Alhamisi, 4 Februari 2016

Kugeuka Nyuma na kuuacha Wokovu !



Mstari wa msingi Mwanzo 19;16-17 “ Akakawiakawia nao wale watu wakamshika mkono na mkono wa mkewe na mkono wa binti zake  wawili , kwa jinsi Bwana alivyomuhurumia , wakamtoa nje  ya mji ikawa walipomtoa nje mmoja alisema jiponye nafsi yako usitazame nyuma wala usisimame katika hilo bonde popote ujiponye nafsi mlimani usije ukapotea “

 Nguzo ya Chumvi

Wewe na mimi siku ile bwana alivyotuokoa Yesu alituhurumia  na kututoa na kutuweka nje ya mji  unaposoma Mwanzo 19;12-19, utaipata picha hii vizuri  kuokolewa ni kama Yesu ametutoa nje ya mji wa Sodoma na Gomora yaani sawa na dunia hii ya watu watendao maovu ambayo wakati wowote itaanguka katika hukumu ya Mungu Isaya 24;19-20, wakati wowote Mungu atauhukumu ulimwengu huu na kelele za ulevi na uasherati havitasikika tena  wakati walimwengu watakapohukumiwa motoni  lakini Lutu alionywa kuwa ajiokoe mwenyewe kwa kutokugeuka nyuma
Mtu awaye yote aliyeokoka anaonywa kuto kurudi nyuma Luka 9;62  Yesu akamwambia mtu aliyetia mkono wake kulima kisha akaangalia nyuma hafai kwa ufalme wa Mungu Biblia inatuonya kuwa tusigeuke nyuma baada ya kuwa tumeokolewa mkewe Lutu yeye baada ya wokovu mkuu aligeuka nyuma  kwa kuipenda dunia Mwanzo 19;26 na tunasoma kuwa akawa nguzo ya chumvi awaye yote ambaye ameokolewa kisha akaangalia nyuma na kukumbuka maisha ya anasa za dunia hii uasherati, uvutaji wa sigara na madawa ya kulevya kukumbuka sinema na dansi huyo anawezea kuharibiwa na ulimwengu huu na kupoteza wokovu mkuu kiasi hiki. 

 NINI MAANA YA KUGEUKA NYUMA 
·         Nikumsaliti bwana Yesu – mtu yeyote aliyeokolewa anapoamua kurudi nyuma hana tofauti na Yuda kwani anamsaliti Bwana Yesu  Luka 22;47-48
·         Kugeuka nyuma na kuacha wokovu ni kumkana Bwana Yesu na kudai kuwa hatumjui kama alivyofanya Petro Mathayo 26;71-72

·         Kugeuka nyuma na kuacha wokovu kunakufanya uwe nguzo ya chumvi Mwanzo 19;26  nchi yenye chumvi ni nchi iliyolaaniwa  hakuna kitu kinaweza kustawi katika inchi ya chumvi hata maji yake hayanyweki  wala kiumbe chochote hakiwezi kuishi Yeremia 17;5-6, Kumbukumbu 29;23 

·         Kurudi nyuma na kuacha wokovu ni kujionyesha kuwa wewe ni mkosaji mbele za Mungu  na wote wakaao mbinguni  Mwanzo 11;3-8  kuacha wokovu ni kuyajenga tena yale uliyoyabomoa  ni kujionyesha jinsi ulivyo mkosaji mbele za Mungu soma Wagalatia 2;18 siku ile ulipookoka mbingu ilishangilia kwaajili yako sasa unaporudi nyuma ni aibu kule mbinguni ni huzuni na kilio kikubwa na masikitiko na ibilisi na ufalme wake unashangilia kukupatawewe tena  huu ni ukosaji mkubwa mbele za Mungu na majeshi yake huko mbinguni.

·         Kugeuka na kuacha wokovu ni kumtukama Mungu Hesabu 15;30
·         Kugeuka nyuma na kuacha wokovu ni kumkanyaga mwana wa Mungu na kumfanyia jeuri Roho wa neema Waebrania 10;26-29
·         Kugeuka nyuma na kuacha wokovu  ni kumsulubisha mwana wa Mungu mara ya pili na kumfedhehi kwa dhahiri Waebrania 6;4-6
·         Kugeuka nyuma na kuacha wokovu kunakufanya uwe nchi inayoota magugu na miiba  soma Waebrania 6;7-8, Yohana 15;1 Kutoka 16;4, Hosea 10;12
·         Kugeuka nyuma na kuacha wokovu ni sawa na mbwa aliyerudia matapishi yake mwenyewe na nguruwe aliyeoshwa kurudi na kugaagaa matopeni 2Petro 2;20-22, Mithali 26;11 

TATIZO LA KURUDI NYUMA HUANZIA MOYONI
Mtu aliyeokoka anaporudi nyuma jambo hili huanzia moyoni Matendo 7;39  ziko dalili kadhaa zinazoweza kuonyesha kwamba mtu Fulani amegeuka nyuma na kuacha wokovu
Hatataka kulitii neno la Mungu tena, Hofu ya Mungu ndani yake inakuwa haiko, hafurahii mafundisho ya neno la Mungu na hufikia hatua ya kulikataa neno la Mungu na kukosoa kila aina ya mahubiri na hakuna cha kumgusa, atalizoea neno la Mungu na kuliona la kawaida, haoni umuhimu wa kukaa katika mafundisho, hufikia hatua ya kulidharau neno la Bwana Hesabu 15;31, Mithali 13;13  mtu wa aina hii anaitwa mtu aliyeshiba njia zake mwenyewe Mithali 14;14 ageukaye moyoni hushiba njia zake mwenyewe.

SABABU ZINAZOSABABISHA WATU WENGI KURUDI NYUMA
·         Kukosa viongozi wanaofundisha kweli ya neno la Mungu Kutoka 32;1 Waamuzi 2 18-19
·         Kuupenda ulimwengu huu wa sasa 2Timotheo 4;10 Mithali 24;1,23,17 Warumi 12;2 2Wafalme 17;15
·         Kukaa katika ushirika uliojaa maasi Mathayo 24;12
·         Kukosa mizizi na hivyo kuogopa dhiki na mateso Luka 8;13 Mathayo 13;20-21,Luka 12;4-5 inatupasa kufahamu kuwa imetupasa kuingia katika ufalme wa Mungu kwa njia ya dhiki nyingi  Matendo 14;19-22
 kwa msingi huo basi inatupasa kuendelea kushikamana na wokovu  kama mwanzo wa uthabiti wetu Waebrania 3;14.

Hakuna maoni: