Alhamisi, 4 Februari 2016

Mfahamu Adui Shetani !



Mstari wa msingi 1Timotheo 5;15 “Kwa maana wengine wamekwisha kugeuka nyuma na kumfuata shetani”
Mtu aliyeokolewa anaweza kugeuka nyuma na kumfuata shetani kama hatamfahamu shetani ni nani na Fikra zake 2Wakoritho 2;11 Shetani ni adui yetu Luka 10;19 Ni adui wa watu waliookoka kama alivyo adui wa Mungu Tutajifunza somo hili kwa kuzingatia vipengele viwili vikuu vifuatavyo;-


·         Historia ya shetani
·         Mbinu za shetani   anazozitumia kutuletea upinzani

Historia ya shetani
 Shetani hapo kwanza hakuwa adui wa Mungu, Yeye aliumbwa na Mungu kama walivyoumbwa malaika wengine, alifanywa kuwa malaika mkuu na kupewa utukufu mwingi na Mungu. Hatimaye alikuwa na tamaa na kiburi cha kutaka kuwa sawa na Mungu na hata kumpindua Mungu aliyemuumba. aliwashawishi malaika wachache kupigana na majeshi ya Mungu na matokeo yake walishindwa vibaya na kutupwa nje ya mbinguni hivyo akawa siyo malaika mkuu tena aliyekuwa na jina Lucifer ambalo maana yake ni mwenye kutoa mwanga kama nyota ya alfajiri na tangu wakati huo aliitwa shetani Ezekiel 28;13-19, Ufunuo 12;7-9 Isaya 14;12. Jina shetani maana yake ni  Adui , mpinzani, mshindani mwenye kuleta vizuizi kazi zake kubwa ziko sawa na majina yake ni adui wa watu wa Mungu ni mshindani ,huleta upinzani  na vizuizi kwa watu wa Mungu hususani waliookolewa  katika hali ya chuki kabisa  ili ikiwezekana waache imani  na njia ya wokovu  ya kweli ya kumfikisha mtu mbinguni  Yeye anaijua njia hiyo ya kweli lakini kwa kusudi anataka kupotosha watu wamuache Yesu ambaye ndiye njia na kweli na uzima  ni shetani anaye waambia watu kuwa hakuana wokovu  na kuwa watu wanaweza kumuona Mungu bila Yesu  na kwa kutumia udanganyifu anawakosesha wengi.Matendo 16;16-18 Shetani anamfahamu Yesu kuwa ni  mwana wa Mungu  na kuwa ndiye wa kuhubiriwa  na kuleta wokovu na kuwa wanaohubiri injili ya wokovu wana nguvu kubwa  na ufalme wa Mungu unawasubiri Marko 3;11 Matendo 19;13-16.

     Shetani baada ya kuasi mbinguni yeye na malaika zake  wamekwisha kuhukumiwa  na mahali pao ni katika ziwa la moto wa Milele na hawana nafasi ya kutubu tena Mathayo 25;41 Ufunuo 20;10  na kwa sababu uzuri wa mbinguni anaufahamu  anachokifanya ni kuwadanganya watu  na kushindana na watu waliookoka  ili wamfuate na kuteswa pamoja naye katika ziwa la moto milele, anaweza kuwafanya waliookoka kuwa na wokovu vuguvugu na hatimaye waweze kutapikwa Ufunuo 3;15-16 safari ya mbinguni ni kama mpira wa miguu katika dunia ambapo mtu anayekwenda kufunga goli huzuiwa kwa namna zote hata kupigwa ngwala  na viatu ilimradi tu asifanikiwe kufunga goli 

Mbinu za shetani anazozitumia kutuletea upinzani.
Ni muhimu kufahamu kuwa shetani wakati wote haji katika njia ambayo utafahamu kuwa ni shetani  kwani kwa njia hiyo watu watashituka upesi , Mara nyingi huja kama malaika wa nuru akiwatumia wachungaji wengine wanaosema kuwa wameokoka  au watu wanaosema kuwa wameokoka  kututoa katika kweli ya wokovu 2Wakoritho 11;14-15 baada ya kushindwa kuuzuia wokovu wako unapokuwa umeokoka shetani kama Farao huwa hakati tama yeye na majeshi yake hujaribu tena na tena  kukurudisha nyuma kama farao alivyo jaribu kuwafuatailia wana wa Isarael shetani atajaribu kufanya hivyo ili turudi nyuma na kumtumikia yeye tena Kutoka 14;5-8 wakati ulipookoka shetani alishindwa  vibaya  kushindana na nguvu za Yesu aliye Bwana na mwokozi wetu na akasalimu amri Kutoka 12;30-36 kwa msingi huo shetani atatumia mbinu mbalimbali kukufanya uache wokovu hususani ukiwa bado mchanga  katika wokovu kwani kuua kitu kichanga ni rahisi zaidi alijaribu kuwaua Yesu na Musa katika uchanga wao Kutoka 1;15-22,2;1-10, Mathayo 2;13 mbinu zote za shetani zinajumuishwa katika kukushawishi uuache wokovu Biblia inasema katika 1Nyakati 21;1 “Tena shetani akasimama akamshawishi Daudi kuwahesabu Israel “ Kushawishi ni kubadili nia ya mtu kwa kumuumbia mawazo mengine  juu ya jambo kinyume na mawazo yale aliyokuwa nayo  mwanzoni kabla ya kushawishiwa shetani  atatumia mbinu mbalimbali katika kushawishi ikiwemo

1.       Kukushawishi yeye mwenyewe ili uache njia ya kweli
Unaweza kuona katika akili yako kunaumbika mawazo yaliyo kinyume na wokovu ulioupokea na hatimaye kukufanya usipige hatua yoyote ya ziada tangu ulipookolewa  mawazo ya aina hii yanatokana na shetani, endapo utayafuata mawazo hayo unakuwa umefuata mawazo ya ibilisi na mawazo yako mwenyewe  na huo ni uasi kwa Mungu Isaya 65;2 Ni lazima ukatae kuafikiana na kila wazo lililo kinyume na njia ya wokovu.

2.       Atatumia watu kukushawishi uiache njia ya kweli
Mara baada ya wokovu utaona watu wanaoandamana kukushawishi kurudi dhambini utashangaa marafiki wa zamani  wakikujia na kukualika katika uvutaji wa sigara bangi na ulevi na dhambi nyinginezo  watakuambia kuwa wana hela nyingi na wahahitaji watu wa kutumia nao , utashangaa watu wanakulaumu kuwa umepotea au kukucheka na kudharau uamuzi wa Busara ulioamua na wanaweza hata kukutenga au kukuchukia kabisa  inakupasa kuwa mwangalifu watu wakikuvuta kurudi dhambini  usiwasikilize wala usiwajali na ujitahidi kujiepusha nao ili wasije wakainyonya nguvu yako  ya wokovu mistari ifuatayo ni muhimu kwako Mithali 1;10-16, Torati 13;6-8 Mithali 24;1 na Hosea 7;8-9

     Shetani atatumia kila njia kuhakikisha kuwa unakosa mafundisho ili ubaki umedumaa bila kukua katika wokovu ili hatimaye urudi nyuma na kuiacha kweli ya wokovu kwa sababu hiyo  utaweza kuona siku za mafundisho  ndio wageni wanakutembelea  nyumbani pamoja na hayo usikubali kuacha kwenda kanisani  na kukaa na wageni  kama watataka uende nao itakuwa vema.

 Wakati mwingine unaweza kuona kama unafanya biashara majira ya siku na saa za ibada ndio biashara inachanganya sana hilo pia ni kusudi la ibilisi kukufanya utafute mapato na kukosa ibada, aidha watu wanaweza kukushawishi na kulaumu kuwa siku hizi umekuwa bise huonekani vyovyote iwavyo ni heri ukose kipato lakini usiikose mbingu Yohana 12;25 ni muhimu kujikana nafsi unaweza kukutana na watu wanaokudhihaki kuwa siku hizi mbona maswala ya ibada yanazidi au watu wanaomsema vibaya mchungaji wako au askofu wako  na kutaka kukutoa katika imani  jihadhari  wajibu watu hao kama nikodemu alivyowajibu wale waliokuwa wakimsema vibaya Yesu mchungaji wetu Yohana 7;45-51 unaweza kuona pia siku za mafundisho na ibada ndio homa zinacharuka na hali za kujisikia vibaya au kuona uvivu au kuumwa kichwa au tumbo la kuhara n.k kemea hali hiyo na chukua hatua ya imani kwenda ibadani utashangaa jinsi ambavyo shetani atakavyokimbia na hali hiyo kutoweka katika dakika usiyoijua Yakobo 4;7,1Petro 5;8-9.

Usimuamini au kumfuata mtu awaye yote ambaye anasema ameokoka lakini anakuvunja moyo kwenda ibadani au kuendelea na wokovu au kuenda katika kanisa linalohubiri wokovulililo tofauti na kanisa au dini yako ya kwanza isiyohubiri wokovu fahamu kuwa huyo ni mpinzani anayetaka kukutoa kwenye kweli akiwa amekuja kama malaika wa nuru au mtumishi wa haki 2wakoritho 11;14-15

Kwa ujumla jihadahari na jambo lolote lile linalokunyima kuenda katika ibada bila sababu za msingi au kukukosesha wokovu, shetani anajua kuwa ukipata mafundisho utaimarika na kuwa askari utakayemdhibiti vilivyo

Usikubali kwenda kwenye mikesha ambayo itakufanya kesho yake ushindwe kulisikia Neno la Mungu vema, Neno la Mungu linauwezo wa kumbadilisha mtu wala usikubali mialiko ya kuhubiri huku wewe ukiwa mchanga kiroho kwani kwa sasa unahitaji kujifunza neno kwanza  na kuwa na muda mrefu wa kujifunza neno kabla ya kuhudumu 1Tomotheo 1;7 Yakobo 3;1 kila jambo linalokuzuia kusikia au kujifunza neno likatae na kujihadhari nalo usikubali kuiacha kweli ya wokovu kaa katika imani uliyoipokea na kudumu katika fundisho hii ndio itakuwa siri ya kukufanya uwe mshindi na zaidi ya mshindi Warumi 8;35-37.

Hakuna maoni: