came to represent the [Pagan] Egyptian Trinity of Osiris, the sun; Isis, the moon goddess; and their child, Horus…” (p. 11-12).

Compton anaelezea kwamba Illuminati hutumia ishara na alama katika kuamrisha watu, na ndio maana walianzisha matumizi ya Piramidi au pembe tatu ambapo juu ya Piramidi hilo kuna jicho lenye maana ya utatu wa miungu wa Misri wanaoitwa Osiris (mungu jua baba), Isis (mungu mwezi mama) na Hurus (mungu mwana). Kumbuka kwamba Shetani huigiza kutoka kwa Mungu na kisha kupotosha maana halisi iliyokusudiwa na Mungu. Shetani hana uwezo wa kuumba wala kutengeneza kitu kipya tofauti na alichoumba Mungu. Katika kuhakikisha kwamba Illuminati wanatawala dini zote, walifanikiwa kuingiza matumizi ya maumbo na namba ndani ya dini mbalimbali ikiwa ni pamoja na matumizi ya alama ya jua, alama ya nusu mwezi, alama za ndimi za moto nk. Nitaelezea kwa undani zaidi dini ambazo zimeathiriwa na Illuminati katika matumizi ya maumbo.

Compton anasema kwamba “By mid-1800
s, the State of Italy had been taken over by the Illuminati” (Compton, The Broken Cross, p. 17). But, still, the religious office of the Papacy was outside their control. Kwamba “kufikia miaka ya katikati ya 1800, taifa la Italia lilikuwa tayari limetekwa na Illuminati” (Compton, The Broken Cross, p. 17). Hata hivyo ofisi ya Papa ilikuwa nje ya utawala wao.

Compton anasema kwamba “by 1960s the liberals or progressives, secure in having brought the designs of the secret societies to a successful conclusion, were exultant…The entire world of religion was now permeated by its influence…” (Compton, The Broken Cross, p. 62) Kwamba kufikia miaka ya 1960 tayari Illuminati walikuwa wamejiingiza katika dini zote ulimwenguni. Hili linathibitishwa na ziara ya Papa Paul VI kwenye umoja wa mataifa (UN) Oktoba 4, 1965 alipohutubia mbele ya viongozi wa dini kubwa sita ulimwenguni ambazo ni Buddhism, Hinduism, Islam, Judaism, Confucianism, na Wakristo. Comptonanasema kwamba hotuba hiyo ilifanyika ndani ya chumba maalumu kwa ajili ya ibada za Illuminati kwenye jengo la Umoja wa mataifa, namnukuu: “This [meditation] room wasa centre of the Illuminati, given over to the Cult of the All-Seeing Eye that under a system of allegories and veiled secrets…was dedicated to the service of pagan cults, and the obliteration of Christian in favour of humanistic beliefs.” (Compton, The Broken Cross, p.68-69).

Je, Compton anakubalika kwa kipimo cha unabii wa Biblia? Ndio, katika kitabu cha Ufunuo 17 tunasoma kuhusu mnyama ambaye yu tayari kupanda kutoka kuzimu akiwa amembeba mwanamke. Jambo muhimu ni kwamba wakati Yohana anaonyeshwa njozi hii alipelekwa jangwani ndipo akamuona mnyama huyu. Jangwani ni mahali pa shida ikimaanisha kipindi kigumu. Historia inatuambia kwamba kanisa la Roma limekuwa jangwani tangu mwaka 1798 wakati Papa Pius VI alipokamatwa na jenerali Bethier wa Ufaransa na kisha kufia huko na kuonekana kana kwamba mwisho wa kanisa hilo ulikuwa umefika. Sasa mwaka 1929 ndipo kanisa likarudishiwa tena utawala wake wa kikanisa na hivyo kuanza kuwa na vichwa, yaani viongozi na hadi sasa wamefika mapapa saba tangu mwaka 1929. Tumekwisha kuonyesha kwamba mnyam huyo ni utawala wa Illuminati na kwa kuwa Yohana alimuona mnyama huyo akiwa amembeba mwanamke (kanisa)—ikimaanisha muungano wa Illuminati na kanisa, Yohana anatudhihirishia kwamba tangu mwaka 1929 tayari Illuminati walikuwa wameungana na kanisa. Hivyo
 Compton kwa kusema kwamba kufikia miaka ya 1960 tayari Illuminati walikuwa wameuteka ulimwengu wa dini, ni wazi kwamba Compton yuko sahihi kwa kipimo cha Biblia.

Huo ukawa mwanzo wa ujenzi wa hekalu linaloitwa “Temple of Understanding” lililojengwa kwenye hekari 50 huko Potomac Washington. Malengo ya ujenzi wa hekalu hilo yalionekana kuwa ni ibada za Illuminati kutokana na idadi ya madhehebu yaliyohudhuria kwenye mkutano huo. Idadi ya madhehebu hayo ilikuwa ni sita ambayo ni Buddhism, Hinduism, Islam, Judaism, Confucianism na Wakristo. Kumbuka kwamba namba sita hutumiwa na Illuminati kuwakilisha utawala wao. Nitaelezea kwa kina kuhusu matumizi ya namba na maana zake.

Uzinduzi huo uliofanywa na Papa Paulo VI ukawa ni tangazo rasmi la kuanzishwa kwa dini moja kutokana na mipango ya Illuminati iliyoanzishwa mwaka 1776 kwa jina la New World Order. Hivyo basi kile tunachokiona leo katika ulimwengu wa dini, siasa, uchumi, utamaduni nk ni matokeo ya mipango ya Illuminati ya kutaka kutawala ulimwengu wote.

Siku chache baada ya Papa Paul VI kurudi Vatican kutoka Marekani kwenye Umoja wa Mataifa, askofu Mendes Arceo wa Cuernavaca alisema kwamba itikadi za Carl Max ni za muhimu kwa ajili ya ufalme wa Mungu, wakati huo Papa Paul VI akasema kwamba Roma ilikuwa tayari kuweka msimamo mpya kuhusu vyama vya siri. Compton anasema:

“Within a few days of Paul’s return to Rome, the Bishop of Cuernavaca, Mendes Arceo, was declaring that ‘Marxism is necessary in order to realize God’s kingdom at the present time’; while Pope Paul let it be known that Rome…was ready to take a new look at secret societies.” (Peirs Compton, The Broken Cross, p.72)

Katika harakati za mipango ya Illuminati ya kutawala dunia, chama hicho cha siri kilianzisha taasisi nyingi ambazo hadi leo zinafanya kazi duniani kote. Lifuatalo ni jedwali la utawala wa Illuminati likiwa na nguzo sita. Namba sita hutumiwa na Illuminati kuashiria utawala wao.

Ili kufanikiwa katika malengo yao ya kuitawala dunia kupitia Dini, uchumi, siasa na Ajira/kazi, Illuminati walifanikiwa kuanzisha taasisi za Kidini, kiuchumi, kisiasa na kazi na ajira, zote hizo zikiwa zinafanya kazi kwa mwongozo wa Illuminati. Katika taasisi za kidini tunakuta Baraza la Umoja wa makanisa ulimwenguni (World Council of Churches) ambalo lilianzishwa na Illuminati kwa makusudi ya kuunganisha dini zote za Kikristo na kutengeneza “Mnara wa Babeli” wa kiroho. Tayari kuna makanisa mengi ambayo yamejiunga kwenye umoja huo. Wengi hawajui kama umoja huo uko chini ya chama cha siri cha Illuminati ambacho kina siri kubwa sana katika kutawala dini na dunia kwa ujumla. Ukitaka kujua kama kanisa lako ni mwanachama wa Baraza hilo unaweza kutembelea mtandao wa Baraza hilo kwenye http//www.wcc-coe.org/. Ieleweke kwamba WCC ina vitengo kama Christian World Communion, Global

Christian Forum, nk. ambapo kanisa linaweza lisiwe member wa WCC moja kwa moja ila likawa member wa vitengo vilivyo chini ya WCC. Siri ambazo Illuminati/Freemason hawataki zifahamike kwa watu Kuna siri muhimu ambazo Freemason na Illuminati hawataki zifahamike kwa watu. Siri hizo ni:
- Viongozi wa dini wamefanikiwa kuwatawala mamilioni ya wanaume na wanawake, ambao wamekuwa wakifundishwa tangu utoto wao, kwamba viongozi hao ni wajumbe kutoka kwa Mungu.
- Leo viongozi hao wamezungukwa na mamia ya alama na mavazi ya Freemason kama vile pete, kofia nk kiasi kwamba watu wengi hawajui hilo.
- Illuminati wanaamini kwamba kuna zaidi ya Mwokozi mmoja aliyesulubiwa. Kwamba wapo zaidi ya ishirini.
- Illuminati wanaamini kwamba Yesu alifundishwa na waalimu kutoka Misri.
- Kisha Yesu akawa “jua” na wale wanafunzi wake kumi na wawili wakawa ndio ishara kumi na mbili zinazotumiwa na Freemason zinazozojulikana kama Zodiac
- Mbingu zinasemekana kuwa ziko “juu” hata hivyo kutokana na mzunguko wa dunia (rotation of the Earth) juu na chini hubadilishana mahali pake.
- Wanaoingia kwenye vyama hivi vya siri huanza kupanda ngazi (uti wa mgongo) hadi juu kwenye kilele cha mlima (ubongo), wakiwa wanapitia kwenye shimo lililoko sakafuni. Mahali hapo ndipo palipo na hekima (wisdom).
- Utatu (trinity au triune) katika mwanadamu ni moyo, ubongo, na viungo vya siri
– kila kimoja kimepewa kiwakilishi cha alama katika degree tatu za kwanza za Freemason. Moyo na ubongo huitwa Kaini na Habili. Vyote viwili vinawajibika kuleta usawa kamili (total equilibrium).
- Mti uitwao Pine wenye majani yenye ncha kama sindano ni sawa na mkia wa nyoka wenye kitu kama kidole kinachoitwa mkuki mtakatifu. Hiki ndicho kinachounganisha mambo ya zamani na yaliyopo (old and present)
- Uti wa mgongo ni sawa na nguzo yenye ngazi 33 ambazo wakati mwingine huitwa nyoka au wachawi. Hii ndio fimbo ya Her-me ikiwa imezungukwa na nyoka wawili, mmoja mweusi mwingine mweupe. Na ndio maana ya degree 33 za Freemason.
- Kiungo kati ya ubongo na viungo vya siri mwilini kinatokana na uti wa mgongo ambao ndicho kiungo chao – yaani ubongo na viungo vya siri huunganishwa na uti wa mgongo wenye ngazi 33.
- Freemason wanafundisha kwamba mtawala wao ambaye wanamwita mungu anajulikana kwa watu wote kama “Mimi niko”

- Freemason wa kiwango cha juu kabisa wanaamini kwamba watu wengi ni wazito kama mawe, wakiwa wanafaa kutumiwa kwenye ujenzi kama matofali, uzito wao unatokana na ugumu wao wa kuamini kwamba maana halisi ya maisha ni kuwa na nguvu za kutoa uhai ulimwengunin (giving life in the world).
- Ini (Liver) ndio ufunguo wa damu mwilini. Jina Lucifa ni jina lenye moto, lisilofanya kazi, sawa na damu isiyo na kazi. Mtu akiwa na ini ni sawa na kusema kwamba anaishi (To have a liver is to live). Neno “Live” ukiligeuza nyuma linakuwa “Evil” yaani uovu na neno “Lived” ukiligeuza linakuwa “Devil” yaani Mwovu. Red (Roth) yaani rangi nyekundu ni rangi ya vita. Yellow (Gold) yaani rangi ya njano au ya dhahabu ni ishara ya kupata nguvu, wakati Blue ni rangi waliyopewa watawala. Green (Yellow+Blue) yaani rangi ya kijani ambayo ni mchanganyiko wa rangi ya Blue na njano ni rangi waliyopewa wanaojiunga kwenye chama cha Freemason (Greenland). Rangi nyeupe (White) humaanisha silaha, wakati rangi nyeusi ni ishara ya uchawi wa watu weusi (Black Magic)
- Bahari (Meru-Mara-Mary) alikuwa ni bikira mama. Uhai wa kwanza (ndani ya bahari) ulitoka kwenye mdomo wa 1) samaki na kisha kutokea kwenye ardhi kupitia 2)chura. baadae uhai ukapatikana kutoka kwa 3)nguruwe pori dume, kasha 4)simba na hatimaye 5)nyani. Kisha uhai ukabadilika na kuonekana kuwa 6)mtu(hatua ya sita). Tumbo lililoleta mabadiliko haya ya uzazi ni Bustani ya Edeni na huwakilishwa na herufi “O”. Kisha mtu akavumbua moto (Lumerian # 7) huko Ethiopia wakiwa ni watu wafugaji. Walivumbua pia bahari ya Atlantic (The Atlanteans # 8) wakati wakifuatilia jua lilipokuwa linazama upande wa magharibi. Mwisho, watu walioitwa (Aryans # 9) walionekana kwa mara ya kwanza huko Georgia kwenye milima ya Caucuses. Hivyo Freemason wakaamini kwamba uumbaji haukukamilika na wao wakawa “miungu.”

- Watu hawa waitwao Aryans wanapatikana kwenye kitabu cha Mwanzo sura ya 2 katika Biblia. Wakiwa wanatumia genes zenye umbo la pembe tatu walianza kazi ya “New World Order”, wakiwafanya watu wazaliane kama nyuki kwenye mzinga, wakati nyuki wa kiume hugeuka na kisha kuanza kuzaa bila msaada wa nyuki wa kike. (Adamu alitolewa ubavu na mahali pake pakawekwa yai lililotolewa kwenye test – tube. Baada ya miezi tisa, akazaliwa mtoto mwanamume aitwaye Tubal Cain, na hatimaye akapelekwa huko Babeli. Hivyo Freemason wakaanzisha mapango wao na kuuona wenye mafanikio kama ya nyuki.
- Freemason wanasema kwamba mtu mpya hazaliwi mara moja. Wanasema kwamba mtu huzaliwa kwa degree. Wakati wa miezi tisa mtu huzaliwa akiwa njiti (pre-mature). Mtu huyo anahitaji kutengenezwa zaidi. Freemason wanasema kwamba utambuzi wa kiroho “Spritual consciousness” ni “mimi niko” wa kweli, ambaye hupatikana baada ya mwaka wa ishirini na moja wakati mawazo huanza kutoka katika viungo wa siri (kukomaa kwa balehe). Hata hivyo kwa Freemason maisha huanza mtu anapofikisha umri wa miaka arobaini, baada ya miaka ishirini ya kujitoa kwake, na kuwa mtumishi mwaminifu.

- Wanawake, hamuoni kwamba mnapaswa kuamka na kuwatuma freemason wa kike kwenye vikao. Mkiendelea kukubali kunyanyaswa kiakili, kimwili na kiroho nguvu zetu zitakwisha. Msikubali kuendelea kunyanyaswa. Jiteteeni katika maisha yenu na taratibu ulimwengu wote utafadhaika.
- Kwamba kanisa au dhehebu lazima liwe chini ya uongozi wa watu katika mfumo wa umbo la pembe tatu (Piramidi) na kwamba mtu hawezi kuokolewa asipokuwa ndani ya kanisa au dhehebu hilo.
- Baada ya miaka elfu kumi ya Freemason, je huu sio wakati wa wanaume na wanawake kujichukulia madaraka ya kisiasa, kidini na kiuchumi na kuunda paradiso ambayo ilikuwa imepotea hapa duniani? Hizo ndizo baadhi ya siri muhimu ambazo Freemason hawataki zijulikane kwa watu. Ukichunguza kwa makini siri hizo utagundua mambo mengi ikiwa ni pamoja na maana ya degree 33. Lakini pia utagundua kwamba katika somo la Historia kuna topic inayosema “Evolution of man” Yaani uibukaji wa mwanadamu. Kwamba mtu hakuumbwa kama Biblia inavyosema ila alitokana na mabadiliko ya viumbe kutoka hatua ya kwanza hadi ya 9. Sasa ieleweke kwamba chanzo cha topic hiyo ni Freemason. Jambo lingine ni kwamba siku za hivi karibuni wanasayansi wamekuwa wakifanya utafiti wa kuzalisha watoto kupitia chupa (Test Tube). Hiyo pia ni imani ya Freemason ambao wanaamini kwamba Adamu alipotolewa ubavu, kama Biblia inavyosema, wanadai aliwekewa yai kupitia kwenye chupa (test tube) na kisha akazaliwa Tubal Cain bila msaada wa mwanamke. Wao wanasema bahari ndio mwanamke na tutaona katika sura za mbeleni kwenye kitabu hiki jinsi freemason wanavyopata nguvu kutoka kwa jinni liitwalo LILITH ili kuwaweka wanawake mahali ambapo hawakuwekwa na Mungu. Ndio maana tunaona harakati za kuwanyanyua wanawake ili washike majukumu ya wanaume, hata hivyo Freemason wanajua kwamba hilo litakapofanikiwa, ulimwengu wote utafadhaika! Lakini pia Freemason wanasema kwamba watu wana mioyo mizito kwa sababu hawawaamini na hivyo wamekuwa wazito kama mawe ambayo yanafaa kutumiwa katika ujenzi. Hivyo wanawatumia watu kujenga babeli yao bila watu kujua. Kwa mfano watu wengi wamekuwa wakiiga mitindo ya kidunia iliyoanzishwa na Freemason, madhehebu mengi yamekuwa yakifuata mafundisho yaliyo maagizo ya wanadamu (Mathayo 15:9), madhehebu mengi yamefuata mfumo wa Piramidi, na kwa kweli wengi wamekuwa ni mawe mazito yanayotumiwa na Freemason kujengea. 3

Freemason na Kazi zao. Sasa tunaingia katika hatua muhimu kabisa ya kujua kazi za vyama hivi vya siri maana tayari vimo ndani ya jamii bila jamii yenyewe kujua. Tumeona mnyama wa namba 666 na Illuminati, ambao malengo yao ni mamoja, ya kuitawala dunia, kisiasa, kiuchumi, kidini nk. Nimegusia pia kundi la Freemason katika sura iliyopita. Ukweli ni kwamba huwezi kutenganisha Illuminati na Freemason kama tulivyoona kwenye sura ya pili. Lakini pia huwezi kuwazungumzia freemason bila kumfahamu na kumtaja Dr. Albert Pike.

Dr. Albert Pike alizaliwa Disemba 29, 1809 akiwa ndiye mtoto mkubwa kwenye familia ya watoto sita ya Benjamin na Sarah Andrews Pike. Pike alizaliwa na kukulia kwenye familia ya Kikristo kwenye dhehebu la Episcopal. Akiwa na umri wa miaka 15 alifanya mtihani wa Harvard College na akafaulu lakini hakuweza kusoma chuoni hapo kwa sababu ya kukosa fedha. Baada ya kusafiri hadi kufika mahali panapoitwa Santa, aliendelea na safari yake hadi Arkansas ambapo aliajiriwa kuwa mhariri wa gazeti kabla ya kufanya kazi bar. Akiwa Arkansas, alikutana na Mary Ann Hamilton na akamuoa Novemba 28, 1834. Aliweza kuzaa watoto 11 pamoja na mkewe. Alipofikisha umri wa miaka 41 aliomba kujiunga na freemason kwenye Loji inayoitwa Western Star Lodge No. 2 huko Little Rock, Ark ikiwa ni mwaka 1850. Alipata Digrii zake 10 za York Rite kuanzia mwaka 1850 hadi 1853. Alipata digrii ya 29 ya Scottish Rite mwezi Machi 1853 akiwa Loji ya Albert Gallatin Mackey huko Charleston.

Kwa mujibu wa maandishi ya mwanzo kabisa kuhusu Freemasons, maandishi hayo yanasema kwamba chanzo cha freemasons ni Adam anayesemekana kuwa ndiye Mason wa kwanza kabisa. Kitambaa kinachoitwa ‘apron’ wanachokivaa Masons wakati wa ibada zao wanadai kuwa ni sawa na ngozi aliyoivaa Adamu na Hawa katika bustani ya Eden. Ujuzi wa kujua mema na mabaya alioupata Adamu baada ya kula tunda walilokatazwa ulichukuliwa hadi kwa mtoto wa Adam aitwaye Seth, na kisha kwa Nimrod ambaye ndiye mwanzilishi wa ujenzi wa mnara wa Babeli, yeye akiwa ni kitukuu wa Nuhu. Dr. Albert Mackey (mwenye digrii 33 na mwandishi wa Freemasonry Encyclopedia) anarejea kwenye maandishi ya mwaka 1560 yakielezea kwamba chanzo cha freemasons ni kwenye mnara wa Babeli na kwamba Nimrodi aliwafundisha wajenzi wa mnara huo imani ya freemasons. Baada ya Mungu kuchafua lugha yao, siri zote za freemasons inasemekana kuwa zilipotea.

Wakati mfalme Sulemani (Solomon) alipokuwa anajenga hekalu, freemasons wanaamini kwamba imani yao ilianzishwa tena. Mackey anasema kwamba Sulemani (Solomon) ndiye aliyekuwa Grand Master wao mkuu na Loji (Lodges) zote zilianzishwa na Sulemani. Hata hivyo Martin L. Wagner ambaye ni muumini wa freemason anafundisha kwamba jina ‘Solomon’ sio jina la kabila ya Israeli kwa sababu maana ya jina hilo yaani Sol-om-on humaanisha jua katika lugha ya kilatini ‘Sol’, katika lugha ya kihindi ‘om’ na katika lugha ya Misri ‘on’ hivyo kumaanisha kwamba Solomon ndiye mungu jua na mkuu wa Freemasons baada ya Nimrod Wakati wa utawala wa Uyunani (Greece) kulikuwa na vikundi vilivyoitwa ‘guilds’ sawa na vyama au ‘unions’ kwa wakati wetu huu. Vikundi kama hivyo viliitwa “Dionysiacs,” huko Roma na ndivyo vilivyohusika na ujenzi wa viwanja vya michezo (stadiums).

Baadae vikundi hivi ndivyo vilivyohusika na ujenzi wa makanisa (cathedrals) na majengo makubwa na baadaye vikapewa majina kama Carpenta, builders, draftsmen, craftsmen katika fani ya ujenzi. Watu hao kulingana na fani zao walikaa kwenye vikundi pamoja na mahali hapo pakaitwa Loji au Lodge. Ndio chanzo cha majengo ya kuabudu ya freemasons kuitwa ‘Lodges’. Wale wote waliokuwa na fani ya ujenzi wa majengo waliitwa ‘Masons’ lakini iwapo mtu asiye na ujuzi wa ujenzi wa majengo huku akitaka kujiunga na chama hicho aliitwa ‘Accepted Mason’. Baadae Dr. Albert Pike aliandika kitabu kinachoitwa ‘Morals and Dogma of the Ancient and Accepted Scottish Rite of Masonry’ alichokiandika mwaka 1871. Kitabu hicho ndicho chenye mafundisho na mwongozo wa imani ya freemasons.

Ndani ya kitabu hicho kuna jumla ya digrii 33 za freemason na walitumia mahesabu katika kutoa digrii zao 33, unadhani waliamua tu? hapana! Walipata digrii 33 kutokana na kinachoaminiwa “human trinity” yaani ‘utatu wa kibinadamu’ kwamba ni moyo, ubongo na viungo vya siri. Wakasema kwamba viungo vya siri na ubongo vinaunganishwa na ngazi 33 za vipingili vya viungo vya uti wa mgongo (joints). Kwamba uti wa mgongo una ngazi 33 kutoka unapoanzia kwenye viungo vya siri hadi kichwani kwenye ubongo. Hapa inabidi tuwaulize madaktari watupe ukweli kuhusu hizo ngazi 33 za uti wa mgongo. Mtu anapobalehe ndipo anapoanza kupanda ngazi na anapofikia umri wa kuwa na akili (ubongo) timamu iliyotulia huwa amefikia ngazi ya juu kabisa katika ubongo, sawa na kumaliza ngazi zote 33 za uti wa ubongo.

Digrii hizo 33 ni kama ifuatavyo: The Blue Lodge (Symbolic Lodge of Hatimaye imani ya freemasonry ilisambaa taratibu katika maeneo mengi duniania: Ufaransa (1718- 25), Ireland (1725-26), Hispania (1726-27), Uholanzi (1731), Ujerumani (1730-33), Africa (1735), Scotland (1736), Ureno (1736), Switzerland (1737), Italia (1733-37), Russia (1731-40), Canada (1745), Sweden (1735-48), Prussia (1738-40), Austria (1742), Poland (1784), na Mexico (1825).

Ili kujiunga na imani hii lazima mtu awe na umri wa miaka 21 (3×7) na kama ni mtoto wa freemason anaweza kujiunga akiwa na umri wa miaka 18 (9+9). Zipo Loji kuu (Grand Lodges) 150 duniani na kuna wanachama wasiopungua 6,000,000 duniani kote. Kila digrii ina mafundisho yake ambapo kadri freemason anavyopanda ngazi kutoka digrii ya chini kwenda digrii ya juu anafunuliwa siri zaidi kuhusu malengo, ibada na utaratibu mzima wa freemason na Illuminati. Albert Pike anasema: “The Blue Degrees

(the Blue Lodge degrees) are but the outer court or portico of the Temple. Part of the symbols are displayed there to the Initiate, but he is intentionally mislead by false interpretations. It is not intended that he shall understand them; but it is intended that he shall imagine he understand them”. [Albert Pike, Morals and Dogma, p. 819; Emphasis added]. Akimaanisha kwamba freemason wa digrii za chini hawapaswi kujua siri na maana halisi ya alama za freemason ila huwa anadanganywa ili afikiri kwamba anazijua.

Unaweza kuona aina za digrii hizo; kwa mfano digrii ya 18 inayoitwa ‘Knight of Rose Croix’ hushughulika na elimu ya aina za misalaba na jinsi ya kufanisha kuziingiza ndani ya taasisi na madhehebu mbalimbali kwa imani ya Illuminati na freemason na kwa kweli freemason wa digrii hiyo wamefanikiwa kwa kiwango cha juu kabisa kuingiza aina nyingizi za misalaba ndani ya makanisa na taasisi bila ya waumini kujua maana ya misalaba hiyo. Tutaona kwenye sura za mbele katika kitabu hiki.

Yapata Januari 22, 1870 Pike alipata maono ya nuru “illuminated” kutoka kwa GAOTU—Shetani—kuhusu mpango maalumu wa jinsi ya kutimiza malengo ya New World Order yaliyowekwa na Adam Weishaupt, miaka 94=9+4=13 au 9×4=36 iliyopita, tangu Mei Mosi, 1776, Malengo hayo yalipangwa yakamilike ifikapo Millenia ya 7. Ndipo akaanza kwa kuandika kitabu mashuhuri kwa freemason kinachoitwa “Morals and Dogma” ambacho kilichapwa kwa mara ya kwanza mwaka 1871, mwaka mmoja tu baada ya kupokea njozi ya kutekeleza mpango mpya wa dunia. Unaweza kujiuliza kwamba hivi mpango wa zamani wa dunia ulikuwa ni upi hadi waweke mpango mpya wa dunia? Freemason wanauita Ukristo kuwa ni “Mpango wa Zamani wa dunia” na hivyo walidhamiria kuharibu Ukristo na hivyo kuanzisha mpango mpya wa dunia (New World Order) ambao ni Upagani. Tayari viongozi wakuu wa mataifa ya dunia (UN) wamekuwa wakikutana mjini New York ili kuangalia malengo ya Millenia yamefikia wapi, na kwa uwazi wamekuwa wakisema kwamba kuna umuhimu wa kuharakisha New World Order kwa visingizio vya umaskini, maradhi na ujinga.

Ni njozi gani aliyoipata Pike mwaka 1870? Pike alivuviwa kwamba lazima kuwepo na vita kuu 3 za dunia na zilipangiliwa kwa kutumia namba na hesabu za Illuminati na freemason. Ilipofika mwaka 1914, miaka 44 kupita tangu njozi ya Pike, ndipo vita ya kwanza ya dunia ikaanza kama ilivyopangwa kwa namba za Illuminati na freemason.
Hapo kuna hesabu za illuminati zilizotumika kupanga vita hizi tatu. Njozi ilikuwa Januari 22, namba 22 = 11 x 2. Kisha ilipita miaka 44 = 11 x 4, ndipo vita ya kwanza ikaanza. Lakini pia vita kuu ya pili ilianza mwaka 1939 ikiwa ni miaka 69 = 3 x 23 kupita tangu njozi ya Pike mwaka 1870, hata hivyo namba 6 na 9 zote huabudiwa na Illuminati. Lakini pia ilikuwa imepita miaka 21 = 3 x 7 tangu kumalizika kwa vita kuu ya kwanza na kuanza vita kuu ya pili. Namba zilizotumika kuandaa vita kuu mbili za dunia ni namba 3, 6, 9 na 11. Ifikapo mwaka 2011 itakuwa imepita miaka 66 tangu kumalizika kwa vita kuu ya pili. Mpangilio wa namba 6, 66, na 666 huwa na nguvu zaidi kwa freemason na ni kutokana na miaka 66 kupita tangu vita ya pili illuminati wamepanga kuanzisha vita ya tatu ya dunia. Tutaona kwenye sura mbeleni.

Pike alifariki manamo Aprili 2, 1892 huko Washington DC. Tutarudi kuchunguza njozi ya Pike na mpango wa vita kuu tatu (3) za dunia zilivyopangwa kwa namba na hesabu za Illuminati. Yesu aliahidi kwamba “……. hakuna neno lililositirika, ambalo halitafunuliwa; wala lililofichwa ambalo halitajulikana. Niwaambialo ninyi katika giza, lisemeni katika nuru; na msikialo kwa siri lihubirini juu ya nyumba.” Mathayo 10:26-28 na sasa siri zilizopangwa na Illuminati zinafichuka na si muda mrefu ulimwengu utashuhudia vita kuu ya 3 na ya mwisho ya dunia itakayotumiwa kama sababu ya kuundwa kwa serikali na dini moja ya dunia. Unajua nini kilitokea mara baada ya vita kuu ya kwanza na ya pili za dunia? Je, vita kuu ya tatu itaanza lini? itakuwaje? Umejiandaaje na vita hiyo? Malengo ya New World Order hatimaye yatakamilika lini? Kumbuka kuwa vita ya kwanza na ya pili za dunia zilipangwa kwa makusudi yenye malengo ya kutekeleza mipango ya Illuminati na hawawezi kutumia namba 2 maana hiyo siyo namba yao hivyo lazima waanzishe tena vita kuu ya 3 ya dunia ndipo wafanikiwe kuanzisha serikali na dini moja.

Hilo tutaliona mbeleni. Kwanza kabisa nini maana ya Freemason? Katika dictionary au kamusi wanasema
kwamba Freemason is a member of a certain secret society. Yaani Freemason ni mwanachama wa chama cha siri au jamii ya siri. Hata hivyo neno Freemason linatokana na maneno mawili, Free na Mason. Maana ya Free ni huru na maana ya Mason ni mtu mjenzi wa majengo katika fani ya uwashi. Tunajua kuna wajenzi wanaoitwa kapenta, ila Masons ni wajenzi uwashi. Kwa mafundi ujenzi wa uwashi wanafahamu kwamba wakati wanajenga hasa kwa kutumia matofali, kila mstari wanaoujenga huitwa kozi, kwa Kingereza course. Hivyo pia Freemason wanapojenga wanajenga kwa kozi wanazoziita degree. Je, Freemason wanatumia nini kwenye ujenzi wao? kama tulivyoona kwenye siri za Freemason, wanajenga kwa kutumia mawe, ambayo ni watu wasiojua kama wanatumiwa kujenga. Freemason wanajenga nini? Wanajenga ulimwengu mzima wa dini, siasa, uchumi na kazi/kilimo/ajira. Katika kitabu cha Ufunuo 7:1 Biblia inataja ‘pepo nne za dunia’ ambazo zinazuiliwa na malaika wanne ili kazi ya kuwapiga muhuri watu wa Mungu ikamilike. Pepo nne za dunia huwakilisha 1)machafuko ya kidini, 2)machafuko ya kisiasa na utawala, 3) machafuko ya uchumi na biashara na 4) machafuko ya wafanyakazi na wakulima. Tutaona kwamba freemason nao wamejigawa katika makundi manne ili kuhakikisha wanafanikisha mpango mpya wa dunia ulioanzishwa na Weishaupt mwaka 1776 na hivyo kumaanisha pepo nne za dunia kama zilivyoelezewa na Mungu kwenye kitabu cha Ufunuo 7:1. Tumeona kwamba Illuminati/freemason wameungana na mnyama wa namba 666 na hili linathibitishwa na

Padre wa kanisa Katoliki Martin Malachi kwa kusema kwamba “He is protected by four governments” “people of the world seem to him ready for strong worldwide moral government with control.” (The keys of this Blood pp. 120, 160), akimaanisha kwamba Papa na Vatican inalindwa na serikali nne na hatimaye ulimwengu wote utatawaliwa na Vatican. Je, serikali hizo nne ni zipi? Ni makundi manne ya freemason. Kuna degree 33 za Freemason. Mtu anapoanza katika hatua ya kwanza atatakiwa kusoma degree ya kwanza inayoitwa Entered Apprentice degree; kisha atpanda na kufika Degree ya pili inayoitwa Fellow Craft Degree na Degree ya tatu inaitwa The Master Mason degree hadi kufikia degree ya 33 ambayo ndiyo ya juu kabisa. Kama tulivyoona utaratibu wa kujiunga na Jesuits ni pamoja na viapo vikali, hapa pia tunaona kwamba unapoingia katika Freemason utatakiwa kuapa katika kila ngazi unayopanda, hapa nitaweka viapo katika kila ngazi tatu za awali, nitaweka katika lugha ya Kingereza bila kutoa tafsiri ya moja kwa moja, nitaelezea kwa ujumla wake maana ya viapo hivyo; kama hujui lugha ya Kingereza, tafadhali naomba umhusishe aliye karibu nawe ili akufafanulie; kabla ya kuapa, atasomewa maneno yafuatayo:

“Mr. _______, before you can proceed further in Freemasonry, it will be necessary for you to take an Obligation appertaining to this degree. It becomes my duty as well as pleasure to inform you that there is nothing contained in the Obligation that conflicts with the duties you owe to God, your country, your neighbor, your family, or yourself. With this assurance on my part, are you willing to take the Obligation?” (Nevada ritual, circa 1984)
Maneno hayo yanamaanisha kwamba unapoingia Feemason utaendelea kuwa na mahusiano na Mungu wako, na nchi yako, na jirani zako, na familia yako kama kawaida. Lakini Freemason wanamwabudu mungu yupi? Wao wanamwabudu mungu anayeitwa GAOTU – Great Architect Of The Universe – yaani ‘Mbunifu mkuu wa ulimwengu.’ Freemason hawamwabudu Mungu wa Ibrahimu, Isaka na Yakobo. Sala zao zote huelekezwa kwa GAOTU. Architect ni mtu anayebuni ramani za majengo, majengo unayoyaona katika nchi mbalimbali yakiwemo yale yaliyomo ndani ya miji ya nchi yetu, yanatokana na ubunifu wa watu wanaoitwa Architects. Ni watu wenye elimu kubwa sana kuhusu mambo ya ubunifu na ujenzi wa majengo. Freemason nao ni wajenzi wa maadili wanayoyataka wao na pia wanaye Architect (mbunifu) wao mkuu ambaye ndiye wanayemwabudu, jina la Architect wao ni GAOTU. Huyo ndiye mbunifu mkuu wa shughuli za Freemason katika ujenzi wa ulimwengu, wengine ni watekelezaji tu.
Wapo watu pia wanaoelekeza sala zao kwa viumbe badala ya kuelekeza kwa Muumbaji. Wao pia hawatofautiani na Freemason maana wote wanakwenda kinyume na Mungu, na ukweli ni kwamba wanafanya hivyo kutokana na ubunifu wa GAOTU maana kazi yake ni kubuni mbinu mbalimbali za kuwafanya watu wawe mbali na Mungu. Yesu anasema kwamba tunapotaka kusali tusali hivi, “Baba yetu uliye mbinguni……” Mathayo 6:9-13, ikimaanisha kwamba sala zetu zote tuzielekeze kwa Mungu aliye mbinguni tena kwa Jina la Yesu. GAOTU anajua kwamba Mungu alisema, “mtu akijikwaa katika neno moja, amekosa juu ya yote” Yakobo 2:10, ndio maana anajitahidi kuwafanya watu wamkosee Mungu hata katika kitu kidogo, na watakuwa wamemkosea juu ya yote. Hivyo unaweza ukawa mlokole, msabato, mkatoliki, muislamu, mbudha, myahudi nk. lakini ukimkosea Mungu katika jambo moja tu umemkosea juu ya yote. Ndio maana leo hii katika dunia nzima kuna utitiri wa madhehebu na dini za kila aina. Wataalamu wanasema kuna dini zaidi ya elfu tatu! Je, wote watakwenda Paradiso? Biblia inasema, “Je! Hamjui ya kuwa wale washindanao kwa kupiga mbio, hupiga mbio wote, lakini apokeaye tuzo ni mmoja?” 1 Wakorintho 9:24. Hivyo pamoja na kuwa na dini nyingi kiasi hicho na dini zote zikiwa zinadai kupiga mbio ili kupata tuzo ya uzima wa milele, ni wale tu wanaotii kila moja ya amri za Mungu ndio wanaopiga mbio vizuri na ndio watakaopata tuzo, nao watatoka katika dhehebu moja tu. Kwa nini watu huingia Freemason? Ni kwa sababu ya kutaka utajiri wa dunia hii. Wakati shetani anamjaribu Yesu, alimwonyesha utajiri, “Kisha ibilisi akamchukua mpaka mlima mrefu mno, akamwonyesha milki zote za ulimwengu, na fahari yake, akamwambia, Haya yote nitakupa, ukianguka kunisujudia.” Mathayo 4:8, 9. Baada ya ibilisi kushindwa kumnasa Yesu, sasa aliendelea kutumia njia hiyo hiyo kwa kumtumia mnyama ili awape watu utajiri kupitia Freemason, tunasoma kwamba, “Lakini katika mahali pake atamheshimu mungu wa ngome; na mungu ambaye baba zake hawakumjua atamheshimu, kwa dhahabu na fedha, na vito vya thamani na vitu vipendezavyo…..na yeye atakayemkubali atamwongeza kwa utukufu; naye atawapa kumiliki wengi; naye ataigawa nchi kwa rushwa.” Danieli 11:38,39. Ndio maana watu wengi wanaingia kwenye vyama vya siri kama Freemason na kila anayeingia humo hufanywa apate kumiliki vitu vingi na kuwa tajiri mkubwa, tena hao ndio chanzo cha rushwa nchini na hata kusababisha ufisadi wa hali ya juu katika nchi mbali mbali.

Unapokubaliana na swali katika maneno ya awali hapo juu, utatakiwa kuapa kwa kuzingatia ngazi unayotaka kupanda katika Freemason. Viapo hivyo ni kama ifuatavyo: Entered Apprentice Degree: “….my throat cut across, my tongue torn out, and with my body buried in the sands of the sea at low-water mark, where the tide ebbs and flows twice in twenty-four hours, should I ever knowingly or willfully violate this, my solemn Obligation of an Entered Apprentice.”
Fellow Craft Degree: “….my left breast torn open, my heart and vitals taken thence, and with my body given as a prey to the vultures of the air, should I ever knowingly, or willfully, violate this, my solemn Obligation of a Fellow Craft.”; Master Mason Degree: “….my body severed in twain, my bowels taken thence, and with my body burned to ashes, and the ashes thereof scattered to the four winds of Heaven, that there might remain neither track, trace nor remembrance among man or Masons of so vile and perjured a wretch as I should be, should I ever knowingly or willfully violate this, my solemn Obligation of a Master Mason.” (Nevada ritual, circa 1984) Viapo hivyo tumevifupisha ili kuonyesha nini kitakachotokea endapo mtu ataamua kuwasaliti Freemason kama amejiunga nao. Mwanachama anapokiuka viapo hivyo hupotea kimuujiza. Wapo wanaoamini kwamba mtu anapokuwa freemason hawezi kutoka kwenye chama hicho, wanasema “Once a mason always a mason” lakini hilo si kweli maana wapo wengi walioingia kwenye vyama vya siri bila kujua kwa undani kuhusu vyama hivyo ikiwa ni pamoja na freemason na walipofahamu kwa undani walitoka, watu hao wamekuwa msaada mkubwa kutoa siri za vyama hivyo. Katika miaka ya 1800 kapteni William Morgan aliachana na chama hicho cha Freemason na alikuwa amejiandaa kutoa siri zao ndipo akakamatwa huko Niagra, New York Marekani na kuuawa, mwili wake haukuonekana hadi hivi leo. Lakini wengi wametoka na hadi leo wapo wakiendelea kutoa siri za vyama hivyo. Ndugu msomaji kama unaweza kuchunguza zaidi utagundua kuwa kuna viapo ambavyo watumishi wa madhehebu kadhaa hutakiwa kuvifanya wanapoingia katika utumishi wao. Freemason huapa kwamba watamtii GAOTU lakini pia hata watumishi wa madhehebu kadhaa huapa kutoa utii wao sio kwa Mungu bali kwa kiongozi mkuu wa kanisa husika na kwa kanisa lenyewe. Tafadhali chunguza katika dhehebu lako pengine ni wachungaji, maaskofu, mitume na manabii wa siku hizi au makasisi, nk. Cha ajabu kuna madhehebu ambayo huwaapisha watu wanapotaka kwenda kubatizwa baada ya kukubali imani yao.

Hata hivyo madhehebu hayo kwa kuwaapisha wachungaji, maaskofu au makasisi, na hata waumini wao wanapokwenda kubatizwa, wanaonyesha kuwa wametekwa na Freemason kutokana na ubunifu wa GAOTU kwa sababu Biblia inasema kwamba: “Tena mmesikia watu wa kale walivyoambiwa, Usiape uongo, ila mtimizie Bwana nyapo zako; lakini mimi nawaambia, Usiape kabisa; hata kwa mbingu, kwa maana ndicho kiti cha enzi cha Mungu; wala kwa nchi, kwa maana ndiyo pa kuweka miguu yake…wala usiape kwa kichwa chako, maana huwezi kufanya unywele mmoja kuwa mweupe au mweusi…..kwa kuwa yazidiyo hayo yatoka kwa yule mwovu.” Mathayo 5:33-37. “Lakini zaidi ya yote, ndugu zangu, msiape….msije mkaangukia hukumu.” Yakobo 5:12. Je, viapo vya watumishi wa makanisa na waumini wao vinatoka wapi kama sio kwa Freemason ambao nao huapa pia? Tena vinatoka kwa GAOTU – mbunifu mkuu wa ujenzi wa maadili yaliyo kinyume na Mungu. Mbona Biblia iko wazi kuhusu kuapa maana Mungu amekataza kuapa na hasa kwenye mambo ya dini. Freemason ni wajenzi walio huru, ambao wanafanya kitu chochote kwa uhuru bila kupingwa. Kwa vile Freemason walianza kuwepo tangu karne ya 18, sio rahisi kwa sasa kuweza kupinga malengo yao maana wao ndio wanaoshikilia uchumi wa dunia, jambo muhimu kwetu ni kujisalimisha kwa Yesu. Sehemu wanapopata mafunzo yao panaitwa Lodge, sawa sawa na chuo mahali wanafunzi wanapopata elimu yao. Lodge pia ni sehemu za ibada za Freemason.

Freemason walianza mnamo karne ya 18 wakiwa ni moja ya kikosi cha mnyama wa 666 katika kutimiza malengo yake. Wakati wa miaka 1260 (Ufunuo 13:1-8) ya mateso ya watu wa Mungu iliyoanza mwaka 538AD na kuishia mwaka 1798 kwa papa Pius VI alipokamatwa na kuifia huko Ufaransa, kulitokea mkakati wa kutaka kuendeleza utawala wa Rumi ya kidini na hivyo kuanzishwa kwa vikosi mbalimbali kwa ajili ya kutimiza malengo hayo ambapo muda si mrefu tutashuhudia lengo lao kuu likitimia.

Moja ya vikosi hivyo ni Freemason ambao nao wamegawanyika katika vikosi kadhaa. Vikosi hivyo ni pamoja na “The Knight of Malta”, ambapo kazi yake ni kushugulika na makanisa ya Kiprotestant ili yageuzwe yafanane na Rumi na kwa kiasi kikubwa kikosi hiki kimefanikiwa sana maana kimeweza kuunda umoja wa makanisa ambapo unatawaliwa na Rumi na hivyo kuwa chini ya Rumi. Hata hivyo Mungu anasema, “Na kama vile ulivyokiona kile chuma kimechanganyika na udongo wa matope, watajichanganya nafsi zao kwa mbegu za wanadamu; lakini hawatashikamana, kama vile chuma kisivyoshikamana na udongo.” Danieli 2:43. Hivyo katika muungano huo wa makanisa kuna chuma na udongo vimechangamana, chuma yakiwa ni madhehebu makubwa na yenye nguvu wakati udongo madhehebu madogomadogo katika muungano huo. Kumbuka kwamba unabii hujirudia (Mhubiri 1:9). Yohana anatuambia kwamba muungano huo utavunjika wakati pigo la saba litakapopigwa, “Na mji ule mkuu ukagawanyika mafungu matatu, na miji ya mataifa ikaanguka; na Babeli mkuu ukakumbukwa mbele za Mungu, kupewa kikombe cha mvinyo ya ghazabu ya hasira yake.” Ufunuo 16:19. Hata hivyo watakuwa wamechelewa maana mda wa kutubu utakuwa umepita. Kuhusu ufafanuzi wa kugawanyika mafungu hayo matatu katika Ufunuo 16:19, nitayaelezea kwa kina mafungu hayo matatu katika sura zitakazofuata. Pia katika kudhoofisha maadili na kuwafanya watu wasipate muda wa kusoma neno la Mungu, kikosi hiki ndicho kinachoshughulika sana na kuvumbua michezo mbalimbali na hasa mpira wa miguu ambao duniani kote una mashabiki wengi sana. Wengi hupenda kuangalia ligi kuu hasa ya Uingereza yenye alama ya Simba, je umewahi kujiuliza pesa nyingi zinazotumika kudhamini mpira, kununua wachezaji na mishahara ya wachezaji nk zinatoka wapi? Je umewahi kujiuliza kuwa unatumia masaa mangapi katika kushabikia michezo ukilinganisha na masaa unayotumia katika kutafuta uhusiano wako na Mungu? je, huoni kwamba hatimaye utajikuta unashindwa kuwa na mahusiano mazuri na Mungu? hivi karibuni kutakuwa na kombe la dunia, hii litafanyikia wapi safari hii? Nadhani kila mtu anajua! Lakini ukimuuliza akutajie mstari wa Biblia unaompa matumaini ya kuingia Paradiso, Mmmh! Kikosi hiki pia kimefanikiwa kwa kiasi kikubwa kuingiza nadharia za kibinadamu katika mambo ya kiroho. Hao ndio wanaoshinikiza wawepo maaskofu mashoga, lakini pia wameweza kuweka hata maaskofu na wachungaji wanawake. Katika Biblia hakuna mchungaji wala askofu mwanamke, Biblia inasema kwamba, “Ni neno la kuaminiwa, mtu akitaka kazi ya askofu, atamani kazi njema. Basi imempasa askofu awe mtu asiyelaumika, mume wa mke mmoja…” 1 Timotheo 3:1-7. Hapo hakuna mke wa mume mmoja, au nimesoma vibaya? Kikosi kingine cha Freemason kinaitwa “The knight of Columbus” kikiwa na kazi ya kushughulika na Siasa na Tawala za serikali zote duniani. Kazi kubwa wanayoifanya ni kuhakikisha katiba za nchi mbalimbali zinabadilishwa ili kukidhi haja zao. Moja ya mafanikio makubwa ambayo kikosi hiki kimefanikiwa ni pamoja na kufanikiwa kuzishawishi nchi mbalimbali ili iwepo sheria ya haki sawa kwa kina mama na watoto ili wawe sawa na wanaume. Ni kweli kwamba Mungu anapenda watu wote wawe na haki sawa, ila ni haki katika mahitaji kama vile hewa, chakula, matibabu, na mambo kama hayo yanayohusu uhai wa mwanadamu lakini sio usawa katika uongozi au utawala. Utasikia viongozi wakisisitiza kwamba watoto wasipigwe viboko – nyumbani wala shuleni, na hata sasa watoto wamewashitaki wazazi wao eti kwa sababu wamechapwa viboko walipofanya makosa; lakini Biblia inasema kwamba, “Usimnyime mtoto wako mapigo, maana ukimpiga kwa fimbo hatakufa. Utampiga kwa fimbo, na kumuokoa nafsi yake na kuzimu.” Mithali 23: 13,14. Maana nyingine ni kwamba Mungu anatuambia kama tunataka watoto wetu tuwaokoe na kuzimu hatuna budi kuwachapa fimbo pale wanapofanya makosa. Pia utaona wanawake nao wakishika nyazifa za utawala na kuongoza wanawake, Biblia inakataza hilo kwa kusema, “Akamwambia mwanamke, Hakika nitakuzidishia uchungu wako, na kuzaa kwako; kwa utungu utazaa watoto; na tamaa yako itakuwa kwa mumeo, naye atakutawala.” Mwanzo 3:16. Mtawala kwa mujibu wa neno la Mungu ni mwanamume. Kikosi cha tatu kinaitwa “The knight Templars”, kikosi hiki kinashughulika na shughuli zote za uchumi na biashara. Hawa wamefaulu kwa kiasi kikubwa kufanikisha biashara huria (free trade) maana kila kitu wanataka kifanyike huru, lengo la biashara huru au soko huria ni kuweza kuweka sheria moja kwa urahisi itakayosimamia shughuli zote za kibiashara, maana kama kila nchi itakuwa na sheria zake za biashara, itakuwa vigumu kukataza watu wasiuze wala kununua, kwa vile katika Biblia tunasoma “Tena kwamba mtu awaye yote asiweze kununua wala kuuza, isipokuwa ana chapa ile, yaani, jina la mnyama yule, au hesabu ya jina lake.” Ufunuo 13:17. Hivyo tunaona tena uhusiano kati ya Freemason na mnyama wa 666. Kazi wanayoifanya Freemason ni kazi ya mnyama wa 666 ndio maana watashinikiza watu wawe na chapa au hesabu ya mnyama ndipo waweze kufanya biashara. Umewahi kusikia juu ya cashless business? Ni biashara ambayo watu watakuwa wakitumia kadi ya electronics na sio fedha katika biashara zao.

Ndio maana tunaona nchi mbalimbali zikijiunga na kutumia sarafu moja, ila lengo ni kutumia sarafu moja kwa dunia nzima. Hatimaye kikosi hiki kitahakikisha kwamba hakuna mfanyabiashara wala mnunuzi atakayefanya biashara au kununua isipokuwa amemkubali mnyama wa 666. The knite Templers ndio wamiliki wa Benki kuu ya dunia na IMF. Benki ya Dunia pamoja na IMF zinamilikiwa na familia mbili za Freemason wa The knite Templers ambazo ni The Rothschilds ya Uingereza, japo wako Marekani ila chimbuko lao ni Uingereza na ni wayahudi wa kuzaliwa, familia ya pili ni The Warbugs ya Ujerumani. Kila moja ya familia hizo ina watoto watano ambao kwa kila wakati wamekuwa wakitawala katika taasisi hizo kubwa za fedha duniani. Hakuna mtu asiyejua kwamba taasisi hizi ndizo zinazotoa mikopo kwa nchi mbalimbali na hutoza riba kubwa kiasi kwamba nchi husika hushindwa kulipa madeni hayo na hatimaye kulazimika kufuata masharti yao ili wapewe msamaha wa madeni yao na kupewa mikopo tena zaidi. Kwa taarifa zaidi nenda na fungua mtandao wa google kasha search the rothschilds au the Warburg. Hebu sasa tumsikilize ndugu Baron M.A Rothschild, yeye anasema kwamba, “Give me control over a nations currency, and I care not who makes its laws.” ~Baron M.A. Rothschild, Yeye anasema kwamba “Nipe utawala wa fedha za mataifa yote, sijali ni nani anayetunga sheria zake.” Zaidi unaweza kwenda kwenye mtandao ambapo utapata kujua sababu za kuanzishwa kwa Benki ya dunia zikitajwa na Rais wa tatu wa Marekani Thomas Jefferson kwamba ilikuwa ni kwa sababu ya kuwawezesha Freemason watawale dunia. wwww.crownempire.org/index.php/illuminati/1621-theilluminati- today/. Hivi karibuni tulishuhudia kile kinachoitwa Kuyumba kwa uchumi duniani, hata nchi yetu ikatangaza mpango wa kunusuru uchumi wa nchi. Tatizo hili lilianzia Marekani kisha kufuatia nchi za Asia na Ulaya. Huo ni mwanzo wa kushinikiza nchi zote kukubaliana na kile kinachoitwa Global Economic Reform ambapo hatima yake ni kukatazwa kuuza wala kununua kama huna chapa au hesabu ya mnyama wa 666. Kikosi cha nne cha Freemason kinaitwa “Scotish Templars”, hiki kinahusika zaidi na maswala ya kazi na kilimo. Hawa wanafanikiwa kwa kiasi kikubwa kushawishi vyama vya wafanyakazi na wakulima ili walete migogoro katika nchi husika, lengo likiwa kudhoofisha serikali husika ili kwamba wapate nafasi kubwa ya kuweza kufanikisha malengo yao. Ni juzi tu kulikuwa na migomo ya waendesha ndege za mashirika makubwa ya ndege duniani wakizishinikiza serikali zao zitekeleze matakwa yao ambayo hatimaye serikali zitadhoofika na kujisalimisha kwenye mpango wa The New World Order. Vikosi vyote hivyo hushirikiana katika kusaidia kutimiza malengo ya kila kikosi na hatimaye kumuwezesha mnyama wa 666 kutimiza mipango yake. Vikosi hivyo ndizo pepo za nne za duniani alizoziona nabii Yohana akiwa katika kisiwa cha patmo. Hadi sasa malakika wanne wanaendelea kushikilia au kuzuia pepo hizo nne hadi kazi ya kupigwa muhuri kwa watu wa Mungu itakapokamilika. Hata hivyo kadri muda unavyokwenda ndivyo malaika hawa wanne wanaachilia taratibu pepo hizo nne na ndio maana tunaona dini na madhehebu ya kila aina yakiibuka na mafundisho ya mashetani, tunashuhudia migomo mikubwa ya wafanyakazi, tunashuhudia kuanguka kwa uchumi wa dunia na hata tunashuhudia nguvu za asili zikitikisa dunia kama vile mafuriko, moto, matetemeko na matukio mengine mengi. Unaweza kurejea jedwali la utawala wa Illuminati na kujifunza katika jedwali hilo utaona vikosi vinne vya freemason

Hakuna maoni: