Alhamisi, 11 Februari 2016

Mfululizo wa masomo yahusuyo Uongozi wa Kanisa 3



******************************************************************
                                     Somo; Kuigwa kwa kiongozi wa Kanisa
     Hakuna furaha kubwa kwa baba yetu wa Mbinguni anayoipata  kuliko anayoipata anapowaona watoto wake wanaitikia wito wa kuwaongoza kondoo wake.kuitikia wito wa kuwaongoza kondoo ni moja ya hatua zinazodhihirisha kukua kwa mtu aliyeokoka.katika hali ya asili Mzazi asingependa kumuona mtoto wake anabaki mchanga tu siku zote na hakui, Furaha ya mzazi hutimia anapoona moja ya watoto wake akiwaongoza wadogo zake na kusaidia kufanya majukumu ya mzazi katika hali kama hiyo Mungu hufurahi anapoona mtu aliyeokoka anakua na kuifikia hatua ya kuwaongoza wengine Lakini ni muhimu kuufahamu mapema kuwa wale ambao tumekubali kuwaongoza huwa wanaiga sana Tabia zetu hivyo ni muhimu kujifunza somo hili “kuigwa kwa kiongozi wa kanisa” tutajifunza somo hili kwa kuzingatia vipengele vitatu;-

*      Jinsi kondoo wanavyomuiga Kiongozi wa Kanisa.
*      Wajibu wa kiongozi wa kanisa kuwa kielelezo
*      Kiongozi wa kanisa ni mwakilishi wa Mchungaji

Jinsi kondoo wanavyomuiga Kiongozi wa Kanisa
     Watoto wa kike huwaangalia kwa makini mama zao wanapopika chakula katika hali ambayo wakati mwingine ni vigumu hata mama kujua kinachoendelea na hatimaye utaona nao wanatafuta vyombo vya kitoto vinavyofanana na kuanza kuwaiga jinsi ya kupika kumbe watoto ndivyo walivyo ni kwa msingi huu watoto wakiroho huwaiga wale wanaowaongoza au waliowatangulia katika wokovu kwa jambo lolote lile liwe jema au baya. Kuna usemi mmoja unaosema “ukitaka kufahamu tabia ya kiongozi waangalie wale anaowaongoza” Kiongozi kamwe hapaswi kuwaambia watu fuateni yale ninayosema na si yale ninayotenda kiongozi huyo hajui analolisema, Kuigwa kwa kiongozi katika Matendo yao ni kanuni iliyoandikwa mioyoni mwa watu  na haiwezi kuepukika  Biblia ina mifano mingi ya jinsi watu wanaooongozwa wanavyowaiga wale waliowaongoza angalia mifano hiyo katika 1Falme 22;51-53, 2Nyakati 22;1-4, Yeremia 9;14, Amosi 2;4, 2 Nyakati 17;3-4,26;3-4, 2Tomotheo 1;5.Biblia inaonyesha kuwa Simeon Petro aliandaliwa mapema kuwa kiongozi wa kanisa Luka 22;31-32,Matendo 1;15,2;14. Simeon Petro wakati mmoja kama kiongozi wa kanisa aliamua kuacha majukumu yake ya kiutumishi na kuamua kwenda kuvua samaki wanafunzi wengine walipomuona waliamua kujiunga na kiongozi wao kuvua samaki Yohana 21;7.Yesu alipowakuta wao Baharini Petro alifahamu kuwa ameonyesha mfano mbaya hususani kwa wanafunzi wale wengine akajuta na kujitupa baharini Yohana 21;7 sisi na si kama Viongozi tunawajibu mkubwa wa kuishi maisha yanayompendeza Mungu na kufahamu kuwa kuishi maisha ambayo si kielelezo ni sawa na kuisaidia kazi ya shetani, Viongozi wataigwa na wale wanaokuja nyuma yao kwa kila kitu kama tunawahi ibada, ni waombaji, tuna bidii,tunatii neno la Mungu na kulitetemekea tunatii wachungaji n.k watu wanaoongozwa humtazama kiongozi wao kwa kila jambo hata kama ni baya kama uvivu, ulegevu, uzembe n.k kwa msingi huo ni muhimu kuwa makini tunapokuwa tumeingia katika ngazio ya maongozi.
      Petro alimwangaluia sana kiongozi wake Yesu jinsi alivyokuwa anafanya maombi ya kufufuka wafu naye akaiga vilevile kabla ya kufanya maombi ya kufufuka wafu  kumbuka kuwa Yesu aliwatoa watu nje  na Petro akaiga vilevile Linganisha Marko 5;39-42 na Matendo 9;39-41 sisi nasi tukiwa kama Viongozi wa kanisa tunaangaliwa katika kila jambo. Waebrania 13;7 Nyakati za kanisa la kwanza waliwaiga Viongozi wao katika kila jambo walichofanya Viongozi ni kuwasihi wauchunguze mwisho wa mwenendo wa Viongozi wao.
Wajibu wa kiongozi wa kanisa kuwa kielelezo
     Mpaka hapo tumeona jinsi kiongozi wa kanisa anavyoweza kujenga ufalme wa Mungu au kuubomoa,kiongozi wa kanisa akafanya vema atawafanya wanaomuongoza nao kufanya vema ni kwa sababu hii ndio maana Mungu huwaheshimu sana Viongozi wa kanisa na ndio maana anataka Viongozi wa kanisa wawe vielelezo Neno la Mungu linatoa wito na wajibu kwa Viongozi wa kanisa kuwa vielelezo 1Timotheo4;12,16 Tito 2;7;1Petro 5;2-4.Viongozi Nyakati za kanisa la kwanza walijitahidi sana kuwa vielelezo na ndio maana ufalme wa Mungu ulijengeka kwa kasi sana na kwa namna ya kipekee katika wakati wao 1Koritho 11;1, 4;16,Wafilipi 3;17,4;9,1Thesalonike 2;10,2Thesalonike 3;7,9, Mungu hana upendeleo Neema ya Mungu iko kwa kila kiongozi  kutusaidia kuwa kielelezo kwa ajili ya kujenga ufalme wake Bwana ampe neema kila mmoja wetu kuwa kielelezo katika jina la Yesu Kristo.

Kiongozi wa kanisa ni mwakilishi wa Mchungaji.
     Ni muhimu kuufahamu kuwa mtu anapoteuliwa kuwa kiongozi katika sehemu yoyote iwe kanisa au cell au makanisa ya nyumbani au vijana au kina mama au maombi au kikundi chochote yeye ni  ana kuwa ni mwakilishi wa Mchungaji katika eneo husika ina maana ya kuwa kiongozi huyo huongoza eneo lake hilo kwa niaba ya Mchungaji hivyo unafanya kile ambacho Mchungaji angekifanya  katika sehemu hiyo Luka 10;1, hivyo anayemsikiliza kiongozi anamsikiliza Mchungaji anayekataa hamkatai Mchungaji tu bali na yeye aliyewatuma Luka 10;16,Kwa msingi huo ingawa Viongozi hawa hawaitwi wachungaji Lakini ni wachungaji wa maeneo yao waliyopewa kuyasimamia hivyo kila unapofanya jambo jiulize kuwa hiki ninachikifanya je Mchungaji angekifanya? Kwa msingi huo wewe kama kiongozi ni muhimu kukumbuka kuwa uko karibu na watu kusaidia huduma ya kichungaji na hivyo maisha yako kama kielelezo yatasaidia kujenga au kubomoa ufalme wa Mungu na kanisa lake kwa nia moja kabisa tukatae kutumiwa na ibilisi kuliharibu kanisa la Mungu na chini ya neema ya Mungu tuseme kama Paulo mtume “MNIFUATE MIMI, KAMA MIMI NINAVYOMFUATA KRISTO”

Hakuna maoni: